Fahamu aina kuu mbili za Madeni

Fahamu aina kuu mbili za Madeni

Kasomi

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2014
Posts
11,030
Reaction score
20,391
AINA KUU 2 ZA MADENI.

Tokomeza madeni.


Kuna aina kuu mbili za madeni.

Aina ya kwanza ni madeni mazuri na aina ya pili ni madeni mabaya.

Soma kwa makini ili kujua unaangukia kwenye aina gani ya madeni.

Madeni mazuri ni yale ambayo marejesho yake hayatokani na chanzo kingine cha mapato bali deni linajilipa lenyewe.

Madeni mabaya ni yale ambayo malipo yake yanatokana na chanzo kingine cha mapato.

Kwa mfano. Umekopa pesa benki na kujenga nyumba, halafu unatarajia kulipa deni hilo kwa kukatwa mshahara wako, hilo deni ni baya.

Kama umekopa pesa ili ulipe ada ya shule, hilo deni ni baya kwa kuwa utalazimika kutumia pesa nyingine kutoka sehemu nyingine ili kuja kulipa deni lako.

Matajiri wengi wana madeni mazuri, kwa sababu wanakopa ili kuzalisha.

Maskini wengi wana madeni mabaya, wanakopa pesa halafu wanaitumia kisha wanaanza kuhangaika kurudisha deni hilo.

Hii husababisha watu kushindwa kusonga mbele kwa kuwa muda mwingi unautumia kulipa deni ambalo pesa yake ulishaitumia pasipo kuizalisha.

Sasa kwa kuwa umeelewa tofauti hizo unaweza kujifanyia tathmini...

Je binafsi uko kundi gani? Na mara nyingi umekuwa ukiishi na madeni mazuri au mabaya?
 
Madeni ya Samia yanaangukia wapi
Madeni mabaya.

Hii ni kwasababu Yanatumika kuwafaidisha wao kwa kiwango kikubwa wakati ulipaji wake unatokea kwa kukatwa na kupandishiwa kodi wananchi.
 
Binafsi nipo kwenye madeni mabaya baada ya kukopa m pawa wanataka kunitoa roho.
Na hapo ukute ulikopa ukanunua K vant lakini kulipa utalipa kwa mapato ya kodi ya nyumba.
 
Usiogope deni, kwa kuwa deni ni ishara ya kupambana. Isitoshe deni halimfungi mtu, we kopa tu!
 
Mkuu, hebu tuangalie mfano huu: mtu amekopa bank hela ya kutosha kijenga nyumba ya kuishi familia. Deni hili analilipa kwa fedha za mshahara wake kwa kipindi cha miaka sita, ambapo anamaliza kulipa deni na riba yake. Na tukumbuke materials zinapanda bei mara kwa mara, hivyo, vifaa ( materials) alizonunua leo, bei yake itakuwa tofauti na atakaponunua miaka sita ijayo, maana bei itapanda sana. Je, hili nalo ni deni baya (bad debt)?

Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu, hebu tuangalie mfano huu: mtu amekopa bank hela ya kutosha kijenga nyumba ya kuishi familia. Deni hili analilipa kwa fedha za mshahara wake kwa kipindi cha miaka sita, ambapo anamaliza kulipa deni na riba yake. Na tukumbuke materials zinapanda bei mara kwa mara, hivyo, vifaa ( materials) alizonunua leo, bei yake itakuwa tofauti na atakaponunua miaka sita ijayo, maana bei itapanda sana. Je, hili nalo ni deni baya (bad debt)?

Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
Japo atakuwa amejisaidia kuepukana na Bei kubwa kwa wakati ujao, lakini deni hilo litabaki kusimamia kwenye upande wa deni baya(Hii ni kwamjubi wa hoja hapo juu).

Sababu ni kwamba deni atalipa nje ya alicho zalisha kutoka kwenye deni lake.
 
Back
Top Bottom