Mwandishi Mohamed Kuyunga wa gazeti la Michezo la Mwanaspoti la leo tarehe 16 Januari 2015 anadai 'eti pamoja na kuibuka kidedea na ubingwa wa kombe la Mapinduzi, Simba yenye maskani yake Mtaa wa Msimbazi bado ina kazi kubwa ya kufanya ili kuweza kuwapa imani mashabiki wake kutokana na kuboronga kwake katika michezo iliyopita ya ligi. Kwa mtazamo wa kila mshabiki wa Simba na wanamichezo wote kwa ujumla hii ni kweli tupu na hata kocha wa Simba Goran Kapunovic ameweka wazi tamaa yake kuona timu inahamishia makali ktk ligi ambako kunatarajiwa kuwa na upinzani mkali zaidi.
Lakini pamoja na kuandika tahadhari hii, ukisoma makala yake huhitaji kuwa mchambuzi uliyobobea kung'amua kuwa hoja zake zimekaa kishabiki na kinazi zaidi kitu mabacho sio sawa kwa mwandishi wa aina yake anayepaswa kuchambua kitu objectively.
Ukianza na kichwa cha makala yake kinajieleza wazi pale mwandishi huyu anaposema 'Hakuna Anayejali kama Simba Ni Bingwa wa Mapinduzi' ambapo kwa mtazamo wangu amekusudia kubeza waziwazi ubingwa wa Simba katika kombe la Mapinduzi. Ni vigumu kuamini kama ingekuwa ni timu nyingine imeshinda kombe hili kama angeweza kupata ''guts' za kuandika kichwa cha namna hii. Hapa mwandishi kwa kujua au kutokujua anaonekana kuwa alikuwa na mabingwa wake wateule kichwani ambapo Simba haikuwa mojawapo. Hili si kosa, lakini kubeza mafanikio ya timu kwa kuwa tu hukuitarajia hakukupi sababu ya kubeza ushindi huu. Hata hivyo kusema 'hakuna anayejali...' amekosea sana. Huu ni ushabiki wake tu kwa kuwa mashabiki wapenzi wa Simba wanajali ndio maana walikesha wakifurahia ushindi.Wachezaji pamoja na benchi la ufundi wote wanajali kiasi cha kudai kuwa ushindi umewapa morali ya kupambana katika michezo ya Ligi. Huyu anayesema hakuna anayejali ni nani?
Ndani ya mada ndio kuna hoja za kishabiki zaidi ambazo ni aibu kwa mwandishi kuonyesha mwelekeo wako wa chuki waziwazi wakati unafanya kazi ya umma. Mwandishi Kuyunga kuna sehemu anasema ''ushindi wa Simba katika kombe la mapinduzi si wa kujivunia sana kwani haikuweza kukutana na timu nyingi zinazocheza Ligi Kuu Bara kama vile Azam, Yanga na KCCA ya Uganda ambazo zingekuwa kipimo tosha kwa kikosi chao.'' Hoja hii inaficha kilichomo katika akili ya kinazi ya mwandishi kuwa Simba haina cha kujisifu sana kwa kuwa imekutana na timu za Zanzibar, kwa maana kama ingekutana na timu nyingine isingeshinda! Huu si uanamichezo. Mwandishi anasahau kuwa timu hizi anazozitaja zilikuwa zimeshatolewa katika hatua za Robo fainali na Nusu Fainali na kwamba Simba ililazimika kuzifunga timu zilizozishinda timu anazojua yeye ni bora kama vile POLISI waliokuwa wababe wa KCCA, JKU waliokuwa wababe wa YANGA na MTIBWA waliokuwa wababe wa AZAM. Mantiki inakataa kuwa Mtibwa, Polisi na JKU zilibahatisha zote kufuzu nusu fainali na fainali yenyewe. Come on mwandishi give credit where it deserves hasa ukizingatia kuwa Mtibwa ndio kiongozi wa Ligi ya Bara, mwandishi unataka ukumbushwe hilo kuwa hakuna timu bora Tanzania Bara kwa sasa zaidi ya Mtibwa kama unazungumzia kiufundi na kimantiki?
