Ethiopia wanaomba hata kilomita 20 tu za ufukwe, Tanzania tuna zaidi ya kilomita 1500 lakini hakuna cha maana. Shida ni nini?

Tanzania tuna adui mmoja tu Chama Cha Mambuzi
Hapo sasa umeleta uchizi bila maarifa.

Ulizuwiwa wapi kuutumia ufukwe wa Tanzania kwa shughuli zako zozote zile?

Wenzako wamechukuwa ardhi za ufukweni nje ya mji huko, wameweka uzio wa mikoko, katikati wamefanya sehemu wanaziita "Beach Camping site" lakini ukweli wamezifanya "nude beach", uwekezaji ni kuielekeza mikoko tu iote watu washindwe kupita kukera watu wenye kujianika. Wanajianika wanalipia kwa kila kichwa 20,000 tu kwa huduma ya maji baridi iliyowekwa.

Ukitaka hema unakodisha, ukitaka uwekewe kinga ya jua ya makuti unalipia.

Wewe kaa tu uwasubiri Ethiopia, wenzako wanapiga pesa kiulaini kabisa, hata TRA hawana ujanja hapo.
 
Coast line yote ni mali ya DPW, hatuna chetu
 
Mwisho umerudi pale pale. Kuwa issue hapo ni kuwa utawala mbovu na watu kuamua kuacha kutumia akili kabisa. Sisi machizi tunaruhusiwa kutotumia akili maana hatuna. Nchi yetu inahitaji Overhaull.

Imechoka haina jipya viongozi na wananchi mmeamua kuwa machawa. Mkiamua kusifia Rais mnasifia. Mkiamua kukosoa mnakosoa. Waziri mkuu wa Ethiopia amefika hapo kwa kuamua kuchapa kazi kweli kweli. Siyo maneno na maigizo.

Watanzania mnapenda sanaa za maigizo hamwezi endelea kama kila kitu mtamtegemea mzungu, mchina au mwarabu. Hamtaki kukaza makalio mpambane. Viongozi wengi mnachagua ni wale wasio na akili, wasio na maono. Lazima nchi ituelemee.
 
Mwisho umerudi pale pale. Kuwa issue hapo ni kuwa utawala mbovu na watu kuamua kuacha kutumia akili kabisa. Sisi machizi tunaruhusiwa kutotumia akili maana hatuna. Nchi yetu inahitaji Overhaull.

Imechoka haina jipya viongozi na wananchi mmeamua kuwa machawa. Mkiamua kusifia Rais mnasifia. Mkiamua kukosoa mnakosoa. Waziri mkuu wa Ethiopia amefika hapo kwa kuamua kuchapa kazi kweli kweli. Siyo maneno na maigizo.

Watanzania mnapenda sanaa za maigizo hamwezi endelea kama kila kitu mtamtegemea mzungu, mchina au mwarabu. Hamtaki kukaza makalio mpambane. Viongozi wengi mnachagua ni wale wasio na akili, wasio na maono. Lazima nchi itulemee.
 
Kweli kabisa mkuu
Wakati mwingine sacrifices ni muhimu kwa nchi
Sisi bado sana
Jamaa ni ngangari amechimbiwa mkwara mkubwa na Egypt, Sudan, US kuhusu bwawa la umeme, hakuyumba, yupo zaidi kwa maslahi ya Ethiopia.

Kwa nchi ya pili kwa ukubwa Afrika, 13 duniani, yenye historia ndefu, utamaduni mkubwa, mzuri, kuliko nchi nyingi duniani kwa zaidi ya miaka 3000. Ethiopia imepata kiongozi sahihi kuweka misingi ya kuirudisha sehemu inayostahili.

Plan yao ni kuwa kama China ya Afrika, kuweka mazingira viwanda vingi kufunguliwa, kuwa hub ya business financial services, hub ya ndege kama Dubai, na kivutio kikubwa cha utalii. Wanakuza zaidi kilimo cha kisasa ngano nk, nafikiri ndio nchi inayouza zaidi nyama Mashariki ya kati.

Hivyo muhimu kwao kuwa na military presence na bandari kutimiza mipango yao.
 
Hutumii akili, wanakuwachia fursa, wanajuwa huyu pesa yenyewe mpaka aje mtu camping, wawache kwenda kukusanya pesa kwa Ghalib huko akiingia kusalimia akitoka anatoka anatoka na guko la caash aje camping sote muangaishane?

Kila mbuzi anakula kwa urefu wa kamba yake. Uambiwe nini tena?
 
Mimi kupiga pesa napiga. Sema kuna kipindi nakuwa na huruma. Kama binadamu. Lakini nikisema kuwa sijafaidika na serikali hii nitakuwa muongo. Lakini huwa nakaa nawaza hawa wananchi wengine wanaishije.
 
