Fahamu Mgogoro wa Taliban na Afghanistan

Fahamu Mgogoro wa Taliban na Afghanistan

Malengo makuu ya Marekani iliyowafanya wao wapeleke majeshi Afghanistan karibu malengo yote yalitekelezwa.
Malengo makuu ya Marekani kupeleka Majeshi Afghanstan takribani yote yalitimia , jambo liliobaki ni kuandaa mpango na makubaliano ya kuondoa majeshi yao kutoka Afghanistan baada ya miaka mingi majeshi yao kuwepo Afghanistan.
Mkuu, 'Abdul Nondo', nawe unaamini malengo yalifikiwa?

Malengo yangefikiwa, hali ya Marekani kuondoka isingekuwa ya vurugu kiasi hiki kinachoonekana.

Huu ni mfano mwingine wa kushindwa kufikia malengo yaliyowapeleka huko.

Bado kuna maswali mengi ambayo hayana majibu katika andiko lako. Nguvu ya Taliban nchini humo inatokana na nini?

Ni kitu gani hasa kinachowafanya wawe na nguvu, kuna makundi ya raia wa nchi hiyo wanaopenda sana aina yao ya uongozi?

Haya, kuna haya mengine ya pembeni: M7 anachukuwa wakimbizi wa Afghanistan, bila shaka kwa kitita alichoahidiwa kupewa! Dunia hii haiwezi kuishiwa na vituko kamwe!
 
E8-728EWQAIRv1s.jpeg
Aise.
 
Sheria zenu za kiislam za kutesa na kuuwana ndio zinachochea mauji maeneo mengi duniani ,Kama dunia isinge kuwa na uislam ingekuwa salama sana


USSR
Kwanza Taliban hawafuati sheria za Kiisilamu Bali Mila zao.

Kwa Dunia Ya sasa hakuna Nchi inayofuata sheria za kiisilimu 100% ila zipo zinazofuata kwa Asilimia kadhaa, na jambo moja ambalo ni Fact nyingi Zina Maisha Mazuri.

Nenda Middle East Angalia Qatar, UAE, Saudia, Oman Etc

Nenda Nchi za South East Asia Angalia Malyasia, Indonesia, Brunei etc.

Nchi zote hizo zimefanikiwa Kutengeneza welfare state, na ndio Uisilamu unavyofundisha. Wanamaisha Mazuri sana ni nadra kukuta watu Wana Umasikini wa kupindukia.

Hizi ni nchi na umasikini

Utaona Nchi zenye masikini wa chache nyingi ni za kiisilamu, na nchi zenye masikini wengi ukikuta za kiisilamu basi ni zile zilizogubikwa na Vita.
 
Kwanza Taliban hawafuati sheria za Kiisilamu Bali Mila zao.

Kwa Dunia Ya sasa hakuna Nchi inayofuata sheria za kiisilimu 100% ila zipo zinazofuata kwa Asilimia kadhaa, na jambo moja ambalo ni Fact nyingi Zina Maisha Mazuri.

Nenda Middle East Angalia Qatar, UAE, Saudia, Oman Etc

Nenda Nchi za South East Asia Angalia Malyasia, Indonesia, Brunei etc.

Nchi zote hizo zimefanikiwa Kutengeneza welfare state, na ndio Uisilamu unavyofundisha. Wanamaisha Mazuri sana ni nadra kukuta watu Wana Umasikini wa kupindukia.

Hizi ni nchi na umasikini

Utaona Nchi zenye masikini wa chache nyingi ni za kiisilamu, na nchi zenye masikini wengi ukikuta za kiisilamu basi ni zile zilizogubikwa na Vita.

kwaiyo unataka kusema uisilamu inabidi ubadilike kutokana na maitaji ya dunia
 
kwaiyo unataka kusema uisilamu inabidi ubadilike kutokana na maitaji ya dunia
Uisilamu hauhitaji kubadilika ila kila unavyo embrace Uisilamu ndio jinsi unavyopata state inayojali wananchi,

Kwa Historia ya Uisilamu kuna kipindi cha Abbasid Nchi inakuwa na hela mpaka anakosekana masikini wa kupewa zaka.

Ndio maana unakuta hizi Nchi zenye waisilamu wengi zikiwa na Rasilimali kidogo tu Basi Nchi nzima inakomboka.

Angalia Nigeria ama Gabon na wao Wana mafuta pia, Nigeria Ni nchi ya 10 Duniani kuwa na Mafuta mengi na ya kwanza Africa nzima, Wanazalisha Mabilioni ya Barells ya Mafuta.

Kwa Siku Nigeria wanazalisha kama Barell 2.5 million za mafuta, kwa bei ya Dola 66 tunaongelea mamia ya Billioni kwa siku na Trilioni zinazokaribia 100 kwa mwaka toka bidhaa moja tu.

Lakini Angalia Maisha ya watu wao, ni hovyo kabisa, masikini kulinganisha na Nchi zenye Mafuta Nyingine. Ila wangekuwa na mfumo wa welfare na kuachana na ubepari leo wangekuwa mbali.
 
Fahamu kundi la Taliban nchini Afghanistan , Mapambano yao dhidi ya Serikali ya Afghanstan na sababu Marekani kupeleka na kutoa Majeshi yake nchini humo.

Abdul Nondo,

Watu wengi wanapata kujiuliza kuhusu hawa Taliban,ni watu gani ,ni kundi gani,waliibuka vipi ,kwanini wanapigana ,wanataka nini na kwanini Marekani ilipeleka majeshi Afghanistan kwa miaka 20 yakawa huko ,kwanini tena Marekani ameyaondoa majeshi hayo sasa,tuwe wote kwa makini kupata kujua.

Nitajiaribu kugusia kila kilicho cha msingi ili ambao tulikuwa hatuelewi jambo hili tupate kulielewa hata kidogo.

Afghanistan ni nchi ambayo imepitia katika mikono ya viongozi wengi na kupitia mikiki mikiki,mapigano,mauaji na mapinduzi ya viongozi. Hii ni orodha ya viongozi wao kadhaa waliotawala hadi Taliban kuchukua madaraka ya kuongoza Serikali 1996.

Ammanullah kiongozi wa Afghanistan alitawala 1923, Mohammed Zahir Shah 1933, Mohammed Doud Khan 1973-1978,Nur Mohammed Tariki (1978-179),Hafizillah Amin Sept.1979-Dec 1979,Babraki Karmal 1979-1986, Muhammed Najibullah 1987-1992, Abdul rahim Hatif Aprili 16, 1992-April 28,1992, Sibghatullah Mojadded April 28, 1992- Juni 28 ,1992 na Burhanuddin Rabbani 28,Juni ,1992- hadi kuondolewa na kundi la Taliban mwaka 1996.

