* Exclusive Scoop *

* Exclusive Scoop *

Kadri mambo yanavyokwenda,nadhani JK na EL watageuka kuwa maadui kama paka na panya.Wahenga walisema USHIRIKA WA WACHAWI HAUDUMU

Na hilo ndilo hasa!

Lakini la kufurahisha ni kwamba hao mafisadi waliobaki humo serikalini sasa watakuwa wanajiuliza mara mbilimbili kabla ya kufanya uhujumu wao. Mosi, kwa kuwaogopa mafisadi waliotupwa nje, kwani wanazijua njia zao zote; pili, hao walio ndani kwa miaka hii mitatu iliyosalia kabla ya uchaguzi hakuna atakayethubutu kuwaibia mali wananchi, unless kama yeye ni 'professional' thief. Sana sana watabaki kubembelezea vinafasi vyao ili wapite tena hapo 2010, na ulaji wa nguvu uanze upya.
 
Mkuu Mlalahoi,

Muungwana na el, walishaachana njia panda siku nyingi sana, isipokuwa tu el alikuwa mjanja sana na ku-delay the process, na ni kutokana na mikakati ya underground ya el kujitayarisha na 2010, muungwana alikuwa amesubiri mkuu ajivishe kitanzi mwenyewe, el aliamini kuwa six atazima ngoma kwa kuzima ripoti, kutokana na ile jamba jamba aliyomtia kwenye kesi ya Malima, and six almost did, lakini hakujua kuwa Mwakyembe, alikuwa amepewa green light na muungwana, maana at one point hata Mwakyembe mwenyewe hakuwa na uhakika kuwa ripoti itakubalika, mpaka alipokwenda kumuona muungwana uso kwa uso na ripoti na kupewa go ahead, six alipotaka ku-punch na gear ya kusafiri, muungwana, alimpigia simu kumuuuliza unakwenda wapi? forget hiyo safari tulia hapo ninakuja, muungwana hakuenda Muhimbili kwa Kubenea bila sababu, na Mwakyembe hakuiweka kwenye ripoti bila sababu, and the rest of the story,

lakini walikuwa wameshaachana njia panda siku nyingi, na sio kwa bahati mbaya muungwana amempa mtu wa idara u-PM, kuna sababu nayo ni el!
 
Kadri mambo yanavyokwenda,nadhani JK na EL watageuka kuwa maadui kama paka na panya.Wahenga walisema USHIRIKA WA WACHAWI HAUDUMU
Kabisa kabisa sijawahi kusikia umedumu, wataanza kutafyutana kwa waganga zaidi yao

hapo ndo vita inakuwa imenoga!

mmoja tayari Ikulu ndo keshaikosa 2015 (au ilikuwa 2010?)
 
What it matters kwangu ni kuona kwamba kumekuwa na mabadiliko na angalau dhana ya uwajibikaji/uwajibishwaji inaonekana sasa.
Ile kauli kuwa kujiuzuru siyo desturi yetu imeanza kubadilika.

Wabunge wameanza kuwa active, na wananchi wengi wameanza kujishirikisha/kufatilia utendaji wa serikali.
Kama wametoana kafara, hyo ni juu yao!
 
Ni kitu ambacho kinanishangaza sana kusikia kuwa watu wanaona kama ni uchuro kwa watu wa opposition kuwa ndani ya baraza la mawaziri, sijui ni katiba gani au sheria gani ya CCM inayokataza mtu kutoka opposition kupewa nafasi ya uwaziri. Kama kuna mtu kutoka nje CCM anayeweza kuhsiriki kutekeleza ilani ya CCM au kipengele kinachofanana na ilani ya chama chake inayohusu maslahi ya taifa kuna tatizo gani?
Naona CCM mentality ina kitu kibaya cha sisi huku, wao kule. Kama kweli JK ataingiza mtu japo hata mmoja kutoka opposition itakuwa vizuri sana. La muhimu ni maslahi ya taifa na sio ya CCM.
Mwanakijiji kama unanipata naomba nijulishe COHEN aliyekuwa waziri wa Ulinzi wakati wa serikali ya BILL CLINTON alikuwa chama gani!! Kama alikuwa Republican labda mtu anaweza kusema DEMS waliishiwa watu wa kuwa minister of defence!!!
 
