Fahamu kinachojiri kuhusiana na kirusi cha Corona (Coronavirus)

Wewe unaamini Corona haijatua Africa mpaka sasa?
Uwezekano ni mkubwa. Lakini sidhani hadi upimaji umehibitishwa (kuamini kwangu ni kwa Mungu na mke wangu).
Misri imethibitishwa. Nchi nyingine uwezekano ni mkubwa.
Nimesoma juzi jinsi gani msafiri mmoja alileta ugonjwa Italia akiambukiza watu 200 hadi kupimwa mwenyewe; nikikumbuka vema yeye hakusikia tatizo ila wengine waligonjeka na wote walikutana na huyu basi alipimwa. Anajisikia mzima lakini aliambukiza.
Sidhani inazuilika.
Virusi siogopi. Lakini hofu yake inaweza kuleta mabaya.
 
UPDATE: Uswisi imeripoti kisa cha kwanza cha COVID-19 nchini humo.

Hii leo hadi hivi sasa, nchi zipatazo tano (5) barani Ulaya zimeripoti visa vipya vya COVID-19 katika nchi zao;
  • Austria
  • Italia
  • Croatia
  • Uswisi
  • Uhispania
 
UPDATE: Kumekuwa na taarifa za ongezeko kubwa la bei za bidhaa na vifaa mbalimbali vinavyotumika kujikinga na virusi vya Corona kama vile maski n.k. katika nchi kadhaa duniani.

Mamlaka za baadhi ya nchi hizo zimeanza kuchukua hatua za kiuchunguzi kuhusiana na ongezeko kubwa la bei za bidhaa hizo muhimu hususani kipindi hiki.
 
NEWS ALERT: Italian authorities have begun an investigation into rocketing online prices for hygienic masks and sanitizing gels following the coronavirus outbreak in northern Italy, two senior magistrates said on Tuesday. [Reuters]
 
UPDATE: Bahrain imeripoti visa vipya sita (6) vya COVID-19 kwa watu waliotokea nchini Iran. Mpaka sasa Bahrain imekwisharipoti visa 23 nchini humo.
 
UPDATE: Italia

Visa vipya 39 pamoja na vifo vipya vinne (4) vimeripotiwa nchini humo. Idadi kamili ya visa vyote imefikia 322 huku watu wapatao 11 hadi sasa wakipoteza maisha.
 
UPDATE: Confirmed coronavirus cases in Europe
  • Italy: 322
  • Germany: 16
  • France: 14
  • UK: 13
  • Spain: 5
  • Russia: 2
  • Austria: 2
  • Finland: 1
  • Sweden: 1
  • Belgium: 1
  • Croatia: 1
  • Switzerland: 1
 
SWALI: Je virusi vya corona vitafika Tanzania?

Jibu:
Ndiyo, haionekani njia ya kuvizuia

Swali: Je tutakufa sote?

Jibu: Mpendwa, sote tunakufa siku moja, lakini si shauri ya virusi hivi. Maana wengi wanaweza kuambukizwa, na wengi wataona matatizo kidogo kama mafua, wengine hawatasikia kitu. Ila wengine (labda 10-20 kati ya 100) watagonjeka, na wengine kati ya hao watagonjeka sana, na 2-3 wanaweza kufa. Asilimia 98 -97 tutaishi – hadi kufa anyway.

Swali: Je tufanye nini?

Jibu:
Tunza akili yako na usianze kuogopaogopa. Mara habari za kufika kwa virusi Tanzania zinapatikana, tumia busara, fuata hatua zifuatazo:

• kunawa mikono mara kwa mara kwa angalau sekunde 20 kwa maji na sabuni. Ukiwa nayo tumia dawa yenye alikoholi (si chini ya asilimia 60) kusafisha mikono.

• usiguse macho, pua na midomo kwa mikono kama hujanawa

• epukana kuwa karibu sana na wagonjwa


• wakati ugonjwa unazuru katika nchi ulipo, epukana kuwasalimu wengine kwa kushika mikono

• kaa nyumbani ukiwa mgonjwa
(ugonjwa wowote - maana kinga chako ni dhaifu katika hali hii, uko hatarini zaidi)

• tembea na karatasi za shashi (kama huna, hata karatasi ya choo / toilet paper) uitumie ukikohoa au kupiga chafya, halafu uitupe mahali pa takataka

• safisha mara kwa mara vitu unavyovigusa (vikiwa pamoja na kikombe, deski, simu yako); kama unayo, tumia dawa la alikoholi (spirit – si konyagi!), lowesha karatasi nayo, futa, tupa
 
UPDATE: Afrika

Algeria imeripoti kisa cha kwanza cha COVID-19 nchini humo. Kisa hicho ni raia wa nchini Italia aliyeingia nchini humo mnamo Februari 17, Wizara ya afya ya Algeria imethibitisha.

Taarifa zaidi zitafuata!
 
Mtu mzima anaweza kufanya hivyo, je wanafunzi watoto wadogo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…