EPA na mambo yake


Source: Michuzi
Jamani JK amefanya tusilotegemea, nimependa sana hii Picha Jeetu Patel akipanda Karandika kwenda rumande. Mahakama itufurahishe watanzania. Nina Imani JK akiamua anaweza, nasubiri siku atakaponda kizimbani Rostam na Manji

Ushi
 
Friends:

This is for you. Please register as early as possible, limited number of seats available. you will get to know more about this kind of Business (Forex Trading). Attached advert has more information.

Free Online Forex Trading Seminar

When: Friday, November 28, 2008:
Time: 05:00 pm-07:00 pm.
Speaker: From Nairobi
Where: Azania Front (Underground Hall)
Register: Mramba Nkalang’ango (mrambagsn@hotmail.com)
 

Attachments



yale yale, kwenda kushawishiwa utajiri, mwisho wa siku unalambwa.....
 
Kuhusu familia hizo kuwa na pesa kabla ya EPA hilo linawezekana...Kwa mfano Njake alikuwa na pesa kabla ya EPA.

Mkuu samahani,
Lema aka Njake aka 7Up ni mtu wa 'shughuli' siku nyingi. Alikuwa na pesa ndio, za uharamia wa kila aina ya biashara. Ameanza hizi kazi za uchafu siku nyingi ndio maana sikushangaa nilipomwona ametajwa kwenye hili. Ila nimeona picha yake kweli wakati ukuta...amezeeka sasa
 

Mkuu sikumaanisha kuwa kinyume na mtizamo wako...Not neccessarilly...Ila nilikuwa nikizungumzia specifically kuhusu kashfa ya EPA vs kuwa nazo ama kutokuwa nazo...I mean before the EPA scandal.
Kuhusu upatikanaji wa pesa zake before EPA ndio hapo sina data za kutosha na hivyo siwezi kusema lolote.
Ila nasikia alianza na biashara ya machinjio na alikuwa na na tenda ya kusupply nyama mahospitali, magereza nk.
Na hiyo ilikuwa miaka ya nyuma nadhani...Then alikuwa akifanya biashara za bia...Na baada ya hapo mafuta...Zaidi ya hapo sijui.
 
Tuko sambamba Mkuu Mushi
Alikuwa ananunua (kama ameacha) mali za 'front line' namaanisha AM style
Hizo biashara za 'kukamua maziwa' kila mwizi anazo kufichia wizi wake
 
Watuhumiwa EPA wafikia 20 kortini
Halima Mlacha
Daily News; Monday,November 10, 2008 @20:01


Wafanyabiashara watatu jumatatu walifikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam kujibu tuhuma za kujipatia mabilioni ya fedha kutoka kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), na hivyo kufanya idadi ya watuhumiwa kufikia 20.

Mbali na wafanyabiashara mbalimbali, watuhumiwa wengine waliopandishwa kizimbani hadi sasa, wamo wafanyakazi wanne wa BoT. Akisoma mashtaka dhidi ya washtakiwa wawili ambao ni Ajay Somani na Jai Somani mbele ya Hakimu Mkazi wa Kisutu Victoria Nongwa, Wakili Mwandamizi wa Serikali Fredrick Nakulilo, alidai watuhumiwa hao wanakabiliwa na makosa matatu.

Alidai katika kosa la kwanza wote wawili walikula njama ya wizi wakiwa na watu wengine ambao hawajafahamika ya kuiibia BoT, na kwamba Septemba 2, 2005, waliiba Sh bilioni 5.9 mali ya benki hiyo.

"Pia mnadaiwa kujipatia ingizo la fedha kwenye akaunti zenu, na Septemba 2, 2005 jijini Dar es Salaam, kwa nia ya kudanganya mlijipatia kutoka BoT ingizo la fedha shilingi bilioni 5.9 kwa kujifanya Kampuni ya Liquidity Services Ltd imepasiwa deni lenye kiasi hicho kutoka Kampuni ya Society Alsacience De Construction De Mashines Textiles," alidai Nakulilo.

Alidai upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na kwamba upande wa mashtaka hauna pingamizi la dhamana iwapo washtakiwa watatimiza masharti yake. Hakimu Nongwa, alitoa masharti ya dhamana kwa washtakiwa hao kuwa dhamana ya kosa zima ni fedha taslimu Sh bilioni 2.9, hivyo kila mshitakiwa atatakiwa atoe nusu yake ambayo ni Sh bilioni 1.4 au mali isiyohamishika yenye thamani ya fedha hizo.

Pia alisema pamoja na fedha hizo, washitakiwa hao wanatakiwa kuwa na wadhamini wawili kila mmoja, ambao ni waajiriwa katika taasisi zinazotambulika na hawatakiwi kutoka nje ya Dar es Salaam na walitakiwa kukabidhi hati za kusafiria. Washtakiwa wote wawili walikana makosa hayo na kurudishwa tena rumande hadi pale watakapotimiza masharti ya dhamana na kesi hiyo itatajwa tena Novemba 25, mwaka huu.

