Ndara Mbovu
Senior Member
- Feb 28, 2017
- 155
- 83
Habarini za siku wana JF
Nilikuwa na mchumba wangu kwa miaka 3, Tuliachana kwa kuwa nilimpa hela ya mkopo akafanyie biashara yeye akachukua hela kwenda kufanyia matumizi yake binafsi kama kukarabati nyumba ya baba yake na nyingine akafanyia biashara, kwa kifupi alinidhurumu pesa yangu.
Alidai ameniacha na amenidhurumu hizo pesa kwa kuwa nina mtoto naye, hivyo pesa itamsaidia kumjengea maisha mtoto. Sababu ya kufanya hivyo ni kwa kuwa nilimsaliti.
Baadaye mtoto wetu alifariki, nikamwambia turudiane mana nilijihisi hasara sana mana pesa ile nilifikiri itamsaidia na mwanangu na sikuona maumivu kudhurumiwa, sasa mwanangu amefariki.
Nikaona basi turudiane nimpe ujauzito mwingine, nilitaka tuishi pamoja, akakataa na kusema anataka kwenda kusoma. Mi sikuona haja ya kuendelea naye. Nikaanzisha mahusiano na mwanamke mwingine ambaye alikuwa mpenzi wangu wa zamani ambaye tulipendana sana.
Ex wangu aliposikia nataka kuoa alikuja kwangu na kuniambia sasa hatoenda shule atabaki tuishi pamoja kama kusoma atasoma open university, nampenda sana huyu binti, nilimjibu haiwezekani kurudiana, alilia sana na kujuta sana.
Sasa nimeoa mwanamke ambaye nampenda naye ananipenda na wala sitaki kumkosa, yule ex wangu bado ananililia anadai ananipenda sana anataka awe hawala yangu na nizae naye.
Naogopa mke wangu akija kujua na pia naona hasara ex wangu anamiliki vitu vingi vya kwangu na biashara, karibuni kuchangia wadau.
Nilikuwa na mchumba wangu kwa miaka 3, Tuliachana kwa kuwa nilimpa hela ya mkopo akafanyie biashara yeye akachukua hela kwenda kufanyia matumizi yake binafsi kama kukarabati nyumba ya baba yake na nyingine akafanyia biashara, kwa kifupi alinidhurumu pesa yangu.
Alidai ameniacha na amenidhurumu hizo pesa kwa kuwa nina mtoto naye, hivyo pesa itamsaidia kumjengea maisha mtoto. Sababu ya kufanya hivyo ni kwa kuwa nilimsaliti.
Baadaye mtoto wetu alifariki, nikamwambia turudiane mana nilijihisi hasara sana mana pesa ile nilifikiri itamsaidia na mwanangu na sikuona maumivu kudhurumiwa, sasa mwanangu amefariki.
Nikaona basi turudiane nimpe ujauzito mwingine, nilitaka tuishi pamoja, akakataa na kusema anataka kwenda kusoma. Mi sikuona haja ya kuendelea naye. Nikaanzisha mahusiano na mwanamke mwingine ambaye alikuwa mpenzi wangu wa zamani ambaye tulipendana sana.
Ex wangu aliposikia nataka kuoa alikuja kwangu na kuniambia sasa hatoenda shule atabaki tuishi pamoja kama kusoma atasoma open university, nampenda sana huyu binti, nilimjibu haiwezekani kurudiana, alilia sana na kujuta sana.
Sasa nimeoa mwanamke ambaye nampenda naye ananipenda na wala sitaki kumkosa, yule ex wangu bado ananililia anadai ananipenda sana anataka awe hawala yangu na nizae naye.
Naogopa mke wangu akija kujua na pia naona hasara ex wangu anamiliki vitu vingi vya kwangu na biashara, karibuni kuchangia wadau.