Experience yangu ya kilimo cha vitunguu ni negative

Experience yangu ya kilimo cha vitunguu ni negative

father-xmas mimi nakubaliana na wewe kwamba uhalisia kamili wa biashara hauzungumzwi.
Mimi nina miti ya teak niliipanda 1994, watu wanasema miti ya teak inatafutwa sana. Lakini mi nimetafuta hao wanunuzi mpaka sasa sijapata. Maneno tu meengi lakini ukweli wenyewe tofauti

Miti ya Teak ina maelezo ya hivyo mengi sana, ila ninachojua ni kwamba, ni kwa scale kubwa ndio unaweza pata soko la maana. Sasa kama una scale ndogo ya shamba itakuwa taabu kidogo. Mfano eka kumi za Mitiki kule Kigoma, mnunuzi anayetaka magogo kama laki moja atakuja kweli? Kwa small scale, teak ni hasara sababu inachukua miaka mingi sana mpaka kukomaa,ndio maana kwa watu binafsi ni mtihani kidogo.

Habari ya mitiki kama unaitaka hasa, basi nenda Longuza Tanga, Kilombero na Lindi ktk misitu ya serikali ambako hata mvunaji anaweza leta mitambo toka nje akijua atapata faida.
 
Hongera sana mkuu.(
Sina lengo la kum discourage yeyote,hii ninayoongelea ni expirience yangu.
Hebu naomba uniambie wewe ulilima wapi,umevuna gunia ngapi kwa ekari,umeuza bei gani kwa gunia na uliuzia wapi.

Mkuu sifalima kwa simu kama unavyodai,nilikwenda mwenyewe front line.
Halafu pia ungeweza kutoa hoja bila kutumia hiyo ´wtf´



pole mkuu ila nishagundua there is no easy going' kwenye swala la ujasiriamali.
kila kitu ni uvumilivu ila inakatisha tamaa wakati mwingine.ukisoma hizi theory huku inavutia kweli ila when it comes to reality lo!
hapa nimenunua gunia za vitunguu kupeleka nairobi ni balaa.Mzigo ni mwingi kila mtu anapeleka na bei inashuka.
 
Pole sana, kilimo ni kigumu sio kirahisi kama watu wengi wanavyosema, mfano mm nililima mahindi na nimeshavuna bei iliyopo sokoni kwa sasa ni ya kutupa, nimeyaivazi (gharama za kuyaivazi pia ni kubwa) nione adi mwakani mwezi wa kwanza bei itakuwaje
 
Pole sana, kilimo ni kigumu sio kirahisi kama watu wengi wanavyosema, mfano mm nililima mahindi na nimeshavuna bei iliyopo sokoni kwa sasa ni ya kutupa, nimeyaivazi (gharama za kuyaivazi pia ni kubwa) nione adi mwakani mwezi wa kwanza bei itakuwaje

Uzoefu sasa unanipeleka hatua ya pili, Taifa letu linauza malighafi ktk soko, kwa hiyo kuanguka kwa wakulima ni lazima. Inabidi tuanzishe viwanda vidogo vidogo vingi ktk ngazi za vijiji ili kuokoa hasara hizi;

Angalia kilio hiki,
Wafuga nyuki wanalalamika soko hakuna, lakini wangeweza kusindika wenyewe,
Walima alizeti nao wanaibiwa
Walima ufuta huko Lindi nao wanalalamikia soko
Walima mahindi ni kilio
Walima viazi huko Njombe nao wamepigwa dafrau la kufa mtu,
Walima nyanya hawana uhakika na kesho
Kahawa/chai/pareto vyote vinaliza wakulima.

Bila viwanda vidogo vidogo vya kusindika mazao yetu, tutaendelea kulia kila siku.
 
kaka tafadhali naomba kuwasiliana nawewe kwa kina juu ya kilimo hiki,nataeajia kuingia ktk kilimo hicho msimu huu,so if possible naomba unisaidie kwa swala la mbegu bora na mchanganua wa gharama,tafadhali kaka naomba tuwasiliane,mimi nipo Morogoro,contacts zangu ni 0714 808196,0765781288.

Mkuu naogopa kukupa maelezo kwa sababu nikikuelezea njia nilizotumia mimi mwisho wake na wewe utaishia kupata hasara kama niliyopata mimi.
Mimi na wewe tunahitaji darasa kutoka kwa wataalam wetu kina Malila.

