Fahamu kwa kina ujenzi wa kituo cha mafuta kutokana na ukubwa wa eneo pamoja na gharama zake

Fahamu kwa kina ujenzi wa kituo cha mafuta kutokana na ukubwa wa eneo pamoja na gharama zake

Joined
Jun 24, 2024
Posts
34
Reaction score
50
Fahamu Kwa kina kuhusu ujenzi wa Kituo /vituo vya mafuta (petrol station ⛽) gharama zake, pamoja na process hasa kuhusu vibali vya ujenzi n.k.

Naitwa Ndama Matandiko najihusisha na ujenzi wa vituo vya mafuta pamoja na ushauri wa gharama za ujenzi , vibali vyake na aina ya eneo pamoja na faida zake au returning ambazo hupatika katika uwekezaji kwenye kituo /vituo vya mafuta.

Kwa ushauri zaidi waweza nipigia 0719639433 . Normal call & Whatsapp. 24 hours.

IMG_20240611_124537_492.jpg
IMG_20240527_142635_048.jpg
 
Katika ujenzi wa petrol station ⛽
Kitu Cha kwanza kuzingatia ni
(a)Eneo ulilopo ni eneo sahihi ukiwa unaanza biashara ya mafta?
(b) Je Kuna barabala yenye wingi wa magari ?
(c) Watu wanaukuzunguka katka eneo lako umekutana nao kuwapa taarifa za mradi huo kuwepo?
(d) Na kabla ya mambo yote mipango mji wanaruhusu mladi huo kuwepo mahara hapo Ili isije ikayokea kama yanayotokea unatumia gharama kubwa Kisha upaswi kuwepo hapo
(e) Baada ya hapo Sasa unaweza kuanza kuomba vibari vya ujenzi na kuanza uwekezaji wa uhakika na N.k
 

Attachments

  • IMG_20240522_173918_586.jpg
    IMG_20240522_173918_586.jpg
    4.7 MB · Views: 36
  • IMG_20231008_073542_786.jpg
    IMG_20231008_073542_786.jpg
    4 MB · Views: 41
  • IMG20210108181438_090630.jpg
    IMG20210108181438_090630.jpg
    1.9 MB · Views: 36
  • IMG20210303070849_090420.jpg
    IMG20210303070849_090420.jpg
    2.1 MB · Views: 36
gharama zake vipi
Gharama mkuu inategemeana na eneo lako na mahitaji ya kituo (shell)
unachotaka kujenga.
Je! Eneo ni la kukata au kujaza?
Canopy yenye ukubwa gani
Pump ngap utahtaji?.
Tank ngap utahitaji?
Ofisi yenye ukubwa gani?
Bango yenye muonekano up?
Karibu boss tubadilishane mawazo
0719639433
 
Ndugu kwanza kabisa unatakiwa kufahamu Kwamba saivi fulusa ipo kubwa katika biashara ya mafuta ni biashara ambayo kula hasala ni wewe mwenyewe kushindwa kuwa MAKINI katika uendeshaji wa Kituo chako.
Lakin Kwa uhakika mafuta yanalipa sana Kwa sasa.

Ukiwa na shell Moja ndani ya miez 12 uhakika wa kujenga nyingne unakuwa nao mkubwa sana. Usikae na PESA BANK bila kuwekeza Ili iongezeke mara dufu ingia katika uwekezaji wa kuuza mafta utanishukulu siku moja.

IMG_20240626_183605_996.jpg
 
Hauja tupa jumla ya pesa ya ujenzi na vibali vyake kama una eneo tayari
 
Hauja tupa jumla ya pesa ya ujenzi na vibali vyake kama una eneo tayari
Mkuu Kwa eneo lenye Square meter 2500.
Kuanzia vibari mpaka ujenzi.
Kama sio korofi ni eneo zuri lita kugharimu kias Cha Sh Milion 500 mpaka 650 milion.
Hapa inaweza kupungua au kuongezeka kulingana na mkoa utakaokuwepo sababu vifaa vya ujenzi hutofautiana gharama kulingana na mkoa husika.
Canopy yenye ukubwa wa meter 24x10
Tenk 3 zenye ukubwa wa lita 45000 na mbili 25000
Ofisi yenye ukubwa wa mita 10x18
Ikiwemo na mambo mengine ambayo siwezi orodhesha yote hapa.
Na hiki ni kituo kikubwa chenye standard nzur.
KARIBU SANA
 

Attachments

  • IMG_20240327_143625_524.jpg
    IMG_20240327_143625_524.jpg
    3.7 MB · Views: 41
Nasikia ukiwa na eneo lenye mzunguko mkubwa Ridhiwani anakuja kukupokonya sheli inakuwa yake, hii imekaaje?
Hili ni uongo mkuu sio kweli na haiwezekani kabsa.
Sio kweli Ridhiwani hawez kufanya hivo labda kama atahitaji aweke bland ya company yake Kwa makubaliano hapo sawa.
Pia tunachoweza kusema ni Kwamba Ridhiwani ingekuwa ni hivo vituo vyote vilivyopo maeneo ya miji mikubwa na majiji vingekuwa vyake.
Usitishwe na maneno ya watu wenye mawazo ya kushindwa.
 
