Fahamu namna ya ukadiriaji tofali katika ujenzi

Fahamu namna ya ukadiriaji tofali katika ujenzi

Njuka II

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2019
Posts
414
Reaction score
733
Habari,

Leo nimeona niwaelimishe ndugu zangu namna ya kujua idadi ya tofali zinazohitajika katika ujenzi wa nyumba.
Katika somo hili, tutatumia ramani ya chumba kidogo cha mita 3 kwa mita 3, chenye madirisha mawili (urefu mita 1.2, upana mita 1) na mlango mmoja (urefu mita 2.4, upana mita 0.9)

Kawaida vipimo vya tofali ni 0.450m urefu, 0.230m upana na 0.120/0.125/0.150m unene.

HATUA ZA UKADIRIAJI
1. Tafuta jumla ya urefu wa kuta zako ( Total Length of the wall)
Tukitumia mfano wa chumba chetu hapo juu, jumla ya urefu wa kuta zote (L) utakuwa
L= 3m+3m+3m+3m
L= 12m

2. Tafuta idadi ya tofali zitakazoweza kujenga mstari (kozi) mmoja wa tofali
Ili kuweza kujua idadi ya tofali zikakazoweza kujenga kozi moja ya tofali, chukua jibu ulilopata katika hatua ya kwanza kisha gawanya na urefu wa tofali moja ambao ni 0.45m

Idadi ya tofali kwa kila kozi, N = L÷0.450
N = 12m/0.45m
N = 26.6 = 27
Kila kozi (mstari) zitatumika tofali 27

3. Tafuta jumla ya tofali zote zitakazohitajika kujenga nyumba nzima.

Hapa sasa utaamua ujenge kozi ngapi, lakini kwa kawaida katika msingi watu wengi hupendelea kujenga kozi 8 mpaka 10 au na zaidi inategemea na eneo lilivyo au ramani yako ilivyo (sisi tutatumia kozi 8) na katika kuta za juu, watu wengi hupendelea kujenga kozi 12 mpaka 14 (sisi tutatumia kozi 12)

Jumla ya kozi zote itakuwa
Kozi 8 za msingi + Kozi 12 za kuta za juu = kozi 20

Jumla ya tofali zote, No. = kozi 20 × tofali 27
No. = tofali 540

4. Toa tofali za Madirisha na Milango

Hapa itabidi utafute eneo (surface area) la madirsha na milango
Jumla ya eneo la madirisha = 1.2m × 1.0m ×2 = 2.4m²
Jumla ya eneo la milango = 2.4m × 0.9m = 2.16m²
Jumla ya eneo lote = 4.56m²

Eneo la tofali moja likiwa limesimamishwa = 0.45m × 0.23m = 0.1035m²

Idadi ya tofali za kutoa katika madirsha na milango = 4.56m²/0.1035m² = 44

JUMLA YA TOFALI ZOTE, N = 540 - 44 = 496

Imeandikwa na Njuka II
Kwa hesabu mbali mbali zinazohusu ujenzi, tuwasiliane
ebusiness.excel@gmail.com

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari,

Leo nimeona niwaelimishe ndugu zangu namna ya kujua idadi ya tofali zinazohitajika katika ujenzi wa nyumba.
Katika somo hili, tutatumia ramani ya chumba kidogo cha mita 3 kwa mita 3, chenye madirisha mawili (urefu mita 1.2, upana mita 1) na mlango mmoja (urefu mita 2.4, upana mita 0.9)

Kawaida vipimo vya tofali ni 0.450m urefu, 0.230m upana na 0.120/0.125/0.150m unene.

