MSEZA MKULU
JF-Expert Member
- Jul 22, 2011
- 3,763
- 5,607
- Thread starter
-
- #81
Soma Mwanzo1:28 linganisha na dhumini la hao jamaa Mwanzo11:4.WORD!.....Yaani mnara wa Babel ulimfanya Mungu ashuke kuja kuzuia ujenzi wake.Huoni kuwa wanasayansi wa zamani(ma engineers na ma Astronauts) walizuiwa na Mungu kufanya tafiti zao?
Hivi kama Mungu alikataza ujenzi wa ule mnara, angeruhusu safari za kwenda Mars kweli?
Hapa mkuu kuna vitu vya kujifunza vingi kama Building ground kabla ya kujadili hiki ulichokileta(BIBLE(which inspired scientists) and Religious sect).Kwa sababu walikuwa wanatafuta facts kujua kweli ipo wapi.
Enlightenment ni neno lililotoholewa kutoka Indian Spirituality kumaanisha utambuzi au awakening. Kuamka katika ujinga na delusions.
Pia Msijifanye kusahau wanasayansi walikuwa wanauawa na kuteswa kikatili na kinyama. Why? Mwanadamu mwenye akili timamu huwezi kumfanyia mwenzako hivyo. Ni dalili za ujinga. Tena mapapa na viongozi wa kidini walichangia mauaji makubwa. Kama religions zilikuwa zinauhakika kwanini ziue na kuchoma kama mishkaki wanadamu ambao walionekana wasomi watakaoleta changamoto? And they teach love thy neighbor. Its a shame.
Michael Servetus - Mwanasayansi wa medicine, sayansi na law.
Kuchomwa kwa Giordano Bruno.
Aliuawa na kuchomwa kama stake mbele ya watu mwaka 1600 kwa maagizo ya papa.
Giordano Bruno supported the Copernican view – the view that the earth orbits the sun, and that the earth is not the center of the universe.
More than this, he held the thoroughly modern view that distant stars are orbited by their own, possibly inhabited, planets. He stated that the universe is infinite in size and has no center.
He was imprisoned for seven years while his trial took place. Eventually the Pope decided that Bruno was a heretic, with the result that he was burned at the stake in Rome. His beliefs about the earth, sun and universe were part of the reasoning behind his death sentence. He was also declared a heretic for his religious views about, for example, the Catholic Mass and the Trinity.
Kuna Archimedes, Antoine Lavoisier, na wengine wengi sana katika list waliuawa na Christianity. Is that what bible says? Shame on those who called themselves christians. Hata hao mapapa nao wanastahili kuchomwa moto kama kweli kuna motoni. Nao ni wanadamu wa kawaida na wajinga kama watu wa kawaida.
Hii ni list ya wanasayansi na philosophers waliochomwa, kunyongwa na kuuawa kikatili kutokana na kuchallenge mitazamo ya bible.
May their souls gets next life safely.
List of people burned as heretics - Wikipedia
Nimeweka mpaka mzuri kabisa (Scientists na Bibilia), Madhehebu ya dini mengi wenda walitumia bibilia kama kofia, au kwa kuhofia kuathiliwa na mabadiliko. au Kuwahukumu kwa uzushi bila kufanya deep analysis na invenstigation sijui. Ila Mimi nipo kati ya Bibilia na Wanasayansi walivyogundua hazina nzito ndani ya bibilia na nature. Hapo walichomwa moto wengi tu sio wanasayansi, Hata bibilia haikutakiwa kumilikiwa au kusomwa na mtu binafsi maana iliaminika kasisi ndio mwenye uwezo wa kutafsiri. Kila aliyeisoma aligundua vingi vilivyokuwa either havisemwi na wakuu au Viko kinyume. Martin Luther aligundua haki inapatikana kwa imani sio kama wanavyofundisha haki kwa matendo akaonekana mzushi na muasi. Ila wanasayansi wengine Walionekana hicho walichogundua tena wengi wakiwa inspired by bible kitasababisha hayo maeneo yasitawalike. Hii likuwa ni hofu tu ya kupandikizwa au kutokuju. Na pia hii ilikuwa sio kweli walikuwepo wapinzani wao waliokuwa wakichochea uzushi maana walivyokuwa wanavigundua inspired by bible vilikuwa kinyume na wengi walivyokuwa wanafundishana based on classical Greece philosophies.Narudia tena kuweka list mjisomee wenyewe jinsi christianity (bible followers) ilivyomaliza uhai wa wanasayansi ambao ni binadamu kama sisi na wenye haki ya kuishi.