Kuhusu mbegu bora sidhani kama mbegu niliyotumia ni bora maana ingekua bora nisingepata mavuno machache kiasi kile.
Mimi mbegu nilinunulia kule kule shambani na niliamiwa ni mbegu nzuri na hata ilipoanza kuota watu waliisifia sana ile mwisho wa siku ikawa hasara.
Bado sijajua nilikosea wapi,sijui tatizo ni mbegu au kuna kingine nilichofanya kimakosa.
Nitalima tena,ila kabla sijalima tena lazima nijue nilichokosea ili nisirudie kosa.
 
Ruaha mbuyuni hapafai, vibarua shida, wanaolima wengi, badili location, kitunguu kitakutoa. Nenda japo mbeya au dumila au hata kifaru moshi
 
Mkuu naogopa kukupa maelezo kwa sababu nikikuelezea njia nilizotumia mimi mwisho wake na wewe utaishia kupata hasara kama niliyopata mimi.
Mimi na wewe tunahitaji darasa kutoka kwa wataalam wetu kina Malila.

Kuhusu mbegu bora sidhani kama mbegu niliyotumia ni bora maana ingekua bora nisingepata mavuno machache kiasi kile.
Mimi mbegu nilinunulia kule kule shambani na niliamiwa ni mbegu nzuri na hata ilipoanza kuota watu waliisifia sana ile mwisho wa siku ikawa hasara.
Bado sijajua nilikosea wapi,sijui tatizo ni mbegu au kuna kingine nilichofanya kimakosa.
Nitalima tena,ila kabla sijalima tena lazima nijue nilichokosea ili nisirudie kosa.

Nimekutumia simu ya mdau mwenzako aliyepo Iringa ambaye naye amekutana na kadhia hiyo msimu huu. Jaribu kupata mawazo yake ili usirudie kosa.

Ila kwa mawazo yangu, nadhani tatizo liko kwa vijana/wazee wa kazi ulio watumia. Kuna wafanyakazi mabingwa wa kuwaliza watu, hata mimi nimekutana nalo hilo pale Mkuranga,lakini baada ya kubadili njia ya kupata wafanyakazi afya ya shamba inaimarika sana.
 
Heshima kwenu viongozi wangu.

Wakuu natumai hamjambo na mnaendelea vyema na shughuli za ujenzi wa taifa letu.
Wakuu baada ya kusikia wengi wetu wakisifia sana kilimo cha vitunguu nikapata muamka na mimi nikaingia katika kilimo cha vitunguu.

Nilikodisha ekari sita pale Ruaha Mbuyuni.
Kwa kweli sitaki kusema mengi ila ninachoweza kusema ni kwamba kutajirika kwa kilimo cha vitunguu LABDA inawezekana lakini sio kiurahisi kama wengi wetu wanavyohubiri humu.

Kwa EKARI ZOTE SITA nilizolima nilivuna gunia mia moja na tano tu.
Gunia moja niliuza kwa shilingi elfu thelathini tu.
Nilivuna mwezi wa saba mwaka huu ,2014.

Nilitumia shilingi karibia MILIONI KUMI NA TATU kulima ekari zote sita halafu nilipovuna nikapata shilingi milioni tatu laki moja na elfu hamsini hivi.3,150,000 kutoka kwenye mavuno ya ekari zote sita.

Nilikua makini sana kutimiza mahitaji yote niliyoambiwa nikitimiza nitavuna na kupata faida.
Anayetaka kuingia kulima na aingie ila tuwaeleze wenzetu ukweli,hichi kilimo ni very risky.

Anyway,mwakani nitalima tena maana jamaa wamenishawishi sana wakidai hasara ya mwaka huu isinikatishe tamaa.Nashindwa kusema kama kinalipa au hakilipi kwa sababu nimelima mara moja tu.Matokeo ya mwaka kesho ndio yatanipa uamuzi wa kujikita kwenye kilimo au kujitoa na kuwaachia kina Malila.

Kitu nilichogundua ni kuwa watu wengi humu hawasemi ukweli kuhusu hichi kilimo.

Mkuu Gagurito njoo basi utupe uzoefu wako kuhusu Ruaha Mbuyuni! !
 
