Fahamu maana ya 'Autopilot'


Niliendesha Volvo XC90 ambayo Ina Autopilot. Kwa kweli ina performance nzuri sana ila niliendesha motorway kwa mda na inapunguza mwendo yenyewe na ikiona msongamano mwingi inakuambia ondoa.

Lakini inatisha kidogo na sikuipenda Bora kuendesha kawaida tu
 
Kumbe ni kweli, basi teknolojia imekuwa sana mkuu, ni vipi gia zinakuwa manual au auto?
 
aloha 243 requesting clearance ran way 3 left
 
Kumbe ni kweli, basi teknolojia imekuwa sana mkuu, ni vipi gia zinakuwa manual au auto?

Hiyo ilikuwa ni auto Mkuu na Volvo ni ndinga ninazozikubali kwani mpaka auto parking assist inayo
Kama unatafuta parking unaingia parking ukiwa na speed ndogo sana halafu unabonyeza kitufe cha parking inaanza kutafuta parking yenyewe kwa kutumia camera zote
Hakuna kushika usukani inaingia yenyewe
Hapo ndio waliniacha hoi
Unaweza usiiamini gari ukasema inagonga
 
Hawa mabeberu ni hatari kila siku wanaumiza vichwa jinsi ya kurahisisha mambo.
 
Uzi wa elimu ya autopilot umeshaingia luba za siasa. Hovyo kabisa.
 
sifa ya maskini ni kujua vitu vingi hata vivyomhusu kama auto pilot nk tajiri hujua vitu vichache vinavyomhusu yeye kupata pesa

huu uzi naona kuna maskini wengi

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwenye meli au boti mfumo wa autopilot ulikuwa msaada mkubwa baada ya kugunduliwa.

Katika meli autopilot husaidia kazi ya kuingoza meli katika njia na uelekeo ambao muongozaji amepanga.

Mfumo huu ufanya kazi kati ya steering na rudder(kata kona ya meli) ambapo meli za kisasa inakuwa imeunganishwa na GPS na ramani ya kielectronic ambapo meli itafata njia elekezi.

Hii autopilot unashauriwa kutumia sehemu ambazo havina meli nyingi,makutano au hali mbaya ya hewa.

Licha ya kuweza kutumia autopilot watu waliopo zamu hawaruhusiwi kutoka sehemu ya kuongozea meli, lazima wawepo ili kama kuna emergency watoe mfumo wa autopilot na kurudi kawaida.

Hii unashauriwa utumie sehemu ya wazi baharini au ziwani,sio kwenye mpango au eneo la bandari.

Autopilot licha ya kusaidia sana, ajali nyingi zimetokea baada ya watu kujisahau na kuacha mfumo huu maeneo yenye hali mbaya ya hewa. Mfano ajali nyingi zinazotokea baharini ya kusini kwa China na ajali kubwa ya meli ya mafuta mwaka 1967 ya Torrey Canyon ambapo baada ya uchunguzi ripoti ilionyesha meli haikutolewa kwenye autopilot ilivyokaribia kwenye mlango wa baharini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…