Ex - CAG Uttoh: Mashirika na Makampuni mengi yalikuwa yanatoa 'Gawio' Serikalini Kimakosa, Kinafiki, Kiuwoga na kwa Kujipendekeza

Ex - CAG Uttoh: Mashirika na Makampuni mengi yalikuwa yanatoa 'Gawio' Serikalini Kimakosa, Kinafiki, Kiuwoga na kwa Kujipendekeza

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
" Siyo sahihi kwamba kila Shirika au Kampuni Kisheria linatakiwa kutoa Gawio kwa Serikali. Ni bahati mbaya mno Watu hatupendi Kusoma Sheria na Taratibu mbalimbali na tukitishwa tu tunalegea na kutoa. Mashirika na Makampuni mengi yalikuwa yakitoa Gawio kwa Makosa, Kinafiki, Kiuwoga na kwa Kujipendekeza zaidi hivyo nategemea kwa miaka hii Watu watajifunza na Kubadilika "

Chanzo: ITV Kipima Joto

Watanzania kwa sasa Wanafunguka tu!!!
 
Kwanini Uttoh hakusema hayo maneno miaka yote hiyo Magufuli akiwa anapokea 'gawio' ?
Jibu ni moja tu, Uttoh alikuwa anaogopa kusema. Hivyo asishangae wala asilaumu wakuu wa mashirika yaliyotoa 'gawio' kwa Magufuli. Kwanini? Uttoh huyu huyu na wale watoa 'gawio' wote walikuwa kwenye kikapu kimoja kinaitwa woga.
 
Kwanini Uttoh hakusema hayo maneno miaka yote hiyo Magufuli akiwa anapokea 'gawio' ?
Jibu ni moja tu, Uttoh alikuwa anaogopa kusema. Hivyo asishangae wala asilaumu wakuu wa mashirika yaliyotoa 'gawio' kwa Magufuli. Kwanini? Uttoh huyu huyu na wale watoa 'gawio' wote walikuwa kwenye kikapu kimoja kinaitwa woga.
hakukua na uhuru wa kuongea !

wewe unadhani LUDOVIC OTTOUH hana familia iliyokua inamtegemea ?

jamani familia kwanza
 
" Siyo sahihi kwamba kila Shirika au Kampuni Kisheria linatakiwa kutoa Gawio kwa Serikali. Ni bahati mbaya mno Watu hatupendi Kusoma Sheria na Taratibu mbalimbali na tukitishwa tu tunalegea na kutoa. Mashirika na Makampuni mengi yalikuwa yakitoa Gawio kwa Makosa, Kinafiki, Kiuwoga na kwa Kujipendekeza zaidi hivyo nategemea kwa miaka hii Watu watajifunza na Kubadilika "

Chanzo: ITV Kipima Joto

Watanzania kwa sasa Wanafunguka tu!!!
Nchi Ilikuwa inaongozwa na mtu mshamba na limbukeni
 
Mwendazake's mixed legacy

Ex - CAG Uttoh anaongea 'Kidiplomasia' ila kuna Mwenzake Mmoja hapo Yeye 'anaua' kabisa na nadhani aliyelala Milele angekuwepo nasi asingemuacha na angemlipizia tu 'Kisasi' kama alivyozoeleka na wanaomjua.
 
hakukua na uhuru wa kuongea !

wewe unadhani LUDOVIC OTTOUH hana familia iliyokua inamtegemea ?

jamani familia kwanza
Vipi kuhusu wale wakuu wa mashirika ya umma yakiyotoa 'gawio'?
Wao walikuwa wana uhuru wa kuongea?
Wao hawakuwa na familia?

Kaa tafakari kwa kina na utagundua kitu kimoja kinachowaweka akina Uttoh na hao wakurugenzi. Wote wanafanana. Woga, woga, woga, woga.
 
Kwanini Uttoh hakusema hayo maneno miaka yote hiyo Magufuli akiwa anapokea 'gawio' ?
Jibu ni moja tu, Uttoh alikuwa anaogopa kusema. Hivyo asishangae wala asilaumu wakuu wa mashirika yaliyotoa 'gawio' kwa Magufuli. Kwanini? Uttoh huyu huyu na wale watoa 'gawio' wote walikuwa kwenye kikapu kimoja kinaitwa woga.
Hapo cha-cha. Watu wanajitojeza kwenye mashimo.
 
Halafu ghafla wanaibuka mataga fulani wameshiba magimbi yaliyochacha anakwamba Uttoh ametumwa kuja kumchafua Magufuli.
Kitendo alichomfanyia Ben Saa Nane, Azory na wengine kilifanya kila MTU amuogope ukitaka kufungua domo lako ni kusifia Tu vinginevyo Baki na mafi yako.
 
Kwa sasa kila mmoja ataongea lake na kujifanya anaijua sheria
Wakati huo waliogopa na kukaa kimya kama sheria hizi zimetungwa leo

Nafikiri ifike mahali anetaka kumsema Magufuli kwa namna moja au nyingine aanze na kusema tulikuwa tunamuogopa
Hapo italeta maana zaidi
 
" Siyo sahihi kwamba kila Shirika au Kampuni Kisheria linatakiwa kutoa Gawio kwa Serikali. Ni bahati mbaya mno Watu hatupendi Kusoma Sheria na Taratibu mbalimbali na tukitishwa tu tunalegea na kutoa. Mashirika na Makampuni mengi yalikuwa yakitoa Gawio kwa Makosa, Kinafiki, Kiuwoga na kwa Kujipendekeza zaidi hivyo nategemea kwa miaka hii Watu watajifunza na Kubadilika "

Chanzo: ITV Kipima Joto

Watanzania kwa sasa Wanafunguka tu!!!
Watasema na huyu ametumwa na mafusadi🤷🤷
 
Ex - CAG Uttoh anaongea 'Kidiplomasia' ila kuna Mwenzake Mmoja hapo Yeye 'anaua' kabisa na nadhani aliyelala Milele angekuwepo nasi asingemuacha na angemlipizia tu 'Kisasi' kama alivyozoeleka na wanaomjua.
Lazima angemlamba risasi Ile damu ya kirundi ishazoea kuua. So unaona walimteka watu wakawahi kupiga kelele ndio akaachiwa. Alikuwa apotezwe.
 
Back
Top Bottom