Fahamu Aina za Kodi Zinazotozwa Pindi unapoingiza Gari Nchini

Fahamu Aina za Kodi Zinazotozwa Pindi unapoingiza Gari Nchini

zachaja

Senior Member
Joined
May 16, 2015
Posts
153
Reaction score
198
Kodi zifuatazo hutozwa kwenye magari yanayoingia nchini;

1. Ushuru wa forodha (Import Duty): asilimia 25% ya thamani ya kununulia gari (CIF Value)
2. Ushuru wa bidhaa (Excise Duty due to CC-EX): asilimia 0%, 5% & 10% kutegemea na ukubwa engine (chini ya 1000cc= 0%, cc 1000 mpaka 1,999=5% & cc zaidi ya 2000= 10%) ya thamani ya gari (CIF) PLUS Ushuru wa Forodha.
3. Uchakavu (Excise Duty due to Age-EXA): asilimia 15% & 30% kutegemea na na umri (zaidi ya miaka 3 na chini ya miaka 8= 15%, zaidi ya miaka 10 toka litengenezwe= 30%) ya thamani ya gari (CIF) PLUS Ushuru wa Forodha.
4. Ushuru wa maendeleo ya Reli (Railway Development Levy-RDL): 1.5% ya thamani ya gari (CIF).
5. Tozo ya Forodha (Customs Processing Fee-CPF):0.6% ya thamani ya gari bila Bima (FOB).
6. Ada ya Usajiri (Motor Vehicle Registration Fee-VEH): TZS-450,000, TZS-500,000 & TZS-550,000 hapa inategemea na ukubwa wa Engine.
7. VAT:18% ya Thamani ya gari (CIF) PLUS kodi zote zilizokokotolewa hapo juu.

NOTE:
a). Kwa magari mapya (gari lisilozidi miaka 3) hayatozwi kodi ya uchakavu
b). Magari yanayotumia umeme hayatozwi kodi ya ushuru wa bidhaa.

“Kwa huduma bora zifuatazo karibu Ruaha Freight Ltd;
1. Clearing & Forwarding kwa mizigo aina yote (Magari, container & Loose Cargo),
2. Kusaidia kuhamisha umiliki wa vyombo vya moto (Motor vehicle ownership transfer-Dar pekee).
 
Mamlaka zinanyanyasa wananchi kwenye upande wa kodi hapa [emoji1430]
 
Kwa style hii sjui kama ntamiliki gari
IMG_20240114_094749.jpg
 
Back
Top Bottom