Ukitizama hapo kuna marais na viongozi wametawala kwa muda mfupi sana , ni kiashiria kwamba Afghanistan ilikuwa katika vita na mapigano ya mara kwa mara . Kuanzia miaka ya 1973 hadi miaka ya 1980 kulikuwa na vita ndani ya Afghanstan iliyochochewa pia na vita baridi kati ya Communist ,Mrusi na Mmarekani . Serikali nyingi za Afghanistan kuanzia miaka ya 1970's hadi 1996 ilikuwa ikiungwa mkono na Soviet (Urusi ) ,huku kukiwa na makundi sio chini 40 ya wapiganaji wa kiislamu chini ya mwamvuli wa jina "Mujahedeen" ambayo yalikuwa yakiungwa mkono na Marekani /CIA,Saudi Arabia , Pakistan na Osama Bin Laden kupambana dhidi ya wanajeshi wa Mrusi (Soviet) pia dhidi ya serikali iliyo madarakani iliyopewa msaada na Mrusi.

Katika hilo kundi la Mujahedeen mmoja wa kiongozi aliyepigana dhidi ya Soviet (Urusi ) alikuwa ni Muhammed Mullah Omary rafiki mkubwa wa Osama Bin Laden na alikuwa kiongozi na muasisi wa kundi la Taliban.(Taliban ikiwa na maana wanafunzi wa Madrasa).

Mwaka 1989 ,Mikhail Gorbachev Rais wa Urusi akasaini kuondoa wanajeshi wake Afghanistan kuanzia 1990.Hivyo serikali ya Afghanstan ikabaki bila msaada wa Mrusi . Kipindi hicho cha 1989 serikali ya Afghanstan ilikuwa chini ya
Muhammed Najibullah 1987-1992, Abdul rahim Hatif Aprili 16, 1992-April 28,1992, Sibghatullah Mojadded April 28, 1992- Juni 28 ,1992 na Burhanuddin Rabbani 28,Juni ,1992 hadi alipoondolewa na Taliban 1996.

Baada ya Urusi kuondoa majeshi yake nchini Afghanistan vita ikawa wao kwa wao sasa ,makundi ya Mujahedeen yakaanza kupigana wao kwa wao ,huduma za msingi zikawa hakuna ,watu wanakufa , maendeleo hakuna ,shida juu ya shida.Mullah Muhamed Omary ambaye ndiye muasisi wa kundi la Taliban ,Taliban ikiwa na maana wanafunzi wa madrasa chini ya Mullah Muhammed Omary na wanafunzi wake (Taliban) walianza kujipanga ili kuiondoa serikali iliyokuwa madarakani kwa lengo la kutambulisha utawala mpya utakaofuata sheria za dini ya kiislamu na utakao kuwa na utawala wa kiislamu.

Kiongozi wa Kundi la Taliban ,Mullah Muhamed Omary akipewa msaada na rafiki yake Osama Bin Laden , Serikali ya Pakistan na Saudi Arabia alianza kuvamia mji wa kwanza wa Kandahari mwaka 1994 akiwa na wanafunzi wake wapiganaji (Taliban ) 50 tuu, baadaye wanafunzi /wapiganaji waliongezeka zaidi kufikia 15,000 wakiamini Muhammed Mullah Omary ndiye mkombozi wa kuleta utawala wa amani na haki nchini Afghanistan.

Kufikia Septemba 1996 ,Kundi la Taliban chini ya Muhammed Mullah likawa tayari limeshika asilimia 90 ya nchi nzima pamoja na mji mkuu wa Afghanistan , Kabul .

Hatimaye Taliban chini ya Mullah Muhammed Omary ikaunda serikali yenye kufuata sheria za kiislamu. Rais wa nchi hiyo Burhanuddin Rabbani akakimbia nchi 1996.

Mullah Muhammed Omary kiongozi wa kundi /Serikali ya Taliban nchini Afghanistan akamkaribisha Osama Bin Laden kiongozi wa kundi la AlQaeda kukaa Afghanistan, hivyo makao makuu ya Alqaeda yakaw Afghanistan . Serikali ya Taliban nchini Afghanistan ilikuwa ina tambuliwa kama serikali halali na nchi tatu tuu , Pakistan, United Arab of Emirates na Saudi Arabia tuu nchi zingine hazikuwahi itambua serikali ya Taliban nchini Afghanistan kama ni serikali halali.

Ndio maana ukisoma mlolongo wa utawala nchini Afghanistan hukuti sehemu yeyote wametaja utawala wa Taliban bali utakuta wametaja utawala wa Burhanuddin Rabbani kuanzia 28-Juni 1992 hadi 2001 mbali na kwamba 1996 Rabbani alikimbia nchi, na kiongozi aliyefuata wanataja alifuata Hamid Karzai 2001 kabla ya Ashraf Ghani 2014 Septemba huyu aliyekimbia nchi juzi .Hivyo utawala wa Taliban nchini Afghanistan ulitambuliwa na nchi tatu tuu.

Ilipofika Septemba 11 ,Osama Bin Laden akaishambulia Marekani (September Eleven Attack katika jengo la World Trade Center) watu zaidi ya 3000 walifariki.

Rais wa Marekani wakati huo George W. Bush, NATO na marafiki wenza wakawaambia Afghanistan chini ya Taliban wamkabidhi Osama Bin Laden kwao ila Afghanistan chini ya Taliban wakagoma na kukataa katakata.

Marekani kwa kushirikiana na NATO na nchi zingine washirika kama Ufaransa wakaamua kuchukua maamuzi ya kuvamia Afghanistan na wakang'oa utawala wa Taliban nchini Afghanistan mwaka 2001,wakisema utawala wa Taliban ulikuwa una saidia na kuficha makundi ya Kigaidi kama Alqaeda chini ya Osama Bin Laden, AlQaeda na Taliban wakakimbilia Pakistan.

Marekani wakanui kuingiza majeshi yao (Deployment) katika nchi ya Afghanstan baada tuu ya kuondoa utawala wa Taliban ,kwa sababu za maslahi ya taifa lao (National interests ) ,kwa kutekeleza malengo makuu matatu.

1.Kukaa Afghanistan ili kusambaratisha kabisa kundi la AlQaeda .

2.Kukaa Afghanistan ili kuhakikisha kwamba ardhi ya nchi ya Afghanstan haitatumiwa tena kama sehemu ya kusaidia, kuficha na kutoa mafunzo kwa makundi ya Kigaida dhidi ya nchi Marekani.

3.Kukaa Afghanistan hadi watakapompata Osama Bin Laden.

Serikali ya muda /mpito(Interim Government ) ikawekwa ndani ya Afghanstan , Hamid Karzai akawa Rais wa Afghanistan kuanzia 2001 hadi 2014, kukawa na mfumo wa chaguzi na Demokrasia.

Majeshi ya Marekani yakiwa nchini Afghanistan wakiendelea kutekeleza missions na malengo yao makuu matatu , huku wakitoa mafunzo ya kijeshi kwa wanajeshi wa Afghanistan, wakilinda Amani ndani ya Afghanstan na kupigana vita dhidi ya makundi ya kiasi kama Taliban, huku Serikali ya Marekani ikiendelea kulipa mishahara wanajeshi wa Afghanistan, kuwapa silaha na vyenzo vyote vya kijeshi walivyohitaji kupata.

Malengo makuu ya Marekani iliyowafanya wao wapeleke majeshi Afghanistan karibu malengo yote yalitekelezwa.

1.Walifanikiwa kumuua Kiongozi wa kundi la Aqaeda Osama Bin .Mei 2 ,2011.

