Experience yangu ya kilimo cha vitunguu ni negative

Mkubwa katika usimamizi nilikua makini.
Tatizo SOKO.
Mtu unalima kwa gharama kuubwa halafu unaishia kuuza gunia elfu 30.
Inasikitisha sana.

mkuu licha ya bei ndogo umepata gunia chache sana..kawaida ilibidi upate hata minimal ya gunia 60 kwa eka, kwa eka 6 ungepata 6*60*30,000=10,800,000
 
Pole. Mie ningezimia.
Ngoja niendelee na miti kwanza japo risiki pia ni nyingi
 
Kuna moto unaweza ingia shambani kwa miti ikiwa na umri fulani.

Hiyo Risk nadhani ni manegeable hasa kupalilia kuzunguka shamba na kufyeka majani. Nataka kununua shamba la miti na mimi nadhani utanisidia mkuu au Malila anisaidie nipate shamba la miti na mimi.
 
Last edited by a moderator:
Hiyo Risk nadhani ni manegeable hasa kupalilia kuzunguka shamba na kufyeka majani. Nataka kununua shamba la miti na mimi nadhani utanisidia mkuu au Malila anisaidie nipate shamba la miti na mimi.

Mimi nitakusaidia kupata shamba la kuotesha miti, bei ni Tsh 60,000/ kwa eka. Unataka eka ngapi? Halafu Mamdenyi si ungemkatia kile kipande chako cha upande wa mashariki pale njiani mbona hakina miti !!!!!!
 
Mimi nitakusaidia kupata shamba la kuotesha miti, bei ni Tsh 60,000/ kwa eka. Unataka eka ngapi? Halafu Mamdenyi si ungemkatia kile kipande chako cha upande wa mashariki pale njiani mbona hakina miti !!!!!!

Kama eka kumi kwa kuanzia mkuu Malila vipi zinapatikana? Mamndenyi msaada wako hapa na je, mti mmoja ni shilingi ngapi? kwa eka kumi naweza kupanda miti migani??
 
Last edited by a moderator:
Kulima Tanzania ni kazi kubwa sana.
Masoko sio ya uhakika.
Kilimo kwa nchi yoyote maskini na serikali tapeli lazima jasho likutoke..ndo maana nchi za wenzetu walioendelea wachache wanajishughulisha na kilimo na serikali zao zinawaenzi kweli wakulima maana wanajua ni biashara kichaa..with very high risk, hasa zama hizi za vimbunga, ukame, mabarafu yasiofuata misimu yake ya asili.

Sasa huku kwetu hali ni mbaya maana kila mkulima anaoperate like a headless chicken..huku serikali yenyewe tapeli iko bize kutengeza katiba ya ccm/tzbara..majuzi nlikua naangalia kwa TV watu wa Kiteto sijui Manyara na huko Katavi sijui wanalalamikia serikali inunue mahindi yao!? Ina maana walikua hawana hata miadi na wanunuaji, wao wamepakia tu mahindi yao kwa magari na kupeleka kwa maeneo bila ya hata kua na uhakika..Pia nimesoma the Guardian la juzi hata huko soko la Kenya limebuma, saa hivi gunia la 90 kg linaenda kwa USD 23!!

Poleni sana wakulima wa Tz.
 
Kwa sasa siuzi tena,
Nilikuwa kwenye project ingine
Ila Mungu akipenda mwishoni mwa mwaka huu nitahamia shambani ili
kupanda na kuweka mambo sawa.

Hata hivyo mie sijanunua hizo za bei hiyo,
Mi niko mjini zaidi na bei iko juu pia.

Mimi nitakusaidia kupata shamba la kuotesha miti, bei ni Tsh 60,000/ kwa eka. Unataka eka ngapi? Halafu Mamdenyi si ungemkatia kile kipande chako cha upande wa mashariki pale njiani mbona hakina miti !!!!!!
 
Kwa sasa siuzi tena,
Nilikuwa kwenye project ingine
Ila Mungu akipenda mwishoni mwa mwaka huu nitahamia shambani ili
kupanda na kuweka mambo sawa.

Hata hivyo mie sijanunua hizo za bei hiyo,
Mi niko mjini zaidi na bei iko juu pia.