Inauma sana. Sio siri, sio kujifanya tunasahau na kuleta topic hii ya kusifia bible kuwa ni sayansi. Kama kweli ni hivyo mbona mliwaua waliosema hizo ideas?☠️[emoji53]
ITS A SHAME. [emoji848]
List of people burned as heretics - Wikipedia
Naona baada ya kukoswa pa kukosoa umejaribu kuja kivingine.Mada iliyopo mezani ni batili.Nasema ni batili kwa sababu Bibilia haiendani na sayansi.
Bibilia inasimama juu ya msingi IMANI lakini Sayansi inasimama juu ya msingi UELEWA(FACTS).
Ingawa kwenye Bibilia kuna mambo mengi yaliyokusudiwa kueleweka, lakini kuna mambo mengi mno yaliyokusudiwa kuaminiwa(Yaani wewe amini tu usiulize yanawezekanika vipi, mf: Miujiza ya Yesu)
Sasa Bibilia haiwezi kuendana na Sayansi kwa sababu Sayansi kama tujuwavyo, inatafuta facts kwa kufanya experiment na siyo kuamini.
Kwenye Sayansi lazima ufanye: Observation, Thinking, Hypothesis formulation, TESTING Pamoja na kufanya conclution(hizi ni baadhi ya procedures)
Sasa hebu chukua haya mambo ya kwenye Bibilia halafu oune kama yana match na Sayansi.
1.Uwepo wa Roho na Mapepo, Bibilia inaamini vipo lakini sayansi haiamini kama vipo kwa sababu haviwezi kuwa tested(untested is unscientific).
2.Maisha ya Yesu: Sayansi inataka kutest ni namna gani mtu alizaliwa na mzazi mmoja pekee bila ya kuwepo kwa mbegu za kiume za Baba.Bibilia inatuaminisha kuwa jambo hilo lilitokea kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.Sayansi inataka ku test ni jinsi gani Yesu alifufuka siku tatu baada ya kufa.
3.Miujiza ya Yesu haiwezi kuwa tested kisayansi.Yesu aligeuza maji kuwa Divai,....Hivi kwenye Organic Chemistry unafanyaje conversion ya water to wine?(lazima uingie lab kufanya experiment itakayohusisha testing.Je ukipewa maji kwenye mtungi bila catalyst wala reactant ya aina yoyote, uyageuze kuwa divai itawezekana?)
Kwa maana hiyo Sayansi haiwezi kutokana na Bibilia kwa sababu misingi ya Sayansi haipo kwenye Bibilia.
Mkuu hii naona ni mambo ya imani na theology. tukiingia huko tutapoteza mwelekeo maana najua kuna watu wanasubiri upenyo tu waingize mambo yao. Hapa tunazungumzia Bibilia its accuracy in many scientific finding and predictions (japo kuna evolutionits scientists wao hata kwa makusudi wako tayari kupindisha ukweli bibilia isionekane iko safi).Hii nadharia ya Vicarius Filii Dei ilitengenezwaje? Maana nilisoma mada fulani humu JF na baadae google nikaona ni jinsi watu walivyopika theory za kupinga RC
amen.CHRIST IS LORD!!!