Aidha, mbele ya Hakimu Mkazi Euphemia Mingi, mfanyabiashara Mwesiga Lukaza, alipandishwa kizimbani akiunganishwa na mshtakiwa mwingine Johnson Lukaza, ambaye alishapandishwa kizimbani juzi, kujibu mashtaka ya kujipatia mabilioni ya fedha za EPA.

Akisoma maelezo ya mshtakiwa huyo, Wakili wa Serikali Bwisalo Maganga, alidai mshtakiwa huyo anakabiliwa na mashtaka matatu ya kula njama, kuiba na kujiingizia katika akaunti kiasi cha Sh bilioni 6.3 mali ya BoT. Alidai Septemba 2, 2005 jijini Dar es Salaam, mshtakiwa akiwa na lengo la kurubuni alijipatia kiasi hicho cha fedha kwa kudanganya kuwa Kampuni ya Kernel Ltd imehamishiwa deni kutoka Kampuni ya Marubeni Corporation ya Japan.

Hakimu Mingi alisema dhamana ya kosa hilo ni Sh bilioni 3.1 hivyo mshtakiwa huyo na mwenzake Johnson kila mmoja atatakiwa kutoa fedha taslim Sh bilioni moja na wadhamini wawili wa kuaminika. Mshtakiwa huyo alikana makosa yote na alirudishwa rumande hadi pale atakapokamilisha masharti ya dhamana na kesi hiyo itatajwa tena Novemba 18, mwaka huu.

Watuhumiwa ambao tayari wamefikishwa mahakamani ni Farijala Hussein, Rajab Maranda, Japhet Lema, Bahati Mahenge, Davis Kamungu, Godfrey Mosha, Manase Mwakale na Eddah Mwakale, Devendra Vinodbhai Patel, Amit Nandy, Ketan Chohan, Jayantkumar Chandubahi Patel na Johnson Lukaza.

Wengine ni wafanyakazi wa BoT ambao ni Mkuu wa Idara ya Madeni ya Biashara, Iman David Mwakyosa, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Madeni, Ester Mary Komu na makaimu Katibu wa benki wawili ambao ni Bosco Ndimbo Kimela na Sofia Joseph Lakila.

Kati ya watuhumiwa hao, ni wawili tu ambao wako nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana hiyo ambao ni Godfrey Mosha na Davis Kamungu. Washitakiwa wengine licha ya dhamana zao kuwa wazi, wanaendelea kusota rumande kutokana na kushindwa kutimiza masharti.
 
naomba ufafanuzi.
tuliambiwa kwamba watuhumiwa wamenyang'anywa
pasi za kusafiria na serikali sasa inakuwaje tena
hapo mahakamani wanatakiwa kuzisalimisha?
mbona sijasikia msoma mashtaka akieleza mahakama
kwamba hati hizo zipo mikononi mwa serikali.
au ndio taratibu za kimahakama kukutaka usalimishe kitu
hata kama kuna taarifa kwamba hicho unachotakiwa
kusalimisha kipo mikononi mwa serikali
 

Wacha waendelee kunyea ndoo kwa siku kidogo.
Lakini usikute wamepelekewa magodoro na dawa ya mbu😀
Kifo cha tajiri huwa ni hatari.
 

Kumbe wako Rumande? Mbona halisemwi hapa hilo mimi sikujua kua wako lupango nilifkiri wote wako nje, eti huu ni utani tu wa muungwana?

Sometimes tumpe crediti japo kidogo rais wetu, yaani kati ya watuhumiwa 20, ni wawili tu wako nje wengine wote wako ndani, na hii eti inatakiwa kuwa kanyaboya?
 
je ni kweli kuwa jamaa mwenye mkanda wa uzito wa juu wa ufisadi( mh. rostam aziz) nae katiwa pingu??, mwenye news alete tafadhali ili tuwanze kupart kabla dansi halijaanza!
 
mwanakijiji ulisha wahi kufanya mahojiano na rostam aziz kuhusu hongo alompa mtikila, jaribu kumpigia sim tena umuulize kama yuko lupango mkuu, natamani sana kujua hili.
 
Rostam hajafungwa na hawezi fungwa unless it becomes absolutetely necessary...as in it becomes certified (with some hard evidence) kwamba jamaa kapiga tukio.. nikama kusema Apson afungwe.. that can never and will never happen...EVER
 
sio kufungwa mkuu kinyambiss, mie binafsi inatosha kabisa hata kama akienda segerea kwa masaa 3 tu kwa wizi wa EPA, yaani akipanda ile karandinga mie roho ita suuzika sana, na hapo nitaamini kuwa kweli kikwete ni mhuni kamili anaeweza kufanya usanii kwenye jumba la sanaa! sababu naamini kabisa kuwa kama rostam aziz akitiwa lupango Lowassa nae atakuwa njiani kuona vijana wa ukonga wanakula vipi!
 
