Fahamu artificial intelligence (AI)

Fahamu artificial intelligence (AI)

Swahili AI

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2016
Posts
10,174
Reaction score
89,364
Katika maisha yetu ya leo, kwa namna moja au nyingine tunatumia Artificial Intelligence- intellijensia ya kutengenezwa(Sijapata Kiswahili Fasaha, wana jamvi waweza saidia) kupitia vifaa vya kieletroniki kama simu, computer, luninga n.k.

Artificial Intelligence (AI) ni nini?
Mwaka 1956, mwana sayansi John McCarty akiwa kwenye mkutano wa Dartmouth alifafanua AI kama sayansi ya kutengeneza mashine ili kufanya kazi na kutenda/kuenenda kama binadamu.

Lakini AI imekua na uhusiano wa moja kwa moja na masiha yetu ya kila siku kupitia vifaa vya kielektroniki tunavyojihusisha navyo katika masiha yetu ya kila siku.

Kwa namna gani?
Unaweza ukawa unajiuliza hivyo, Je ushawahi jiuliza kwanini search engines kama GOOGLE inaweza kukupa matokeo sahihi ya kile unachokiuliza au kukitafuta kupitia mtandao wao?

Zile post feed za instagram au facebook unazopenda kuziangalia ndizo watakazokuletea kwenye search page yako?

Zile suggestions(mapendekezo ya marafiki au matangazo au watu wakuwafuata(follow) mitandao ya kijamii inayokuletea inatokana na nini?

Mfano SIRI na Google Assistant zinavyokuletea matokeo kwa kile unachokihitaji?

Ni kwamba AI ime-base sana kukusanya data katika masiha yetu ya kila siku, hivyo katika ukusanyaji wa data kutoka kwa binadamu ndivyo hivyo mashine hizo zinachakata data hizo na kuzihifadhi kwa matumizi ya baadae kwa watumiaji wa vifaa ivyo pamoja na huduma toka kwenye kifaa husika.

Aina za AIs - Zipo 3.
1. Artificial Narrow intelligence

Aina hii inahusika sana na intelijensia kwa kazi kwa lengo fulani tu, pia hufaamika kama intelijensia dhaifu. Mfano mzuri ni Alexa ambapo.

ina uwezo wa kutambua mwingiliano wa sauti, uchezaji wa muziki, kutengeneza orodha za kufanya, kuweka kengele, utiririshaji wa podcast, kucheza vitabu vya sauti, na kutoa hali ya hewa, trafiki, michezo, na habari zingine za wakati halisi, kama habari. Alexa inaweza pia kudhibiti vifaa kadhaa mahiri ikitumia yenyewe kama mfumo wa kiotomatiki wa nyumbani.
Mfano mwingine ni FACE ID kwenye simu janja, Kuendesha magari/ndege bila dereva.

2. Artificial General Intelligence
Hii ni intelijensia yenye nguvu sana ambapo inahusisha uwezo wa kufanya kazi nyingi za kutumia akili ambazo mwanadamu wa kawaida anaweza kuzifanya.

Mashine zinazotumia aina hii ya AI zina uwezo wa kufanya kazi za kibinadamu na kutumia kaili bila kuwa na uwezo kufikiri kama binadamu. Kwa mfano michezo kama karata, Draughts( maarufu kama drafti) kwenye kompyuta au simu zetu

3. Artificial Super Intelligence.
Aina hii sasa ina uwezo wa kufanya kazi kwa kiwango cha juu sana kupita uwezo wa kibinadamu. Mchawi wa teknolojia, Elon Musk anaamini kwamba ifikapo mwaka 2040 ASI ita-take over dunia nzima.

Itaendelea....
 
Mada kama hizi zinatakiwa ziwe Sticky lakini sijui JF inakwama wapi..

Naomba mum tag moderator yeyote aiweke hii mada Sticky ili iwe inajadiliwa mara kwa mara tafadhali

Okay ngoja niweke nondo zangu ambazo ninazojua kuhusu Artificial Intelligence

Dunia sasa hivi ina evolve sana katika matumizi ya Artificial Intelligence

Ikumbukwe Artificial Intelligence inatumika maeneo mbalimbali sana kuanzia kwenye Autonomous mpaka kwenye IoT

Kinachonisikitisha ni kwamba Giants wa tech ndio wanawekeza sana kwenye AI na inaanza kuwalipa

Like wamekwenda mbali kwa maana wameweza tengeneza vitu mbalimbali ambavyo msingi wake ulianza kwenye AI

Leo hii tunaona Google wana Waymo as Autonomous project from them

Amazon wamedevelop Alexa as Virtual Assistance

Mie mwisho ninakuja kusema kuwa sisi Africa bado tumelala

Hivi tumeshindwa nini kutengeneza our own Alexa version
Kwa maana Virtual Asiistance

Tumeshindwa nini kuja na mfumo huu ambao tunaweza uza kwa third part companies kuanzia IoT mpaka kwenye Autonomous

Amazon wamepanga Alexa ku run everyday life of human being

Africa tumeshindwa kuanzisha kitu kama hichi

Costech mpo?
Silicon Dar?
Tech hubs mpo? Au mko busy na health projects [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Kuna mengi sana tunatakiwa tujifunze na kwamba tuweze kuumiza vichwa vyetu

I believe kuna beautiful souls down there ambao kwa namna moja au nyingine wana mpango wa kuja na AI projects

Niwaambie ukweli pursue your dreams na siku zote ndoto huwa reality

Africa tunaweza sio kila siku wazungu tu
 
🥰🥰🥰 big up tunawatu wachache wenye kufikiri sawasawa
 
Yote haya kama msomeshe mtoto software engineering.ndo utajua matunda ya mwanao,sio unasomesha tu IT .baba lao ni software engineering unaweza kujitegemea na ukakataa ajira.huku zaidi ya wale waokota makombo
IMG_4421.jpg

IMG_4423.jpg


IMG_4424.jpg

IMG_4422.jpg


Na zaidi
 
Ev
Yote haya kama msomeshe mtoto software engineering.ndo utajua matunda ya mwanao,sio unasomesha tu IT .baba lao ni software engineering unaweza kujitegemea na ukakataa ajira.huku zaidi ya wale waokota makombo
View attachment 1733872
View attachment 1733874

View attachment 1733875
View attachment 1733876

Na zaidi
Hata IT ni good starting point kwamaana AI field its like independent field kinachotakiwa ni programing skills so mtu mwenye IT anaweza explore vizuri Sana bila kupata shida yoyote
 
Back
Top Bottom