Mimi kupiga pesa napiga. Sema kuna kipindi nakuwa na huruma. Kama binadamu. Lakini nikisema kuwa sijafaidika na serikali hii nitakuwa muongo. Lakini huwa nakaa nawaza hawa wananchi wengine wanaishije.
Serikali hii imeshatangaza inatengeneza mabilionea.

Kila awamu na kitabu chake. Ukiweza tengeneza, ukishikwa usilalamike.

Kenyatta alikuwa anawaambia wakenya "uchumi mnao mnaukalia" akatengeneza mamilionea kibao wakikenya. Watu wakasingizia eti msemo wa nyerere. Nyerere alikuwa anataka mtu awe tajiri? Nyerere ni kama Magufuli walitaka wote tuwe masikini isipokuwa wanaowataka wao tu.


Mama Samia alivyoziwachia fursa sasa hivi, ushindwe mwenyewe tu.
 
Nakubaliana nawe. Wacha tule kwa urefu wa kamba zetu. Kila mwenye meno ajipakulie minyama... Safi sana.
 
Lazima afanye hivyo kwa maslahi ya nchi
Ukiangalia mataifa mengi makubwa yako maeneo hayo haswa Djibouti na ndio maana mpaka Mchina kasogea hapo
Walianza usa
Na yeye kaona fursa kubwa kijeshi na bandari pia ni kuiomba serikali ya Muse ajisogeze nae baharini

Mkuu nchi bila bahari ni msala mkubwa sana
Huna nguvu kabisa ila upo tu
Nilienda Addis mara mbili aisee ila kwa utawala wa huyu jamaa sijaenda
Ila ntaenda tena nikaone mwamba kafanikisha mangapi kwa macho
 
Kabisa imagine unanunua silaha zinapitia kwa wengine. Export, import zako zote lazima zipitie kwa wengine. Meli zako huko baharini zilindwe na navy za wengine. Ukigombana na jirani, anaweza kukuzuia kutumia bandari yake. Kupiga hatua haraka ni changamoto kidogo.
 
Mkuu, Iraq is almost landlocked country
Nilikuwa huko miaka ya 80 na Iraq alipoivamia Kuwait, jamaa alifurahi sana na kutangaza kuwa sasa tumeongeza mkoa wenye bahari
Yaani tunatoka Zakho mpaka baharini (Q8)
Imagine wairaq walifurahi sana kuwa na bahari ila kwa mda tu
Halafu sisi tuna bahari tena kipande kikubwa sana ila wala
 
Lack of vision. Tuna nchi kibao zinatuzunguka kuna watu zaidi ya milioni mia moja wanahitaji kutumia bandari zetu kwa mahitaji yao muhimu. Hii rasilimali moja tu ya kimkakati kwa nchi makini ingetutoa.
 
Lack of vision. Tuna nchi kibao zinatuzunguka kuna watu zaidi ya milioni mia moja wanahitaji kutumia bandari zetu kwa mahitaji yao muhimu. Hii rasilimali moja tu ya kimkakati kwa nchi makini ingetutoa.
Unafikiri hawalijui hilo, wanalijua sana ila ni uroho wao tu
Huwa naomba Mungu aje mtu ambae atapambana na wizi wa mali ya umma na sio bla bla ooh naanzisha mahakama ya wahujuma uchumi hell No tunataka watu wafungwe hata miaka 50 na wafie jela
Wangefungwa hata 300 haraka basi naona wangenyooka
Wonasiasa kama wanahonga ili wachaguliwe na kuja kuiba mali za umma hao ndio wa kufungwa maisha
Ila tatizo wanajuana wote
Tuliaminishwa Magu hana makundi lakini hakufunga majizi
Mpaka anakufa kuna miradi mingi ilipigwa haswa
Na kuna watu wametajirika sana kwa haramu wakati wa utawala wake

Kwa unafiki hawajambo sana na sidhani kama tutafika mahali
Zanzibar wanaibeza ila ipo siku watafika mbali sana
 

JPM hakuwa perfect, lakini amefanya mambo mengi ya msingi kulisaidia taifa, vitu ambavyo watu walifikiri haviwezekana. Angalia nchi ilipokuwa 2015.

Alifanya vitu kama :-Umeme wa uhakika, maji, tunapata share yetu kwenye madini, Elimu bure, kukamilisha Terminal three, vituo vya afya nchi nzima, SGR, Bwala la Nyerere, barabara ya Kimara, barabara nchi nzima. Nidhamu serikalini, kupunguza ukiritimba rushwa, upigaji wa miradi,Madaraja nchi nzima, ukarabati wa meli na kununua meli mpya katika maziwa mbalimbali.

Alijaribu kuhimiza uchapakazi, kukemea rushwa, wizi, ufisadi, udini. Mafisadi wengi aliwabana ila ni kweli hakuwamaliza wote.

Alijaribu kuhimiza nchi kuwa na mentality na attitude ya kujitegemea badala ya kuombaomba. Aliwahimiza Watanzania wajiamini na kutembea kifua mbele. Aliweka misingi thabiti ili kujenga nchi imara.
 
Benevolent dictator
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…