Hahahaaa...naona una urge kisiasa sana.Naona baada ya kukoswa pa kukosoa umejaribu kuja kivingine.
Kwanza sio hayo tu;
1: Elisha alitupa kijiti kwenye maji kichwa cha SHOKA(Chuma kikaelea), UNSCIENTIFIC. Where was g?Archmedes, Floatation principle?
2: Waebrania watatu walitupwa motoni, HAwaKUUNGUA isipokuwa kamba walizofungiwa na Waliowatupa wakafa kwa mionzi ya moto.UNSCIENTIFIC, energy transformation
3:Eliya alichukuliwa na Gari la farasi la Moto likapotea nae Mbinguni kama movie lakini ni kweli.
Upande huo ni Beyond science ndio maana hawawezi wataishia kusema tu yesu alitembea juu ya barafu, wakishindwa wanasema Yesu hakuwepo.UNSCIENTIFIC maana hapa alivunja Gravitation force.
LAKINI KWENYE HIYOHIYO BIBILIA, wakati wasomi magenius wa dunia nzima walipokutana BABELI na kuagiza nyama, Masupu, mavyakulaya kila aina, Daniel, Shedrack, MEshack na abednego wao waliomba maji, Cereals na Plant products kwalipotestiwa hawa wa bibilia walikuwa na akili mara kumi zaidi ya hao waliokula kila kitu, THIS GIVES ROOM FOR SCIENTIFIC RESEARCH AND PREDICTIONS maana This was what God Proposed as food to Human Race before Sin. Kuna mambo ambayo yamesemwa na ni halisi kuhusu ukuu wa Mungu. Mengi saana sana Hayana uhusiano na Miujiza bali ni reality they inspired humble scientists and changed the face of the world. THREAD HII inazungumzia Bible as a tool for scientific innovation and predictions. You can explore What it said and enjoy the reality. Hapa ndipo wanapopenya Evolutionist scientists ambao wao kazi yao kushirikiana na Ethiests kupinga bibilia. Wanashindwa kujua Gregol Mendel founder wa Genetics alikuwa creationists na alivyokugundua kilisababisha wafanye faster kumuokoa jamaa yao Darwin asijekuaibika ndio wakaja na uongo wa genetic-evolution.
Nakushauri tena Soma thread njoo tujadili
Nimeweka mpaka mzuri kabisa (Scientists na Bibilia), Madhehebu ya dini mengi wenda walitumia bibilia kama kofia, au kwa kuhofia kuathiliwa na mabadiliko. au Kuwahukumu kwa uzushi bila kufanya deep analysis na invenstigation sijui. Ila Mimi nipo kati ya Bibilia na Wanasayansi walivyogundua hazina nzito ndani ya bibilia na nature. Hapo walichomwa moto wengi tu sio wanasayansi, Hata bibilia haikutakiwa kumilikiwa au kusomwa na mtu binafsi maana iliaminika kasisi ndio mwenye uwezo wa kutafsiri. Kila aliyeisoma aligundua vingi vilivyokuwa either havisemwi na wakuu au Viko kinyume. Martin Luther aligundua haki inapatikana kwa imani sio kama wanavyofundisha haki kwa matendo akaonekana mzushi na muasi. Ila wanasayansi wengine Walionekana hicho walichogundua tena wengi wakiwa inspired by bible kitasababisha hayo maeneo yasitawalike. Hii likuwa ni hofu tu ya kupandikizwa au kutokuju. Na pia hii ilikuwa sio kweli walikuwepo wapinzani wao waliokuwa wakichochea uzushi maana walivyokuwa wanavigundua inspired by bible vilikuwa kinyume na wengi walivyokuwa wanafundishana based on classical Greece philosophies.
Narudia BIBLE AND SCIENTIFIC ACCURACY
Nimeisoma historia ya Europe vyema sana.Hapa mkuu kuna vitu vya kujifunza vingi kama Building ground kabla ya kujadili hiki ulichokileta(BIBLE(which inspired scientists) and Religious sect).
