Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,030
- 20,391
AINA KUU 2 ZA MADENI.
Tokomeza madeni.
Kuna aina kuu mbili za madeni.
Aina ya kwanza ni madeni mazuri na aina ya pili ni madeni mabaya.
Soma kwa makini ili kujua unaangukia kwenye aina gani ya madeni.
Madeni mazuri ni yale ambayo marejesho yake hayatokani na chanzo kingine cha mapato bali deni linajilipa lenyewe.
Madeni mabaya ni yale ambayo malipo yake yanatokana na chanzo kingine cha mapato.
Kwa mfano. Umekopa pesa benki na kujenga nyumba, halafu unatarajia kulipa deni hilo kwa kukatwa mshahara wako, hilo deni ni baya.
Kama umekopa pesa ili ulipe ada ya shule, hilo deni ni baya kwa kuwa utalazimika kutumia pesa nyingine kutoka sehemu nyingine ili kuja kulipa deni lako.
Matajiri wengi wana madeni mazuri, kwa sababu wanakopa ili kuzalisha.
Maskini wengi wana madeni mabaya, wanakopa pesa halafu wanaitumia kisha wanaanza kuhangaika kurudisha deni hilo.
Hii husababisha watu kushindwa kusonga mbele kwa kuwa muda mwingi unautumia kulipa deni ambalo pesa yake ulishaitumia pasipo kuizalisha.
Sasa kwa kuwa umeelewa tofauti hizo unaweza kujifanyia tathmini...
Je binafsi uko kundi gani? Na mara nyingi umekuwa ukiishi na madeni mazuri au mabaya?
Tokomeza madeni.
Kuna aina kuu mbili za madeni.
Aina ya kwanza ni madeni mazuri na aina ya pili ni madeni mabaya.
Soma kwa makini ili kujua unaangukia kwenye aina gani ya madeni.
Madeni mazuri ni yale ambayo marejesho yake hayatokani na chanzo kingine cha mapato bali deni linajilipa lenyewe.
Madeni mabaya ni yale ambayo malipo yake yanatokana na chanzo kingine cha mapato.
Kwa mfano. Umekopa pesa benki na kujenga nyumba, halafu unatarajia kulipa deni hilo kwa kukatwa mshahara wako, hilo deni ni baya.
Kama umekopa pesa ili ulipe ada ya shule, hilo deni ni baya kwa kuwa utalazimika kutumia pesa nyingine kutoka sehemu nyingine ili kuja kulipa deni lako.
Matajiri wengi wana madeni mazuri, kwa sababu wanakopa ili kuzalisha.
Maskini wengi wana madeni mabaya, wanakopa pesa halafu wanaitumia kisha wanaanza kuhangaika kurudisha deni hilo.
Hii husababisha watu kushindwa kusonga mbele kwa kuwa muda mwingi unautumia kulipa deni ambalo pesa yake ulishaitumia pasipo kuizalisha.
Sasa kwa kuwa umeelewa tofauti hizo unaweza kujifanyia tathmini...
Je binafsi uko kundi gani? Na mara nyingi umekuwa ukiishi na madeni mazuri au mabaya?