Fahamu kuhusu Fao la Kukosa Ajira Tanzania (Unemployment Benefit)

Fahamu kuhusu Fao la Kukosa Ajira Tanzania (Unemployment Benefit)

Ni mbaya toka Magufuli amezileta ulitumika ubabe kwasababu wana madaraka, huwezi kumzuia mtu kuchukua 9M wakati wabunge wanazoa zaidi ya 250M, ni uhuni huu
Sababu kubwa inayofanya Unemployment benefits kulipwa hivyo, ni kulinda mwanachama asipoteze sifa ya kuwa pensioner.... Kuwa na wazee wengi tegemezi ni mzigo katika taifa lolote lile duniani.
 
Sababu kubwa inayofanya Unemployment benefits kulipwa hivyo, ni kulinda mwanachama asipoteze sifa ya kuwa pensioner.... Kuwa na wazee wengi tegemezi ni mzigo katika taifa lolote lile duniani.
Hii ni kwa stable job sio mikataba yetu ya miezi 6 au mwaka 1, unamaliza mkataba unakaa mtaani miaka kibao huna ajira wakati una pesa yako nssf watu wanatumia tu, hizi sheria ni za kipuuzi sana, hakuna wanacho linda zaidi kuzuia pesa na kutumia watakavyo
 
Hii ni kwa stable job sio mikataba yetu ya miezi 6 au mwaka 1, unamaliza mkataba unakaa mtaani miaka kibao huna ajira wakati una pesa yako nssf watu wanatumia tu, hizi sheria ni za kipuuzi sana, hakuna wanacho linda zaidi kuzuia pesa na kutumia watakavyo
Sasa hapa tatizo ni upatikanaji wa ajira nyengine .... Ndio tatizo sio sheria...!?
 
Sasa hapa tatizo ni upatikanaji wa ajira nyengine .... Ndio tatizo sio sheria...!?
Tatizo ni sheria kwasababu mtu analipwa mshahara mdogo kusave ni ngumu, sasa anapomaliza kazi apewe nssf yake akafanye mambo yake badala ya kuendelea kusubiri ajira za kuunga unga, shida watunga sheria wao wanapata pesa watakavyo wanataka kuzuia masikini wasipate
 
Hapana, baada ya kulipwa 33.3% ya mshahara wako wa mwisho, utasubiri miezi 18+ ukitafuta ajira, ukikosa ndio utaruhusiwa kuchukua kiasi kilichobaki
I Mean unalipwa kwa mkupuo au unalipwa kila mwezi 33.3% ndani ya miezi sita?
 
Wanahesabu miezi 18 baada ya tarehe ya mwisho kumaliza kulipwa fao la kukosa ajira (mie walihesabu yaani ukifika tu counter anaangalia mwisho ulilipwa lini alafu ana count miezi 18 baada ya kumaliza kulipwa kisha anakupa maelekezo ya kuandika barua pamoja na kuchukua kiapo mahakamani / mwanasheria kudhibitisha huna ajira)
Ilichukua muda gani kulipwa mkuu baada ya kujaza fomu ya withdrawal benefits supplementary?
 
Fao la Kukosa Ajira ni faida/msaada wa kifedha unaotolewa kwa mwanachama wa mfuko wa pensheni aliyepoteza ajira kwa sababu zisizo za hiari, kama vile kufukuzwa kazi, kuisha kwa mkataba, au sababu nyingine za halali. Hata hivyo, fao hili halitolewi kwa mtu aliyeacha kazi kwa hiari, kwani kufanya hivyo humfanya apoteze sifa za kupata fao hili.

Sifa za Kupata Fao la Kukosa Ajira

Umri: Mtu anayestahili fao hili anatakiwa kuwa chini ya umri wa miaka 55, ikiwa umepoteza kazi na umri wako ni zaidi ya miaka 55 basi italazimika ulipwe fao la uzee (Old age pension)

Mchango: Fao hili ulipwa kwa Mwanachama aliye changia kwenye mfuko chini ya miezi 180, ikiwa umechangia zaidi ya miezi 180 na uko chini ya miaka 55 ukapoteza ajira, basi utalipwa pensheni iliyo cheleweshwa, (differed pension).

Sababu za Kupoteza Ajira: Ajira inatakiwa kuwa imekoma kwa sababu zisizo za hiari kama vile: kufukuzwa kazi, Mkataba kuisha, au kupunguzwa kazini (retrenchment).

Malipo ya Fao la Kukosa Ajira
Fao la kukosa ajira hulipwa kwa awamu mbili. Kwa Aliyechangia Zaidi ya Miezi 18: Malipo ya Awamu ya Kwanza: Unalipwa 33.3% ya mshahara wako wa mwisho kwa kipindi cha miezi 6. Baada ya Malipo ya Kwanza: utakuwa na kipindi cha miezi 18 (miaka miwili) cha kutafuta ajira, ukipata ajira, utaendelea kuchangia katika mfuko pale ulipoishia na ikitokea umekosa ajira ndani ya kipindi hiki, utaandika barua kwenda kwa Mkurugenzi mkuu wa mfuko kuhama uchangiaji, toka uchangiaji wa lazima kwenda hiari, baada ya kuhama uchangiaji unaweza endelea kujichangia mwenyewe au utaruhusiwa kuchukua kiasi kilichobaki kwenye mfuko.

