Niliinuka mzimamzima wakati huo nikiangalia mlangoni huko kwa ndani mlevi yule mkorofi niliemtia ngumi alitaka kunifata kwa fujo huku wengine wakijaribu kumzuia wakimvuta kwa nyuma na kumsihi arudi baada ya dakika mbili alirudi na kuendeleza kasheshe zake!.
Niliirudia saa yangu na kukuta mishale ikisoma saa tatu na robo za usiku,akili yangu ikanena nitafute kiwanja chengine! Lakini likanijia swali kwanini nisichukue vilevi na kwenda kunywea gheto..? Nikaona hili wazo lapili ndo linalofaa zaidi.. katika kujivuta nikaona nishike njia ya kwenda gheto nitanunulia huko mbele yasafari!.. kibaridi chepesi bado kiliendelea kupiga ktk namna isiyokera bali kuhamasisha zaidi.
Katika njia hii ya rami nilipita pembezoni kabisa mwa barabara huku yakikatiza magari machache na pikipiki kadhaa,lakini baada ya tembea yangu ya kama dakika kadhaa nyuma yangu ilikuja gari iliyokuwa ikinikaribia!.. nilishitushwa kidogo baada ya kuona gari ile ikinikaribia na kunipiga mwanga wake,ilipofika mkabala na mimi ilipunguza mwendo nami nikaipa attention nikasogea karibu na kuchungulia ndani yake!.. nilipokelewa na sauti tamu yakike ikinena "Mambo" sikujibu haraka bali nilibaki nikitafakari kitu ambacho hata hakikuwa na maana!! Dada wa watu akanena tena "Mambo kaka" Mara hii nikagutuka na kujibu poa huku nikijilaumu mawazoni kwa kushindwa kujibu salamu yake yakwanza!.. alikuwa ni mwanadada mwenye jingi tabasam na sura fulani yenye kunena umboga Saba!. Punde Tena sauti yake ikakita masikioni pangu ikinitaka niingie garini Kama sitajari anisaidie kunifikisha mahali niendapo!. Sikutaka kukubali haraka nionekane kama boya fulani!,nikaligeuza shingo langu ili nitizame siti za nyuma nione Kama kuna viumbe wengine lakini hakukuwapo kiumbe zaidi yake tu!.
Sikujibu chochote bali nilifungua mlango na kutumbukiza roho yangu katika gari lile aina ya Benz nyeusi.. mrembo alikanyagamoto na gari ikaendelea kukanyaga rami.. kilipita kitambo kidogo tukiwa kimya ndipo mrembo yule akaamua avunje ukimya!.
Nilikuwepo mule!
Nikauliza wapi..?
Kule ulipoitwa ndama!
Kabla sijanena chochote akaendelea "Mule hawatumii bia bali wanakunywa wine!"
Nilikubali kwa kusemo "ohoo mi sikujua!" Likafata swali jengine
"Kwani we ni mgeni huku..?" Nikajibu hapana isipokuwa sio mwenyeji eneo lile ni mara ya kwanza kuwepo pale!..
Wakati nikimjibu hayo alikuwa akinitazama huku akiliangua tabasam hafifu,macho yake yakiwa hayajatulia yakitazama mbele huku akinigeukia tena mimi!. Kilipita tena kimya Kisha akaniuliza " unaitwa nani..?" Kabla sijajibu nilitafakari nikinaribu kufikiri nimpe jina bandia au halisi!. Lakini nilitupilia mbali ubandia nikaona nimpe kile kilicho halisi!.. "naitwa Jonas"
Tabasam lake likachanua zaidi! Huku akitupia kiingereza "such a good name!" Bila hiana nikaachia kiingereza changu chakilevi " thanks".
Mara hii ndio ulikuwa muda wangu wa kuanza kumfaidi mrembo huyu kwa macho yangu yakilevi!. Nilitupia jicho katika viunga vya mwili wake aliouvisha kigauni chepesi chekundu kilichoishia magotini ila kilivyo na purukushani za kikorofi kilijivuta kidogo mpaka juu ya mapaja yake hivyo kufanya mtazamaji kukata kiu cha macho!.
uzuri wa mapaja yake tu ulitosha kuanza kunitia dosari za tamaa nilizozikata kwa kuanza kumuangalia usoni ambako sura yake nzuri ilijihamasisha kuangalia mbele tu!,niliyafanya haya kwa kuibia nisijeonekana fisi mfilisi!.
chengine kilichonivutia zaidi ni ule weupe wake ambao haukuwa wa kununua madukani!,hata lips zangu hazikupakwa marangi ya husuda kama ukuta wa jiji!.
kimya kidogo nikaona usiwe tabu nikatupia swali nami kutaka kulijua jina lake "mrembo unaitwa nani..?" Alitabasam nakujibu "naitwa hivyohivyo mrembo!" Alijibu hivyo huku akisindikiza na kicheko chepesi!.
nikaongeza "ohoo ni haki yako hata hivyo kuitwa hivyo!" Akaguna na kuuliza tena "kwanini.?"
Nikajibu "kwasababu hata ile nywele yako moja tu inatosha kuhubiri kuwa wewe ni mzuri!!"
alicheka huku akiunyonga usukuni kuelekea upande wakulia ambapo alikata kona iliyonifanya niwe natuswali hafifu juu ya mabadiliko hayo! Alilitambua hilo hapohapo akanena "sorry napita hapo supermarket Kuna vitu vichache nachukua!" Nilikubali kwa kutikisa kichwa..
Narudi..