Fahamu jinsi ya kutengeneza chakula chako cha kuku ili kupata faida

Fahamu jinsi ya kutengeneza chakula chako cha kuku ili kupata faida

theriogenology

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2016
Posts
8,748
Reaction score
15,681
JINSI YA KUJITENGENEZA CHAKULA CHA KUKU NYUMBANI KWA AJILI YA KUONGEZA UZALISHAJI

Kutokana na kuongezeka kwa gharama za chakula cha kuku iwewawia vigumu wafugaji wa kuku kupata faida kupitia ufugaji wa kuku. N akwa jinsi utengenezaji wa chakula cha kuku hasa hasa kuku wa kisasa kama broiler na layers kwa wafugaji ni ngumu leo nakuja na somo jepesi la jinsi ya kutengeneza chakula kwa kuku chotara (hybrid) or kuku wa kienyeji wanaofugwa ndani ya banda kwa kutumia Pearson Square method nah ii yote yawezekana kama mkulima atakuwa na raw materials zinazohitajika katika utengenezaji wa chakula.

Njia HII ya pearson square mara nyingi ina base sana katika Digestable crude protein (DCP) ya malighafi husika katika utengenezaji wa chakula. Na malighafi zinazotahitajika hapa ni kama vile Mahindi, mashudu ya pamba, mashudu ya alzeti, maharage ya soya na dagaa.

Jinsi ya kutengeneza chakula cha kuku wa mayai (70kg) (chotara) unahitaji vifuatavyo;

34 kg Mahindi
12 kg Soya beans
8 kg Dagaa
10 kg pumba za mahindi
6 kg Chokaa (kwa ajili ya calcium)

Jinsi ya kutengeneza chakula(70kg) kwa ajili ya kuku wa nyama

Mahindi= 40 kg
Dagaa = 12 kg
Maharage ya soya = 14 kg
Chokaa = 4 kg

NB: Hakikisha unaongeza chumvi 250g katika kila mfuko wa 70kg wa chakula chako

Ndondoo muhimu ya jinsi ya kuwalisha kuku wako Nyumbani

Kuku anaetaga mayai anahitaji kula angalau 130g za chakula kwa siku. Kumbuka kuwapa maji masafi muda wote.

Kifaranga kimoja anahitaji 2.2 kg za chakula kwa wiki 8 (hivyo basi vifaranga 100 = 2.2 kg x 100=220 kg. Vifaranga wanahitaji kula muda wote na pia suala la maji ni muhimu kwao pia na unakumbushwa kuwapa mboga mboga baada ya mlo wao kuisha.

Kuku mdogo anayekaribia kutaga anatakiwa kula 4.5 kg ya chakula kwa muda wa miezi miwili na nusu mpaka watakapoanza kutaga yai kwa mara ya kwanza. Baada ya hapo wanabadilishiwa chakula na kupewa chakula cha utagaji (layer diet).

Malighafi zinazotakiwa katika utengenezaji wa chakula zinatakiwa zile za kiwango cha juu kabisa usitumie mahindi yenye uozo maana utafanya kuku wako kupata ugonjwa wa aflatoxins poisoning.

Ukitumia dagaa hakikisha ni wasafi na hawana mchanga ama shells wa aina yoyote.

Na mwisho hakikisha chakula hicho unakichanganya vizuri kabisa ili kuleta uwiano au mchanganyo ulio sahihi.

Hitimisho
Kwa formular za Chakula za Kuku wa kisasa kama Broiler na Layer tunaweza wasiliana kwa namba zangu hapo chini na hakika zitakuongezea uzalishaji maradufu ya chakula cha kununua.

Imeandaliwa na Dr of Veterinary Medicine

Nami naomba nichangie kiduchu ingawa mleta uzi amajibu kwaa usahihi na kwa ufupi unaoleweka.

Kung'atana kitaalamu wanaita "cannibalism" hii ni moja ya tabia mbaya kwa kuku wanaofugwa muda mwingi wakiwa ndani.
Hii hutokana na baadhi ya haya yafuatayo

1. Kukosa madini lishe kama fosiforasi na kalisiam, madini haya hupatikani kwa wingi kwenye unga wa mifupa na chokaa ya mifugo.

2. Msongo(Stress), hii hutokana na Msongamano ama mrundikano wa kuku (kuku wengi eneo dogo).

3. Kuweka kuku wa umri tofauti ndani ya banda moja, hii usababisha kuku wakubwa kupiga na kuwadonoa kuku wadogo.

Tiba na kinga.
1. Kuwapa chakula chenye uwiano sahihi wa chokaa na unga wa mifupa.

2. Kuwaongezea nafasi ili wawe na eneo pana la kucheza kuepusha kusongamana.

3. Wapatie mchanganyiko wa maji na vitamini(Anti-stress) kwa kipindi kilichoelekezwa katika mfuko ama kibandiko.

3. Kuwafungia majani ama mboga za majani ili wapate sehemu ya kupunguzia msongo kwa kula majani yaliyo ning'inia.

4. Kuwatenga walioathirika haraka sana maana kuku anapoona damu ile sehemu itashambuliwa sana, kwa hiyo unapomtenga muathirika unaokoa maisha yake.

5. Mpe huduma ya kwanza kuku aliyeathirika kwa kumpaka "iodine tincture" na kumpa mchanganyiko wa maji na vitamini (kipunguza msongo ama "anti-stress").
 
Vifaranga Wangu walikuwa wana toa kama maj maj mdomoni then miguu kama imekauka. Akishaanza hivyo anakufa haraka. Walikuwa na wiki 3 chanjo ya kideri nilishawapa nikawapa na OCT lakn vifo vikawa palepale. Hiyo shida ni ya nini?
 
Vifaranga Wangu walikuwa wana toa kama maj maj mdomoni then miguu kama imekauka. Akishaanza hivyo anakufa haraka. Walikuwa na wiki 3 chanjo ya kideri nilishawapa nikawapa na OCT lakini vifo vikawa palepale. Hiyo shida ni ya nn?
Hiyo chanjo ya kidelii uliowapa ni ile ya kuchanganya katika maji or ya tone la maji katika jicho?
 
Kwa Vifaranga wa siku had wiki vp maana naona wanapata sana shida ya kula. Huwa nawapa unga mlain.
Dagaa hawawez kula.
Hata pumba ni shida.

Cha kula gan kinaweza kuwa sahh kwao?
Kwa upande wa vifaranga wanahitaji chick mash ambayo hupatikana dukani na kama kuku wako ni chotara na layers then utawalisha for 8 weeks na kama ni broiler then unatakiwa uwape hicho kwa wiki 3 then starter kuanzia 3-6 then umalizie na finisher.

Ila niko na formular ya starter ila itabidi niku charge ukihitaji.

Karibu sana
 
  • Thanks
Reactions: Ok9
Back
Top Bottom