Kwa Aliyechangia Chini ya Miezi 18: Malipo: Utalipwa nusu ya kiasi ulichochangia kwenye mfuko. Baada ya Malipo: utakuwa na kipindi cha miezi 18 (Miaka miwili) cha kutafuta ajira. Ukipata ajira, utaendelea kuchangia pale ulipoishia, na Ukikosa ajira ndani ya kipindi hiki, utaandika barua kwenda kwa Mkurugenzi mkuu wa mfuko kuhama uchangiaji, toka uchangiaji wa lazima kwenda hiari, baada ya kuhama uchangiaji unaweza endelea kujichangia mwenyewe kwa mfumo wa hiari au kuchukua kiasi kilichobaki kwenye mfuko.

Pia malipo ya fao la kukosa ajira yanatofautina kwa mtu mwenye ujuzi (skilled) na Mtu asiye na ujuzi (Unskilled) kwa mtu asiye na ujuzi yeye hulipwa kiasi chote alicho changia kwenye mfuko na mwenye ujuzi yeye hulipwa kwa kufuata maelekezo hayo juu, hii ni kwasababu ni ngumu mtu asiye na ujuzi kupata ajira kwa urahisi ukilinganisha na mtu mwenye ujuzi

Kumbuka: Malipo ya fao la kukosa ajira yatakoma pale tu unapo pata ajira nyingine.

Sababu za Malipo Kufanyika kwa Awamu

Mfumo wa malipo kwa awamu una lengo la kuhakikisha mwanachama anaendelea kuwa na sifa za kupata pensheni ya uzee. Kama kiasi chote kingetolewa mara moja, kuna hatari ya mwanachama kufika umri wa kustaafu bila kufikia michango ya miezi 180 inayotakiwa kwa ajili ya pensheni ya uzee.

Hivyo, malipo kwa awamu yanasaidia kulinda michango iliyopo ili mwanachama awe na nafasi ya kufanikisha sifa za pensheni ya uzee.

Faida ya Fao la Kukosa Ajira

Hutoa msaada wa kifedha kwa kipindi cha mpito baada ya kupoteza ajira. Hakuna kupunguzwa kwa michango ya awali kwenye mfuko, Mfano: Ulikuwa na michango 20, ukalipwa fao la kukosa ajira, lakini hukuchukua kiasi chote. Ukipata ajira mpya, utaanza kuchangia kuanzia mchango wa 21 na kuendelea.

Kumbuka: Fao hili ni haki ya mwanachama aliyepoteza ajira kwa sababu halali zilizopo kwenye sheria, Mchakato wa kudai fao hili unahitaji nyaraka zinazothibitisha hali ya kuachishwa kazi kama barua ya kusitishwa kwa ajira.
Elimu nzuri kwa Wahusika
 
Ilichukua muda gani kulipwa mkuu baada ya kujaza fomu ya withdrawal benefits supplementary?
Ndani ya miezi miwili, nilifungua mwezi wa 10 mpaka December katikati ikawa tayari, hiyo form uliyotaja (withdraw benefits.. ) sikujaza ila niliandika barua ya kuhamisha michango yangu niwe mcyangoaji wa hiari na kuomba kulipwa mafao yangu yote na nikaambatanisha viambatanisho vya "letter of service" na kiapo alafu nikasikilizia baadae nikaitwa kuweka sahihi ya dole gumba kwenye biometric machine. Baadae nikatia timu bank kuchukua japo elfu hamsini nashangaa salio lina digit sita
 
Ndani ya miezi miwili, nilifungua mwezi wa 10 mpaka December katikati ikawa tayari, hiyo form uliyotaja (withdraw benefits.. ) sikujaza ila niliandika barua ya kuhamisha michango yangu niwe mcyangoaji wa hiari na kuomba kulipwa mafao yangu yote na nikaambatanisha viambatanisho vya "letter of service" na kiapo alafu nikasikilizia baadae nikaitwa kuweka sahihi ya dole gumba kwenye biometric machine. Baadae nikatia timu bank kuchukua japo elfu hamsini nashangaa salio lina digit sita
Asante sana mkuu. Itakua utaratibu umebadilika ila ndio hivyo tu maana saa hivi unaanza kuandika barua ya kuomba kuhamisha michango kweny uchangiaji wa Hiari unasubiri uitwe then ndio inafuata hiyo ya kujaza form ya withdrawal benefits.
 
Asante sana mkuu. Itakua utaratibu umebadilika ila ndio hivyo tu maana saa hivi unaanza kuandika barua ya kuomba kuhamisha michango kweny uchangiaji wa Hiari unasubiri uitwe then ndio inafuata hiyo ya kujaza form ya withdrawal benefits.
Okay ila haichukui muda mrefu kikubwa uwe umetimiza vigezo na masharti vya umemaliza miezi 18, alafu unapigwa kalenda kidogo za njoo baada ya wiki 2 alafu unarudi tena unapigwa kalenda ya njoo wiki ijayo. Mie ilichelewa kwa kuwa walipoteza document zangu ikabidi niandike barua upya na nikatoa tena copy ya kiapo baada ya muda mfupi wakanipa hela zangu na niliombea nje ya eneo ambalo nilikuwa nafanya kazi
 
Back
Top Bottom