Tetesi: ESTIM kujenga barabara Kimara - Kibaha

Tetesi: ESTIM kujenga barabara Kimara - Kibaha

Lakini nakumbuka kuna uzi uliletwa hapa ukionesha barabara imepasuka, (sina uhakika kama ilikuwa kwa lengo la kuichafua kampuni au vinginevyo) kwa mtazamo wangu naona barabara iliyojengwa kwa kiwango kizuri ni ile inaanzia daraja mbili kwenda Iringa japo sijui ni kampuni gani iliijenga
Wale walikuwa wanaitwa interbetton ambao sasa wanajiita BAM...dutch!
 
Unajua kazi ya Bank ya Baroda na Bank of India hapa Tanzania?Chunguza hapo ndio utajua kama hela za wahindi zinabaki nchini au zinarudi India.

Au wao kua na makazi Bongo inakudatisha saaaana?
Acha chuki kiogozi, unajua mawaziri gani wastaafu watanzania ambao wametorosha hela nje ya nchi kupitia BOT kupeleka uswis? tena wanaenda kuendeleza kujenga nchi za wazungu?
 
Acha chuki kiogozi, unajua mawaziri gani wastaafu watanzania ambao wametorosha hela nje ya nchi kupitia BOT kupeleka uswis? tena wanaenda kuendeleza kujenga nchi za wazungu?
Ndio nawajua,kwa hio ina justify sio?
 
Estim wapo vizuri kupita makampuni yote ya Tanzania hata africa mashariki.

Ukiangalia madaraja ya bonde la bagamoyo japo sijapita baada ya barabara kuisha hasa majira ya mvua wamejitahidi.

Tatizo kubwa walilo nalo kidogo ni kwenye ubunifu kidogo .

Mfano barabara ya goba kwenye kona max speed ni ndogo sana, ukizidi kidogo unamwaga gari.

Makumbusho wamefanya kazi nzuri sana lakini kwenye junction kidogo wangeweka ubunifu kuruhusu magari kupishana kwa urahisi ila kazi yao ipo bora kupita hata wachina na wajapan.

Tuwaunge mkono kwa sababu pesaa inabaki bongo na waongeze watalaam hasa kwenye design. Ujenzi wapo njema sana.

Kuhusu mradi wa kimara kibaha cha msingi consultant awe mzoefu na mambo ya highway design.

Estim kama contructor ana uwezo wa kudeliver on time.

Mungu ibariki tz.

kuna consultant na contractor , design ni shughuli ya consultant, mkandarasi kazi yake ni kufuata kile consultant alichodesign!
 
Ile barabara hata dereva unajihisi hupo tz, barabara inaongea, usiku ndio usiseme, kitu kinaongea balaa
Inapendeza sana hata kwa kuiangalia, kuna ujenzi unaendelea kutoka mafinga hadi igawa inajengwa na wachina inaonekana barabara nayo ipo vizuri japo haijaisha natamani sana nayo iwe kama ya iyovi - mafinga.
 
Naomba kujua kampun inayojenga barabara pale mafinga ukiwa unaenda mbeya kiukwel uki drive kwenye njia ile unahisi hauko Tanzania ingawa haijakamilika ila hongera kampuni hiyo.
 
Barabara toka daraja mbili pale msitu wa Simba mpaka Mafinga - Iringa urefu wa km 230 imejengwa na kampuni ya intaberton kutoka Denmark.

Pia ndo kampuni iliyojenga barabara ya Tunduma - Sumbawanga urefu wa km 215.

Barabara ya Iringa - Dodoma urefu wa km 260 imejengwa na kampuni ya kichina baada ya intaberton kukataa tenda kutokana na ufinyu wa bajeti.
Umepotosha.
Interbeton(BAM Internation bv Tanzania branch) ni kampuni la Kiholanzi.
Barabara ya Tunduma - Swax imejengwa na makampuni ma3 ikiwemo BAM na sio yeye peke yake.
 
1. Bomoa bomoa ya ubungo kimara imesitishwa hadi mwakani kupisha upanuzi wa mwendo kasi kuanzia kibo hadi kimara.

2. Estim wamekabidhiwa upanuzi wa kimara kibaha njia sita.

Haya yamesemwa na mkuu wa tanroads Dar akihojiwa na mwananchi.

TANROADS wameamua kucheza na akili zetu na kuchezea fedha zetu na maisha yetu.
Sijaelewa Mkuu...Barabara ya Njia Sita Si kutoka kimara mpaka Chalinze? Au Wameamua kuugawanya huo Mradi kwa Phase?
 
Cha muhimu barabara ijengwe hii michakato ya tenda sometimes ni ubabaishaji tu
Sio kweli,
1. Bomoa bomoa ya ubungo kimara imesitishwa hadi mwakani kupisha upanuzi wa mwendo kasi kuanzia kibo hadi kimara.

2. Estim wamekabidhiwa upanuzi wa kimara kibaha njia sita.

Haya yamesemwa na mkuu wa tanroads Dar akihojiwa na mwananchi.

TANROADS wameamua kucheza na akili zetu na kuchezea fedha zetu na maisha yetu.
 
Tender ilitangazwa mwezi wa 12 kama sikosei Estim wanapiga kazi istoshe JPM anamkubali sana yule mdosi wa Estim walitoka mbali tangu enzi za ujenzi
Kama ni ESTIM kazi zo huwa ni viwango pamoja na gharama kuwa juu kidogo!
 
Back
Top Bottom