1:History of reformation Hasa kipindi cha Luther 1517–1521
2:Situation of the church that time of reformation
3:Formation of Jesuit order by ignatus loyola during reformation (spanish 1495 -1556)
4:The greatest war ever fought in history of europe (Thirty years war 1618-48)
5:The age of reasoning/ The enlightenment(1685-1815)
6:Industrial revolution 1760 -1840
Vyote hivyo vipo kwa mfuatano na vinaushawishi mkubwa kwa tunachojadili na Utagundua kwa upana hakuna uhusiano na USOMAJI WA BIBILIA ninaouzungumzia kwenye bandiko hili.
Mfano Huyu Bruno pamoja na Galileo wote walikuwa wanaresearch kile ambacho Copernicus alikiasisi. Lakini wote watatu walikikuwa inspired not by Church but Bible and its recommendation of studying nature. Kulikuwa na Vita vya kisayansi kati ya hawa na Pro-aristosle kama nilivyoongea mwanzoni huko. Chochote ambacho kingeonekana ni Uzushi na kuhatarisha uwepo wa organization ilikuwa ni kosa la kifo. Wengi waliuwawa sio kwa sababu ya Sayansi bali Hofu ya watawala(Kanisa) wanashindwa kuwatwala watu kama kirahisi tena wakianza kusoma bibilia wao wenyewe. Kuna reliable sources zinazosema sababu ya kuuwawa Huyo Bruno inawezekana isiwe tu kama unavyosema maana mbona Gallileo alisema hivyohivyo na akaongezewa mshahara na pope, lakn pro-aristotle scientists kwa kuona kijicho waliwashawishi wengi watawala ili aonekane anaeneza uzushi. Wengi waliuwawa Sio kwa kupinga bibilia bali kwa kupingana na taratibu za kanisa la kirumi. Usomaji wa bibilia kwa watu binafsi ulikuwa unahatarisha uwepo wa kanisa maana mambo mengi yalikuwa yanahojiwa. Ila wengi bibilia iliwafungua kichwa. Copernican was a creationist.
Mfano:Michael Servetus he studied bible at its orgin language which inspired him in his career. Remember he participated in protestant reformation.
Hoja ni BIBLE AND SCIENTISTS sio SCIENTISTS with the church affairs and interests or Scientists who were against Greece philosophic ideas. Nilijitahidi kuwa makini nisiingize taasisi wala chochote katikati ya Bibilia Na Scientists na hapa ndipo tunapojadili tena most of them creationsist.
Tuanzia hapo kwanza. Pitia zile Hints 6, ndio utajua what was going on in europe mida hiyo
kwa mujibu wa argument yako ulioleta miujiza ili kunullify dhumuni la mada. Mungu anahamasisha wanadamu wachunguze packages za his creative work. hii kazi ingeanza zamani tungekuwa mbali. nikatoa mifano ya hydrology, electromagnetism and telecomunicaton, cosmology, archtectural designing, sea transportation, mfano newton kapatent few constants ambazo zimesaidia revolutions za aironautics na space navigation, wind formation. hata wale brothers waliopatent aircraft invention were creationists trying to explore his creative powers. mbona mambo mepesi unataka kuforce ubishi ili iugurahishe moyo.Hahahaaa...naona una urge kisiasa sana.
Wewe unalazimisha watu tuamini kwamba Bibilia ingesaidia kuharakisha maendeleo ya kisayansi wakati Bibilia imesheheni mambo lukuki ambayo hayachunguziki kisayansi bali kuamini tu.
Je unaposema Bibilia ingefaa kutumika kama Scientific manual ili hali imejaa mambo yasiyochunguzika kisayansi, una maana kuwa sayansi ingebadili msingi wake wa kutafuta facts kutoka experiments kuja kwenye imani?