Yaani kama mafisaidi hawajaachiwa hivi hivi bila kujijua mimi nipo hapa maana sasa hivi kila mtu anamega kivyake sasa nyinyi kaeni muangalie wakati huko wanaongea kitasha......
 
Jamani tusilale..lalelale.... nahisi kama hile ari ya kufuatilia hii kashfa inapungua kadiri watuhumiwa wanavyozidi kufikishwa mahakamani! Naona mijadara inaanza kuwa ni myepesi! Bado makampuni 12 (thenashara), na kwahiyo ninashauri ule MOTO tulionzanao kujadili hili suala usizimike....

Kwa maana tukiridhika na ufikishwaji wa watuhumiwa mahakamani itakuwa ni sawa sawa na kumbembeleza mtoto aache kulia kwa kumpa pipi! Inawezekana kulia kwake si pipi bali ana minyoo!
 

Yale yale ya zima moto. Habari ina-hit vyombo vya habari halafu ghafla ziiiima inapotea. Kuna mtu aliwahi kuuliza humu kuhusu aina yetu ya ufuatiliaji habari. Hii ni aina mpya ya uandishi wa habari. Unauza zikiwa za motomoto. Zikipoa hazina ladha. Hakuna tena mtu mwenyekutaka kufuatilia hizi habari zilishachuja tayari. Kubenea aliwahi kuambiwa kuwa kila siku Lowasa anatawala gazeti lake hana habari nyingine zaidi? Hatuna utamaduni wa kuandika na kufuatilia issue mpaka mwisho. This is bongo fleva now, hata bongo fleva nazo kuna nyingine zinakaa kwenye chat kwa muda mwa mwaka angalao.
 
Hivi hawa Godfrey Mosha na Davis Kamungu ni akina nani? Maana katika kundi lote hilo na masharti magumu kiasi hicho hawa tu ndio wameweza kuwekewa dhamana.

Kama kuna mtu ana habari zaidi tafadhali tumwagie hapa.

Kumbe Lukaza bado yuko ndani?

Mwaka huu kazi ipo kweli kweli.
 
No wonder this njake guy has littered the ms - ars highway with gas stations..... Lile ghorofa kule njiro halitakalika vizuri sasa.


Huyu njake ni Fisadi tangu enzi na enzi tukianzia biashara ya Boarder Kenya na Tzania. Amedhulumu watu wengi sana na nina imani anavuna matendo aliyofanyia watu wengi. Hayo ni machozi ya wengi. Hili zee ni kigeugeu sana. Ukifanya naye biashara na akipata mteja mwingine mwenye cha juu zaidi anakukana na anakurudishia hela ili hata apate mia tano zaidi. Ana tamaa ya pesa na tamaa ndiyo itamdidimiza.

Alikuwa hakosi kukutana na Marehemu Balali kule Holiday Inn, maana ndo Hotel aliyokuwa anashukuia wakati huo. Siku hizi nasikia akija Dar hashukii tena Holiday Inn.

Balali alikuwa anatuma vijana wake hadi Arusha kwa Njake ili kupanga dili vizuri ila kwa bahati mbaya kwa kuwa Njake hajasoma hata darasa moja zaidi ya kufundishwa kusoma na kusaini cheki basi walimdanganya wao kina Balali na vijana wake wakachukua kiasi kikubwa cha hela naye akabakiwa na kiasi kidogo sana. Mwishowe anazilipa zote mwenyewe. Ila alimaliza mapema sana kulipa deni, nafikiri alikuwa wa kwanza kumaliza kurejesha ila tena sielewi imekuwaje kukamatwa???

Kwa ufadhili wa ssm ni nambari moja. Ofisi yake kila kona kuna certificate of appreciation toka ssm kwa mchango wake mkubwa wakati wa campaign na shughuli za kichama. Kuna gas station yake kukl Hanang Katesh imeandikwa CCM na kabisa. Arusha yote na Moshi ni gas station, ukiachilia mbali majumba, hotels and camp sites, tours, kiwanda cha maji ya kunywa, you name all. Ati ameokoka anasali kwenye makanisa ya kiroho!!!!!

Habari ndo hiyo!!! Tusubiri.
 
hotels and camp sites, tours, kiwanda cha maji ya kunywa, you name all. Ati ameokoka anasali kwenye makanisa ya kiroho!!!!!

Habari ndo hiyo!!! Tusubiri.

Huku ndo walimmaliza kabisaaaaaaaaaaa Njake wa watu! jamaa alikuwa anamezea group ya Leopard Tours. Wapambe walimwambia kuna kampuni inataka kujitenga na Leopard hivyo wanatafuta mtu mwenye uwezo wa kuwa na gari nyingi ambacho kilikuwa kigezo muhimu. Baada ya mzee kufungua tours aliagiza toyota landcruiser 15 zote long base. At the end of the day hakukuwepo na kampuni iliyojitenga na Leopard akabakia na biashara ya car hiring. Magari yameanza kuchoka ile mbaya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…