Fahamu mbinu mbalimbali za kuongeza mauzo ya biashara yako

Fahamu mbinu mbalimbali za kuongeza mauzo ya biashara yako

Biashara za Tanzania ni zaidi ya uijuavyo npo mkoa flani kanda ya ziwa kikazi nilichoona wanaofanya biashara ni wazawa na wenyeji tu nikawauliza wageni wng mbona nyie amchangamkii fursa wakaniambia wengi wao washafungua biashara ila zikafa ili wateja waje kununua kwako inabidii uwe kabila lao au uwe umeoa au kuolewa na mtu wa kabila lao.
Mmh!
 
Biashara za Tanzania ni zaidi ya uijuavyo npo mkoa flani kanda ya ziwa kikazi nilichoona wanaofanya biashara ni wazawa na wenyeji tu nikawauliza wageni wng mbona nyie amchangamkii fursa wakaniambia wengi wao washafungua biashara ila zikafa ili wateja waje kununua kwako inabidii uwe kabila lao au uwe umeoa au kuolewa na mtu wa kabila lao.
Du unataka kusema wafanya biashara wa huko ni wasuma tu na makabila mengine namna?
 
Hapa tanzania, karibia Biashara 1000+ huanzishwa kwenye Mwezi ya January na Kufikia mwezi wa November, Karibia 85% ya hizo biashara hufeli.

Wengi wetu tuliwahi kuwa kweye hiyo 85% ya biashara zinazo feli. Na wengine tuko kwenye ile 15% ya wanaondeleza biashars kwa bahati au kwa kuwa tuna elewa tunachokifanya.

Kuna mambo kadhaa ambayo tunayafanya vibaya na hivyo kutufanya kuwa wale wale, kufanya biashara zetu zisitofautiane na wengine kwa kuwa tunaona matokeo ni yale yale.

Ukitambua Kosa liko wapi, na hata kama bado biashara yako inasonga; Kutambua nini kinakufanya uwe yuleyule itasaidia kukuza biashara yako kwa kiasi kikubwa.

Ukifanya yafuatayo, nakuhaidi utapata matokeo mazuri na kwa mda mfupi.

1. "Kama Huwezi Nunua Vyote Kwa Pamoja, Huwezi Kununua Kimoja Wapo!"

Uliwahi kuanza kupungukiwa bidhaa dukani na pesa iliyopo mfukoni haitoshi? Mfano unauza Madaftari, Michele, Sukari, Mafuta , Na mengineyo ila ukaishiwa Madaftari na Mafuta labda na Unga. Kama hutoweza kuvinunua vyote kwa pamoja, huwezi kununua kimoja wapo.

Namaanisha kwamba; Umeishiwa madaftari, mafita na unga; Ukasema ngoja uanze kununua Unga kwa kuwa hela uliyo nayo haitoshi, basi ukinunua unga ukianza kuuza pesa utakayoipata utanunua Mafuta...Na ukianz kuuza mafuta ndipo utanunua Madaftari.Ina maana kwamba kila pesa itakayokuwa inaingia inatumika na sio Kuhifadhiwa.

Je, unafanya nini ili kukwepa hali hii?

2.Matumizi Yasizidi Mapato.

Unaweza kuwa umeweka vitu vya Laki Tano Dukani(Ni Mfano) Ukiaanza kuuza. sasa ukaanza kuagiza Vitu vya Ziada ambavyo Bei yake itazidi ile uliyoingiza mda huo, Basi utakuwa umejiingiza kwenye mzunguko ambao utafanya Ufunge Duka; Madeni!

Inamana kila hela utakayopata Utaanza luitumia kulipia bidhaa ulizoagiza mwanzo na bado hizi zitaanza kuisha na huna hela ya kununua nyingine maana imetumika kulipia bidhaa za awali hivyo utaendelea kujikopa ili uendelee kuwa na vitu Dukani. Process itajirudia na huyokuwa na Faida jivyo utafunga Duka

Nacho jaribu kukwambia ni kuwa usifanye matumizi yakazidi mapato.Numua Vile Unavyoweza kununua Na kubaki na Faida ya awali!

3.Epuka Mikopo

Hakuna litu ambacho kinaonelana kirahisi kama kupokea mkopo kutoka kwa rafiki au benki ili uendelee kukuza biashara yako. Jambo hili uonelana jema kwa kuwa wengi uahidi Kuweka riba chache na wengine kukupa mda mrefu wa marejesho.