Last edited by a moderator:
mimi nilichojifunza hiki kilimo ni kizuri sana na watu wengi humu wanapotosha kuhusiana na mbegu. kuna watu wanasema mbegu za shamban ni nzuri ila mimi napinga. pili hata mapato yanakuzwa sana kuliko kiwango. mimi gharama zangu mpaka navuna kwa eka moja nimetumia laki nne tu mpaka navuna. mbegu nilinununu gram 100 ambazo kusema kweli nilipanda mpaka nyingine nikauza.
garama ya kukodi shamba 70000
mbegu gram 1000 redcreole 90000
vitalu total cost 100k
mbolea sikuwa nanua kwa gunia nilikuw nanua kwa kupimiwa mchanganyiko wa kutosha eka moja 8000 niliweka mara mbili so total cost ya mbolea 30000 za kitalu. dawa wakat naanza nilinunua dawa za dhaman ya 100k. mengine naona nimesahau ila nikrudi mbeya wik ijayo nitacopy tota cost zangu mavuno jumla nilipta gunia 50, challenge imekuwa soko lakin hta nikisema niuze kwa elfu 30,bado kwangu sio kilio. tunachotakiwa tusikate tamaa pia hii kazi inahitaji ujitoe upate ushauri wakitalaamu uchanganye na za kwako. pia usiingie kwenye kilimo kutafuta pesa ingia kwenye kilimo ukiwa kama una mapenz na kilimo hata pale inapotokea umeingia hasara iwe kwako ni challenge. jaman weng waliomo humu wamekaa kibiashara zaidi, mtu anakushawishi ufanye kilimo ili akuuzie mbegu na madwa tu hakuna kingine. tunachotakiwa hapa ni kutengeneza syndicate ya wakulima sisi ndo tuwe wapanga bei masoko ya mazao yapo meng tu. juzi hapa kuna watu wametoa maelezo kuhusiana na wathailand wanao nunua mahindi ya njano hamuwez amini mpaka leo ni watu wawili ndo wanaosupply.sisi niwaogaa
 
Nimekutumia simu ya mdau mwenzako aliyepo Iringa ambaye naye amekutana na kadhia hiyo msimu huu. Jaribu kupata mawazo yake ili usirudie kosa.

Ila kwa mawazo yangu, nadhani tatizo liko kwa vijana/wazee wa kazi ulio watumia. Kuna wafanyakazi mabingwa wa kuwaliza watu, hata mimi nimekutana nalo hilo pale Mkuranga,lakini baada ya kubadili njia ya kupata wafanyakazi afya ya shamba inaimarika sana.

Asante sana mkuu.
Nimeiona.
 
Tanzania watu wanafanya kitu kwa kusikiliza story za watu
 
Pole sana mkuu, na pia nakushukuru kwa ujasiri wa kushare experience yako hapa. Mie sio mjuzi wa kilimo lakini ninacho kushauri ni kujifunza nini kimefanya mavuno hayakuwa mazuri - inaonyesha umepata magunia 18 kwa eka ambayo kwa kweli ni kidogo sana. sababu inaweza kuwa ardhi, mazingira, mbegu, matayarisho ya shamba, mpandikizo, mvua, wadudu, kudhibiti gharama, jaribu pata ushauri wa wakulima wenzio ambao wamekua katika eneo lako kwa muda - waulize mwaka mwema walipata kiasi gani cha mazao ? . Asante . Endelea na jitihada na chukulia huu ni mtihani na funzo
 
Shukruni mkuu.
Nilikua nakwenda kila wiki.
Kila lilipofanyika jambo la muhimu mfano kutia mbolea kumwagilia madawa au palizi nilikuwepo mwanzo hadi mwisho.
Wakati wa kuvuna mpaka kuuza nilikuwepo.
Kwa kifupi sijapoteza pesa tu,bali nili invest muda wangu mwingi sana.
Mkuu hebu acha uongo bana. Au unaogopa watu wengi wataanza kulima soko lifurike vitunguu? Nilidhani umelima Kwa simu watu wakakuibia huko na kukudanganya. Lakini kama ulikuwa unakwendaa mwenyewe na kila hatua muhimu ulikuwepo huwezi kuvuna gunia 18 Kwa ekari moja, NARUDIA kusema huwezi kuvuna magunia 18 Kwa ekari moja. Kama ulisimamia mwenyewe namna ile na ukavitunza vitunguu lazima upate gunia si chini ya 60 Kwa ekari moja NARUDIA kusema kama ulisimamia hatua muhimu mwenyewe na kila wiki ulikuwa huko huwezi kukosa gunia 60 Kwa ekari moja. Hapo ungekuwa na gunia 360 na Kwa bei ya chini ya 50,000 Kwa gunia Kwa uchache ungepata milioni 18. Vilevile nina mashaka na matumizi ya milioni 13 kwenye ekari 6 si kawaida.
 