HATUA ZA UKADIRIAJI
1. Tafuta jumla ya urefu wa kuta zako ( Total Length of the wall)
Tukitumia mfano wa chumba chetu hapo juu, jumla ya urefu wa kuta zote (L) utakuwa
L= 3m+3m+3m+3m
L= 12m

2. Tafuta idadi ya tofali zitakazoweza kujenga mstari (kozi) mmoja wa tofali
Ili kuweza kujua idadi ya tofali zikakazoweza kujenga kozi moja ya tofali, chukua jibu ulilopata katika hatua ya kwanza kisha gawanya na urefu wa tofali moja ambao ni 0.45m

Idadi ya tofali kwa kila kozi, N = L÷0.450
N = 12m/0.45m
N = 26.6 = 27
Kila kozi (mstari) zitatumika tofali 27

3. Tafuta jumla ya tofali zote zitakazohitajika kujenga nyumba nzima.

Hapa sasa utaamua ujenge kozi ngapi, lakini kwa kawaida katika msingi watu wengi hupendelea kujenga kozi 8 mpaka 10 au na zaidi inategemea na eneo lilivyo au ramani yako ilivyo (sisi tutatumia kozi 8) na katika kuta za juu, watu wengi hupendelea kujenga kozi 12 mpaka 14 (sisi tutatumia kozi 12)

Jumla ya kozi zote itakuwa
Kozi 8 za msingi + Kozi 12 za kuta za juu = kozi 20

Jumla ya tofali zote, No. = kozi 20 × tofali 27
No. = tofali 540

4. Toa tofali za Madirisha na Milango

Hapa itabidi utafute eneo (surface area) la madirsha na milango
Jumla ya eneo la madirisha = 1.2m × 1.0m ×2 = 2.4m²
Jumla ya eneo la milango = 2.4m × 0.9m = 2.16m²
Jumla ya eneo lote = 4.56m²

Eneo la tofali moja likiwa limesimamishwa = 0.45m × 0.23m = 0.1035m²

Idadi ya tofali za kutoa katika madirsha na milango = 4.56m²/0.1035m² = 44

JUMLA YA TOFALI ZOTE, N = 540 - 44 = 496

Imeandikwa na Njuka II
Kwa hesabu mbali mbali zinazohusu ujenzi, tuwasiliane
ebusiness.excel@gmail.com

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Njuka II hivi nyumba yenye vyumba 3 vya kulala (kimoja kiwe masta), sitting room, dinning, jiko, store na publi toilet, kwa wastani inatakiwa iwe na ukubwa gani? Yaani urefu mita ngapi na upana mita ngapi?
 
Mkuu Njuka II hivi nyumba yenye vyumba 3 vya kulala (kimoja kiwe masta), sitting room, dinning, jiko, store na publi toilet, kwa wastani inatakiwa iwe na ukubwa gani? Yaani urefu mita ngapi na upana mita ngapi?
Urefu mita 11/12, upana mita 9/10. Hilo ni eneo kwa nyumba pekee japo inategemea na design ama mpangilio pamoja na ukubwa wa vyumba katika ramani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari,

Leo nimeona niwaelimishe ndugu zangu namna ya kujua idadi ya tofali zinazohitajika katika ujenzi wa nyumba.
Katika somo hili, tutatumia ramani ya chumba kidogo cha mita 3 kwa mita 3, chenye madirisha mawili (urefu mita 1.2, upana mita 1) na mlango mmoja (urefu mita 2.4, upana mita 0.9)

Kawaida vipimo vya tofali ni 0.450m urefu, 0.230m upana na 0.120/0.125/0.150m unene.