Hoja kwamba safu ya ushambuliaji ya Simba ni butu kwa kushindwa kupachika mabao ya kutosha nayo imekaa kishabiki zaidi hasa ukizingatia kuwa ni Yanga pekee ndio timu iliyofunga magoli mengi zaidi kuliko Simba! Tofauti pia ni goli 1 pekee! Hapa kuna mambo mawili ambayo ni ama timu nyingi zilijaandaa kiasi cha kufanya mashindano kuwa makali, au, timu zote ikiwemo hizo Yanga, Azam na KCCA zilikuwa na safu mbovu za ushambuliaji! Wakati anajadili hili mwandishi angepaswa kuzingatia kuwa kundi alilotokea Simba lilikuwa 'gumu' zaidi kuliko makundi mengine ambako timu zilikuwa zinapigwa magoli anayoyaita ya kutosha. Ikumbukwe kundi la Simba liliingiza timu 3 nusu fainali labda kwa faida ya mwandishi, timu zilizotoka kundi la Simba hazijafungwa na timu yoyote kutoka kundi tofauti na la Simba katika mashindano haya. Kwa mantiki hii mwandishi angejenga hoja kuwa timu zote zilizoshoriki katika mashindano haya hazikuwa ktk ubra wao angeeleweka kuliko kudai kuwa timu zilitolewa mapema zilikuwa bora kuliko zilizofika nusu fainali na fainali! Mwandishi anaweza kutoa ushihidi upi ukakubalika katika hili zaidi ya ushabiki?
Hoja kuwa safu ya ulinzi ya Simba bado haijathibitisha uimara wake na yenyewe ni ya kishabiki zaidi kwa kuwa Simba ingefanya nini kuthibitisha hili? Kuruhusu bao 1 pekee ktk mechi 6 ni ushahidi ambao haujavunjwa na timu yoyote ktk michezo hii. Mtibwa, Yanga na Azam zote zimeruhusu idadi hii au zaidi so huwezi ukatofautisha beki hzi zinazoonekana kuwa bora na ile ya Simba.
Mwisho ningeweza kuendelea zaidi na zaidi kuelezea 'ushabiki' wa waziwazi wa mwandishi lakini bora niishie hapa. Niseme tu sitaki kuaminisha jamii kuwa Simba iko kamili kabisa lakini si vizuri pia kubeza mafanikio yao hata kama ni kidogo kwa hadhi ya Simba. Ni jambo baya mwandishi kuchukua hoja za mashabiki mtaani kisha unakuja kujaza gazeti bila kufanya due diligence ya kutosha. Uchambuzi unaofaa ni ule unaoelezea ubora na ubovu wa timu fairly bila mwelekeo wa chuki au husuda.
Ni vizuri waandishi wetu kujua kuwa manpoandika maandishi yenu yanasomwa na wengi, na wengine wetu tunapenda sana mtu afanye critique iliyojaa hoja, mifano, takwimu na facts nyinginezo na sio criticism ya kishabiki kwa kujenga hoja zilezile ambazo Yanga Azam au Mtibwa wanahukumiwa nazo lakini zinatumika kubeza timu moja pekee? Ni nini hiki zaidi ya ushabiki?
Lakini pamoja na kuandika tahadhari hii, ukisoma makala yake huhitaji kuwa mchambuzi uliyobobea kung'amua kuwa hoja zake zimekaa kishabiki na kinazi zaidi kitu mabacho sio sawa kwa mwandishi wa aina yake anayepaswa kuchambua kitu objectively.
Ukianza na kichwa cha makala yake kinajieleza wazi pale mwandishi huyu anaposema 'Hakuna Anayejali kama Simba Ni Bingwa wa Mapinduzi' ambapo kwa mtazamo wangu amekusudia kubeza waziwazi ubingwa wa Simba katika kombe la Mapinduzi. Ni vigumu kuamini kama ingekuwa ni timu nyingine imeshinda kombe hili kama angeweza kupata ''guts' za kuandika kichwa cha namna hii. Hapa mwandishi kwa kujua au kutokujua anaonekana kuwa alikuwa na mabingwa wake wateule kichwani ambapo Simba haikuwa mojawapo. Hili si kosa, lakini kubeza mafanikio ya timu kwa kuwa tu hukuitarajia hakukupi sababu ya kubeza ushindi huu. Hata hivyo kusema 'hakuna anayejali...' amekosea sana. Huu ni ushabiki wake tu kwa kuwa mashabiki wapenzi wa Simba wanajali ndio maana walikesha wakifurahia ushindi.Wachezaji pamoja na benchi la ufundi wote wanajali kiasi cha kudai kuwa ushindi umewapa morali ya kupambana katika michezo ya Ligi. Huyu anayesema hakuna anayejali ni nani?
