Fahamu matokeo ya meditation

Fahamu matokeo ya meditation

Dogoli kinyamkela

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
618
Reaction score
1,440
Changamoto kubwa ya wengi si kushindwa kufanya meditation, bali ni kitopata matokeo ya nia zao za kumeditate.

Mabingwa wa meditation kila wakati wanasisitiza faida zitokanazo na meditation, lakini sijaona hata mmoja akitaja hasara na kutoa suruhu kwa wanaofanya hivyo bila kuona mabadiliko yoyote, au kuona matokeo ya dhahiri.

MUNGU.Akinipa fursa nitaposti madhara ya meditation, sababu hakuna kisicho na madhara ukitumia vibaya, acha leo nitoe sababu za wanaohisi hawaoni matokeo.

Baada ya visa vya wanaoshindwa kuwa vingi nilirejea katika chanzo na haya ni sehemu ya niliyopata.

Mlango wa tano wa fahamu, chakra ya tano, kanisa la tano au kinara cha tano.
Katika Biblia ni kanisa lililoko Sardi.

Katika mwili wako mlango huu upo eneo lilipo koo.

Eneo lenye kuupa mwili uwezo wa kujielezea wenyewe pia kukuwezesha wewe kujielezea na Kubwa usilojua ndiyo mlango ambao unawezesha mwili kujilinda na hatari usizoziona, mambo ya kichawi, mapepo, machale n.k.

Mlango huu ukiwa wazi muhusika huwa muwazi, mkweli popote na kwa kila jambo, na maneno yake huchukuliwa kwa uzito mkubwa.

Mtu Ambaye mlango huu uko wazi mbali na kwamba hawezi kusema uongo, ukweli huohuo ambao unaweza kumdhuru mwenyewe, humfanya kutoka salama katika jambo baya.

Ndiyo wale wanaosamehewa katika jambo zito walilolifanya, kwa sababu walisema ukweli.

Mbali na hilo ni eneo zinakozalishwa hisia, taarifa dalili za mwili, dalili nzuri na mbaya juu ya jambo fulani na hata kukulinda na hatari zisizoonekana.

Mlango huu ukiwa wazi hulogeki, wala hudhuriki na vitu vibaya visivyoonekana.
Mfano wachawi wakikuvamia usiku utaamka gafla, na usingizi hauji mpaka watu au vitu vibaya viondoke au hali kuwa shwari.

Eneo hili ndiko hutokea nguvu zinazoweza kukukinga na madhara upitapo maeneo yenye roho wabaya Bila kunaswa.

Ni sehemu ya kazi za mlango wa tano, Sababu si sehemu ya mada wacha niendelee na vilivyo sehemu ya Mada.

Kila mtu ana ishara fulani za kimwili, zinazomsaidia kupata taarifa fulani kabla ya Jambo kutokea.
Mfano, kuna watu wakikaribia kupata pesa au kupoteza, huwashwa viganja vya mikono, kope za jicho hucheza n.k.

Mwingine kope, sikio, unywele hucheza akikaribia kupata taarifa ya msiba, harusi, au taarifa fulani mbaya au nzuri.

Zipo ishara nyingi zenye kutoa taarifa Ya yajayo kwa kila mwili wa mtu na ni mwili husika ndiyo unajua maana ya kila ishara Au aina ya taarifa.

Wanaojua ishara hizi, hutoa taarifa kabla ya tukio.
Mfano mimi, mboni ya chini ya jicho la kushoto ikicheza/ kuvuta, lazima msiba utokee.

Hilo ujue usijue lipo, ujue usijue hutokea. Busara ni kujua maana ya taarifa za mwili wako ili ujue kinachokujia mbele, Bila kupiga ramli kwa waganguzi.

Ishara kila mtu anazo, wengi hawajui tu ishara zao ni zipi, Sababu ishara zinatofautiana kati ya mtu na mtu.

Kwa kutojua ishara, alama au lugha ya mwili wako, ni sawa na kushindwa kusikia sauti ya Mungu baba, au Kristo walioko ndani yako, hivyo kukosa masikilizano baina yako wewe wa nje na wewe wa ndani.

Tukirudi kwenye meditation, nako pia tumetofautiana namna ya kupokea matokeo, sababu ya utofauti wa lugha Za miili.

