Fahamu kama namba yako ya NIDA ilitumika kusajili laini za simu usizozifahamu kwa mawakala wajanja wa kusajili laini

Fahamu kama namba yako ya NIDA ilitumika kusajili laini za simu usizozifahamu kwa mawakala wajanja wa kusajili laini

Ubarikiwe kwa elimu nzuri sana,,,,Ila october usikubali kutumiwa kama ambavyo umekuwa mzalendo kutuelimisha kuhusu uhakiki..Vivyo hivyo ukafanye uzalendo kwa kusimamia uchaguzi eneo lako ukawe huru na wa haki. Ukifanya wewe mema. Mungu atakuona na atakubarikia uzao wako wote.
Wasalaam.

Ili kujua unabonyeza *106# kisha usajili wa NIDA (Utaingiza NIDA ID yako), baada ya hapo zitakuja namba zote zilizosajiliwa kwa ID yako ya NIDA. Kama namba haijui siyo yako maana yake wakala (agent) alifanya ujanja kutumia ID yako kusajili line nyingine.

Ukishaona kwenye list namba haijui basi unaenda kwenye shop iliyokaribu nawe una claim, then customer care anakuambia uweke finger print kisha hiyo namba inafutwa.

Kutokana na watu wengi kutokuwa na NIDA, mawakala wengi walitumia ujanjaujanja wa kusajili line kwa kutumia ID ya mtu mwingine na kuuza hizo line kati ya elfu 5 hadi elfu 20, inategemea watakavyokuona na uhitaji wako.

Mawakala wanafanyaje ujanja? Ukienda kusajili line yako atakwambia weka dole gumba lako baada ya dakika atakwambia network inasumbua hebu ingiza tena, ukifanya hivyo basi hapo jua umeumia, ile ya kwanza amesajili line ya mtu mwingine na ya pili anasajili line yako, kama haujui hiyo mbinu hauwezi kumstukia maana wapo very smart.

Kwahiyo, wote mlionunua line kwa mawakala zilizosajiliwa kwa NIDA maarufu kama Take Away, mjiandae kisaikolojia.

Utabonyeza mbili halafu utaweka namba yako ya NIDA, mwisho utatumiwa SMS ya namba zako zote ulizozisajili kama kuna namba haujaisajili utaenda kwenye shop yoyote ya kampuni ya simu ambayo wewe ni mteja wao halafu utapewa fomu ya ku-remove namba ambazo huzitambui.



Jumanne NJEMA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ubarikiwe kwa elimu nzuri sana,,,,Ila october usikubali kutumiwa kama ambavyo umekuwa mzalendo kutuelimisha kuhusu uhakiki..Vivyo hivyo ukafanye uzalendo kwa kusimamia uchaguzi eneo lako ukawe huru na wa haki. Ukifanya wewe mema. Mungu atakuona na atakubarikia uzao wako wote.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nitasimamia kwa haki mkuu ....nina hofu ya Mungu zaidi nitatimiza matakwa ya kisheria na kufuata katiba ...
 
Asee nimecheki nimekuta kitambulisho changu imesajili namba ambazo sizijui 2 daaah!!Bora wamehtukia maana mtu unaweza kuja jikuta kwenye matatizo kwa line ambayo imesajiliwa kwa jina lako.
 
Back
Top Bottom