Fahamu matumizi mbalimbali ya Baking Soda

Fahamu matumizi mbalimbali ya Baking Soda

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Wote tunafahamu kuwa Baking Soda hutumika katika uandaaji wa vyakula kama keki na mikate. Lakini huwa na matumizi mbalimbali ya nyumbani ikiwemo kuwa mbadala wa kusafishia kinywa kwa kuwa na uwezo wa kuua bakteria.​

1728648092750.png

Pia, baking soda ni nzuri kwa kuondoa madoa sugu. Inaweza kuchanganywa na sabuni kwa ajili ya kufua nguo, kusafisha mazulia, vyoo, na masinki. Hutumika kuondoa harufu mbaya kwenye jokofu, microwave na hata katika usafishaji wa viatu.

Baking soda ni njia bora ya kuondoa mabaki ya dawa za kuulia wadudu kwenye matunda na mboga kwa kuosha na machanganyiko wa maji ya moto.

Pia inatumika kung’arisha vifaa vya chuma kama vijiko, uma, na sufuria kwa kuchanganya na sabuni pamoja na maji ya moto kwa matokeo bora.

Kana una sinki limeziba unaweza kuzibua kwa kutumia mchanganyiko wa baking powder na vinegar saa kadhaa kisha mininia maji ya moto ili kuzibua uchafu.

Mchanganyiko wa baking soda na chumvi pia husaidia kufukuza wadudu kama siafu, sisimizi, na mende nyumbani, hivyo kuimarisha usafi na usalama.
 
Wote tunafahamu kuwa Baking Soda hutumika katika uandaaji wa vyakula kama keki na mikate. Lakini huwa na matumizi mbalimbali ya nyumbani ikiwemo kuwa mbadala wa kusafishia kinywa kwa kuwa na uwezo wa kuua bakteria.​

Pia, baking soda ni nzuri kwa kuondoa madoa sugu. Inaweza kuchanganywa na sabuni kwa ajili ya kufua nguo, kusafisha mazulia, vyoo, na masinki. Hutumika kuondoa harufu mbaya kwenye jokofu, microwave na hata katika usafishaji wa viatu.

Baking soda ni njia bora ya kuondoa mabaki ya dawa za kuulia wadudu kwenye matunda na mboga kwa kuosha na machanganyiko wa maji ya moto.

Pia inatumika kung’arisha vifaa vya chuma kama vijiko, uma, na sufuria kwa kuchanganya na sabuni pamoja na maji ya moto kwa matokeo bora.

Kana una sinki limeziba unaweza kuzibua kwa kutumia mchanganyiko wa baking powder na vinegar saa kadhaa kisha mininia maji ya moto ili kuzibua uchafu.

Mchanganyiko wa baking soda na chumvi pia husaidia kufukuza wadudu kama siafu, sisimizi, na mende nyumbani, hivyo kuimarisha usafi na usalama.
Napenda kujua tofauti ya baking soda &baking powder huwaga sielewi
 
Pia husafisha meno nakua meupe kabisa pamoja nakutoa harufu mbaya mdomoni.
utafanya hivi walau ×2 kwa wiki.
Chunusi naupele,
Kifupi inafaida nyingi sana mno hizo nichache kwenye nyingi.
 
Baking powder
Baking soda
Je ni vitu viwili tofauti..
Unavyosema inasafisha kunywa ana meno matumizi yake ni yapi
 
Back
Top Bottom