Kadri siku zitakavyoenda...ndipo uatakapo gundua kuwa huwezi tena kuingiza faida au kulipa mkopo kwa wakati kwa kuwa labda wateja ni kidogo ila / au mahitaji yanaongezeka kila kukicha.

Badala ya Mikopo unaweza kuchagua Crowd Funding. Hapa jamii inayo kuzunguka itakupa Hela (Labda kuanzia 10,000/ Kila Mtu) Na In Return watapokea Punguzo la kiasi fulani wakiwa wana nunua vitu kutoka Dukani mwako na Pumguzo litaendelea kwa mda gani.

Hii ni rahisi maana sio mkopo, huto warudishia pesa bali huduma ya.kipekee labda punguzo la asilimia fulani mpaka kiasi alichokupa kikiishia kwenye hayo mapunguzo na kuongeza kidogo tu!

Faida nyingine ni kuwa utajipatia wateja wa paop kwa papo..Kwa kuwa hawato nunua kwingine bali kwako ili wapate punguzo.

Shida ni kwamba luwapata watakao fanya hivyo mara nyingi ni ngumu.

Unaweza kusambaza Offer yako kwa Vipeperushi au kutoa tangazo kwenye Local Radio Station.

4." Mteja Huwa Sahihi Wakati Wote!"

Ili biashara yako kuwa ya kitofauti na za wengine utahitaji kumuondolea mteja kitu kinachoitwa "No Money Out" Syndrome...Hichi kila mtu anacho. Kumshawishi mtu kunua bidhaa kwako kila mara na kila siku ni jambo ambalo unapaswa kufanya ili kufanikiwa. Na njia rahisi ya kufanya hivyo ni kwa kumfanya ajisikie huru, na anae thaminiwa. Hapa ni kwa kumsikiliza na kuepuka mabishano.

5.Tenga Fungu La Matangazo



Itimisho.

Natumai kuwa baadhi ya njoa hizi ulikuwa huzifahamu. Na kama umefunguka Share na unao wapenda...Na soma makal nyinhine za Ujasiriamali.
 
Nzuri sana,ila naamini ukikopa unakuwa na nidhamu ya matumizi kuliko ukifanya biashara bila kuwa na mkopo.
 
Nzuri sana,ila naamini ukikopa unakuwa na nidhamu ya matumizi kuliko ukifanya biashara bila kuwa na mkopo.
Yep....Ila sio kila mtu anae kopa anaweza ku manage biashara, faida na mkopo....Wengi wetu tutaanza kufikiria kurejesha mkopo..
Hivyo hautusaidii..bali unaleta hasara
 
Yep....Ila sio kila mtu anae kopa anaweza ku manage biashara, faida na mkopo....Wengi wetu tutaanza kufikiria kurejesha mkopo..
Hivyo hautusaidii..bali unaleta hasara
Binafsi nimeanza kuwa na adabu ya matumizi baada ya kuanza kukopa.Kabla ya hapo nilikuwa kila wakati nahisi ninazo.
 
Kama wewe ni mjasiriamali au mfanyabiashara unaehangaika kupata wateja kutokana na ushindani basi naomba unisikilize kwa umakini sana, kwani katika makala hii nataka nikuonyeshe mbinu ambayo itakusaidia:-

  1. Kuua ushindani kwenye soko lako na
  2. Kuwafanya wateja wavutiwe kuja kununua bidhaa/huduma unayotoa kutoka kwako badala ya washindani wako.


Mbinu hii nimejifunza kwenye kitabu kiitwacho Blue Ocean Strategy (Stratejia za Bahari ya Bluu) iliyoandikwa na Chan Kim.

Ndani ya kitabu hicho anazungumza stratejia za aina mbili:
  1. Red Ocean (yenye kufatwa na 90% ya wajasiriamali wanaohangaika) na
  2. Blue Ocean (yenye kufuatwa na wachache wenye kuteka soko)

Tofauti ya stretejia (mbinu) hizi mbili inatokana na mfano ambao ametoa wa mapapa wenye kutafuta samaki.

Anasema mfanyabiashara ni kama papa mwenye kutafuta eneo lenye samaki samaki kwa ajili ya kula. Na samaki ni mteja wa mfanyabiashara yule.