2.Walifanikiwa kusambaratisha kundi la AlQaeda.

3.Suala la Afghanistan kutotumiwa kama ardhi ya kuficha , kusaidia na kufunza Magaidi dhidi ya Marekani hasa AlQaeda ,hili suala utekelezaji wake ni kuhakikisha ya kwamba Afghanistan inakuwa nchi ya Amani, serikali ya Afghanstan ijadiliane na kundi la Taliban kuongoza nchi yao ya Afghanstan pamoja,ndiyo wanaweza kwa pamoja kuzuia nchi yao ya Afghanstan isiwe ardhi ya kuficha,kufunza na kusaidia makundi ya Kigaida yenye shabaha ya kuishambulia Marekani.

Malengo makuu ya Marekani kupeleka Majeshi Afghanstan takribani yote yalitimia , jambo liliobaki ni kuandaa mpango na makubaliano ya kuondoa majeshi yao kutoka Afghanistan baada ya miaka mingi majeshi yao kuwepo Afghanistan.

Mpango wa kuyaondoa Majeshi ya Marekani nchini Afghanstan alianza nao Barack Obama , yeye alinuia kufikia mwisho mwaka 2014 atatoa Majeshi ya Marekani nchini Afghanstan. Msisitizo mkubwa uliokuwa unawekwa na Marekani ni makundi ya kisiasa nchini Afghanstan yakae pamoja na kukubaliana pamoja wawe wamoja kwa maendeleo ya nchi yao.

Obama alikuwa akimsisitiza sana Hamid Karzai kukaa meza moja na kundi la Taliban ili nchi iwe na amani.Bahati mbaya hadi Obama anamaliza utawala wake hakufanikiwa kuondoa majeshi ya Marekani Afghanstan.

Katika utawala wa Rais Trump. Kuanzia mwaka 2018 Rais Trump alianza kuonesha nia ya kuondoa majeshi ya Marekani kutoka Afghanstan , Afghanstan ikiwa chini ya Rais Ashrafi Ghani aliyeingia madarakani Septemba 2014 baada ya Hamid Karzai , kulianza kufanyika jitahida za mazungumzo kati ya Serikali ya Marekani chini ya Trump na kundi la Taliban ili kutafuta suluhu ya amani na Marekani iondoe majeshi yake nchini Afghanistan.Kwani taarifa zinasema tangu 2007 , takribani wanajeshi 6000 wa Marekani wamefariki , NATO wanajeshi 1100 wamefariki , Wanajeshi wa Afghanistan 73000 wamefariki, Taliban wanajeshi wamefariki . Huku Jeshi la Taliban likiendelea kupanuka ikikadiriwa kuwa na wapiganaji kati ya 60000 hadi 100,000.

Katika mchakato wa kuhakikisha Marekani inatoa majeshi yake Afghanistan na kuhakikisha Afghanistan inabaki na Amani . Tar 29 , Februari 2020 Serikali ya Marekani chini ya Donald Trump na kundi la Talibani wawakilishi wa pande zote walikutana Qatar -Doha na kuingia Makubaliano yaliyoitwa,

"Agreement for Bringing Peace to Afghanistan
between the Islamic Emirate of Afghanistan which is not recognized by the United States
as a state and is known as the Taliban and the United States of America."

Makubaliano haya yalijumuisha vifungu vifuatavyo.

1.Marekani kuondoa majeshi yake Afghanstan, miezi 14 ,baada ya Februari 2020 yaani kufikia Mei 1 2021.

2 .Kuwe na Mazungumzo ya amani kati ya Kundi la Taliban na serikali ya Afghanstan ili kuunda serikali ya pamoja (To enter into power sharing negotiations with Afghanstan Government) , pamoja na kusitisha mapigano.

3.Taliban pamoja na serikali ya Afghanstan kwa pamoja wazuie na wasiruhusu kundi lolote la Kigaidi kujificha ,kukaa na kupata mafunzo nchini Afghanistan dhidi ya Marekani au nchi yeyote.

Bahati mbaya hadi Rais Trump anaondoka madarakani hakufanikiwa kuondoa majeshi yote ya Marekani nchini Afghanstan. Ila alikuwa tayari ameanza kupunguza majeshi kutoka Afghanistan kutoka idadi ya wanajeshi 15,500 hadi 2500 .

Baada ya Rais Joe Biden kuingia madarakani , hili jambo la majeshi ya Marekani nchini Afghanstan lilikuwa na sura mbili , moja ilikuwa ni ahadi yake katika kampeni kwamba ataondoa majeshi yote ya Marekani kutoka Afghanstan lakini mbili alikuta kuna makubaliano tayari yaliyowekwa na Serikali ya Marekani chini ya Rais Donald Trump na Kundi la Taliban mnamo Februari 2020 ya kuondoa majeshi ya Marekani nchini Afghanstan kuanzia Mei 1 ,2021 .

Huku wanamgambo wa Taliban wakimkumbusha Rais Joe Biden juu ya makubaliano kati yao na Marekani ya kuondoa majeshi Mei 1 ,2021 kwamba asivunje Mkataba kabisa .

Rais Biden hakuwa na namna zaidi ya kuangalia namna ya kutekeleza makubaliano hayo , ila aliwaomba Taliban wakutane , Februari 2021 ili kujadili na kupitia tena hayo makubaliano ya Februari 2020 chini ya Trump.

Februari 2021 ,katika Mji wa Doha , Qatar. Kundi la Taliban likiwakilishwa (Mkuu wa Kamisheni ya siasa ) ,Abdul Ghan Baradar huku Marekani ikiwakilishwa na Mwanadiplomasia wa Marekani Zalmay Khalilzad , jambo kubwa lililojadiliwa ni kuongeza muda wa kuondoka Afghanstan ambapo ilikubaliwa kwamba Serikali ya Marekani chini ya Rais Biden itaondoa Majeshi yake Tar 11 Septemba 2021 badala ya Mei 1 ,2021 iliyoekwa na Trump ila Biden alipaswa kutoa Majeshi yote siku Septemba 11 (Siku ya kuenzi waliokufa katika shambulio la Septemba 11 ,2001).

Ila bila kutarajia Rais Biden aliamua kuondoa Majeshi yote ya Marekani kutoka Afghanstan Aprili 2021 ,huku kundi la Taliban likipata Mwanya wa kujipanua zaidi kuelekea mji mkuu wa Kabul na miji mingine . Hadi sasa haijulikani Rais wa nchi hiyo Ashraf Ghani aliyetorika tar 15 Agost 2021, ameenda nchi gani au mji gani aliandika kabla ya kutoroka kupitia mtandao wake wa Facebook kwamba "Nachukua maamuzi magumu ya kuondoka kupisha wanamgambo wa Taliban ambao wanataka urais , maamuzi haya yana lengo la kulinda wananchi wangu kuliko kulinda cheo changu, najua kama ningelibaki wananchi wengi wazalendo wangekufa na mji wa Kabuli ungeharibiwa sana " .Mbali na maneno haya mazito ya Rais Ashrafi Ghani bado wachambuzi wa mambo na wananchi baadhi wanamuona kama ni muoga .

