Penye nyeupe pawe peupe na penye Nyeusi pasemwe ni peusi, Tusipinfishe.
Big up sana Kenya.
Ujue zamani huku Tz ili ufungue account process ilikuwa ni ndefu sana, sijui kusaini barua ya balozi wa nyumba kumi, mwenyekiti wa mtaa, bla bla bla, yani it was a lengthy and exhausting process.... yani hata kupata atm card hapo inabidi usubiri hata wiki 2 baada ya kufungua account.
Nikasema wacha nifungue account Equity nihakikishe kama kweli wanafungua account haraka, Zap!! in a finger snap within 5 minutes nikawa namiliki account na atm card, nlishangaa sana.
Kitu kingine ni internet banking, Tangu zamani nlikiwa na account Crdb bank ambayo ni kubwa huku Tz, Sasa nlikiwa siwezi kutransact online payments hata nikiingiza zile namba za atm inakataa, nikaenda tawi la crdb kucheki utaratibu wa internet banking, nakumbuka nimesainishwa sana forms kila nikienda naambiwa subiri subir subiri, miezi 9 imepita tunapigishana kiswahili tu hakuna vitendo, nilivyoenda equity kufungua account na kupewa atm kadi nikauliza kama maweza fanya malipo online wakaniambia kila kitu tayari, Nakumbuka niliingia ebay nikaagiza vitu, vikafika baada ya 3 weeks posta, i was just so amazed.
Kitu kingine, hizi benki zetu hasa crdb zamani ikifika saa 10 benki ishafungwa na siku za weekends ni jumamosi tu hadi saa sita, Equity akaja huku yani benki inafungwa saa 12 na hata jumamosi ni kazi kazi, kilichotokea ni kwamba nao crdb nao wakaanza kuchelewa kufunga, siku hizi hata jumapili benki zipo wazi 😁😁, hii ilifanyika kwajili ya ushindani mkali wa equity maana wangeleagea basi equity ange dominate in a long run.
Equity benki safi, upinzani walioleta naushukuru sana maana umezipa wake up call benki zetu za hapa Tz.
Equity huwa naitumia sana mambo ya online ila kutunzia pesa nipo kule kule crdb.
Tuwe tunapeana changamoto, ndio undugu mzuri, Sio kuponda ponda tu kila kitu,
To conclude, kuna maendeleo kenya wanapata sababu ya tz na tz wanapata kutoka kenya, Mambo ya kutambiana huyu hana hiki sisi tunacho au huyu ana shida flani sisi hatuna ni kama ujinga tu, lets focus on development.