Papa huyo akigundua eneo lenye samaki na kuanza kula wale samaki, baada ya muda fulani atapita papa mwengine kuja kula samaki katika eneo lile.

Na baada ya muda atakuja mwengine na mwengine hadi itafika wakati papa hao wanakuwa wengi kuliko idadi ya samaki na wanashtukizia kuwa wanatafunana wenyewe kwa wenyewe hadi damu kumwagika na kufanya rangi ya ile bahari kuwa nyekundu, na ndio maana ikaitwa red ocean strategy.

Huo ndio mfano wa wafanyabiashara wengi.

Utakuta mtu anaanzisha duka lake. Mambo yake yanaenda vizuri na anaanza kupata wateja.

Mtu mwengine anaona ile biashara na kusema “Kumbe biashara ile inalipa! Wacha na mimi nianzishe duka langu.”,

Anaanzisha duka lake na kuingia kwenye ushindani na yule aliyefungua duka la mwanzo. Baada ya muda, mwengine nae anaanzisha duka lake na kuingia kwenye ushindani na wale wawili.

Inafika wakati mlolongo wa watu wanafungua biashara kama ile na wanaingia katika ushindani hadi wanafikia 20, 30 hali ya kuwa idadi ya wateja bado ni ileile.

Inafika wakati wanajikuta wapo katika ushindani na biashara zote zinakuwa zinaumia.

Lakini Blue Ocean Strategy inakufanya wewe kujichomoa katika eneo lile la bahari na kuenda katika eneo jengine ambalo halina mapapa na kuwavuta samaki kuja kwako.

Na kwa vile lile eneo ni lako na ushaweka bendera yako hata papa mwengine akija hawezi kushindana na wewe kwa sababu eneo lile unalifahamu vizuri na samaki wale wamevutiwa na wewe kuliko mapapa wengine.

Vipi unaanzisha Blue Ocean Strategy?


Kwanza unatakiwa kufahamu kuwa kuna aina mbili za wajasiriamali au wafanyabiashara ambao ni
  1. Generalist na
  2. Specialist
Generalist ni mfanyabiashara anayewalenga wateja wote na Specialist ni mfanyabiashara anayelenga kundi fulani tu la watu na anafanya hivyo kwa sababu anajuwa kuwa hakuna mtu mwengine kama yeye anayeweza kutatua matatizo ya kikundi hilo kama yeye.

Ingawa watu wengi wanaona ni bora kuwa generalist kwa sababu soko lake ni kubwa, kitu wasichokifahamu kuwa kuwa generalist haitaji taaluma kubwa na soko lenye taalum ndogo linakuwa na ushindani mkubwa kuliko soko lenye taaluma ndogo.

Lakini ukiwa specialist unakuwa na uwezo wa kuwanasa watu wengi kwa sababu wewe unaonekana kuwa ni mtaalamu mbele ya macho ya soko lako na watu wanakufata wewe na wapo tayari kukulipa pesa zaidi kuliko yule mtu ambaye anaonekana anafanya kila kitu (generalist).

Na mfano mzuri ni kama madaktari.

Daktari ambaye anatibu wagonjwa wote ni generalist (MD) na daktari ambaye ni specialist anaona wagonjwa wachache lakini analipwa pesa nyingi na super specialist analipwa pesa nyingi zaidi kuliko wote.

Na kama wewe unataka kuua soko lako basi huna budi kuwa specialist au hata super specialist.

Mfano mimi (Dr Said) nilivyoanza biashara yangu niliingia katika soko la web design ambalo lilikuwa na ushindani mkubwa.

Nilianza kuwatengenezea tovuti wafanyabiashara, lakini nikaona nikijiweka kama Web Designer watu watanifananisha na Web Designer wengine na kunihoji kuhusu bei zangu kuwa juu kulinganisha na web designers wengine.

Hivyo sikujiweka kama Web Designer, na hata nilipokuwa nawapigia simu nilikuwa nikiwaambia

“Hello! Kwa jina naitwa Dr. Said Said, ninawasaidia wafanyabiashara kama wewe kutumia tovuti kunasa wateja kwenye mtandao. Na sasa hivi natoa consultation ya bure ya saa 1. Je ungependa kupata consultation ya bure kujifunza namna unavyoweza kutumia tovuti yako kunasa wateja?”


