Experience yangu ya kilimo cha vitunguu ni negative

Experience yangu ya kilimo cha vitunguu ni negative

hua sifanyi biashara kichaa... hasara ya milioni kumi alafu nirudi kufanya hiyo business? piga ua...
Shamba bora nifanyie biashara tofauti tu.. jipange utafute wataalam wa hii mambo naona ulionao wamekupeleka njia mbaya... something can be risky ila sio kwa extent ya 13M inarudisha 3M... angalau ingerudisha 10M
 
Acha kudiscourage watu wengine Mbona tulipata sawasawa na investment zetu
The issue here is the management basi,ukulima wa simu wtf you expect lazima utavuna mabua tu

Tatizo mnakurupuka kujibu bila kualewa. Soma elewa ujumbe ammemaanisha nini
 
Mkuu milioni 10 kuzipoteza sio jambo dogo.., pia huo muda uliopoteza ni priceless..; sasa unavyosema utalima tena ni kama kubahatisha sababu ukifanya kitu kile kile ulichofanya mwaka huu huenda matokeo yakawa yaleyale...

Kwa ushauri mimi naona kwa yoyote anayeanza kufanya kitu chochote kwa kuanzia ni bora aanze kidogo kidogo.., hii itakupa experience na wewe kujionea mambo yanavyokwenda. Sababu mkuu just imagine haujawahi kuuza alafu ghafla una gunia mia na kitu.., alafu jambo lenyewe ni perishable hata wanunuzi wataona desperation na inaweza kupelekea wewe kuuza bei ya kutupa.

Pili nimeshaona wabongo wengi kitu kama kina faida sana kwa wakati fulani basi inapelekea kila mtu kufanya kitu kile kile.., hii inapelekea supply kuwa kubwa sana ghafla na huenda zile bei zilizozoeleka zikashuka..

Kwahio mkuu Ushauri kama Utalima tena...

  • Anza kidogo ili upate uzoefu.., hata ekari moja kwanza watu wakujue na ufahamu mwenendo wote mpaka wa soko
  • Tafuta soko kwanza ujue kabisa unauzia wapi na uwe na plan B..., yaani kama soko likiwa baya hakikisha unao uwezo wa ku-store kwa muda mpaka bei zitakapopanda
  • Kama Kilimo chako kinategemea hali ya hewa (na sio umwagiliaji) basi kuwekeza pesa nyingi ni kama kamali
  • Katika Hesabu zako za kupata faida weka the worse case scenario.., yaani fikiria kwamba mfano bei ikiwa mbovu kuliko zote bei ni kiasi gani ?, alafu hii ndio pigia hesabu
  • Ukisikia fulani kauza labda yeye anao mtandao wake.., madalali mara nyingi ukiwa hauna mzigo wanasema lete hakuna neno na kama unautoa mbali siku ukiuleta wanaanza story za kwamba mzigo mara mbovu au kuna malori yameingia toka vijijini kwahio kuna mzigo wa kumwaga n.k. (hii yote ni kujaribu kushusha bei na wanajua hauna jinsi utashusha tu..) Point yangu hapa hakikisha kabla una sehemu za masoko zaidi ya moja ili moja likikataa basi lingine unaweza kufanika..

Zaidi ya hapo hakuna tofauti na mtu anayeweka pesa zake kwenye Betting Manchester United inapocheza na Chelsea ukitegemea mmojawapo ashinde

Tatizo la msingi ni yeye kuvuna gunia 105 kwenye ekari 6...
 
Aaaa mjomba eka sita huwezi tumia milioni 13. ungemuona afisa kilimo akupe makadilio ya gharama na kazi zitakazo fanyika
mfano wa ekari moja
1. kulima 50 000*3 =150 000
2.mbegu 200 000
3.palizi 40 000*3 =120 000
4.dawa 70 000
5.mbolea 160 000
jumla700 000
umwagiliaji unategemea
 
Nilichojifunza mimi siri ya kilimo cha kitunguu ni USIMAMIZI.
 
Nimesikia hiki kilimo cha vitunguu kinastawi hasa maeneo ya Iringa ila sijajua sehemu gani ila kuna jamaa Fulani nimeona anakisifia hiki kilimo na nimevutika nacho coz amelima kama ekari 5 ana expect kupata more than 40 million akivuna na amenambia mpaka anavuna atakuwa ametumia more than 10 million kwa hyo anafaida ya 30 million.Ila mzigo bado upo shambani bado hajavuna. Na kwa maelezo yake soko lipo la kutosha Me nilitaka nianzie ekari mbili tu nami nijaribu kulima.Ila naanza ku doubt
ila ntatoa mrejesho akivuna inaweza kuwa biashara nzuri
 
Mkuu Kuwa Makini na Washauri wako wa karibu,Washakuona Hela unayo so wanachofanya ni kukupa Moyo ili uendelee kulima tu kwa sababu wao wanafaidika kwa kukuuzia mbegu,kukulimia,kupalilia,kuvuna,wewe unafikiri usipolima tena wao watapata ajira? Lazima wakushawishi tena kwamba jaribu mara ya pili utapata lakini kwa other hand utabaki kupata hasara tena.