Mkuu hebu acha uongo bana. Au unaogopa watu wengi wataanza kulima soko lifurike vitunguu? Nilidhani umelima Kwa simu watu wakakuibia huko na kukudanganya. Lakini kama ulikuwa unakwendaa mwenyewe na kila hatua muhimu ulikuwepo huwezi kuvuna gunia 18 Kwa ekari moja, NARUDIA kusema huwezi kuvuna magunia 18 Kwa ekari moja. Kama ulisimamia mwenyewe namna ile na ukavitunza vitunguu lazima upate gunia si chini ya 60 Kwa ekari moja NARUDIA kusema kama ulisimamia hatua muhimu mwenyewe na kila wiki ulikuwa huko huwezi kukosa gunia 60 Kwa ekari moja. Hapo ungekuwa na gunia 360 na Kwa bei ya chini ya 50,000 Kwa gunia Kwa uchache ungepata milioni 18. Vilevile nina mashaka na matumizi ya milioni 13 kwenye ekari 6 si kawaida.

Mkubwa una uhuru wa kutoa maoni yako,sitegemei kila mmoja aamini nilichosema.Wewe sio wa kwanza kunipinga ktk uzi huu,na nimaheshimu michango yenu nyote mlionipinga,mlionielewa na mlioni support kwa kudhibitisha kuwa na nyie mmekumbana na hali kama hii.

Tuko hapa kuelimishana,ningependa kujua hiyo elfu 50 kwa gunia uliuzia wapi na mwezi gani.
 
Mkuu malila unatisha kwelikweli nimesoma michango yako mingi humu JF.....niwe muwazi kuwa unasaidia sana. pointi zako zina kilo nyingi. mi bila shaka najipanga ili nianze kupanda miti huko maeneo umesema yanapatikana. kama utapata mda naomba uni-pm contacts zako.
natanguliza shukrani nyingi kwa kazi nzuri. mana tukizubaa wakenya watamaliza maeneo na tuishie kulalamika.
 
Miti ya Teak ina maelezo ya hivyo mengi sana, ila ninachojua ni kwamba, ni kwa scale kubwa ndio unaweza pata soko la maana. Sasa kama una scale ndogo ya shamba itakuwa taabu kidogo. Mfano eka kumi za Mitiki kule Kigoma, mnunuzi anayetaka magogo kama laki moja atakuja kweli? Kwa small scale, teak ni hasara sababu inachukua miaka mingi sana mpaka kukomaa,ndio maana kwa watu binafsi ni mtihani kidogo.

Habari ya mitiki kama unaitaka hasa, basi nenda Longuza Tanga, Kilombero na Lindi ktk misitu ya serikali ambako hata mvunaji anaweza leta mitambo toka nje akijua atapata faida.
Mkuu malila unatisha kwelikweli nimesoma michango yako mingi humu JF.....niwe muwazi kuwa unasaidia sana. pointi zako zina kilo nyingi. mi bila shaka najipanga ili nianze kupanda miti huko maeneo umesema yanapatikana. kama utapata mda naomba uni-pm contacts zako.
natanguliza shukrani nyingi kwa kazi nzuri. mana tukizubaa wakenya watamaliza maeneo na tuishie kulalamika.
 
Mkuu malila unatisha kwelikweli nimesoma michango yako mingi humu JF.....niwe muwazi kuwa unasaidia sana. pointi zako zina kilo nyingi. mi bila shaka najipanga ili nianze kupanda miti huko maeneo umesema yanapatikana. kama utapata mda naomba uni-pm contacts zako.
natanguliza shukrani nyingi kwa kazi nzuri. mana tukizubaa wakenya watamaliza maeneo na tuishie kulalamika.

Asante mkuu,
Angalia inbox yako.
 
Back
Top Bottom