Bibilia haiwezi kupatana na sayansi kwa maana Bibilia imejaa mambo mengi yasiyochunguzika kitu ambacho ni kinyume na sayansi ambayo ni lazima ichunguze kila jambo.kwa mujibu wa argument yako ulioleta miujiza ili kunullify dhumuni la mada. Mungu anahamasisha wanadamu wachunguze packages za his creative work. hii kazi ingeanza zamani tungekuwa mbali. nikatoa mifano ya hydrology, electromagnetism and telecomunicaton, cosmology, archtectural designing, sea transportation, mfano newton kapatent few constants ambazo zimesaidia revolutions za aironautics na space navigation, wind formation. hata wale brothers waliopatent aircraft invention were creationists trying to explore his creative powers. mbona mambo mepesi unataka kuforce ubishi ili iugurahishe moyo.
Dunia inamchanganyiko wa kila aina ya Mlengo wa Maisha. Lakini Sayansi ni kitu ambacho kila kiumbe duniani kimenufaika nayo kwa kujua au kutokujua.
Ukisoma Bibilia kuna mambo ambayo Yangebadili kabisa dunia miaka mingi iliyopita na sio hizi karibuni. Pia ni kitabu sahihi kwa kufanya Scientific predictions.
Katika Bibilia kuna Ushahidi wa;
1PHYSICS;
AYUBU 38:19
anazungumzia Mwanga upo katika Njia (unatoka mahala flani) na Giza lipo katika nafasi.
Katika Phsics imethibitishwa mwanga unatembea kwa speed ya 299 792 458 m / s na spidi ya Giza ni 0. hadi karne ya 16 Dunia ilijua mwanga Huwa unatokea tu yaani upo hauko katika mwendo. Ni mwaka 1675 Sir Isaack newton alipogundua Light packets ambazo zinamove.
Mungu alikwa ameshayasema hayo miaka zaidi ya 3000 iliyopita na anasema aliumba yeye.
AYUBU38:35
Waweza kuutuma umeme, nao ukaenda, Ukakuambia, Sisi tupo hapa?
Umeme unatumika kutuma Ujumbe. Kila kinachofanyika katika mawasiliano ya yaani email, simu, kuchat, JF posting, Voice recording, sms, mawasiliano ya simu n.k ni Umeme.
Pia Umeme kwa maana ya RADI sio to ni flow of electricity bali pia inategeneza mawimbi la kielectromagnetiki (Electromagnetic Waves) ambazo zinatumika kusafirisha mawimbi ya sauti kutoka sehemu mija kwenda nyingine. Yote haya yalisemwa kwa mara ya kwanza zaidi ya miaka 4000 na Mungu akimweleza ayubu lakini karne ya 19 ndio walianza kugundua vitu hivi. Hata mwanasayansi NICOLA TESLA alipokuwa anajaribu kutuma signal (Umeme)huko marekani kwenye kituo chake, alishangaa anasikia sauti za ajabu akaanza kusema ni Maraika wanaongeo huko angani kumbe ilikuwa ni SIginal aliyokuwa anaipokea kutoka Italy ambapo mwenzak Marconi alikuwa anatest antena yake kurusha sauti kwa nji ya umeme.
2:OCEANOGRAPHY
Ayubu 38:16
Mungu anamuuluza ayubu ni nani aliyeumba za bahari? kwa kiebrania neno lilitoumika hi NEBEK kwa maana ya Chemchem ndani ya bahari. Hii ni Ushahidi kuwa Chini ya Mwamba ambayo juu yake kuna bahari au chini ya earths crust kuna maji mengi tu. Kama inavyoelezwa Mwanzo 7:11 Kipindi cha gharika mengine yalitoka chini.
Mwaka 1977 Scientists kutoka Origan state university waligungua Shooting ya maku kama chemichemi. sehemu panapoitwa Galapagos Maili 2 kutoka chini ya bahari watu wa oceanography wanaiita hii kitu GEOTHERMAL VENT. Baadae nyingine zikaonekana Indian Pacific na North atrantic. Mungu kayasema hayo zaidi ya miaka 4000 iliyopita.