Huyu atapata matokeo ndani ya meditation, na yule nje ya meditation.

Nikiwa na maana kuna wanaopewa matokeo katika maono, ndoto, moja kwa moja, kupitia mtu mwingine n.k.
Hivyo Namna mwingine anavyoweza kupata matokeo inaweza kutofautiana sana na wewe.

Mwili wa mtu ni kama mashine au mtambo ambao unaweka mzigo huku, matokeo unayapata upande mwingine.

Kama kupakua kitu U tube, unapakua kitu huku unakikuta katika eneo fulani la hifadhi.
Kama ni video ina sehemu yake, picha zinasehemu yake, nyaraka na kila kitu kina sehemu yake kinakohifadhiwa.

Kama hujui una weza tafuta kitu katika simu yako na usijue kimehifadhiwa wapi, sababu hujui wapi kwa kupata unachokikusidia kinachoingia na kutoka ndani ya simu.

ishara za mwili hutoa taarifa kupitia mwili bila ubongo, ikiwa na maana ni tendo ambalo liko nje ya uwezo wa mtu.

Katika mlango huohuo ndipo hupitia pia taarifa au maelezo ya kimungu ya moja kwa moja, yanayochakatwa kupitia ubongo.

Taarifa au maelezo hayo ambayo huletwa kupitia ubongo, unaweza kuyaona moja kwa moja kupitia mlango wako wa asili wa mwili wako.

Nimesema mlango wa asili wa mwili wako, nikimaanisha kila mmoja ana mlango wake wa asili wa kupokea maelekezo ya moja kwa moja ya kiMungu.

Katika post ya meditation, nilisema kuna wakati ambao anayemeditate anaweza kuona maono au kupata majibu umo ndani ya meditation.

Hili linawahusu wenye mlango wa asili wa maono, ( wenye uwezo wa kuwasiliana na roho).
Wengine wana milango ya asili ya ndoto.

Mtu huyu akimaliza kumeditate matokeo yake kwa ufasaha atayaona kupitia ndoto, kwa namna tofauti tofauti
Wenye asili ya akili au mawazo.

Mtu huyu akimeditate, matokeo yake yatakuja kwa kuzama katika fikra na kila atakachojiuliza kuhusiana na ombi lake, ataona anapata majibu, na kila kitu kinafunguka kirahisi.

Tuwe pamoja
SISI NI AFRIKA TU UMOJA.
 

Attachments

  • 1736505857516.jpg
    1736505857516.jpg
    74.6 KB · Views: 9
SPIRITUAL MEDITATION (TAHAJUDI YA KIROHO).
1736506222209.jpg

Spiritual Meditation ni aina ya meditation ambayo inakupeleka kujua wewe ni nini na vipi unatakiwa kuwa. Hii ni meditation ya kujitafuta, ni msako wa roho yako katika ulimwengu uliojaa uongo na kelele nyingi. Tangu ulipozaliwa umepewa utambulisho na watu wengine. Walisema mtoto wa kiume au wa kike amezaliwa, wakakuchagulia jina walilojisikia furaha wao kuliita, wakakupeleka kwenye nyumba za ibada na kukupa mafundisho usiyotaka lakini umejikuta umeyapokea, ukapelekwa shule na kuanza kufundishwa na kijazwa kichwani vitu mbalimbali. Ulimwengu na mazingira vimekupa utambulisho na kukufahamu kama mtu fulani, lakini je huo utambulisho unaojulikana ndiyo wewe halisi?

Wewe ni roho hakuna awezaye kukujua wala kukutambulisha wewe katika hali yako ya kiroho lakini utambulisho wa nje umekuziba ufahamu wa kujua wewe ni nini.

Ninaposema wewe ni nini ni lazima unielewe. Nani ni matokeo ya jinsi uonekanavyo, uongevyo na uitwavyo lakini Nini ni vile haswa ulivyo. Unavyojulikana na unavyoitwa sivyo ulivyo. Unaweza kukuta kuna mtu anatambulishwa kutokana na ukubwa wa mwili wake, utasikia "bonge mambo vipi" na yeye anaitikia poa. Au utasikia vipi mambo cheupe, wengine hutambulishwa kwa taaluma na kazi zao kwa mfano mwalimu, doctor n.k. Je huo utambulisho ndiyo wewe. Jibu ni hapana, kwa kuwa huo utambulisho wote unaishia mwilini na kwenye akili lakini siyo rohoni. Unaitwa doctor au mwalimu kutokana na vitu ulivyoweka kwenye akili yako lakini rohoni mwako wewe ni kitu kingine.

