Fahamu mambo yafuatayo yanayofanyika katika urejeshaji wa mkopo wa elimu ya juu "HESLB".

Fahamu mambo yafuatayo yanayofanyika katika urejeshaji wa mkopo wa elimu ya juu "HESLB".

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
Kwanza kabisa ni ukweli usiopingika yapo maboresho makubwa yaliyofanywa na Bodi ya mikopo miaka ya karibuni kwa lengo la kuwa mfuko endelevu na kunufaisha Wanafunzi wengi zaidi.

Mabadiliko hayo kwa kiasi kikubwa yamewaumiza walipaji wengi hususani walioanza kulipa kabla ya mwaka 2017.

Kuna mambo makubwa matatu yanayofanya madeni ya walipaji kuonekana ni makubwa kuliko kiasi walichokopeshwa " principal loan"na mambo hayo ni:-

1.Asilimia sita(6%)inayokatwa kila mwaka kwenye kiasi cha mkopo kilichobaki " outstanding loan" baada ya kulipa. Hapa ina maana unapolipa mwaka mzima kiasi kitakachobaki kitatafutiwa asilimia sita na itajumlishwa kwenye deni lako.

2.Asilimia kumi (10%) penalty fee.Wahitimu wa kabla ya mwaka 2016 walipaswa kurejesha mikopo yao kabla ya miezi kumi na miwili kuisha tangu wahitimu chuo na kuchelewa kufanya hivyo ndani ya muda huo wa miezi 12 kunasababisha kukatwa asilimia kumi.

Baada ya mwaka 2017 ipo sheria iliyopitishwa na imefanya wanufaika kuanza kurejesha baada ya miezi ishirini na minne 24( miaka miwili) na miezi hii huanza kuhesabiwa baada ya kuhitimu ( graduation).

3.Asilimia moja 1% ada ya uendeshaji ". Administration fee "Ada hii hukatwa mara moja kwa mwaka kwenye kiasi kikuu(principal loan) cha deni la mkopaji.

Haya ndiyo mambo yanayosababisha tuone madeni kuwa makubwa kuliko kiasi tulichokopa.Ni vizuri tukijenga utaratibu wa kufuatilia ili kufahamu zaidi kwa kutembelea ofisi za bodi ya mikopo.
 
HESLB is a Debt-trap.

Utalipa mpaka unastaafu, unakatwa kwenye pension ( kama ikitokea ukapewa ).
 
Unapewa nini Mkuu?..loan au?
Watu mbona wanamaliza tena wengi tu
Je, Unapata kazi ndani ya miaka 2 baada ya graduation kuepuka penalty ya 10% ?

Mshahara Wako Ni Kiasi Gani, Tsh 500,000 Kwa Mwezi ?

Hilo Deni La HESLB linaisha baada ya muda gani ?

Uko Tayari Kuishi Kwa Mshahara Wa Tsh 200,000 Au Chini Ya Hapo Kwa Mwezi Kwa Muda Usiopungua Miaka 10 ?

Kumbuka Hapo Umeanza Kazi Ukiwa Labda 28 - 30 Years Old, Deni Unamaliza Ukiwa Late 38-40 !

Ukistaafu Unazungushwa Kwenye Corridor Za PSSF kama mara 200 then wakikusaidia sana wanakupa Milioni 75 Baada Ya Kukutumikisha Miaka 30.

Try To Think !
 
kuna kipindi walitangaza kwenye magazeti kuhusu wadaiwa wajipeleke wenyewe kabla hawajaanza kutafutwa..mfanyakazi mwenzangu akajipeleka HESLB mwenyewe..ameanza kukatwa..sasa anachobakiwa nacho ni kidogo sana(ashachukua mkopo)..anateseka sana mpk namuonea huruma

alinishawish weeeee mi nikamwambia SIENDI..labda wanikamate wenyewe ila hvhv SIJIPELEKI NG'O...mwezi wa 4 nilienda kuchungulia deni nnalodaiwa nikakuta nadaiwa milioni 14+ wakati mkopo wangu wote mpk namaliza haukufika milioni 8
 
Leo nmetembelea ofisi za bodi ya mikopo.
Nmekutana na hayo makato aliyotaja mtoa mada.
Nilitegemea deni kupungua kwa takribani milioni 1 ila deni liko palepale.
Nadhani ni muda muafaka tupaze sauti kwa serikali iondoe hizo tozo hasa 6% kwa wanaorejesha mkopo.
Vinginevyo mahesabu haya yanaongeza ugumu wa maisha kwa wanufaika wa mikopo.
 
Mimi wataniijia huku mtaani na greda silipi na sina mpango wa kulipa na hivi life linaenda poa tu kwa kuajiajiri mwenyewe labda waje na mabunduki kunitafuta kitaa
 
Leo nmetembelea ofisi za bodi ya mikopo.
Nmekutana na hayo makato aliyotaja mtoa mada.
Nilitegemea deni kupungua kwa takribani milioni 1 ila deni liko palepale.
Nadhani ni muda muafaka tupaze sauti kwa serikali iondoe hizo tozo hasa 6% kwa wanaorejesha mkopo.
Vinginevyo mahesabu haya yanaongeza ugumu wa maisha kwa wanufaika wa mikopo.
HIVI NI ASILIMIA 6 AU 15. MBONA MNANICHANGANYA?
 
HIVI NI ASILIMIA 6 AU 15. MBONA MNANICHANGANYA?
Asilimia 15 ni pesa unayokatwa kulipa deni kila mwezi kutoka kwenye Basic salary.
Asilimia 6% ni riba inayoongezeka kwenye deni kila mwaka. Hii ni asilimia 6 ya deni lote likilobaki. (Compound interest).
Nmepiga mahesabu kila mwaka narejesha 990,000/= halafu napata riba ya 900,000/= kwa hiyo kila mwaka napunguza deni kwa 90,000/= pekee pesa nyingine inaenda kufidia riba.
Nadhani kuna haja ya kupiga kelele ili hii 6% ifutwe.
Pia ni vizuri kama mshahara mkubwa au kipato kikubwa ukalipa pesa nyingi zaidi ili outstanding debt ipungue.
 
kuna kipindi walitangaza kwenye magazeti kuhusu wadaiwa wajipeleke wenyewe kabla hawajaanza kutafutwa..mfanyakazi mwenzangu akajipeleka HESLB mwenyewe..ameanza kukatwa..sasa anachobakiwa nacho ni kidogo sana(ashachukua mkopo)..anateseka sana mpk namuonea huruma

alinishawish weeeee mi nikamwambia SIENDI..labda wanikamate wenyewe ila hvhv SIJIPELEKI NG'O...mwezi wa 4 nilienda kuchungulia deni nnalodaiwa nikakuta nadaiwa milioni 14+ wakati mkopo wangu wote mpk namaliza haukufika milioni 8
Tuko wengi sijawai kuwaza hata siku moja kwenda kujisalimisha.
 
HESLB ni life trap!
Waliopendekeza hayo makato wanapaswa kulaaniwa! Naam, KULAANIWA!
Yaani zaidi ya 23% ya annual salary inajwenda HESLB. Ukiongeza penalty inafika 33%. REALLY!
Hapo bado makato mengine lukuki.
Ndio maana walisoma kozi za gharama wanaweweseka wakisikia bodi.
 
tuliokimbilia kufanya kazi nchi za nje kukwepa deni la HESLB tujuane tafadhali...
 
Back
Top Bottom