Habar ?
Leo nataka tuzungumzie hili suala la namna ya kufukia TANK la mafuta (kuzika tank)
Ndugu yangu ukiwa unajenga kituo Cha mafta ( petrol station)
Cha kuzingatia sana na kuwa MAKINI ni Tank namna ya kuziweka make hicho ndio kituo chako. Tank ndio mama katika
Petro station ukicheza mistake kidogo tu unaweza pata hasala kubwa katika biashara yoko
" Cha kuzingatia ni "
1) Tangi inatakiwa itengenezwe kiustad na Uimara zaid katika uchomaji wake
2) baada ya matengenezo yake inatakiwa ijazwe upepo Ili kubaini kama inavuja au haivuji.
3) Kisha baada ya hatua ya 2 inatakiwa kupakwa rangi ya kuzuia kutu, na inafuatiwa na upakaji wa Lami Ili kulilinda tank lako.
4) ni mchakato wa kulizika chini hapa napo panahitaji umakini sana kwanza kabla ya kuchimba shimo lake unatakiwa upate level ya eneo Ili lisije likaonekana lipo juu ama chini zaid.
5) imalisha chini Kwa kuweka Beem Ili uweze kulifuna tank lako Kwa minyololo.
6) hi ni hatua ya mwisho kulishusha chini na hakikisha linakaa pima maji na uhakikishe umelifunga minyololo Ili uwe na uhakika wa Tank kutokuyumba na kuibuka juu (kupanda juu)
Hapo fukia Kwa mchanga Ili kuilinda chuma ya Tank kuliwa na kutu.
Naomba niishie hapa Kwa leo lakin ukitaka kujua zaidi karibu Kwa majadiliano ya kina.
 

Attachments

  • IMG_20240628_133103_311.jpg
    IMG_20240628_133103_311.jpg
    7.8 MB · Views: 37
  • IMG_20240505_154546_153.jpg
    IMG_20240505_154546_153.jpg
    5 MB · Views: 38
Habar ?
Leo nataka tuzungumzie hili suala la namna ya kufukia TANK la mafuta (kuzika tank)
Ndugu yangu ukiwa unajenga kituo Cha mafta ( petrol station)
Cha kuzingatia sana na kuwa MAKINI ni Tank namna ya kuziweka make hicho ndio kituo chako. Tank ndio mama katika
Petro station ukicheza mistake kidogo tu unaweza pata hasala kubwa katika biashara yoko
" Cha kuzingatia ni "
1) Tangi inatakiwa itengenezwe kiustad na Uimara zaid katika uchomaji wake
2) baada ya matengenezo yake inatakiwa ijazwe upepo Ili kubaini kama inavuja au haivuji.
3) Kisha baada ya hatua ya 2 inatakiwa kupakwa rangi ya kuzuia kutu, na inafuatiwa na upakaji wa Lami Ili kulilinda tank lako.
4) ni mchakato wa kulizika chini hapa napo panahitaji umakini sana kwanza kabla ya kuchimba shimo lake unatakiwa upate level ya eneo Ili lisije likaonekana lipo juu ama chini zaid.
5) imalisha chini Kwa kuweka Beem Ili uweze kulifuna tank lako Kwa minyololo.
6) hi ni hatua ya mwisho kulishusha chini na hakikisha linakaa pima maji na uhakikishe umelifunga minyololo Ili uwe na uhakika wa Tank kutokuyumba na kuibuka juu (kupanda juu)
Hapo fukia Kwa mchanga Ili kuilinda chuma ya Tank kuliwa na kutu.
Naomba niishie hapa Kwa leo lakin ukitaka kujua zaidi karibu Kwa majadiliano ya kina.
Hakuna business plan ya kituo cha mafuta ? Çhenye pump hata 2 tunkuanzia na paa lake dogo tu ?
 
My next target! Toa mchele mkuu kuku tudonoe.
 
Back
Top Bottom