Rais wa Marekani baada ya tukio hili aliidhinisha kundi la wanajeshi 6000 kwenda kusaidia kuwaondoa Rai wa Marekani, mafisa wake na wananchi wa Afghanistan ambao walijitoa miaka 20 kufanya kazi na mafisa wa Marekani kwa lengo la kuwapa VISA kuishi Marekani.Taliban walionywa katika hatua hii ya Marekani kuondoa watu wake Talib isihatarishe maisha ya Raia wa Marekani hata mmoja ,ikifanya hivyo Marekani itajibu.

Watu wengi wanatokea kumlaumu Joe Biden kwa maamuzi ya kuondoa Majeshi Afghanstan kwa uharaka , Joe Biden amejibu kwa kusema hajutii maamuzi yake kwani hakuna maslahi yeyote kwa nchi ya Marekani kwa kuendelea kuyaweka majeshi yake nchini Afghanistan ."Staying in Afghanistan is not national interest"

Akisema malengo yote ya kuweka Majeshi ya Marekani Afghanstan tayari yametimia kumuuwa Osama , kusambaratisha AlQaeda na kuhakikisha Afghanistan haitumiki kama ngome ya magaidi dhidi ya Marekani .

Rais Biden aliendelea kusema kwamba ameingia ofisini akakuta tayari kuna makubaliano yaliyowekwa kati ya Trump na Taliban tangu Februari 2020 kwamba hadi mwezi Mei 2021 Majeshi yote ya Marekani yatapaswa kuondoka ."I inherited a deal that Trump negotiated with Taliban under his agreement would be out May 1,2021.

Hakukuwa na namna ya kuacha majeshi sababu hakukuwa na makubaliano ya amani na kulinda watu wetu ikiwa majeshi hayataondoka baada ya Mei 2021 ambaye yeye aliomba iwe Septemba 2021.(He said ,No agreement to protect our forces and people after Mei 1 ,2021) "No status if Stability after May one "

Watu wanamlaumu kwamba anaiacha Afghanistan katika machafuko na watu kuendelea kufa , Rais Biden anasema Mission ya Marekani nchini Afghanstan haikuwa kujenga Taifa au kuimarisha Demokrasia bali mission ilikuwa kuzuia ugaidi dhidi ya Nchi ya Marekani. (Mission is not National building , not creating unified , centralized Democracy but to prevent a terrorist attack on American Homeland .

Rais Biden ,anaendelea kusema hakuna muda rasmi au muda mzuri wa kuondoa majeshi zaidi ya viongozi wa Serikali ya Afghanstan na Taliban kutafuta suluhu za kisiasa jambo ambalo alimshauru Rais Ashrafi Ghani walipozungumza Juni 2021 ,ila Ghani alionesha kutaka kutumia nguvu na kuinua silaha badala ya suluhu ya amani na mazungumzo.

Anasema ,"Majeshi ya Marekani hayawezi na hayapaswi kuendelea kupigana katika vita na kufa katika vita ikiwa majeshi ya Afghanstan hayapo tayari kujipigania wao wenyewe"

"American troops cannot and should not be fighting in a war and dying in a war that Afghanistan forces are not willing to fight for themselves".

Joe Biden akiendelea kusema , Marekani itaendelea kulinda sera yake ya mambo ya nje (Foreign Policy) kuheshimu haki za binadamu , kuzuia vita na mapigano kama ambavyo mara zote wanafanya Dunia nzima ila sio kwa kuendekelea kuweka Majeshi nchini Afghanistan (Not through endless military deployment).

Huku upande wa Taliban wanaendelea kutangaza kwamba nchi itakuwa ya amani , ila wananchi wanaonekana kuwa na hofu kuwa chini ya utawala wa Taliban , wakikumbuka mateso waliyopitia 1996 hadi 2001 chini ya utawala wao , utawala wa nguvu na kutumia sheria kali . Kupiga mawe wazinifu hadi kufa, kutoruhusu mziki wala kuangalia Tv , kulazimisha kuvaa hijabu kufunika nyuso kwa wanawake .

Lengo kubwa la Taliban ni kusimamisha utawala wa kiislamu na utakaofuata sheria za kiislamu.

Kiongozi na muasisi wa kundi la Taliban aliitwa Mullah Mohammed Omary ,ambaye ndiye alikuwa kiongozi mkubwa yaani Amir -Ali-Muuminin mkuu wa Rahbar Shura (Mkuu wa Baraza linalofanya maamuzi yote juu ya siasa na Jeshi ).Mullah Muhammed Omary alifariki nchini Pakistan hospital ya Karachi mwaka 2013 kwa ugonjwa wa TB lakini kifo chake kilitangazwa na Taliban mwaka 2015.

Kiongozi Mkubwa aliyefuata baada ya Mullah Muhamed Omary ni Mullah Akhtar Mohammed Mansour ambaye aliuwawa 2016 na Marekani nchini Pakistan.

Kiongozi wa sasa wa kundi la Taliban ni Mawlawi Haibutullah Akhundzada. Akisaidiwa na viongozi wengine Mullah Muhammed Yakoub , Mullah Abdallah Ghan Baradar , Sirijuddin Haqqan pia wana idara mbalimbali (Commission) zikisimama kama wizara kwa lugha ya kawaida.

Imeandaliwa kwa kukusanya taarifa mbalimbali kutoka katika vyanzo vya magazeti Washington Posts, Vyombo vya habari CNN, ALJAZEERA,BBC na vyombo vingine lakini vitabu mbalimbali juu ya Mapigano ya Taliban na Afghanistan.

Ahsante.

Imeandaliwa na,

Abdul Omary Nondo.
Safi mzeee...sijawahi kujua kuwa upo jf...naomba uandike makala kuelezea urafiki ulikuwepo baina ya osama,mullah omar na marekani kabla hawajagombana
 
Pmj sana mkuu uko vzr Sana
siku moja nikiwa na ole sabaya usku kati ya saa nne usku mwak jan mwez wa tano HV ole sabaya alikupigia simu na ulifurahi Sana [emoji38][emoji38] naomba usibishe mmkuu sabay alikuwa na nmba zako anapenda kukupigiaa Sana kukusihii kuacha kumkosoa jiwe ....au siwew
 
Uisilamu hauhitaji kubadilika ila kila unavyo embrace Uisilamu ndio jinsi unavyopata state inayojali wananchi,

Kwa Historia ya Uisilamu kuna kipindi cha Abbasid Nchi inakuwa na hela mpaka anakosekana masikini wa kupewa zaka.

Ndio maana unakuta hizi Nchi zenye waisilamu wengi zikiwa na Rasilimali kidogo tu Basi Nchi nzima inakomboka.

Angalia Nigeria ama Gabon na wao Wana mafuta pia, Nigeria Ni nchi ya 10 Duniani kuwa na Mafuta mengi na ya kwanza Africa nzima, Wanazalisha Mabilioni ya Barells ya Mafuta.

Kwa Siku Nigeria wanazalisha kama Barell 2.5 million za mafuta, kwa bei ya Dola 66 tunaongelea mamia ya Billioni kwa siku na Trilioni zinazokaribia 100 kwa mwaka toka bidhaa moja tu.

