Fahamu kwanini Matajiri huendelea kuwa matajiri

Fahamu kwanini Matajiri huendelea kuwa matajiri

Kinachotupambanua maskini na matajiri ni uwekezaji tu,wapi umewekeza muda wako na pesa yako ndio itadetermine hali yako kiuchumi,tukitaka tufanikiwe kimaisha tujitahidi kuwekeza muda wetu katika mambo ya msingi kama kujiongezea maarifa,kujenga connections,kuchapa kazi,kusaidia wengine na ibada.siku zote mtu huvuna alichokipanda.hakuna kitu muhimu duniani kamamilelehata dakika moja ikipotea ndo imepotea hutakaa uipate tena milele.tuache kutumia muda wetu kwenye mambo yasiyo na tija.siku isiishe bila kujifunza vitu vipya,kusogea mbele kimaendeleo,kusaidia wenzio(hata kimawazo),nakusali/meditate
 
If you don't find a way to make money while you sleep, you will work until you die. - Warren Buffet
“Someone’s sitting in the shade today because someone planted a tree a long time ago.”
 
mkuu nimekua najiuliza maswali mengi, hivi utajiri unapimwa kwakua na pesa nyingi au ni spiritual thing? kwanini kuna watu wengine anaweza ishiwa fedha zote na miradi yote kufilisika ila baada ya muda flani anarudi kivingine na kua bora zaidi ya mwanzo? nadahani pia utajiri na umasikini unatokana na mindset ya mtu, unaweza kupewa pesa nyingi au kubahatika kurithi mali ila kama una poor mentality zitaisha tu na utarudi kwenye state yako tu.
nadhani somo la muhimu saana katika harakati za kuukimbia umasikini cha muhimu ni kuanza na kubadilisha mitazamo yetu dhidi ya umasikini na utajiri.
Well said kabisa 😹😹 😵
 
absolutely, upo sahihi, pia nimejifunza kua wengi wetu wanaishi bila kua na malengo wala kujua nini wanahitaji katika maisha, kuna mtu mmoja ni graduate wa sheria ila cha kushangaza alihangaika kutafuta kazi yoyote ili aweze ku survive na mwisho wa siku akaishia kua muhudumu wa super market, nikamuuliza sasa kwanini alipoteza miaka mi4 kusoma sheria? akaniambia kua alisoma kwakua alihisi akiwa mwanasheria atakua na maisha mazuri na matokeo yake kakwama na kushindwa kwenda law school ili afikie ndoto yake, pia vilevile mifumo ya elimu yetu inawaharibia watu wengi maisha kwa kuwafanya wawe watafutaji wa ajira baada ya watazamaji wa fursa na kuzifanyia kazi, mwisho wa siku tunakua na idadi kubwa ya watafuta ajira kuliko watengenezaji wa ajira wenyewe....

naamini umasikini wa mtu hauwezi isha kwa kutegemea mshahara kwakua kila mara mshahara hua hautoshi kutatua kero na mahitaji yote.
mimi naamini kila mtu ni mzuri na ana kipaji au uwezo flani wa kufanya kitu flani kwa ufanisi zaidi, ila tatizo mfumo wa malezi pamoja na elimu unawakaririsha watu kua bila kusoma sana na kuajiriwa na kulipwa mshahara hauwezi kua na maisha bora na matokeo yake imepelekea watu kurogana kugombania madaraka na kushinda kwa waganga ili ajira isiishe.

najiuliza kwanini mwanafunzi wa havard mark zukerberg alikataa ofa ya kuajiriwa na microsoft huku akiahidiwa mamilioni ya dola toka kwa bill gates na kuamua kukomaa na mradi wake wa face book? jibu ni lepesi sana aliisikia sauti ndani yake na kuifanyia kazi na matokeo yake leo ni kijana tajiri saana nadhani kuliko vijana wote wa umri wake.

kuna mtu mmoja aliwahi niuliza kwanini sitaki kuajiriwa na kwenda kufanya kazi kwenye taasisi yao? nikamjibu kua maisha ni kama maji na pia sisi nikama aina ya samaki, kuna vidagaa,samaki wa saizi ya kati na wale nyangumi sasa basi maji yangu ni marefu deep see, hivyo basi nitakomaa zaidi mpaka nifikie level ya maji yangu, na ujasiri huo niliupata baada ya kusoma vitabu vingi kama vile think and grow rich, retire young and retire rich, rich daddy and poor daddy, how to increase financial IQ na vinginevyo....
naendeleza mapambano huku nikiwa na imani kuu kua lazima nitafikia malengo yangu na kuacha legacy behind.

nachoamini ni kwamba kuzaliwa masikini sio kosa au uamuzi wa mtu bali kufa masikini ni maamuzi na makosa yetu yenyewe.
watu wengi wanafikiri utajiri ni lazima uwe na pesa kwanza kumbe unaanzia katika state of mind.
we become who we are from what we think.
nawasilisha.
Facts. Pamoja na mindset naomba niongeze vitu vitatu 1. Watu hatuna na hatutafuti information za kutosha 2.hatuna utayari 3. Hatutaki kujaribu au kuthubutu.

Kuna mjasiriamali mmoja alisema kama wakitokea watu wanahitaji hela kwaajili ya biashara ataweka hela yake kwa yule aliefeli biashara mara nyingi kwasababu amejaribu na kuna vitu amejifunza katika kufeli.

Kiukweli wengi hatupo tayari kujaribu na kuthubutu kwasababu tunaweza kufeli ila kila aliefanikiwa anakwambia ukifeli kwa haraka zaidi utafanikiwa kwa haraka zaidi.

Ujasiriamali na biashara utendaji sio jambo la theory inamaana hata upewe knowledge kila siku na vitabu vya kusoma kuhusu kuogelea kwa miaka mitatu straight, ukiingizwa kwenye maji iwe baharini au swimming lazima uzame kwasababu kuogelea sio theory lazima ufanye practical ushindwe ujaribu ten ushindwe mwisho unakua mzoefu kwakufeli sana mwanzoni na hii inaapply kwenye kila kitu uoga wa watu kuanguka unawafanya wasipige hatua mwisho wa siku watachelewa kutembea au hawatatembea kabisa Asante.
 
Back
Top Bottom