Ex-CIA Chief Panetta: IDF hutekeleza majukumu yao kama Wenda wazimu

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
1. Hili si jambo dogo kwani hata Police Tanzania (PT) ya Muliro, achilia mbali wale wengine wa kwetu au hata HAMAS hawawezi kuwa hivi:



2. Kwamba hivi hawakuanza juzi, ila ndiyo hulka yao,



3. Sasa kumbe kipi kingekuwa tofauti hapa?

Your browser is not able to play this audio.


4. Kwamba kwa hakika ndiyo hivyo msemaji wa IDF anavyo thibitisha:

Your browser is not able to play this audio.


5. Kwamba haikupaswa kuwa hivi? Haikupaswa kutokea?

6. Wakati imetokea kwa wafanyakazi zaidi ya 200 wa kutoa misaada; mamia kwa wahudumu mahospitalini; maelfu ya wagonjwa mahospitalini; makumi maelfu ya watoto wadogo; nk wakiwamo kumi maelfu ya wanawake na wanaume wasio na hatia?

7. Anamalizia Leon Panetta;

 


TUMEANZA KUWA QUOTE HADI CIA? KWELI HALI IMETUBANA SANA....
 
Kweli Israel ni makatili, ila wangekuwa nyoro nyoro waarab wangewasumbua sana...Israel pasingekalika kwa vitimbwi vya kila siku!.

1. Kwamba kwao kila kinachotembea ni HAMAS?

2. Mbona kihoro kitawamaliza?
 
TUMEANZA KUWA QUOTE HADI CIA? KWELI HALI IMETUBANA SANA....

Tofautisha wao kuwanukuu walichosema na kuwashabikia au kuwasifia; bila kusahau:

1. Sisi tusiokuwa sehemu kwenye haya:

Makundi saba ya chawa kindaki ndaki yanayotatiza mabadiliko

humkwoti, mama, mwamba, CCM, Chadema, Mtume, Yesu, Papa, Mossad nk; kwa lolote lenye tija, kwa raha zetu tukiwa vifua mbele!

2. Muyaweze vipi ninyi hayo chawa kindaki ndaki?

3. Hapo #2, wayaweze vipi MK254, @lucas_mwashambwa, Moisemusajiografii au wale wengine?

Kwamba ni machizi yenye kudhani yana maarifa? Hiyo mbona ni tusi? Siyo sifa!
 
Kwa hiyo Israeli wawe wanapiga polepole?🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣

1. Umekurupuka big time ndugu chawa:

Your browser is not able to play this audio.


2. Haya si maneno yàngu ndugu; bali ya nduguzo tena wale wa damu!
 
Adui gaidi atapigwa aina zote za vipigo yeye na washirika wake.Una haki ya kulia utakavyo ila huna haki ya kujichagulia vipigo.

1. Ipo tofauti baina ya mpigania uhuru na gaidi.

2. Gaidi ni gaidi tu bila kujali ni mtu au nchi.

3. Mandela, Gaddafi, ANC, SWAPO, nk Kuna waliowaita magaidi.

Your browser is not able to display this video.


4. Waungwana hatuwachukii Israel Bali kwa ugaidi wao.

5. Waungwana hatuna tatizo na wapalestina au HAMAS kwani hao wanapigania uhuru wao:

 
Bila hivyo wangekuwa wameshafutwa kitambo sana.
Hiyo “Wendawazimu” ameitumia kama sifa
 
Bila hivyo wangekuwa wameshafutwa kitambo sana.

Hiyo “Wendawazimu” ameitumia kama sifa

1. Kama hizi ni sifa:



2. Sina hakika kama Waisrael wenyewe au Natenyahu watakubaliana nawe.

3. Labda tu, kwenu nyie waisrael wa pale Buza.
 
Dunia inampendelea mwenye uwezo. Wayahudi hawakurupuka na kuamka siku moja na kuanzisha taifa la Israel. Wapalestina wanajitesa bure kubaki hapo maana hawana maarifa na akili ya kujitetea dhidi ya mashambulizi. Kama wanakazana na Madrasa badala ya shule unategemea nini. Marekani ameweka kambi karibia nchi zote za kiarabu zinazowazunguka .Mataifa makubwa yanaendeshwa na wayahudi. Kuambiwa kwamba mataifa makubwa ni rafiki wa Israel ni uwongo. Ukweli ni kuwa mataifa makubwa (U.S.A na E.U) viongozi wao wakubwa na wafanyabiashara wakubwa ni wayahudi. Wapalestina waondoke wakubali matokeo wajipange kushika nyadhifa katika nyanja mbali mbali za dunia. Halafu ndio waje wajitetee.
 

1. Kwamba unapendekeza wapalestina waondoke tu pale?

2. Kwa hIyo hata sisi kumbe tulipaswa kuwapisha tu wakoloni wajerumani na hatimaye waingereza kwa kuwa tusingewaweza?

3. Labda unachosema kina apply kwa nchi zingine zote zilizokuwa makoloni kama Kenya, Uganda, Rwanda Hadi Afrika kusini kwa kina madiba huko?



4. Hapo #3, hujishangai kudai pasipokuwa na uhalali kuwa wapalestina wanadai nchi yao kupitia madrasa?

5. Bila kusahau kuwa katika dunia haupo udhwalimu uliodumu milele!
 
Iran anaendelea kuwajambisha wayahudi hawaelewi anakuja saa ngapi kuwatembelea. Naomba UN iingilie kati hii si Haki

1. Psychological warfare - ni hatari zaidi kuliko vita yenyewe waliyoizowea.

2. Akiendelea nao hivyo, hadi wa kule Buza kina MK254 watakuwa wanavikimbia hata vivuli vyao wenyewe milele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…