Erasto Nyoni, na golikipa Nduda ni mali ya Simba Sc

Simba nao kuna muda wanachekesha. Hivi ni nani aliyewashauri kusajili hao wazee? Ukianza na huyo Nyoni, Okwi na hata John Bocco?

Rage aliwahi kuwaita mashabiki wa Simba kuwa ni Mbumbumbu na wala hakukosea hata kidogo.
Na kesho ukisikia nyoni sio simba ila kasajiliwa yanga uje hapa kuomba radhi.yeboyebowewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Simba imemsajili beki wa kiraka, Erasto Nyoni kwa mkataba wa miaka miwili.
Nyoni amejiunga na Simba akitokea Azam FC ikiwa ni siku chache baada ya kufanya vizuri katika michuano ya Cosafa.

Kitu kizuri kwa Nyoni ni uwezo wake wa kucheza namba zote nne za ulinzi.

Pia anaweza kucheza nafasi ya kiungo mkabaji kwa ufasaha hali inayomfanya kuwa na nafasi kubwa ya kucheza.

Nyoni alirejea nchini na kujiunga na Azam FC akitokea Vital'O ya Burundi.

Kwa Hisani ya Salehe Jembe
 
Acha utani bhana! Kwa hiyo Erasto ana miaka 27? Tangu 2007 yupo timu taifa! Sijui alianza soka lini! Hivi ni nani anapendekeza usajili wa simba msimu huu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Simba hivi sasa imeachana na wavulana sasa inasajili wazee wa kazi ,wavulana wanaleta sana utoto
Pili simba ikisajili watoto watu wanawarubuni hao watoto kisha wanaanza kuleta maringo na kucheza chini ya kiwango,ni kheri usajili wazee wanao jituma kuliko kusajili wavulana wanyoa viduku ubishoo mwingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nini tafsiri yako kuhusu wachezaji wazee?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…