Tafakari sana kama mwalimu nyerere alivyofikiria kipindi alivyotaka kung'atuka,Kuna watu wake wa pembeni mawaziri walimshauri kwamba mwalimu using'atuke endelee tu kuongoza lkn mwalimu aliwastukia kwamba hao wote wanahofia anayekuja anaweza asiwape nafasi walizokuwa nazo.

This is what we call a bizness:
Kuna Mzee alimwambia mwanawe wa kiume kwamba nataka kukuchagulia mchumba ninayemtaka mimi,Mwanawe wa kiume akakataa,lakini Mzee akamwambia huyu mchumba ni mtoto wa Bill gate,Yule mwanae akakubali fasta.

Mzee akatoka akaenda kwa Bill Gate akamwambia mwanangu anataka kumuoa Binti yako,Bill Gate akakataa lakini Mzee akamwambia Mwanangu anayetaka kumuoa binti yako Ni Moja wa Ma-Director wa World Bank,Bill Gate akakubali Binti yake aolewe.

Mzee akatoka hapo akenda kwa CEO wa World bank kumuombea kazi Mwanawe wa Kiume,alivyofika CEO wa World Bank akasema hakuna nafasi lakini akamwabia Mwanangu amemuoa Binti wa Bill Gate,Yule CEO akampatia nafasi World bank.
 
Muda wote wanaotuibia ni wenyeji wetu! Wanakijiji ,vibarua! Unaweza kusimamia vizuri lakini wasikwambie kwamba shamba hilo limechoka, halina rutuba hata utumie mbolea gani utapata hasara tu, yashanikuta!
 
Heshima kwenu viongozi wangu.

Wakuu natumai hamjambo na mnaendelea vyema na shughuli za ujenzi wa taifa letu.
Wakuu baada ya kusikia wengi wetu wakisifia sana kilimo cha vitunguu nikapata muamka na mimi nikaingia katika kilimo cha vitunguu.

Nilikodisha ekari sita pale Ruaha Mbuyuni.
Kwa kweli sitaki kusema mengi ila ninachoweza kusema ni kwamba kutajirika kwa kilimo cha vitunguu LABDA inawezekana lakini sio kiurahisi kama wengi wetu wanavyohubiri humu.

Kwa EKARI ZOTE SITA nilizolima nilivuna gunia mia moja na tano tu.
Gunia moja niliuza kwa shilingi elfu thelathini tu.
Nilivuna mwezi wa saba mwaka huu ,2014.

Nilitumia shilingi karibia MILIONI KUMI NA TATU kulima ekari zote sita halafu nilipovuna nikapata shilingi milioni tatu laki moja na elfu hamsini hivi.3,150,000 kutoka kwenye mavuno ya ekari zote sita.

garama hzo za uendeshaj ilikuwa kubwa sna kwa eka hzo
 
Muda wote wanaotuibia ni wenyeji wetu! Wanakijiji ,vibarua! Unaweza kusimamia vizuri lakini wasikwambie kwamba shamba hilo limechoka, halina rutuba hata utumie mbolea gani utapata hasara tu, yashanikuta!

Umesema vyema kabisa!!
 
Muda wote wanaotuibia ni wenyeji wetu! Wanakijiji ,vibarua! Unaweza kusimamia vizuri lakini wasikwambie kwamba shamba hilo limechoka, halina rutuba hata utumie mbolea gani utapata hasara tu, yashanikuta!

sahihi
 
mkuu licha ya bei ndogo umepata gunia chache sana..kawaida ilibidi upate hata minimal ya gunia 60 kwa eka, kwa eka 6 ungepata 6*60*30,000=10,800,000

nafahamu hapo alipolimia pato lao huwa ni ndogo ni wastani ya gunia 50 au 60 aliyepata sna ni 70 kwe eka.tofouti na igawa na mangola arusha.kilichomtia hasara yawezekana ni .1.ardhi ina magadi 2 mbegu 3 usimamizi mbovu.km hujazingatia hayo lazima ufeli tu.kitunguu na nyanya inahitaji usimamizi na uangalifu wahali ya juu
 
nafahamu hapo alipolimia pato lao huwa ni ndogo ni wastani ya gunia 50 au 60 aliyepata sna ni 70 kwe eka.tofouti na igawa na mangola arusha.kilichomtia hasara yawezekana ni .1.ardhi ina magadi 2 mbegu 3 usimamizi mbovu.km hujazingatia hayo lazima ufeli tu.kitunguu na nyanya inahitaji usimamizi na uangalifu wahali ya juu
kilimo cha pale balaa..nimeshakila hasara ya m3 mwezi huu...eka moja na nusu imetoabgunia chache sana
 
kwanza ardhi ya pale imechoka,pili kuna wajanja wengi inawezekana wewe ulikuwa unatoa pesa ila usimamizi ukawa mbovu wajanja wakawa wanakupiga kama umeingia ujasiliamali hasara ni sehemu ya biashara cha muhimu ni kukaa na kutafakari ni biashara gani imekuingizia hasara
 
Back
Top Bottom