Wengi walikuwa wanajibu kuwa wangependa kupata consultation hiyo.

Na mimi nikienda kule nawaonyesha njia wanazoweza kutumia kupata wateja kwenye biashara zao kupitia website (tovuti) na sio jinsi wanavyoweza kumiliki website yenye kupendeza.

Najua wateja wangu hawajali sana kuhusu kumiliki website nzuri kama wanavyojali kupata wateja kupitia website zao.

Kujiweka kwangu kama Specialist (Online Marketer) kumenisaidia sana kupata projects nyingi zenye thamani (Blue Ocean Strategy) badala ya kujitangaza kama web Designer ambayo ni Red Ocean fani yenye ushindani mkubwa.

Mbinu hiyo na wewe unaweza kuitumia katika biashara yoyote ile.

Tuchukulie mfano wa biashara ya tour:

Muda si mrefu nimetoka kupigiwa simu na mmiliki wa kampuni ya tour na anataka ushauri vipi aitumie website yake kupata wateja.

Kitu cha mwanzo nilichomwambia ni kujiposition vizuri kwenye soko kama specialist badala ya generalist, ushauri huohuo ambao niliokupa wewe nilimpa yeye.

Badala ya kusema sisi ni tour company ambao tunapokea wageni kutoka nje sema sisi tunaspecialise kuwasaidia kundi fulani la watu kupata jambo fulani.

Kwa mfano nina rafiki yangu ambaye yeye amejikita kwenye motorbike safari.

Anasema “Sisi tunashughulika na Adventure safari za Motorbike tu! Kama wewe hujui kuendesha pikipiki hapa sio kwako”.

Kwa haraka haraka unaweza kuona kuwa atapata wateja wachache lakini kwa vile hana ushindani, wateja anaowapata wanamtosha sana na anatengeneza pesa nzuri sana na anaweza kuweka chaji ambayo washindani wake hawawezi kuweka kwa sababu washindani wake hawafanyi motorbike safari.

Swali unalotakiwa kujiuliza nia nijiweke vipi kwenye soko kama mtaalam wa kitu fulani ili niwavute watu waje kwangu?

Siku zote angalia wateja wako wana matatizo gani na kitu gani maalumu utafanya.

Usijaribu kufanya mambo mengi . Chagua kitu kimoja tu cha kufanya.

Muhimu hilo tatizo liwepo katika soko na watu wachache waweze kutatua hilo tatizo. Kama wewe ni miongoni mwa hao wachache ambao wanaweza kutatua tatizo hilo basi nakuhakikishia utapata wateja wengi na utakuwa huna ushindani katika biashara yako.

Ifanyie kazi na unijulishe umefaidika vipi na mbinu hiyo.

Kama umependa makala hii basi utapenda video yangu niliyotengeneza yenye kukuonyesha Jinsi ya Kutumia Mtandao wa Facebook na Instagram Kunasa Wateja (Bofya hapa).

Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako,

Dr. Said Said
Mkurugenzi wa Online Profits

[Makala hii imechapwa na Abdallah Hemedi - Content Manager | Online Profits] .
mmh..Dr Said rafiki yangu....
nakukumbuka.karibu tena Zanzibar.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwana nini nyuzi za hivi wachangiaji huwa ni wachache saaana



Dr. Unaleta nondo kama hizi lini??
 
Hivi kweli umeelewa vizuri anachokielezea Dr. Said? Maana naona wewe badala ya kwenda kulia unakwenda kushoto mwa mada! Negativity will not take you anywhere! Learn the blue ocean strategy utaachana na hayo mawazo mgando!
 
Kama wewe ni mjasiriamali au mfanyabiashara unaehangaika kupata wateja kutokana na ushindani basi naomba unisikilize kwa umakini sana, kwani katika makala hii nataka nikuonyeshe mbinu ambayo itakusaidia:-

  1. Kuua ushindani kwenye soko lako na
  2. Kuwafanya wateja wavutiwe kuja kununua bidhaa/huduma unayotoa kutoka kwako badala ya washindani wako.


Mbinu hii nimejifunza kwenye kitabu kiitwacho Blue Ocean Strategy (Stratejia za Bahari ya Bluu) iliyoandikwa na Chan Kim.