Ni kitu ambacho kinanishangaza sana kusikia kuwa watu wanaona kama ni uchuro kwa watu wa opposition kuwa ndani ya baraza la mawaziri, sijui ni katiba gani au sheria gani ya CCM inayokataza mtu kutoka opposition kupewa nafasi ya uwaziri. Kama kuna mtu kutoka nje CCM anayeweza kuhsiriki kutekeleza ilani ya CCM au kipengele kinachofanana na ilani ya chama chake inayohusu maslahi ya taifa kuna tatizo gani?
Naona CCM mentality ina kitu kibaya cha sisi huku, wao kule. Kama kweli JK ataingiza mtu japo hata mmoja kutoka opposition itakuwa vizuri sana. La muhimu ni maslahi ya taifa na sio ya CCM.
Mwanakijiji kama unanipata naomba nijulishe COHEN aliyekuwa waziri wa Ulinzi wakati wa serikali ya BILL CLINTON alikuwa chama gani!! Kama alikuwa Republican labda mtu anaweza kusema DEMS waliishiwa watu wa kuwa minister of defence!!!

Bongo,

Wanaosita ni CHADEMA na si vijembe kutoka CCM.

JK inaelekea anataka kujenga Serikali yenye mtazamo wa Utaifa, ameshagundua kuwa katika CCM, kuna uozo mkubwa na itakuwa vigumu kujenga maslahi ya Taifa kama atakuwa na serikali ya Chama kimoja.

Pamoja na kuwa Serikali inafuata Ilani ya CCM ya uchaguzi, itakuwa jambo la BUSARA kama Upinzani wote ukikubali mwaliko huu na kuanza shirikiana na CCM kwa manufaa ya Taifa.

Tusisahau kuwa kama Ushirikiano utaonekana kwenye Serikali ya Muungano, hivyo basi CCM Zanzibar na serikali yake SMZ itabidi zijirudi na kuwaita CUF mezani kujenga Taifa na si kutengana!
 
hainogi FD... uzuri wa siasa ni speculation...

kwa mfano, kwanini hawakutangaza baraza jana kama ilivyoahidiwa?

Jibu langu la kukisia ni kuwa Rais alikuwa ametoa nafasi ya Uwaziri kwa watu wawili ambao siyo wabunge bado na hawakuwa DDM na watu hao hatimaye wamefika leo na watatangazwa hapo kesho, kuapishwa mchana kama wabunge na kesho yake kama Mawaziri...
 
Mwanakijiji,

Nimekubali naona IMEKATIKA!

Hongera kwa utabiri
 
EL aliamini kuwa six atazima ngoma kwa kuzima ripoti, kutokana na ile jamba jamba aliyomtia kwenye kesi ya Malima, and six almost did, lakini hakujua kuwa Mwakyembe, alikuwa amepewa green light na muungwana, maana at one point hata Mwakyembe mwenyewe hakuwa na uhakika kuwa ripoti itakubalika, mpaka alipokwenda kumuona muungwana uso kwa uso na ripoti na kupewa go ahead, six alipotaka ku-punch na gear ya kusafiri, muungwana, alimpigia simu kumuuuliza unakwenda wapi? forget hiyo safari tulia hapo ninakuja, muungwana hakuenda Muhimbili kwa Kubenea bila sababu, na Mwakyembe hakuiweka kwenye ripoti bila sababu, and the rest of the story,
lakini walikuwa wameshaachana njia panda siku nyingi, na sio kwa bahati mbaya muungwana amempa mtu wa idara u-PM, kuna sababu nayo ni el!

Mkuu this is good observation. NIlikuwa najiuliza sana kuwa JK toka ameingia amekuwa kama mbumbumbu, lakini kumbe yeye aliona mengi na aliona mbali zaidi kuliko baadhi yetu tulivyodhani. Naona hapa itakuwa ndio mwisho wa maisha ya kisiasa ya EL, nadhani hatafurukuta tena hasa ukizingatia sasa idara imekamata U-PM, EL hatakuwa na connections na influence tena kwenye ofisi hiyo, nadhani vumbi bado litakuwa linatimka, ningependa sana kujua this time EL anapanga kecheza karata gani!
 
EL haendi popote. Itabidi wamtenge kiakili sana kama Mrema. Lakini kwa jinsi mizizi ilivyoingiliana, EL haendi popote. FMES we mtu wa CCM, mtu wa 'nyeti', unajua kabisa EL hatupwi wala hashughulikiwi. CCM are crooks at a higher level.

Kuhusu kuweka opposition kwenye baraza la mawaziri, wazo zuri in theory. Je, hawa opposition wakipewa hizo kazi, na wakawa under-mined kufanya kazi zao (hata kama wana nia nzuri na wachapa kazi), yaani hamuoni kwamba CCM/JK watakuwa wanatumia akili sana kuua opposition? C'mon, kwa siasa za bongo, utakuwa unajiweka kitanzini wewe mwenyewe. Ila navyoona vyama vya opposition vilivyo na uchu, mtu anaweza sema duuh, uwaziri? Ngoja nirukie, maana naweza nisiuone maishani kwangu lol!! Njia tamu sana kuua opposition, maana watagombana wenyewe.
 