Imebidi niingie huko kidogo ili upate kunielewa ninachotaka kukufundisha kuhusu spiritual meditation. Huu ni msako wa roho yako, ni zoezi la kutafuta utambulisho wako hali (divine identify).q
 
Je meditation Ina uhusiano Gani na dini?
1736534136315.jpg




Meditation ni mbinu ya kiakili na kimwili inayolenga kutuliza akili, kuongeza umakini, na kuimarisha uwiano wa kihisia. Ingawa meditation mara nyingi imekuwa ikihusishwa na dini na mafundisho ya kiroho kama vile Ubudha, Uhindu, na dini za Mashariki, si lazima iwe ya kidini.

Watu wengi hutumia meditation kama njia ya kupunguza msongo wa mawazo, kuongeza afya ya akili, na kuimarisha ubora wa maisha bila kujihusisha na masuala ya kidini. Hii inathibitisha kuwa meditation ni mbinu ya ulimwengu mzima inayoweza kubadilishwa kulingana na mahitaji ya mtu binafsi.

Kwa upande mwingine, katika baadhi ya dini, meditation ni sehemu muhimu ya mazoea ya kiroho. Kwa mfano, katika Ubudha, meditation hutumika kama njia ya kufikia mwamko wa kiroho na kuelewa asili ya maisha. Vivyo hivyo, baadhi ya Wakristo hutumia meditation kwa tafakari ya Maandiko Matakatifu na maombi ya kina.

Hii inaonyesha kuwa ingawa meditation inaweza kuwa na asili ya kiroho, haijazuiliwa kwa matumizi ya kidini pekee. Kila mtu ana uhuru wa kuitumia kwa namna inayolingana na maisha yao, iwe ni kwa ajili ya kiroho, afya ya akili, au kuimarisha ustawi wa kila siku.
 
🌹Faida Za Meditation kiafya.
1736534322706.jpg


Meditation ina faida nyingi za kiafya, ikiwa ni pamoja na kupunguza msongo wa mawazo na kuboresha hali ya kiakili na kihemko. Husaidia kupunguza viwango vya cortisol, homoni inayohusiana na msongo, na kuongeza utulivu wa akili, hivyo kupunguza wasiwasi na hali ya huzuni. Meditation pia inaboresha ubora wa usingizi na inaweza kupunguza dalili za insomnia, jambo ambalo linafaa kwa afya ya akili na mwili. Hali ya utulivu inayopatikana wakati wa meditation inasaidia kupunguza maumivu ya mwili na kuimarisha kinga ya mwili dhidi ya magonjwa.

Aidha, meditation husaidia kuboresha umakinifu na uwezo wa kumbukumbu kwa kuongeza uwezo wa ubongo kutafakari na kushughulikia mawazo kwa kina. Inapunguza mtindo wa mawazo yanayozunguka na inakuza hali ya kujitambua na kujiamini, jambo ambalo ni muhimu kwa afya ya kiakili. Meditation pia inasaidia kuimarisha shinikizo la damu na kupunguza mvutano wa misuli, hali inayosaidia katika kutunza afya ya kimwili na kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo.

Zaidi ya hayo, meditation ina faida za kiroho, kama vile kukuza hali ya amani ya ndani na huruma kwa wengine. Inasaidia kuongeza uhusiano wa kiroho na mazingira ya nje, na hivyo kukuza furaha na kuridhika na maisha. Kwa watu wanaotafuta kuunganishwa na hali ya juu ya fahamu, meditation husaidia kufungua milango ya nguvu za ndani na hali ya utulivu wa kiroho. Hivyo, meditation ni njia bora ya kuboresha afya ya mwili, akili, na roho kwa ujumla.
 
🌼🌹Maana ya Meditation.
Meditation ni zoezi la kiakili linalolenga kutuliza akili na kufikia hali ya utulivu wa ndani. Ni mchakato wa kuzingatia mawazo, pumzi, au maneno maalum (mantra) ili kuleta uwiano wa kimwili na kihisia. Meditation hutumiwa na watu wengi kama njia ya kuondoa msongo wa mawazo, kuongeza umakini, na kujenga ufahamu wa kina wa nafsi. Zoezi hili linaweza kufanywa mahali popote palipo tulivu na halihitaji vifaa maalum.

