Fahamu kama namba yako ya NIDA ilitumika kusajili laini za simu usizozifahamu kwa mawakala wajanja wa kusajili laini

Hellow, naomba kuuliza coz na mm ni muhanga,
Je, nikitumia option ya remove, inamaana namba ake unafungwa tena. Or hadi nikachome Customer care

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaweza kuzifuta ila hakikisho nenda kwenye shop ya huo mtandao Unaweza kuta jamaa alotumia line kwa ajili yako ameshaifanyia utapeli.
 
tuma hela kwenye namba hii jina litakuja Big Soap. ni kamchezo kanacho endelea. mawakala wa usajiri wanapoteza uaminifu. yaani wanakwambia weka tena kidole (finger print) kumbe ushasajirishwa line bila kujua. piga *106# akiki nambazi zilizosajiliwa na kitambulisho chako. msaidie ndugu zako na watu wa karibu kuhakiki. asante
 
N Nenda shop yao ukazifunge
 
Msaada. Kama unataka kuangalia namba Zote za mitandao Zote zilizosajiliwa na Nida yangu nafanyaje. Km MTU kasajili na halotel na Nida yangu Mimi Sina halotel laini kuhakiki nitajuaje?
 
Msaada. Kama unataka kuangalia namba Zote za mitandao Zote zilizosajiliwa na Nida yangu nafanyaje. Km MTU kasajili na halotel na Nida yangu Mimi Sina halotel laini kuhakiki nitajuaje?
Piga,*106# kisha chagua ANGALIA NAMBA ZILIZOSAJILIWA MITANDAO YOTE
 
Msaada. Kama unataka kuangalia namba Zote za mitandao Zote zilizosajiliwa na Nida yangu nafanyaje. Km MTU kasajili na halotel na Nida yangu Mimi Sina halotel laini kuhakiki nitajuaje?
Piga *106#
Then kuna Sehemu wanakupa option ya kuondoa hiyo namba
 
Shukurani sana mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…