MAHALI PA SIRI PA VILINDI
Zamani watu waliamini kutoka bara lingine kwenda lingine ni mchanga tu. 1875 waligundua kina chente 5.09 HMS CHALLENGER wanasayansi wa uingereza. 1899 USS NERO wakagundua kina chenye urefu wa 5.99 Miles Decemba 2011 British Royal Navy HMS CHALLENGER waligundua kina kirefu kabisa ambacho unaweza kuuweka mlima mzima wa Everest na bado ukawa hujafikia kwenye level ya sakafu ya bahari.
Haya Mungu kayasema miaka mingi kibao Yona 2:3
3:HYDROLOGY
Muhubiri 1:7, Zaburi135:7,Amos 9:6
Jinsi gani Maji ya Mito Uingia bahari na Kurudi ulikotoka. Huu mchakato mzima umekuja kuwa wazi na kuhesimiwa kama kitu cha kusomwa na kubadili maisha ya watu karne ya 17. Laiti kama sayansi ingejisalimisha kwa Maandiko ya Mungu zamani Haya mambo dunia hii ya leo ingekuwepo miaka ya 300bc.
4:MATEOROLOGY (Study of Atmosphere and Weather conditions)
Ayubu 38:24 kuna concept inaelezewa kuwa mwanga unasababisha Upepo.
Mwanga unatoka juani, unatanua hewa na kusababisha upepo duniani.
Muhubiri 1:6 Hapa panazungumziwa scientific concept iitwayo CORIOLIS EFFECT imegunduliwa 1912. Na hii Concept imesaidia pia kuinvent Baloon kama chombo cha usafiri. Karibu na Ikweta kuna joto na Kule Polar kuna baridi muhutasari wake Huo hapo chini.
PIa MITHALI 8:26
While as yet he had not made the earth, nor the fields, nor the highest part of the dust of the world. Mavumbi ya juu ya ardhi kutokana na Tafsiri ya kwanza ya kiebrania.
Tunapata kitu kinaitwa CONDENSATION NUCLEI yaani huko juu ya dunia kunahitajika vumbi ili mvua au mawingu yatokee. Bila hivyo hakuna mvua wala wingu litakalotokea. Mungu aliumba hivyo vyote. Na concept hii hii wanasayansi wako maabara kujaribu kutengeneza mvua Jangwani.Have scientists discovered how to create downpours in the desert? | Daily Mail Online
Yoote haya yameandikwa maelfu ya miaka ya nyuma kama wapenzi wa science wangependa kufuatilia hivi vitu Dunia ingekuwa hivi miaka mingi iliyopita.
5:ASTRONOMY/UNAJIMU
Isaya40:22 Dunia ni Duara. Yaani hili suala linasumbua watu kibao hadi kesho hadi humu JF. Na kuna wazushi wachache wakiongozwa na EVOLUTIONISTS JOHN DRAPER ANDREW DICSONWHITE waliingiza huu uongo zaidi miaka 1800. Na leo kuna chama duniani anakiongoza kinasambaza uongo dunia nzima kuiwa Dunia ni KAMA MEZA (Flat earth society).
Imeichukua dunia miaka kibao kujua siri iliyoandikwa kwenye mstari mmoja tu.
Pia YEREMIA33:22 Nyota haziesabiki. 1997 NASA haiwezekani kuhesabu nyota.
AYUBU 38:6-9 - Jee? Nyota zinaimba? Hii inatasiriwa kitheolojia tofauti lakini hata moja kwa moja ni kwamba Mwaka 1932 - NASA waligundua Nyota zinatoa RADIO WAVES na kuna mziki ndani yake. Na ni mziki ulio na mpangilio wa ajabu.Singing stars, huu ni mfano mdogo kabisa lakn tutarajie mengi.