♥️🌼 Faida za Meditation.
Meditation ina faida nyingi za kimwili, kiakili, na kiroho. Kwa kimwili, husaidia kupunguza shinikizo la damu, kuimarisha usingizi, na kupunguza matatizo ya kiafya yanayosababishwa na msongo wa mawazo. Kihisia, meditation husaidia kuleta utulivu wa akili, kupunguza wasiwasi, na kuongeza hisia za furaha. Aidha, kiroho, zoezi hili huchangia kuongeza ufahamu wa ndani na kufanikisha hali ya amani. Kwa ujumla, meditation ni njia bora ya kuboresha maisha na kufikia ustawi wa kiakili na wa mwili.

1736534412807.jpg
 
Lakini pia tuseme tu kwamba pengine bila meditation kusingekua na uislam.

Kwa maana tabia ya mtume ya kupenda kukaa katika hali ya utulivu wa akili ndio iliyo pelekea akutane na malaika moja kwa moja.

Kwahiyo meditation inanguvu kuliko kawaida.

Tuendelee kumeditate ndugu zangu, aye 😅😅😅
 
SPIRITUAL MEDITATION (TAHAJUDI YA KIROHO).
View attachment 3197482
Spiritual Meditation ni aina ya meditation ambayo inakupeleka kujua wewe ni nini na vipi unatakiwa kuwa. Hii ni meditation ya kujitafuta, ni msako wa roho yako katika ulimwengu uliojaa uongo na kelele nyingi. Tangu ulipozaliwa umepewa utambulisho na watu wengine. Walisema mtoto wa kiume au wa kike amezaliwa, wakakuchagulia jina walilojisikia furaha wao kuliita, wakakupeleka kwenye nyumba za ibada na kukupa mafundisho usiyotaka lakini umejikuta umeyapokea, ukapelekwa shule na kuanza kufundishwa na kijazwa kichwani vitu mbalimbali. Ulimwengu na mazingira vimekupa utambulisho na kukufahamu kama mtu fulani, lakini je huo utambulisho unaojulikana ndiyo wewe halisi?

Wewe ni roho hakuna awezaye kukujua wala kukutambulisha wewe katika hali yako ya kiroho lakini utambulisho wa nje umekuziba ufahamu wa kujua wewe ni nini.

Ninaposema wewe ni nini ni lazima unielewe. Nani ni matokeo ya jinsi uonekanavyo, uongevyo na uitwavyo lakini Nini ni vile haswa ulivyo. Unavyojulikana na unavyoitwa sivyo ulivyo. Unaweza kukuta kuna mtu anatambulishwa kutokana na ukubwa wa mwili wake, utasikia "bonge mambo vipi" na yeye anaitikia poa. Au utasikia vipi mambo cheupe, wengine hutambulishwa kwa taaluma na kazi zao kwa mfano mwalimu, doctor n.k. Je huo utambulisho ndiyo wewe. Jibu ni hapana, kwa kuwa huo utambulisho wote unaishia mwilini na kwenye akili lakini siyo rohoni. Unaitwa doctor au mwalimu kutokana na vitu ulivyoweka kwenye akili yako lakini rohoni mwako wewe ni kitu kingine.

Imebidi niingie huko kidogo ili upate kunielewa ninachotaka kukufundisha kuhusu spiritual meditation. Huu ni msako wa roho yako, ni zoezi la kutafuta utambulisho wako hali (divine identify).q
Unaposema meditation ya kutafuta roho yangu, hapo swali linabaki mimi ni nani. Maana kilichotafutwa na roho yangu na sio mimi. Je mimi ni roho?
 
Meditation bora mtu akuelekeze ufanye mwenyewe na upate experiences zako mwenyewe. Kwa kusoma kitabu am afraid unaweza kuwa unafanya Meditation huku unatafuta experiences za aliyeandika kitabu, and this won't be a Meditation at all. Kama ni breath Meditation mtu akufundisha inavyofanyika then nawe unatoka na your own experiences. You will get your own story to tell. Thanks
 
Back
Top Bottom