Juzi nikiwa Iringa nilipita Kiponzero pale ndani Kidogo, bei iko juu ikabidi niamue kuacha. Nikaenda Mtula karibu na kwako, pia bei iko juu kidogo, nadhani sbb ni ukaribu na mjini. Inabidi nibaki Kisusa na bei hizi za buku sitini.

Asante Mamdenyi.
 
Kama eka kumi kwa kuanzia mkuu Malila vipi zinapatikana? Mamndenyi msaada wako hapa na je, mti mmoja ni shilingi ngapi? kwa eka kumi naweza kupanda miti migani??

Niko vijijini ndani ndani sana, huko hata 1000 unapata,kama unataka za mjini aliko Mamdenyi pia utapata. Bei zinatofautiana, mjini miche inauzwa kimjinimjini, na kule kwetu vijijini bei iko poa, ila wastani wa kitalaam wa miti ya mbao ni vizuri usizidi miti 530/540 kwa eka. Vijana wanapiga hadi 600 kwa makosa. Kama ni boriti, eka moja inaweza kwenda hadi miche 1000/1200
 
father-xmas mimi nakubaliana na wewe kwamba uhalisia kamili wa biashara hauzungumzwi.
Mimi nina miti ya teak niliipanda 1994, watu wanasema miti ya teak inatafutwa sana. Lakini mi nimetafuta hao wanunuzi mpaka sasa sijapata. Maneno tu meengi lakini ukweli wenyewe tofauti
 
Last edited by a moderator:
Mkubwa katika usimamizi nilikua makini.
Tatizo SOKO.
Mtu unalima kwa gharama kuubwa halafu unaishia kuuza gunia elfu 30.
Inasikitisha sana.

Ndugu pole sana;


Ingawa mimi siyo mtaalamu lakini zao la vitunguu linaweza kukaa muda ghalani kabla ya kusafirishwa sokoni( Kama utunzaji mzuri havitoharibika. Hivyo ninavyoelewa ni kwamba tatizo la nchi yetu na hasa kwa sisi wakulima wadogo ni mtaji. Ukifika muda wa kuvuna tunatamani tuuze haraka ili tupate pesa ya kuandaa shamba kwa msimu unaofuata au kulipa madeni tuliyokopa wakati wa kulima msimu uliopita.

Usikate tamaa mwanzo daima mgumu isipokuwa kaza buti chunguza hali ya soko baada ya kuvuna na kama hairiridhishi weka mazao yako ghalani subiri kipindi kizuri cha biashara ndipo uuze.
 

Sawa mkuu Malila ngoja nijipange nitakuja nipate Ka shamba na mimi.
 
Last edited by a moderator:

kaka tafadhali naomba kuwasiliana nawewe kwa kina juu ya kilimo hiki,nataeajia kuingia ktk kilimo hicho msimu huu,so if possible naomba unisaidie kwa swala la mbegu bora na mchanganua wa gharama,tafadhali kaka naomba tuwasiliane,mimi nipo Morogoro,contacts zangu ni 0714 808196,0765781288.
 
Mimi nitakusaidia kupata shamba la kuotesha miti, bei ni Tsh 60,000/ kwa eka. Unataka eka ngapi? Halafu Mamdenyi si ungemkatia kile kipande chako cha upande wa mashariki pale njiani mbona hakina miti !!!!!!

mhh!!hayo Mashamba ya sh.60000 kwa ekari moja yako wapi mkuu,ni hapa hapa Tanzania!!!?
 
mhh!!hayo Mashamba ya sh.60000 kwa ekari moja yako wapi mkuu,ni hapa hapa Tanzania!!!?

Tatizo ni ww kutojua, ila yapo mpaka ya BURE kabisa, kuna kijiji pwani hii bei ni Tsh 5000/ eka moja na bado vijana hawataki kwenda. Kuna mahali ndani ya Bongo yetu niliambiwa njoo ulime na kufuga tani yako, changamoto ikawa soko la bidhaa zangu liko mbali.

Huko mahali wakati naanza, tulikuwa tunanunua Tsh 15,000/ kwa eka, sasa hivi imepanda. Kijiji cha Banduka pale Lindi mwaka jana walikuwa wanagawa bure kwa kila atakaye. Haya nimekutajia sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…