HATUA ZA UKADIRIAJI
1. Tafuta jumla ya urefu wa kuta zako ( Total Length of the wall)
Tukitumia mfano wa chumba chetu hapo juu, jumla ya urefu wa kuta zote (L) utakuwa
L= 3m+3m+3m+3m
L= 12m

2. Tafuta idadi ya tofali zitakazoweza kujenga mstari (kozi) mmoja wa tofali
Ili kuweza kujua idadi ya tofali zikakazoweza kujenga kozi moja ya tofali, chukua jibu ulilopata katika hatua ya kwanza kisha gawanya na urefu wa tofali moja ambao ni 0.45m

Idadi ya tofali kwa kila kozi, N = L÷0.450
N = 12m/0.45m
N = 26.6 = 27
Kila kozi (mstari) zitatumika tofali 27

3. Tafuta jumla ya tofali zote zitakazohitajika kujenga nyumba nzima.

Hapa sasa utaamua ujenge kozi ngapi, lakini kwa kawaida katika msingi watu wengi hupendelea kujenga kozi 8 mpaka 10 au na zaidi inategemea na eneo lilivyo au ramani yako ilivyo (sisi tutatumia kozi 8) na katika kuta za juu, watu wengi hupendelea kujenga kozi 12 mpaka 14 (sisi tutatumia kozi 12)

Jumla ya kozi zote itakuwa
Kozi 8 za msingi + Kozi 12 za kuta za juu = kozi 20

Jumla ya tofali zote, No. = kozi 20 × tofali 27
No. = tofali 540

4. Toa tofali za Madirisha na Milango

Hapa itabidi utafute eneo (surface area) la madirsha na milango
Jumla ya eneo la madirisha = 1.2m × 1.0m ×2 = 2.4m²
Jumla ya eneo la milango = 2.4m × 0.9m = 2.16m²
Jumla ya eneo lote = 4.56m²

Eneo la tofali moja likiwa limesimamishwa = 0.45m × 0.23m = 0.1035m²

Idadi ya tofali za kutoa katika madirsha na milango = 4.56m²/0.1035m² = 44

JUMLA YA TOFALI ZOTE, N = 540 - 44 = 496

Imeandikwa na Njuka II
Kwa hesabu mbali mbali zinazohusu ujenzi, tuwasiliane
ebusiness.excel@gmail.com

Sent using Jamii Forums mobile app
Ahsante sana ndugu yangu naomba npate kujua jinsi ya kukadilia msingi wa mawe
 
Ahsante sana ndugu yangu naomba npate kujua jinsi ya kukadilia msingi wa mawe
Kujua kiasi cha mawe kitakachohitajika kujenga msingi, itabidi ujue kina cha msingi, unene wa msingi na urefu (length) wa ukuta.

Mfano kwa hicho chumba cha mita 3 kwa mita 3, kama utatumia msingi wa kina cha 0.6m, na unene wa msingi 0.40m

Kiasi cha mawe kitakuwa
V= 0.6m × 0.4m × (3m+3m+3m+3m)
V= 2.88m³ approx 3.0m³
 
Mkuu Njuka II ,vipi nafasi ya udongo baini ya matofali inachukua sehemu gani katika makadirio ya idadi ya matofali?
Kuna mtu amewahi nidokeza kuwa ule mchanga unachukua kama 1cm hivi hasa naona kama kwa sehemu fulani itachukua sehemu ya tofali na kupunguza gharama.
ASANTE
 
Mkuu Njuka II ,vipi nafasi ya udongo baini ya matofali inachukua sehemu gani katika makadirio ya idadi ya matofali?
Kuna mtu amewahi nidokeza kuwa ule mchanga unachukua kama 1cm hivi hasa naona kama kwa sehemu fulani itachukua sehemu ya tofali na kupunguza gharama.
ASANTE
Ndio ni sahihi, kama utahesabia nafasi ya udongo katika makadirio tofali zitapungua.
Mfano kwa hapo juu, urefu wa tofali utakuwa 450mm + nusu ya unene wa udongo kushoto na kulia = 450mm+15mm+15mm=480mm

Idadi ya tofali kwa kozi moja N = 12m÷(480/1000m)
N= 25
Idadi ya tofali kwa kila kozi imepungua kutoka 27 mpaka 25. Kadri unene wa udongo unavyokuwa mkubwa, tofali zinazidi kupungua zaidi
 