Mimi kwa maoni yangu ninadhani iwapo muungwana ataunda baraza la mawaziri na kuwaingiza watu wa upinzani itakuwa ni hatua moja nzuri katika kukomaza demokrasia na utawala bora, itaweka precedent kwa tawala zijazo kwamba iwapo kunatokea mushkeli na nchi kuyumba tufanye nini. lakini pia inaweza kuwa advantage kwa ccm na upinzani kutegemea ni waziri gani anachapa kazi vizuri.

ni advantage kwa ccm kwa sababu wananchi wataona kwamba ni chama chenye kuweka mlengo wa utaifa mbele badala ya kukumbatia mfumo wa kizamani wa chama mbele,taifa nyuma.

na ni advantage kwa upinzani pia kwa maana kwamba hawa mawaziri wa kutoka upinzani wakichapa kazi vizuri,wananchi watawaona na wataweza kuwashawashi kwamba kazi tunaiweza ,hivyo kuwa katika nafasi ya kuweza kuchaguliwa(one day yes)
 
Mkuu Mwanakijiji,

huu Usiri umeanzia wapi JF,Nahisi watu kununuliwa na wamekuwa waoga baada ya kusikia CIA wanapitia Pages za Jambo Forums kwa umakini Mkubwa.watu wanaingia n akutoka na wamekuwa wajanja sana.

hao watu wawili walioitwa dodoma ni kina nani?Je ndio hawa ambao JF iliwapendekeza?
 
kuhusu wapinzani kuwekwa katika Barza jipya la Mawaziri,Basi utabiri utakuwa umetimia,JK to be one term president.Kwanza itakuwa aibu kwa chama.ina maana chama kimekosa watu mpya achague watu wa upinzani??kama kashauriwa hivyo atakuwa anajimaliza mwenyewe katika CCM.

Upande wa Wapinzani kukubali kuingia madarakani ni kukubali kutekeleza seara ya chama cha Mapinduzi ambayo inapingana na sera zao,na ninavyofahamu kiapo cha pili anachoaapa waziri au Naibu waziri kinamfunga kufanya mambo kwa matakwa yake binafsi.(kumbuka Mrema).hapo hapo hata serikali ikishindwa kutekeleza Matakwa yao ina maana na wapinzani watakuwa wameungana nao katika hilo.

Huu utakuwa Mtaji Mkubwa wa kisisasa kwa wanasiasa kama Mtikila na Vyama Vyao ambao hawatakuwamo katika baraza la Mawaziri,Mtaungana nao katika uchafu wote wa EPA,Suala la Madini na mambo yote machafu ambayo CCM ya wafanyabiashara wanayasimamia. sababu mtakuwa ndani ya kiapo!labda mje mseme nje ya kiapo kwamba mlitolewa 'Bangusilo'.

Kimsingi kama Jk akiwap wapinzani na wakakubali,Basi sitakipa chama cha Upinzani Kura yangu,au ndio mambo ya kina Mzee Mwanakijiji,Kama ukiona mtu anakushinda unaungana naye?au ndio walichukuwa wanakitaka(rejea Hotuba ya Waziri Mkuu wakati akitangaza adhma yake kujizuru).

Kama Zitto,Mdee na Hamad Rashid Mko Tayari,Kila la kheri. Na huu ndio utakuwa Mwisho wenu kisiasa.Ndio mtakuwa mnawapa Ushindi CCM,

Naamini JF huru ndio itakuwa Chama Cha Upinzani.tusikate Tamaa Bali tuweke Msimamo thabiti sababu Subira huvuta Heri
 
Kama Zitto,Mdee na Hamad Rashid Mko Tayari,Kila la kheri. Na huu ndio utakuwa Mwisho wenu kisiasa.Ndio mtakuwa mnawapa Ushindi CCM

i like dat......hawa awapo hata mmoja tunajisumbua.....sikiliza moto wa sanane mtaamini hii ni jf for info kuna baraza liko na viumbe 42..nani stay in tune...chamwino akukaliki,,,nduguzanguni tunatamani tulete zindiko la JF kudodosa..muungwana safari hii amkuwa muungwana kweli....nampongeza kwa watakaochaguliwa natumaini dhumuni la kuchaguliwa wameshaelezwa na muungwana,,,haya LOWASA ANGALIA mafisadi wenzake wamepona????
 
Wazee mi niliamini kuanzia mwanzo report ya Mwakyembe itazua mambo mengi ambayo hatujui (it was too professionally compiled to be left without protest from the victims..Hawakutegemea kwamba kuna daring Tanzanians!!!). Politics is a game and who scores takes the cup! EL played well ila aliondoka kama Cameroon. Politically Lowassa is now wounded badly. Influence yake ilikuwepo wakati bado ana-call shots kwenye system. Guys make no mistake, when you are out..you are out! Kama unabisha muulize Sumaye..the man was too powerful to ever think his life outside politics..where is he? Take it from me! all subordinates walikuwa wanamuogopa kwa sababu ya cheo. Currently Lowassa is not and will never be a threat to JK!