Lakini Angalia Maisha ya watu wao, ni hovyo kabisa, masikini kulinganisha na Nchi zenye Mafuta Nyingine. Ila wangekuwa na mfumo wa welfare na kuachana na ubepari leo wangekuwa mbali.

kwanini haujagusia swala la terrolism???
 
kwanini haujagusia swala la terrolism???
Ni Terrorism sio Terrolism.

Mkuu definition Ya Terrorism ni mtu anaetia hofu, huwa hawa wanaua ama kufanya Uhalifu Bila Material gain, Taliban sio Terrorist sababu inajulikana kabisa wa nataka Nchi hawa ni waasi,

Kuhusu Uisilamu na ugaidi Almost Maeneo yote yenye ugaidi kuna mkono wa USA na washirika wake.

Miaka kadhaa iliopita Libya, Iraq, Syria, Yemen, Somalia na kwengineko zilikuwa ni nchi zenye Maendeleo na maisha yanakwenda kama kawaida, hao jamaa kuingia Affairs za watu na kupindua viongozi, kufadhili makundi na kuua Raia wasio na hatia ndio wanaleta machafuko kila eneo.

Kuhudumia Jeshi mkuu si jambo la kitoto, tunazungumzia matrilioni ya Hela, wanajeshi most of times hawazalishi imagine umlishe, umvishe, umnunulie silaha, umlipe etc unafkiri tu somewhere unaweza ukaanzisha kikundi cha ugaidi ukawa na silaha na funds za kuweka watu kambini bila ufadhili?

Magaidi wengi wanafadhiliwa na Nchi kubwa na Historia Angalia vikundi vingi vya ugaidi zamani vilikuwa funded na USA. Hata hawa wetu AL shabaab ukiangalia Historia yao imeanzishwa na mwanadada Samantha.

Tafuta Makundi yote ya kigaidi kuanzia Hao kina isis mpaka huku kwetu Al shabaab wanaua zaidi waisilamu kushinda watu wowote, zaidi ya Asilimia 90 ya watu wanaouliwa ni waisilamu, why vikundi vimavyojinasibisha na Uisilamu vinaua kila siku waisilamu na hata havitetei haki za waisilamu.

Kama kweli kuna vikundi vya waisilamu
1. Palestine wasingekuwa wanaouliwa vile.
2. Tumeona Myanmar waisilamu wanavyochinjwa kwa maelfu
3. Tunaona Uyghur China waisilamu wanavyoteswa.

Kote huko husikii vikundi vya waisilamu wala hakuna anaewatetea, ila kina Isis Wana operate Maeneo ambayo ni almost 100% waisilamu na wanaua waisilamu, huoni hizi ni danganya toto tu?.
 
nikadhani sasa naenda kupata uchambuzi wa maana kumbe habari ni zile zile ambazo kila mtu anazijua hkn uchambuzi wowote wa maana ulioufanya hpo zaidi kuzipata kwa kifupi sn kwenye blogs uchwara
 
Fahamu kundi la Taliban nchini Afghanistan , Mapambano yao dhidi ya Serikali ya Afghanstan na sababu Marekani kupeleka na kutoa Majeshi yake nchini humo.

Abdul Nondo,

Watu wengi wanapata kujiuliza kuhusu hawa Taliban,ni watu gani ,ni kundi gani,waliibuka vipi ,kwanini wanapigana ,wanataka nini na kwanini Marekani ilipeleka majeshi Afghanistan kwa miaka 20 yakawa huko ,kwanini tena Marekani ameyaondoa majeshi hayo sasa,tuwe wote kwa makini kupata kujua.

Nitajiaribu kugusia kila kilicho cha msingi ili ambao tulikuwa hatuelewi jambo hili tupate kulielewa hata kidogo.

Afghanistan ni nchi ambayo imepitia katika mikono ya viongozi wengi na kupitia mikiki mikiki,mapigano,mauaji na mapinduzi ya viongozi. Hii ni orodha ya viongozi wao kadhaa waliotawala hadi Taliban kuchukua madaraka ya kuongoza Serikali 1996.

Ammanullah kiongozi wa Afghanistan alitawala 1923, Mohammed Zahir Shah 1933, Mohammed Doud Khan 1973-1978,Nur Mohammed Tariki (1978-179),Hafizillah Amin Sept.1979-Dec 1979,Babraki Karmal 1979-1986, Muhammed Najibullah 1987-1992, Abdul rahim Hatif Aprili 16, 1992-April 28,1992, Sibghatullah Mojadded April 28, 1992- Juni 28 ,1992 na Burhanuddin Rabbani 28,Juni ,1992- hadi kuondolewa na kundi la Taliban mwaka 1996.

Ukitizama hapo kuna marais na viongozi wametawala kwa muda mfupi sana , ni kiashiria kwamba Afghanistan ilikuwa katika vita na mapigano ya mara kwa mara . Kuanzia miaka ya 1973 hadi miaka ya 1980 kulikuwa na vita ndani ya Afghanstan iliyochochewa pia na vita baridi kati ya Communist ,Mrusi na Mmarekani . Serikali nyingi za Afghanistan kuanzia miaka ya 1970's hadi 1996 ilikuwa ikiungwa mkono na Soviet (Urusi ) ,huku kukiwa na makundi sio chini 40 ya wapiganaji wa kiislamu chini ya mwamvuli wa jina "Mujahedeen" ambayo yalikuwa yakiungwa mkono na Marekani /CIA,Saudi Arabia , Pakistan na Osama Bin Laden kupambana dhidi ya wanajeshi wa Mrusi (Soviet) pia dhidi ya serikali iliyo madarakani iliyopewa msaada na Mrusi.

Katika hilo kundi la Mujahedeen mmoja wa kiongozi aliyepigana dhidi ya Soviet (Urusi ) alikuwa ni Muhammed Mullah Omary rafiki mkubwa wa Osama Bin Laden na alikuwa kiongozi na muasisi wa kundi la Taliban.(Taliban ikiwa na maana wanafunzi wa Madrasa).

Mwaka 1989 ,Mikhail Gorbachev Rais wa Urusi akasaini kuondoa wanajeshi wake Afghanistan kuanzia 1990.Hivyo serikali ya Afghanstan ikabaki bila msaada wa Mrusi . Kipindi hicho cha 1989 serikali ya Afghanstan ilikuwa chini ya
Muhammed Najibullah 1987-1992, Abdul rahim Hatif Aprili 16, 1992-April 28,1992, Sibghatullah Mojadded April 28, 1992- Juni 28 ,1992 na Burhanuddin Rabbani 28,Juni ,1992 hadi alipoondolewa na Taliban 1996.

Baada ya Urusi kuondoa majeshi yake nchini Afghanistan vita ikawa wao kwa wao sasa ,makundi ya Mujahedeen yakaanza kupigana wao kwa wao ,huduma za msingi zikawa hakuna ,watu wanakufa , maendeleo hakuna ,shida juu ya shida.Mullah Muhamed Omary ambaye ndiye muasisi wa kundi la Taliban ,Taliban ikiwa na maana wanafunzi wa madrasa chini ya Mullah Muhammed Omary na wanafunzi wake (Taliban) walianza kujipanga ili kuiondoa serikali iliyokuwa madarakani kwa lengo la kutambulisha utawala mpya utakaofuata sheria za dini ya kiislamu na utakao kuwa na utawala wa kiislamu.

