KWA umoja wao vyombo vya habari Tanzania baada ya kuwa co-opted na wajanjuzi wa Chama twawala waliwaona wagombea ukuu wa chama hicho kuwa ni malaika.
Miaka miwili na nusu baadaye leo Alhamisi 28 Agosti 2008 vyombo vyote vinamkamia mkuu kutokana na suala la EPA!
Hata hivyo, mie ninaona jamaa hawa wanashughulikia dalili za ugonjwa na sio chanzo cha gonjwa lenyewe.
Nina maana kwamba ukiangalia toka huko nyuma iwe suala la NOLAN na miradi ya ajabu; suala la rada mbovu; suala la Benki Kuu; suala la Richmond na masuala mengi mengi tu ya ~ISSUE- za tenda kuna mzizi ambao tunapaswa kuuangalia ili masuala kama haya yasiwe yanajirudia rudia.#
Kama hamjalijua angalau nishavizindua vyombo vya habari vya nje. Suala lenyewe jamani ni kwa namna gani vyama vyetu vya kisiasa vinajiendesha, vinapata pesa wapi, toka kwa nani, kwa sababu gani, kwa njia gani na kwa malengo yepi.
Kama vyama vyetu vya siasa vitaendelea kuchota toka hazina au toka Social Security or Pension funds or Health Insurance funds -kila anayechota atadaia ilikuwa ni kwa ajili ya shughuli za chama.
Hebu basi acheni nyie waandishi kuwa bendera fuata upepo. Fuatilieni au anzisheni ajenda zenye msisimko wa kitaifa na zinazokusuia kubadili nchi kwa kuwa na uongozi mzuri badala ya uongozi mbovu.
MWANZO wa yote mkumbuke kuwa nyie kama vyombo vya habari mna uwezo mkubwa wa kuwa na mfululizo wa makala na vipindi vinavyoweza kushinikiza serikali kuanzisha mchakato wa KATIBA MPYA. Maana tupende tusipende viraka ndivyo vilivyotufikisha hapa tulipo. Ingawa Kenya walikuwa nyuma sana kwenye masuala ya demokrasia tusishangae baada ya miaka michache wakawa mbele yetu. Na kama tumejifunza kutoka Kenya na kwingineko Afrika muda ukifika wa kuwa na KATIBA MPYA hakuna namna ya kuahirisha mambo. Mkiwaachia hawa jamaa kuahirisha mambo, mwaka njoo, mwaka nenda, hatima yake yote ni kuwa na matatizo sampuli hii yanayojirudia tena na tena.
Miaka miwili na nusu baadaye leo Alhamisi 28 Agosti 2008 vyombo vyote vinamkamia mkuu kutokana na suala la EPA!
Hata hivyo, mie ninaona jamaa hawa wanashughulikia dalili za ugonjwa na sio chanzo cha gonjwa lenyewe.
Nina maana kwamba ukiangalia toka huko nyuma iwe suala la NOLAN na miradi ya ajabu; suala la rada mbovu; suala la Benki Kuu; suala la Richmond na masuala mengi mengi tu ya ~ISSUE- za tenda kuna mzizi ambao tunapaswa kuuangalia ili masuala kama haya yasiwe yanajirudia rudia.#
Kama hamjalijua angalau nishavizindua vyombo vya habari vya nje. Suala lenyewe jamani ni kwa namna gani vyama vyetu vya kisiasa vinajiendesha, vinapata pesa wapi, toka kwa nani, kwa sababu gani, kwa njia gani na kwa malengo yepi.
Kama vyama vyetu vya siasa vitaendelea kuchota toka hazina au toka Social Security or Pension funds or Health Insurance funds -kila anayechota atadaia ilikuwa ni kwa ajili ya shughuli za chama.
Hebu basi acheni nyie waandishi kuwa bendera fuata upepo. Fuatilieni au anzisheni ajenda zenye msisimko wa kitaifa na zinazokusuia kubadili nchi kwa kuwa na uongozi mzuri badala ya uongozi mbovu.
MWANZO wa yote mkumbuke kuwa nyie kama vyombo vya habari mna uwezo mkubwa wa kuwa na mfululizo wa makala na vipindi vinavyoweza kushinikiza serikali kuanzisha mchakato wa KATIBA MPYA. Maana tupende tusipende viraka ndivyo vilivyotufikisha hapa tulipo. Ingawa Kenya walikuwa nyuma sana kwenye masuala ya demokrasia tusishangae baada ya miaka michache wakawa mbele yetu. Na kama tumejifunza kutoka Kenya na kwingineko Afrika muda ukifika wa kuwa na KATIBA MPYA hakuna namna ya kuahirisha mambo. Mkiwaachia hawa jamaa kuahirisha mambo, mwaka njoo, mwaka nenda, hatima yake yote ni kuwa na matatizo sampuli hii yanayojirudia tena na tena.