Pia Dunia Inaelea, Ayubu 26:7 na ayubu 38:6
Hili linamethibitishwa miaka ya 1960 watu walipoanza kwenda anga za nje wakati tulishamaliza huu utata kwenye bibilia kitambo sana miaka 3000 Iliyopita. Kuna watu dini na wabishi wachache duniani walikuwa wanaamini dunia imebebwa na kobe hadi kesho wapo.
Dunia inaelea. haikuhitaji matrillion ya shillingi wakati ukweli huu upo zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Hapa ndio unapata connection ya sayansi na imani.
6:BIOLOGY
WALAWI17:11 --MAISHA YA KIUMBE YAKO KWENYE DAMU YAKE. Kwa maana nyingine ukiacha damu itoke kuna uwezekano huyo kiumbe akafa. Sasa Dec 14, 1799 rais wa marekani George Washington alikufa kizembe kabisa kwa Medical treatment ambayo ilijumuisha kumtoa huyo mgonjwa damu kama njia ya uponyaji(BLOOD letting). Watu mamia walikufa wakidhani wanaokolewa. Mungu kusema hiyo alijua anamaanisha nini.
Tumepoteza marafiki wengi katika ajali kwa kutokwa na damu nyingi.
bloodletting 1860
7:GEOMETRY na HESABU.
Ayubu 38:4,5 Ni nani aliyeamrisha vipimo vyake, kama ukijua? Au ni nani aliyenyosha kamba juu yake? Mungu ndiye Muanzilishi wa Hisabati, vipimo na Geometry.
2Nyakati 4:2 Hapa zinapigwa calculations. Katika hesabu hizi kutafuta mzingo haikutumika pai. waleta changamoto dhidi ya Mungu huwa wanatumia fungu hili kusema Mungu alikuwa haijui Pai. Wanasahau fungu hili 2Nyakati 4:5 wanashindwa kujua kulikuwa na duara mbili na kipenyo cha duara la ndani na la nje ni tofauti kwa kuzingatia unene kati ya maduara hayo 9.014 jibu utalopata ni sawa na mtu akitumia Pai. Pia Mungu aliwapa watu wachache vipaji vya heasbu katika ujenzi wa Hema ya kukutania na design nzima na kumtajia majina Musa watumie hao kukamilisha kazi yake huku akimpa dimensions na Materials ya kutumia kila kitu kikaenda kama kilivyopangwa.
8:GEOLOGY (Study of Rocks and earth)
Ukisoma Mwanzo7:8(Gharika dunia nzima), Mwanzo 7:18-19 (Maji yalicover dunia nzima), Mwanzo 7:21-23(wanyama,mimea,watu,vitu,ndge wote walifunikwa na kuzikwa chini ya maji), Mwanzo 7-8(Maji yalikaa juu ya uso wa dunia siku 371). Hili tukio ni kama Uchukue Jagi uweke maji kisha uchanganye udogo na michanga yenye sifa mbalimbali changanya kisha uache kwa muda kadhaa, utaona jinsi ambayo kuakuwa na matabaka yaliyojipanga kama sehemu nyingi za dunia zinavyoonekana.
9PALEONTOLOGY (study of fossil animals and plants)
Kama vitu vyote mimea,watu,ndege,wanyama na vitu vyote vilizikwa(Mwanzo7:22-23),Unategemea nini kwenye huu mchakato? Jibu ni Fossilization . Hiki kitendo kinahitaji Kifo cha ghafla, kuzikwa ghafla na Presha kubwa.Kwa ufupi tunategemea kukutana na Fossils katika hizo layers au matabaka ya miamba.Hii inahitaji gharika kutengeneza fossils vinginevyo wangebaki juu na kuoza.Utakutana na konokono, samaki tena wengine wakiwa wakiwa na mimba wengine katikati ya kuzaa wamekufa na kukauka katikati ya miamba.