Kiongozi wa Kundi la Taliban ,Mullah Muhamed Omary akipewa msaada na rafiki yake Osama Bin Laden , Serikali ya Pakistan na Saudi Arabia alianza kuvamia mji wa kwanza wa Kandahari mwaka 1994 akiwa na wanafunzi wake wapiganaji (Taliban ) 50 tuu, baadaye wanafunzi /wapiganaji waliongezeka zaidi kufikia 15,000 wakiamini Muhammed Mullah Omary ndiye mkombozi wa kuleta utawala wa amani na haki nchini Afghanistan.

Kufikia Septemba 1996 ,Kundi la Taliban chini ya Muhammed Mullah likawa tayari limeshika asilimia 90 ya nchi nzima pamoja na mji mkuu wa Afghanistan , Kabul .

Hatimaye Taliban chini ya Mullah Muhammed Omary ikaunda serikali yenye kufuata sheria za kiislamu. Rais wa nchi hiyo Burhanuddin Rabbani akakimbia nchi 1996.

Mullah Muhammed Omary kiongozi wa kundi /Serikali ya Taliban nchini Afghanistan akamkaribisha Osama Bin Laden kiongozi wa kundi la AlQaeda kukaa Afghanistan, hivyo makao makuu ya Alqaeda yakaw Afghanistan . Serikali ya Taliban nchini Afghanistan ilikuwa ina tambuliwa kama serikali halali na nchi tatu tuu , Pakistan, United Arab of Emirates na Saudi Arabia tuu nchi zingine hazikuwahi itambua serikali ya Taliban nchini Afghanistan kama ni serikali halali.

Ndio maana ukisoma mlolongo wa utawala nchini Afghanistan hukuti sehemu yeyote wametaja utawala wa Taliban bali utakuta wametaja utawala wa Burhanuddin Rabbani kuanzia 28-Juni 1992 hadi 2001 mbali na kwamba 1996 Rabbani alikimbia nchi, na kiongozi aliyefuata wanataja alifuata Hamid Karzai 2001 kabla ya Ashraf Ghani 2014 Septemba huyu aliyekimbia nchi juzi .Hivyo utawala wa Taliban nchini Afghanistan ulitambuliwa na nchi tatu tuu.

Ilipofika Septemba 11 ,Osama Bin Laden akaishambulia Marekani (September Eleven Attack katika jengo la World Trade Center) watu zaidi ya 3000 walifariki.

Rais wa Marekani wakati huo George W. Bush, NATO na marafiki wenza wakawaambia Afghanistan chini ya Taliban wamkabidhi Osama Bin Laden kwao ila Afghanistan chini ya Taliban wakagoma na kukataa katakata.

Marekani kwa kushirikiana na NATO na nchi zingine washirika kama Ufaransa wakaamua kuchukua maamuzi ya kuvamia Afghanistan na wakang'oa utawala wa Taliban nchini Afghanistan mwaka 2001,wakisema utawala wa Taliban ulikuwa una saidia na kuficha makundi ya Kigaidi kama Alqaeda chini ya Osama Bin Laden, AlQaeda na Taliban wakakimbilia Pakistan.

Marekani wakanui kuingiza majeshi yao (Deployment) katika nchi ya Afghanstan baada tuu ya kuondoa utawala wa Taliban ,kwa sababu za maslahi ya taifa lao (National interests ) ,kwa kutekeleza malengo makuu matatu.

1.Kukaa Afghanistan ili kusambaratisha kabisa kundi la AlQaeda .

2.Kukaa Afghanistan ili kuhakikisha kwamba ardhi ya nchi ya Afghanstan haitatumiwa tena kama sehemu ya kusaidia, kuficha na kutoa mafunzo kwa makundi ya Kigaida dhidi ya nchi Marekani.

3.Kukaa Afghanistan hadi watakapompata Osama Bin Laden.

Serikali ya muda /mpito(Interim Government ) ikawekwa ndani ya Afghanstan , Hamid Karzai akawa Rais wa Afghanistan kuanzia 2001 hadi 2014, kukawa na mfumo wa chaguzi na Demokrasia.

Majeshi ya Marekani yakiwa nchini Afghanistan wakiendelea kutekeleza missions na malengo yao makuu matatu , huku wakitoa mafunzo ya kijeshi kwa wanajeshi wa Afghanistan, wakilinda Amani ndani ya Afghanstan na kupigana vita dhidi ya makundi ya kiasi kama Taliban, huku Serikali ya Marekani ikiendelea kulipa mishahara wanajeshi wa Afghanistan, kuwapa silaha na vyenzo vyote vya kijeshi walivyohitaji kupata.

Malengo makuu ya Marekani iliyowafanya wao wapeleke majeshi Afghanistan karibu malengo yote yalitekelezwa.

1.Walifanikiwa kumuua Kiongozi wa kundi la Aqaeda Osama Bin .Mei 2 ,2011.

2.Walifanikiwa kusambaratisha kundi la AlQaeda.

3.Suala la Afghanistan kutotumiwa kama ardhi ya kuficha , kusaidia na kufunza Magaidi dhidi ya Marekani hasa AlQaeda ,hili suala utekelezaji wake ni kuhakikisha ya kwamba Afghanistan inakuwa nchi ya Amani, serikali ya Afghanstan ijadiliane na kundi la Taliban kuongoza nchi yao ya Afghanstan pamoja,ndiyo wanaweza kwa pamoja kuzuia nchi yao ya Afghanstan isiwe ardhi ya kuficha,kufunza na kusaidia makundi ya Kigaida yenye shabaha ya kuishambulia Marekani.

Malengo makuu ya Marekani kupeleka Majeshi Afghanstan takribani yote yalitimia , jambo liliobaki ni kuandaa mpango na makubaliano ya kuondoa majeshi yao kutoka Afghanistan baada ya miaka mingi majeshi yao kuwepo Afghanistan.

Mpango wa kuyaondoa Majeshi ya Marekani nchini Afghanstan alianza nao Barack Obama , yeye alinuia kufikia mwisho mwaka 2014 atatoa Majeshi ya Marekani nchini Afghanstan. Msisitizo mkubwa uliokuwa unawekwa na Marekani ni makundi ya kisiasa nchini Afghanstan yakae pamoja na kukubaliana pamoja wawe wamoja kwa maendeleo ya nchi yao.

Obama alikuwa akimsisitiza sana Hamid Karzai kukaa meza moja na kundi la Taliban ili nchi iwe na amani.Bahati mbaya hadi Obama anamaliza utawala wake hakufanikiwa kuondoa majeshi ya Marekani Afghanstan.

