kama alivyosema ADII...inawezekana wengine kwa kumhitaji mtu anasema hayo baada ya hapo anapotezea na wengine ni maisha waliyonayo ndani ya nyumba yanapelekea kusema hayo.
Uko sahihi kbs mamito,mie huwa nawaulizaga ulilazimishiwa ndoa?yani ni unafiki usiokuwa na kipimo na kutuona hatujawashtukia jaman nasema kbs ole wake mtu ameoa alafu anijie na hii gia atajuta kunifahamu!
DA naomba nikunyooshee kuwa tamaa tu ndiyo inayowasumbua watu wa dizaini hiyo. Hivi ukimtongoza mtu mpaka umdanganye ndiyo akukubali? Inaeleweka kuwa inaweza kutokea kutokuelewana ndani ya nyumba lakini siyo kufikia kusema ulikosea kufanya uchaguzi. Mimi nadhani kama unataka kazi za nje fanya lakini siyo kwa kumkandia mkeo/girl friend wako vinginevyo muache umuoe huyo unayeona anakuvutia kwa kipindi hicho.Habari zenu wapendwa wote wa jukwaa letu pendwa la MMU.
......Nimekuwa nikisikia nikikutana na watu mbalimbali wakisema " Ningekuwa sijaoa ningekuoa wewe"
AU "Ningekuwa sijaolewa ningeolewa na wewe" Nimejaribu kuzitafakari hizi kauli nimekosa majibu hebu waungwana na wataalamu hebu nisaidieni?
Unaoa au kuolewa kwa lazima mpaka ufikie kusema maneno kama hayo???
Au nitamaa tu ndo zinasumbua? Ama ni nini hasa?? Hebu nisaidieni
Nawatakia maandalizi mema ya weekend.
DA
Edson kwani ulilazimishwa jamani
Edson kwani ulilazimishwa jamani
Yani DA wananikera sn hawa viumbe wa aina hii maneno mengi kumbe tamaa tu hana lolote tena wengine utakuta wanawekwa mjin na wake zao,nishasema OLE WAKE,kwanza hii ni kushushiana hadhi tu kwan mie sistahili kuwa na wangu mpaka watake kunifanya nyumba ndogo!EboHa ha ha ha Cantalisia wewe mkali aisee atajuta kukufahamu tunatakiwa kuwa kama wewe ndo watu watapunguza huu usaniii
hizo ni lugha tu za kimihemko dada
watu wakiwa kwenye mihemko akili na mdomo havifanyi kazi kwa ushirikiano
Ila mkwara uliopiga haki ya nani hakuna mume wa mtu JF atayetia pua kwako! Lakini nina ka swali ka uchokozi, rejea bold yangu ina maana mtu akiwa ameoa akija na gia tofauti na hiyo labda akawa mkweli katika mambo yake yote ila tu imetokea amekupenda siyo kwa kukuoa wala nini vipi anaweza kuchukua ikulu?Uko sahihi kbs mamito,mie huwa nawaulizaga ulilazimishiwa ndoa?yani ni unafiki usiokuwa na kipimo na kutuona hatujawashtukia jaman nasema kbs ole wake mtu ameoa alafu anijie na hii gia atajuta kunifahamu!
Hii ndio sababu kubwa watu wengi wanapenda kutoa/kutamka hiyo kauli, naona hata AshaDii kailezea mwishoni kabisa:
Yani haijalishi amekuja na gia gani,ile kujua tu ni mume wa mtu naomba asithubutu kbs kwan hakubaliki kwangu,hiyo ni ishara tosha ya unafiki,km ameweza kuwa mnafiki kwa mkewe aliempenda na kumuoa itakuwaje kwangu mm anayetaka kunidhalilisha kwa kutaka niwe nyumba ndogo yake?Ila mkwara uliopiga haki ya nani hakuna mume wa mtu JF atayetia pua kwako! Lakini nina ka swali ka uchokozi, rejea bold yangu ina maana mtu akiwa ameoa akija na gia tofauti na hiyo labda akawa mkweli katika mambo yake yote ila tu imetokea amekupenda siyo kwa kukuoa wala nini vipi anaweza kuchukua ikulu?