Eti, mifuko ya plastiki marufuku!

Eti, mifuko ya plastiki marufuku!

nakumbuka nilishaishi nyumba moja na muinjilist jamaa alikua chenga sana siku moja usiku upepo umeleta ule mfuki mweusi basi nimeenda kukojoa nje nikauokota nikaweka kwenye dust bin .....
badae ngoma 8 hivi paka wakafurumusha dude la uchafu mifuko kadhaa ikawa nje upepo ukipiga mfuko ukawa unazunguka kwenye mlango wa jamaa asee ilipigwa maombi hapo ndani sio mchezo
akipiga maombi kuna muda upepo unatulia anasifu asante yesu umemshinda shetani😂😂😂😂😂😂
akikaa kidogo upepo unaanza tena aloo maombi yanaanza upya nilicheka sana usiku huo.

asubuhi jamaa anawaelezea majirani eti katumiwa jini kalipiga na moto wa yesu hapo ndipo alinivunja mbavu maana angejua ni mfuko sijui angejisikiaje na mimi nikapiga kimya sikutia neno😂😂😂
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Utakuwa huelewi! Kuna thickness iliyoruhusiwa!
Lakini hata hii ya sasa haiozi Mana si naona kwenye maeneo mengi ipo tu.sasa hiyo thickness unayosema inasaidia nini ikiwa kutooza na kuchafuwa mazingira kupo pale pale?
 
Hakuna cha kuzuiwa ila ni mabadiliko ya aina ya mifuko. Nenda sokoni kanunuwe mboga, mihogo utapewa mfuko wa plastiki, chumvi zipo kwenye mifuko ya plastiki mi nadhani yalikuwa maamuzi ya kukurupuka tu.
Hivyo wanatukia kwa kisingizio cha vifungashio, ni muda dasa vifungashio vya plastiki nje ya viwanda rasmi vipigwe marufuku
 
Back
Top Bottom