Ndio ni sahihi, kama utahesabia nafasi ya udongo katika makadirio tofali zitapungua.
Mfano kwa hapo juu, urefu wa tofali utakuwa 450mm + nusu ya unene wa udongo kushoto na kulia = 450mm+15mm+15mm=480mm

Idadi ya tofali kwa kozi moja N = 12m÷(480/1000m)
N= 25
Idadi ya tofali kwa kila kozi imepungua kutoka 27 mpaka 25. Kadri unene wa udongo unavyokuwa mkubwa, tofali zinazidi kupungua zaidi
Asante sana mkuu
 
Habari,

Leo nimeona niwaelimishe ndugu zangu namna ya kujua idadi ya tofali zinazohitajika katika ujenzi wa nyumba.
Katika somo hili, tutatumia ramani ya chumba kidogo cha mita 3 kwa mita 3, chenye madirisha mawili (urefu mita 1.2, upana mita 1) na mlango mmoja (urefu mita 2.4, upana mita 0.9)

Kawaida vipimo vya tofali ni 0.450m urefu, 0.230m upana na 0.120/0.125/0.150m unene.

HATUA ZA UKADIRIAJI
1. Tafuta jumla ya urefu wa kuta zako ( Total Length of the wall)
Tukitumia mfano wa chumba chetu hapo juu, jumla ya urefu wa kuta zote (L) utakuwa
L= 3m+3m+3m+3m
L= 12m

2. Tafuta idadi ya tofali zitakazoweza kujenga mstari (kozi) mmoja wa tofali
Ili kuweza kujua idadi ya tofali zikakazoweza kujenga kozi moja ya tofali, chukua jibu ulilopata katika hatua ya kwanza kisha gawanya na urefu wa tofali moja ambao ni 0.45m

Idadi ya tofali kwa kila kozi, N = L÷0.450
N = 12m/0.45m
N = 26.6 = 27
Kila kozi (mstari) zitatumika tofali 27

3. Tafuta jumla ya tofali zote zitakazohitajika kujenga nyumba nzima.

Hapa sasa utaamua ujenge kozi ngapi, lakini kwa kawaida katika msingi watu wengi hupendelea kujenga kozi 8 mpaka 10 au na zaidi inategemea na eneo lilivyo au ramani yako ilivyo (sisi tutatumia kozi 8) na katika kuta za juu, watu wengi hupendelea kujenga kozi 12 mpaka 14 (sisi tutatumia kozi 12)

Jumla ya kozi zote itakuwa
Kozi 8 za msingi + Kozi 12 za kuta za juu = kozi 20

Jumla ya tofali zote, No. = kozi 20 × tofali 27
No. = tofali 540

4. Toa tofali za Madirisha na Milango

Hapa itabidi utafute eneo (surface area) la madirsha na milango
Jumla ya eneo la madirisha = 1.2m × 1.0m ×2 = 2.4m²
Jumla ya eneo la milango = 2.4m × 0.9m = 2.16m²
Jumla ya eneo lote = 4.56m²

Eneo la tofali moja likiwa limesimamishwa = 0.45m × 0.23m = 0.1035m²

Idadi ya tofali za kutoa katika madirsha na milango = 4.56m²/0.1035m² = 44

JUMLA YA TOFALI ZOTE, N = 540 - 44 = 496

Imeandikwa na Njuka II
Kwa hesabu mbali mbali zinazohusu ujenzi, tuwasiliane
ebusiness.excel@gmail.com

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu, Kwenye hicho chumba makadirio ya bati na mbao yapoje?
 
Njuka II na vipi kuhusu mawe ya msingi kwa nyumba ya vyumba vitatu/viwili
Ili niweze kufanya makaridio inabidi niwe na ramani yenye vipimo, kama ni vyumba viwili tu vilivyoungana vyenye urefu na upana wa futi kumi kumi utahitaji uwe na mawe ya ujazo wa 4m³ . Kina cha msingi futi 2, upana futi 1
 
Back
Top Bottom