Ndani ya kitabu hicho anazungumza stratejia za aina mbili:
  1. Red Ocean (yenye kufatwa na 90% ya wajasiriamali wanaohangaika) na
  2. Blue Ocean (yenye kufuatwa na wachache wenye kuteka soko)

Tofauti ya stretejia (mbinu) hizi mbili inatokana na mfano ambao ametoa wa mapapa wenye kutafuta samaki.

Anasema mfanyabiashara ni kama papa mwenye kutafuta eneo lenye samaki samaki kwa ajili ya kula. Na samaki ni mteja wa mfanyabiashara yule.

Papa huyo akigundua eneo lenye samaki na kuanza kula wale samaki, baada ya muda fulani atapita papa mwengine kuja kula samaki katika eneo lile.

Na baada ya muda atakuja mwengine na mwengine hadi itafika wakati papa hao wanakuwa wengi kuliko idadi ya samaki na wanashtukizia kuwa wanatafunana wenyewe kwa wenyewe hadi damu kumwagika na kufanya rangi ya ile bahari kuwa nyekundu, na ndio maana ikaitwa red ocean strategy.

Huo ndio mfano wa wafanyabiashara wengi.

Utakuta mtu anaanzisha duka lake. Mambo yake yanaenda vizuri na anaanza kupata wateja.

Mtu mwengine anaona ile biashara na kusema “Kumbe biashara ile inalipa! Wacha na mimi nianzishe duka langu.”,

Anaanzisha duka lake na kuingia kwenye ushindani na yule aliyefungua duka la mwanzo. Baada ya muda, mwengine nae anaanzisha duka lake na kuingia kwenye ushindani na wale wawili.

Inafika wakati mlolongo wa watu wanafungua biashara kama ile na wanaingia katika ushindani hadi wanafikia 20, 30 hali ya kuwa idadi ya wateja bado ni ileile.

Inafika wakati wanajikuta wapo katika ushindani na biashara zote zinakuwa zinaumia.

Lakini Blue Ocean Strategy inakufanya wewe kujichomoa katika eneo lile la bahari na kuenda katika eneo jengine ambalo halina mapapa na kuwavuta samaki kuja kwako.

Na kwa vile lile eneo ni lako na ushaweka bendera yako hata papa mwengine akija hawezi kushindana na wewe kwa sababu eneo lile unalifahamu vizuri na samaki wale wamevutiwa na wewe kuliko mapapa wengine.

Vipi unaanzisha Blue Ocean Strategy?

Kwanza unatakiwa kufahamu kuwa kuna aina mbili za wajasiriamali au wafanyabiashara ambao ni
  1. Generalist na
  2. Specialist
Generalist ni mfanyabiashara anayewalenga wateja wote na Specialist ni mfanyabiashara anayelenga kundi fulani tu la watu na anafanya hivyo kwa sababu anajuwa kuwa hakuna mtu mwengine kama yeye anayeweza kutatua matatizo ya kikundi hilo kama yeye.

Ingawa watu wengi wanaona ni bora kuwa generalist kwa sababu soko lake ni kubwa, kitu wasichokifahamu kuwa kuwa generalist haitaji taaluma kubwa na soko lenye taalum ndogo linakuwa na ushindani mkubwa kuliko soko lenye taaluma ndogo.

Lakini ukiwa specialist unakuwa na uwezo wa kuwanasa watu wengi kwa sababu wewe unaonekana kuwa ni mtaalamu mbele ya macho ya soko lako na watu wanakufata wewe na wapo tayari kukulipa pesa zaidi kuliko yule mtu ambaye anaonekana anafanya kila kitu (generalist).

Na mfano mzuri ni kama madaktari.

Daktari ambaye anatibu wagonjwa wote ni generalist (MD) na daktari ambaye ni specialist anaona wagonjwa wachache lakini analipwa pesa nyingi na super specialist analipwa pesa nyingi zaidi kuliko wote.

Na kama wewe unataka kuua soko lako basi huna budi kuwa specialist au hata super specialist.

Mfano mimi (Dr Said) nilivyoanza biashara yangu niliingia katika soko la web design ambalo lilikuwa na ushindani mkubwa.

Nilianza kuwatengenezea tovuti wafanyabiashara, lakini nikaona nikijiweka kama Web Designer watu watanifananisha na Web Designer wengine na kunihoji kuhusu bei zangu kuwa juu kulinganisha na web designers wengine.