10: CHEMISTRY
Watu binafsi hadi hapa tanzania wanaproject za kutengeneza mafuta, Kampuni uingereza wanatengeneza almasi kutoka kwa majivu vya umpendaye aliyekutoka, Kuna jamaa 1976 alitengeneza makaa ya mawe, Vyote hivi viliwezekana kwa concept za kilichotokea kwenye mafuriko ya nuhu. Ni rahisi na Muda mfupi sio miaka mamillioni kama tunavyoambiwa.http://www.lifegem-uk.com/
11:ARCHAEOLOGY
Kwa evolutionists makaa ya mawe alitokea miaka mamillioni yaliyopita kabla hata ya mtu, Ila leo ndani ya makaa ya mawe kumekutwa Cheni, Sarafu, silaha, vyombo vya kutumia, mikuki etc.Husikii vikitangazwa kwa sababu viko kinyume na wanavyofundisha madarasani. Vitu hivi na vingine vingi vinapatikana sehemu nyingi mno kila siku duniani na hadi wamefipa jina OOPARTS (Out of place artifacts). Haya yote ni matokeo ya tukio lililotokea miaka 4400 iliyopita TENA ZIMEKUTWA HADI SORE ZA VIATU KUNYESHA SIO MUDA MREFU ULIOPITA.
12:medicine
WALAWI11
Mtu yoyote akiguza kitu kilichokufa, au afue nguo zake kabla ya kufanya chochote anawe awe safi kwa maji. Ignaz Phillip Semmelwies . alikuwa director wa Viena general Hospital Austrial, Mwaka 1847 aligundua hadi asilimia 3o Ya wanawake waliokuwa wanajifungua walikufa. Hii asilimia ilikuwa sio huko tu bali hata ireland, UK ,US etc. Alizama kutafuta sababu na kugundua Madaktari waliokuwa wanawahudumia wajawazito. Wakitoka kumuandaa mama aliyekufa walinawa na damu kwenye maji hayohayo na wengine hawakunawa kwa sababu waliona haina sababu.Dunia ya sasa hakuna Daktari atakayetoka kwa maiti na kwenda kumuhudumia mgonjwa aliyehai bila kunawa au hata kubadili mavazi. Hii ilikuwa ni matokeo ya utafiti wa huyu Ndugu lakini Mungu alishawaelekeza jamaa zamani sana.
Sayansi na biblia ni kama East and West. Haviendani kabisa. Katika concepts nyingi na methodologies za interpretation.
Pia katika vitabu vya imani vilivyotumika katika science ni Vedas na Eastern Spirituality. Zimezidi Biblican ideologies katika kuleta elimu. Mfano Tesla alipata wazo la Free Energy kutoka kwa Swami Vevakananda aliyekuwa mwalimu wa kihindi na explorer. Alimpa idea ya free energy exists na Tesla akaweza kuprove kwa kugundua umeme. Akaita kiini cha umeme AKASHA, ni neno la kihindu linalomaanisha the core of energy. Huo ni mfano mmoja wenye ushahidi.
Nipatie ugunduzi au elimu iliyopatikana kwenye biblia, nipatie na jina la mwanasayansi aliyetumia.
Elimu iwe unique kwenye biblia tu, yaani iwe imepatikana kwenye bible tu. Kwa sababu mpaka leo sijaona. Na pia kanisa now days linadanganya kuwa biblia inasema dunia inazunguka jua na inajizungusha na jua ndio centre of the universe na bible imesema hivyo, lakini sio kweli. Christianity haikujua elimu hiyo na ni mojawapo ya dini zilizojua dunia ni flat na inazungukwa na jua. Just like Quran nayo ilivyokosea. Na waliua wengie waliosema dunia ni duara na leo hii mnasema bible said its round. Then why killing of scientists kama biblia ni scientific!
Pia usisahau kuna zaidi ya scientific contradiction 100 kwenye bible.