Katika utawala wa Rais Trump. Kuanzia mwaka 2018 Rais Trump alianza kuonesha nia ya kuondoa majeshi ya Marekani kutoka Afghanstan , Afghanstan ikiwa chini ya Rais Ashrafi Ghani aliyeingia madarakani Septemba 2014 baada ya Hamid Karzai , kulianza kufanyika jitahida za mazungumzo kati ya Serikali ya Marekani chini ya Trump na kundi la Taliban ili kutafuta suluhu ya amani na Marekani iondoe majeshi yake nchini Afghanistan.Kwani taarifa zinasema tangu 2007 , takribani wanajeshi 6000 wa Marekani wamefariki , NATO wanajeshi 1100 wamefariki , Wanajeshi wa Afghanistan 73000 wamefariki, Taliban wanajeshi wamefariki . Huku Jeshi la Taliban likiendelea kupanuka ikikadiriwa kuwa na wapiganaji kati ya 60000 hadi 100,000.

Katika mchakato wa kuhakikisha Marekani inatoa majeshi yake Afghanistan na kuhakikisha Afghanistan inabaki na Amani . Tar 29 , Februari 2020 Serikali ya Marekani chini ya Donald Trump na kundi la Talibani wawakilishi wa pande zote walikutana Qatar -Doha na kuingia Makubaliano yaliyoitwa,

"Agreement for Bringing Peace to Afghanistan
between the Islamic Emirate of Afghanistan which is not recognized by the United States
as a state and is known as the Taliban and the United States of America."

Makubaliano haya yalijumuisha vifungu vifuatavyo.

1.Marekani kuondoa majeshi yake Afghanstan, miezi 14 ,baada ya Februari 2020 yaani kufikia Mei 1 2021.

2 .Kuwe na Mazungumzo ya amani kati ya Kundi la Taliban na serikali ya Afghanstan ili kuunda serikali ya pamoja (To enter into power sharing negotiations with Afghanstan Government) , pamoja na kusitisha mapigano.

3.Taliban pamoja na serikali ya Afghanstan kwa pamoja wazuie na wasiruhusu kundi lolote la Kigaidi kujificha ,kukaa na kupata mafunzo nchini Afghanistan dhidi ya Marekani au nchi yeyote.

Bahati mbaya hadi Rais Trump anaondoka madarakani hakufanikiwa kuondoa majeshi yote ya Marekani nchini Afghanstan. Ila alikuwa tayari ameanza kupunguza majeshi kutoka Afghanistan kutoka idadi ya wanajeshi 15,500 hadi 2500 .

Baada ya Rais Joe Biden kuingia madarakani , hili jambo la majeshi ya Marekani nchini Afghanstan lilikuwa na sura mbili , moja ilikuwa ni ahadi yake katika kampeni kwamba ataondoa majeshi yote ya Marekani kutoka Afghanstan lakini mbili alikuta kuna makubaliano tayari yaliyowekwa na Serikali ya Marekani chini ya Rais Donald Trump na Kundi la Taliban mnamo Februari 2020 ya kuondoa majeshi ya Marekani nchini Afghanstan kuanzia Mei 1 ,2021 .

Huku wanamgambo wa Taliban wakimkumbusha Rais Joe Biden juu ya makubaliano kati yao na Marekani ya kuondoa majeshi Mei 1 ,2021 kwamba asivunje Mkataba kabisa .

Rais Biden hakuwa na namna zaidi ya kuangalia namna ya kutekeleza makubaliano hayo , ila aliwaomba Taliban wakutane , Februari 2021 ili kujadili na kupitia tena hayo makubaliano ya Februari 2020 chini ya Trump.

Februari 2021 ,katika Mji wa Doha , Qatar. Kundi la Taliban likiwakilishwa (Mkuu wa Kamisheni ya siasa ) ,Abdul Ghan Baradar huku Marekani ikiwakilishwa na Mwanadiplomasia wa Marekani Zalmay Khalilzad , jambo kubwa lililojadiliwa ni kuongeza muda wa kuondoka Afghanstan ambapo ilikubaliwa kwamba Serikali ya Marekani chini ya Rais Biden itaondoa Majeshi yake Tar 11 Septemba 2021 badala ya Mei 1 ,2021 iliyoekwa na Trump ila Biden alipaswa kutoa Majeshi yote siku Septemba 11 (Siku ya kuenzi waliokufa katika shambulio la Septemba 11 ,2001).

Ila bila kutarajia Rais Biden aliamua kuondoa Majeshi yote ya Marekani kutoka Afghanstan Aprili 2021 ,huku kundi la Taliban likipata Mwanya wa kujipanua zaidi kuelekea mji mkuu wa Kabul na miji mingine . Hadi sasa haijulikani Rais wa nchi hiyo Ashraf Ghani aliyetorika tar 15 Agost 2021, ameenda nchi gani au mji gani aliandika kabla ya kutoroka kupitia mtandao wake wa Facebook kwamba "Nachukua maamuzi magumu ya kuondoka kupisha wanamgambo wa Taliban ambao wanataka urais , maamuzi haya yana lengo la kulinda wananchi wangu kuliko kulinda cheo changu, najua kama ningelibaki wananchi wengi wazalendo wangekufa na mji wa Kabuli ungeharibiwa sana " .Mbali na maneno haya mazito ya Rais Ashrafi Ghani bado wachambuzi wa mambo na wananchi baadhi wanamuona kama ni muoga .

Rais wa Marekani baada ya tukio hili aliidhinisha kundi la wanajeshi 6000 kwenda kusaidia kuwaondoa Rai wa Marekani, mafisa wake na wananchi wa Afghanistan ambao walijitoa miaka 20 kufanya kazi na mafisa wa Marekani kwa lengo la kuwapa VISA kuishi Marekani.Taliban walionywa katika hatua hii ya Marekani kuondoa watu wake Talib isihatarishe maisha ya Raia wa Marekani hata mmoja ,ikifanya hivyo Marekani itajibu.

Watu wengi wanatokea kumlaumu Joe Biden kwa maamuzi ya kuondoa Majeshi Afghanstan kwa uharaka , Joe Biden amejibu kwa kusema hajutii maamuzi yake kwani hakuna maslahi yeyote kwa nchi ya Marekani kwa kuendelea kuyaweka majeshi yake nchini Afghanistan ."Staying in Afghanistan is not national interest"

Akisema malengo yote ya kuweka Majeshi ya Marekani Afghanstan tayari yametimia kumuuwa Osama , kusambaratisha AlQaeda na kuhakikisha Afghanistan haitumiki kama ngome ya magaidi dhidi ya Marekani .

Rais Biden aliendelea kusema kwamba ameingia ofisini akakuta tayari kuna makubaliano yaliyowekwa kati ya Trump na Taliban tangu Februari 2020 kwamba hadi mwezi Mei 2021 Majeshi yote ya Marekani yatapaswa kuondoka ."I inherited a deal that Trump negotiated with Taliban under his agreement would be out May 1,2021.

Hakukuwa na namna ya kuacha majeshi sababu hakukuwa na makubaliano ya amani na kulinda watu wetu ikiwa majeshi hayataondoka baada ya Mei 2021 ambaye yeye aliomba iwe Septemba 2021.(He said ,No agreement to protect our forces and people after Mei 1 ,2021) "No status if Stability after May one "

Watu wanamlaumu kwamba anaiacha Afghanistan katika machafuko na watu kuendelea kufa , Rais Biden anasema Mission ya Marekani nchini Afghanstan haikuwa kujenga Taifa au kuimarisha Demokrasia bali mission ilikuwa kuzuia ugaidi dhidi ya Nchi ya Marekani. (Mission is not National building , not creating unified , centralized Democracy but to prevent a terrorist attack on American Homeland .

