badiebey
JF-Expert Member
- Nov 29, 2013
- 5,875
- 3,112
...........Mimi hii kitu nina uzoefu nayo, nilipofika labor tu niliambiwa nipewe epidural.
Niliwakatalia, nikasema mimi nataka kuzaa kwa uchungu, tena uzazi wangu wa kwanza
nataka nisikie uchungu. Sasa uchungu ulivyokuja, weweeeee!! Bahati Mbaya mtoto aligoma kutoka,
hivyo nikaa na uchungu for almost 10 hrs, ile uchungu unakuja, unatoka. Baadaye uchungu ulivyochanganya
na mtoto hatoki, weeeeeee!! Nilihitaji mwenyewe epidural!! Niliwaambia nichomeni tu epidural.
Baada ya kupewa epidural tu, sikusikia uchungu hata kidogo. na Tv nilitazama!! Chezea epidural!!
Hata hivyo mwanangu bado aligoma kutoka, after 18 hrs ya labor... nikaishia emergency C-section.
Nikija kuzaa tena, lazima nipewe epidural. Ya nini kupata uchungu mkali vile na wakati kuna option ya kutopata uchungu. Ukipata mtaalamu mzuri haina tatizo lolote.
polehh mwayaa, such a long labour