Hivyo sikujiweka kama Web Designer, na hata nilipokuwa nawapigia simu nilikuwa nikiwaambia

“Hello! Kwa jina naitwa Dr. Said Said, ninawasaidia wafanyabiashara kama wewe kutumia tovuti kunasa wateja kwenye mtandao. Na sasa hivi natoa consultation ya bure ya saa 1. Je ungependa kupata consultation ya bure kujifunza namna unavyoweza kutumia tovuti yako kunasa wateja?”

Wengi walikuwa wanajibu kuwa wangependa kupata consultation hiyo.

Na mimi nikienda kule nawaonyesha njia wanazoweza kutumia kupata wateja kwenye biashara zao kupitia website (tovuti) na sio jinsi wanavyoweza kumiliki website yenye kupendeza.

Najua wateja wangu hawajali sana kuhusu kumiliki website nzuri kama wanavyojali kupata wateja kupitia website zao.

Kujiweka kwangu kama Specialist (Online Marketer) kumenisaidia sana kupata projects nyingi zenye thamani (Blue Ocean Strategy) badala ya kujitangaza kama web Designer ambayo ni Red Ocean fani yenye ushindani mkubwa.

Mbinu hiyo na wewe unaweza kuitumia katika biashara yoyote ile.

Tuchukulie mfano wa biashara ya tour:

Muda si mrefu nimetoka kupigiwa simu na mmiliki wa kampuni ya tour na anataka ushauri vipi aitumie website yake kupata wateja.

Kitu cha mwanzo nilichomwambia ni kujiposition vizuri kwenye soko kama specialist badala ya generalist, ushauri huohuo ambao niliokupa wewe nilimpa yeye.

Badala ya kusema sisi ni tour company ambao tunapokea wageni kutoka nje sema sisi tunaspecialise kuwasaidia kundi fulani la watu kupata jambo fulani.

Kwa mfano nina rafiki yangu ambaye yeye amejikita kwenye motorbike safari.

Anasema “Sisi tunashughulika na Adventure safari za Motorbike tu! Kama wewe hujui kuendesha pikipiki hapa sio kwako”.

Kwa haraka haraka unaweza kuona kuwa atapata wateja wachache lakini kwa vile hana ushindani, wateja anaowapata wanamtosha sana na anatengeneza pesa nzuri sana na anaweza kuweka chaji ambayo washindani wake hawawezi kuweka kwa sababu washindani wake hawafanyi motorbike safari.

Swali unalotakiwa kujiuliza nia nijiweke vipi kwenye soko kama mtaalam wa kitu fulani ili niwavute watu waje kwangu?

Siku zote angalia wateja wako wana matatizo gani na kitu gani maalumu utafanya.

Usijaribu kufanya mambo mengi . Chagua kitu kimoja tu cha kufanya.

Muhimu hilo tatizo liwepo katika soko na watu wachache waweze kutatua hilo tatizo. Kama wewe ni miongoni mwa hao wachache ambao wanaweza kutatua tatizo hilo basi nakuhakikishia utapata wateja wengi na utakuwa huna ushindani katika biashara yako.

Ifanyie kazi na unijulishe umefaidika vipi na mbinu hiyo.

Kama umependa makala hii basi utapenda video yangu niliyotengeneza yenye kukuonyesha Jinsi ya Kutumia Mtandao wa Facebook na Instagram Kunasa Wateja (Bofya hapa).

Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako,

Dr. Said Said
Mkurugenzi wa Online Profits

[Makala hii imechapwa na Abdallah Hemedi - Content Manager | Online Profits] .

Dr. Said nataka kukutana na wewe physically. Nakupatsje?
 
Biashara za Tanzania ni zaidi ya uijuavyo npo mkoa flani kanda ya ziwa kikazi nilichoona wanaofanya biashara ni wazawa na wenyeji tu nikawauliza wageni wng mbona nyie amchangamkii fursa wakaniambia wengi wao washafungua biashara ila zikafa ili wateja waje kununua kwako inabidii uwe kabila lao au uwe umeoa au kuolewa na mtu wa kabila lao.
hiyo hata Njombe iko kama wewe sio mbena au mkinga biashara lazima ife
 
Back
Top Bottom