Rais Biden ,anaendelea kusema hakuna muda rasmi au muda mzuri wa kuondoa majeshi zaidi ya viongozi wa Serikali ya Afghanstan na Taliban kutafuta suluhu za kisiasa jambo ambalo alimshauru Rais Ashrafi Ghani walipozungumza Juni 2021 ,ila Ghani alionesha kutaka kutumia nguvu na kuinua silaha badala ya suluhu ya amani na mazungumzo.

Anasema ,"Majeshi ya Marekani hayawezi na hayapaswi kuendelea kupigana katika vita na kufa katika vita ikiwa majeshi ya Afghanstan hayapo tayari kujipigania wao wenyewe"

"American troops cannot and should not be fighting in a war and dying in a war that Afghanistan forces are not willing to fight for themselves".

Joe Biden akiendelea kusema , Marekani itaendelea kulinda sera yake ya mambo ya nje (Foreign Policy) kuheshimu haki za binadamu , kuzuia vita na mapigano kama ambavyo mara zote wanafanya Dunia nzima ila sio kwa kuendekelea kuweka Majeshi nchini Afghanistan (Not through endless military deployment).

Huku upande wa Taliban wanaendelea kutangaza kwamba nchi itakuwa ya amani , ila wananchi wanaonekana kuwa na hofu kuwa chini ya utawala wa Taliban , wakikumbuka mateso waliyopitia 1996 hadi 2001 chini ya utawala wao , utawala wa nguvu na kutumia sheria kali . Kupiga mawe wazinifu hadi kufa, kutoruhusu mziki wala kuangalia Tv , kulazimisha kuvaa hijabu kufunika nyuso kwa wanawake .

Lengo kubwa la Taliban ni kusimamisha utawala wa kiislamu na utakaofuata sheria za kiislamu.

Kiongozi na muasisi wa kundi la Taliban aliitwa Mullah Mohammed Omary ,ambaye ndiye alikuwa kiongozi mkubwa yaani Amir -Ali-Muuminin mkuu wa Rahbar Shura (Mkuu wa Baraza linalofanya maamuzi yote juu ya siasa na Jeshi ).Mullah Muhammed Omary alifariki nchini Pakistan hospital ya Karachi mwaka 2013 kwa ugonjwa wa TB lakini kifo chake kilitangazwa na Taliban mwaka 2015.

Kiongozi Mkubwa aliyefuata baada ya Mullah Muhamed Omary ni Mullah Akhtar Mohammed Mansour ambaye aliuwawa 2016 na Marekani nchini Pakistan.

Kiongozi wa sasa wa kundi la Taliban ni Mawlawi Haibutullah Akhundzada. Akisaidiwa na viongozi wengine Mullah Muhammed Yakoub , Mullah Abdallah Ghan Baradar , Sirijuddin Haqqan pia wana idara mbalimbali (Commission) zikisimama kama wizara kwa lugha ya kawaida.

Imeandaliwa kwa kukusanya taarifa mbalimbali kutoka katika vyanzo vya magazeti Washington Posts, Vyombo vya habari CNN, ALJAZEERA,BBC na vyombo vingine lakini vitabu mbalimbali juu ya Mapigano ya Taliban na Afghanistan.

Ahsante.

Imeandaliwa na,

Abdul Omary Nondo.
Nashukuru nimepata mwangaza kidogo
Nini maoni yako kuhusu Serikali ya Wataleban itakuwa ni ya namna gani?
 
Ni Terrorism sio Terrolism.

Mkuu definition Ya Terrorism ni mtu anaetia hofu, huwa hawa wanaua ama kufanya Uhalifu Bila Material gain, Taliban sio Terrorist sababu inajulikana kabisa wa nataka Nchi hawa ni waasi,

Kuhusu Uisilamu na ugaidi Almost Maeneo yote yenye ugaidi kuna mkono wa USA na washirika wake.

Miaka kadhaa iliopita Libya, Iraq, Syria, Yemen, Somalia na kwengineko zilikuwa ni nchi zenye Maendeleo na maisha yanakwenda kama kawaida, hao jamaa kuingia Affairs za watu na kupindua viongozi, kufadhili makundi na kuua Raia wasio na hatia ndio wanaleta machafuko kila eneo.

Kuhudumia Jeshi mkuu si jambo la kitoto, tunazungumzia matrilioni ya Hela, wanajeshi most of times hawazalishi imagine umlishe, umvishe, umnunulie silaha, umlipe etc unafkiri tu somewhere unaweza ukaanzisha kikundi cha ugaidi ukawa na silaha na funds za kuweka watu kambini bila ufadhili?

Magaidi wengi wanafadhiliwa na Nchi kubwa na Historia Angalia vikundi vingi vya ugaidi zamani vilikuwa funded na USA. Hata hawa wetu AL shabaab ukiangalia Historia yao imeanzishwa na mwanadada Samantha.

Tafuta Makundi yote ya kigaidi kuanzia Hao kina isis mpaka huku kwetu Al shabaab wanaua zaidi waisilamu kushinda watu wowote, zaidi ya Asilimia 90 ya watu wanaouliwa ni waisilamu, why vikundi vimavyojinasibisha na Uisilamu vinaua kila siku waisilamu na hata havitetei haki za waisilamu.

Kama kweli kuna vikundi vya waisilamu
1. Palestine wasingekuwa wanaouliwa vile.
2. Tumeona Myanmar waisilamu wanavyochinjwa kwa maelfu
3. Tunaona Uyghur China waisilamu wanavyoteswa.

Kote huko husikii vikundi vya waisilamu wala hakuna anaewatetea, ila kina Isis Wana operate Maeneo ambayo ni almost 100% waisilamu na wanaua waisilamu, huoni hizi ni danganya toto tu?.

Shukrani kwa majibu mazuri JF inaitaji watu kama wewe, kaswali kangu ka mwisho, nini mtazamo wako juu ya bakwata unazani inalinda na kutetea uisilamu na waisilamu kama inavyotakiwa?
 
Nimeishia kusoma paragraph hii. ...... Ilipofika Septemba 11 , Osama Bin Laden akaishambulia Marekani (September Eleven Attack katika jengo la World Trade Center) watu zaidi ya 3000 walifariki.

Nikaona utafiti wako umebumba kuwa kubeba fake info.

Challenge.

1. Tupatie ushahidi wa kuhusika kwa Osama ktk sept 11.

2. Kama kweli Alkaida ilikuwepo Duniani. Tutajie ofisi yao popote pale ndani ya Afghanistan au hata nje ya nchi hivyo.

Alqaida ni hadithi ya kusadikika. Haijawahi kuwepo ktk ardhi ya dunia.

Niinshie hapo kwa sasa.
Sasa wewe ndio hueleweki kabisa nadhani una mihemko ya hali ya juu
 
Back
Top Bottom