Kuhusu wanao retrieve statements the Kazaura`s and co., They are dead wrong! perhaps wangeomba msaada wa sheria. Mwakyembe siyo mjinga asome report just for the sake of it? kwa kuhisi na majungu? no way.... He knew the fall back na alijua lazima watu wata jaribu kuichallenge..But with my simple knowdge..hakuna mwenye sound reasons au credibility ya kufanya hivyo... Note (all damaging records za akina Bangusilo et al..were given off record..and what next? Mwakyembe was categorical to the effect that..much that those statements (za kina Bangusilo) were sweet and revealing but couldnt be used by the Kamati to make any decisions because they were like hearsay..nevertheless the message was delivered!). (by the way hii kitu hata mahakamani inaruhusiwa...) judge kukataa evidence but nevertheless aka-take note ya hizo evidence..) (hivi hamkuona hata lugha aliyotumia..eg..msabaha ALIIFINYA KAMATI SIKIO..its a loaded statement kisheria kwa mtu mchambuzi wa mambo...

Harafu hii report iko MIKONONI MWA WANANCHI we are the jury now!!! Let them ask us wananchi. Hivi kweli kwa akili zenu mwananchi wa kawaida na machungu tunayoyapata ya akina BOT, BUZWAGI et al.... can Believe KAZAURA OR MSABAHA OR KARAMAGI OR LOWASSA than Mwakyembe?? No way! I said it before hawa wanataka kutafuta pakutokea but the damage is done!
 
Wazee mi niliamini kuanzia mwanzo report ya Mwakyembe itazua mambo mengi ambayo hatujui (it was too professionally compiled to be left without protest from the victims..Hawakutegemea kwamba kuna daring Tanzanians!!!). Politics is a game and who scores takes the cup! EL played well ila aliondoka kama Cameroon. Politically Lowassa is now wounded badly. Influence yake ilikuwepo wakati bado ana-call shots kwenye system. Guys make no mistake, when you are out..you are out! Kama unabisha muulize Sumaye..the man was too powerful to ever think his life outside politics..where is he? Take it from me! all subordinates walikuwa wanamuogopa kwa sababu ya cheo. Currently Lowassa is not and will never be a threat to JK!




Hili suala la El kuwa tishio kwa JK ni kweli sana tu, si utaona kwani JK atamfanya nini? Hatomfanya chochote kile mali na pesa zake zote atabaki nazo na zitaendelea kuzalisha mamilioni ya hela hapo hapo Tz. Trust me wakati El akiiba haya mamilioni, yeye JK alikuwa anajua sana na alikuwa anaona, there is a connection bwana, sema tu Tz ni waoga bado, we have no balls to impeach a president, hata kama amefanya kitu kama hiki, tunaangalia pembeni tu kama vile makondoo fulani. And guess what, the easy way out ni El na JK kuongea na kukubaliana bwana EL wewe acha kazi tu sasa, kwani JK akiacha kazi si kifo kwa CCM, na unajua What CCM stands for.
Always keep in mind hii issue itakufa tu kimya kimya na El na JK will never be enermies. kwani Jk ndio ata-lose a lot kama urafiki na EL utageuka kuwa mchungu.
Just think kwa budget ya Tz, dola milioni200 zitapitishwaje bila ya waziri wa fedha kujua na raisi kujua, hata USA yenyewe lazima Bush ajue tu hizo hela zinakwendaje, Je where is the Parliament and where was the Parliament? Wanalala tu bungeni kwa kushiba sana eeh.
 
....and meanwhile,during this euphoria of baraza jipya na Mwakyembe thing, Daud Ballali is laughing loud and gone......; hakuna tena atakayeuliza yupo wapi. Tusubiri miezi sita ndio tuanze kuuliza upya, kama hatutakuwa tumesahaulishwa kila kitu kama walevi na hangover!
 
Mwanamama,
Umesema mambo ya kweli. Nakubaliana nawewe kwamba serikali yetu haiwezi kulipa zaidi ya $ million 200 bila ofisi kubwa kujua. Kuna tatizo kubwa hapa ambalo linakwenda mpaka ofisi kubwa. Na kwa sasa ishu ya Richmond imekuwa distraction, ingawa nafurahi kuona wananchi wameona ukweli, baadhi ya ukweli. Haiwezekana nchi yenye budget ya $3-3.5 billion inaweza kutoa malipo ya dola million 200 bila mkuu wa nchi kujua. Na kama alikuwa hajui, au kiongozi aliopita alikuwa hajui, basi inaonyesha kazi zao hawafanyi vizuri.
 
Back
Top Bottom