Ndani ya mada ndio kuna hoja za kishabiki zaidi ambazo ni aibu kwa mwandishi kuonyesha mwelekeo wako wa chuki waziwazi wakati unafanya kazi ya umma. Mwandishi Kuyunga kuna sehemu anasema ''ushindi wa Simba katika kombe la mapinduzi si wa kujivunia sana kwani haikuweza kukutana na timu nyingi zinazocheza Ligi Kuu Bara kama vile Azam, Yanga na KCCA ya Uganda ambazo zingekuwa kipimo tosha kwa kikosi chao.'' Hoja hii inaficha kilichomo katika akili ya kinazi ya mwandishi kuwa Simba haina cha kujisifu sana kwa kuwa imekutana na timu za Zanzibar, kwa maana kama ingekutana na timu nyingine isingeshinda! Huu si uanamichezo. Mwandishi anasahau kuwa timu hizi anazozitaja zilikuwa zimeshatolewa katika hatua za Robo fainali na Nusu Fainali na kwamba Simba ililazimika kuzifunga timu zilizozishinda timu anazojua yeye ni bora kama vile POLISI waliokuwa wababe wa KCCA, JKU waliokuwa wababe wa YANGA na MTIBWA waliokuwa wababe wa AZAM. Mantiki inakataa kuwa Mtibwa, Polisi na JKU zilibahatisha zote kufuzu nusu fainali na fainali yenyewe. Come on mwandishi give credit where it deserves hasa ukizingatia kuwa Mtibwa ndio kiongozi wa Ligi ya Bara, mwandishi unataka ukumbushwe hilo kuwa hakuna timu bora Tanzania Bara kwa sasa zaidi ya Mtibwa kama unazungumzia kiufundi na kimantiki?
Hoja kwamba safu ya ushambuliaji ya Simba ni butu kwa kushindwa kupachika mabao ya kutosha nayo imekaa kishabiki zaidi hasa ukizingatia kuwa ni Yanga pekee ndio timu iliyofunga magoli mengi zaidi kuliko Simba! Tofauti pia ni goli 1 pekee! Hapa kuna mambo mawili ambayo ni ama timu nyingi zilijaandaa kiasi cha kufanya mashindano kuwa makali, au, timu zote ikiwemo hizo Yanga, Azam na KCCA zilikuwa na safu mbovu za ushambuliaji! Wakati anajadili hili mwandishi angepaswa kuzingatia kuwa kundi alilotokea Simba lilikuwa 'gumu' zaidi kuliko makundi mengine ambako timu zilikuwa zinapigwa magoli anayoyaita ya kutosha. Ikumbukwe kundi la Simba liliingiza timu 3 nusu fainali labda kwa faida ya mwandishi, timu zilizotoka kundi la Simba hazijafungwa na timu yoyote kutoka kundi tofauti na la Simba katika mashindano haya. Kwa mantiki hii mwandishi angejenga hoja kuwa timu zote zilizoshoriki katika mashindano haya hazikuwa ktk ubra wao angeeleweka kuliko kudai kuwa timu zilitolewa mapema zilikuwa bora kuliko zilizofika nusu fainali na fainali! Mwandishi anaweza kutoa ushihidi upi ukakubalika katika hili zaidi ya ushabiki?
Hoja kuwa safu ya ulinzi ya Simba bado haijathibitisha uimara wake na yenyewe ni ya kishabiki zaidi kwa kuwa Simba ingefanya nini kuthibitisha hili? Kuruhusu bao 1 pekee ktk mechi 6 ni ushahidi ambao haujavunjwa na timu yoyote ktk michezo hii. Mtibwa, Yanga na Azam zote zimeruhusu idadi hii au zaidi so huwezi ukatofautisha beki hzi zinazoonekana kuwa bora na ile ya Simba.
Mwisho ningeweza kuendelea zaidi na zaidi kuelezea 'ushabiki' wa waziwazi wa mwandishi lakini bora niishie hapa. Niseme tu sitaki kuaminisha jamii kuwa Simba iko kamili kabisa lakini si vizuri pia kubeza mafanikio yao hata kama ni kidogo kwa hadhi ya Simba. Ni jambo baya mwandishi kuchukua hoja za mashabiki mtaani kisha unakuja kujaza gazeti bila kufanya due diligence ya kutosha. Uchambuzi unaofaa ni ule unaoelezea ubora na ubovu wa timu fairly bila mwelekeo wa chuki au husuda.
Ni vizuri waandishi wetu kujua kuwa manpoandika maandishi yenu yanasomwa na wengi, na wengine wetu tunapenda sana mtu afanye critique iliyojaa hoja, mifano, takwimu na facts nyinginezo na sio criticism ya kishabiki kwa kujenga hoja zilezile ambazo Yanga Azam au Mtibwa wanahukumiwa nazo lakini zinatumika kubeza timu moja pekee? Ni nini hiki zaidi ya ushabiki?