Part Asifiwe kilen Malila
Member
- May 16, 2022
- 22
- 57
Siku ya Leo nitazungumzia juu ya madhara ya marafiki wabaya na kuwa nao katika maisha yako. Kwa kawaida katika maisha Kuna rafiki mzuri na rafiki mbaya ,sifa za rafiki mzuri ni kama kutunza Siri, uaminifu, uwazi, upendo na kutokuwa mnafiki.
Yafuatayo ni madhara ya marafiki wabaya ktk maisha:
1. Marafiki wabaya huvujisha Siri; watu wengi ktk jamii zetu za Kila siku wamekuwa wakilizwa na marafiki,washikaji na hata ndugu zao wa Karibu Kwa sababu wanawapatia Siri zao na mwisho kuzivujisha. Kulingana na moja ya mafundisho ya Joel nanauka alipozungumzia kuhusu aina za maadui ,alieleza kuhusu adui Delilah ambaye huchukua Siri na kuzitoa nje. Hivyo rafiki mbaya hutoa siri na kuzivujisha.
2. Marafiki wabaya humfanya mtu kuingia katika makundi mabaya; wazazi na walimu wamekuwa wakilaumiwa na wanajamii kuhusu watoto wao na tabia zao bila kujua kwamba tabia za marafiki wa watoto hao ndizo huchochea mabadiliko ya watoto wao.Mathalani makundi maovu kama ya wizi, ukahaba na madawa ya kulevya huvutia vijana Kwa sababu hupata pesa Kwa haraka sana na hivyo watoto hujihusisha na makundi hayo.
3. Marafiki wabaya ni chanzo cha kuvunjika Kwa mahusiano ya watu; suala hili linaonekana Kwa wanavyuo wengi ambapo marafiki wanaovujisha Siri na wachonganishi wamekuwa wakivujisha Siri na kupeleka maneno yasiyo ya kweli baina ya pande mbili hivyo hufanya mahusiano kuharibika katika jamii.
4. Marifiki wabaya huchochea usaliti na chuki; suala hili linaonekana hata katika mitaani kwetu ambapo marafiki huingia katika chuki na usaliti baada ya kuchonganishwa. Hivi Sasa jambo hili linaonekana Kwa wasichana ambao huitana "mashosti" lakini baadae huingia katika chuki na usaliti mkubwa.
NB: Kwa ujumla marafiki ni muhimu kutazamwa kwani ni moja kati ya vigezo vya kuzingatia katika maisha na ndio maana waingereza husema show me your friends and I will tell who you are! Asanteni. Tafadhali unaweza ongeza hasara nyingine unazofahamu
Yafuatayo ni madhara ya marafiki wabaya ktk maisha:
1. Marafiki wabaya huvujisha Siri; watu wengi ktk jamii zetu za Kila siku wamekuwa wakilizwa na marafiki,washikaji na hata ndugu zao wa Karibu Kwa sababu wanawapatia Siri zao na mwisho kuzivujisha. Kulingana na moja ya mafundisho ya Joel nanauka alipozungumzia kuhusu aina za maadui ,alieleza kuhusu adui Delilah ambaye huchukua Siri na kuzitoa nje. Hivyo rafiki mbaya hutoa siri na kuzivujisha.
2. Marafiki wabaya humfanya mtu kuingia katika makundi mabaya; wazazi na walimu wamekuwa wakilaumiwa na wanajamii kuhusu watoto wao na tabia zao bila kujua kwamba tabia za marafiki wa watoto hao ndizo huchochea mabadiliko ya watoto wao.Mathalani makundi maovu kama ya wizi, ukahaba na madawa ya kulevya huvutia vijana Kwa sababu hupata pesa Kwa haraka sana na hivyo watoto hujihusisha na makundi hayo.
3. Marafiki wabaya ni chanzo cha kuvunjika Kwa mahusiano ya watu; suala hili linaonekana Kwa wanavyuo wengi ambapo marafiki wanaovujisha Siri na wachonganishi wamekuwa wakivujisha Siri na kupeleka maneno yasiyo ya kweli baina ya pande mbili hivyo hufanya mahusiano kuharibika katika jamii.
4. Marifiki wabaya huchochea usaliti na chuki; suala hili linaonekana hata katika mitaani kwetu ambapo marafiki huingia katika chuki na usaliti baada ya kuchonganishwa. Hivi Sasa jambo hili linaonekana Kwa wasichana ambao huitana "mashosti" lakini baadae huingia katika chuki na usaliti mkubwa.
NB: Kwa ujumla marafiki ni muhimu kutazamwa kwani ni moja kati ya vigezo vya kuzingatia katika maisha na ndio maana waingereza husema show me your friends and I will tell who you are! Asanteni. Tafadhali unaweza ongeza hasara nyingine unazofahamu