Fahamu utajiri uliopo kwenye uwekezaji wa dhamana za Serikali (Treasury Bills & Bonds)

Fahamu utajiri uliopo kwenye uwekezaji wa dhamana za Serikali (Treasury Bills & Bonds)

Swali zuri mkuu
1.Kwa treasury bills minimum ni 500000/= kwa mafungu ya 10000/= mfano unaweza wekeza 550000/= na sio 555000/=
2.Kwa treasury bond minimum ni 1m kwa mafungu ya 100000/= mfano 1500000/= na sio 1550000/=
Kuwekeza kwenye hz dhamana za serikali kuna faida zifuatazo.

1.Serikali haitegemei kukiuka mategemeo ya wadai wake wakati wa malipo( hapa hata tuingie kwenye vita pesa yako utalipwa tofauti na commercial banks ni 50/50).

2.Dhamana za serikali zinahamishika hapa unaweza kuziuza DSE kabla ya mda wake kuiva

3.Dhamana za serikali zinaweza kutolewa kama dhamana kwa ajili ya mkopo(yaani ukishawekeza unaweza kupata mkopo bank yyte kulingana na pesa ulizowekeza,,kama umegundua ktu hapa unawekeza kwenye dhamana then unaenda kuchukua mkopo unapiga biashara unatengeneza faida mara mbili wakati bank unawalipa mdomdo mangi)

4.Faida inayopatikana katika uwekezaji wa dhamana inaridhisha) hakuna commercial bank yyte utakayowekeza upate interest kama za BOT na wengi ni matapeli maana walishanifanyia umafia that's why nimewekeza huku
Karibu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ila serikali ya sasahivi inaweza 😂 wazee wa kikokotoo
 
Kuna jamaa anawekeza huko...
Na anasema hana wasi na ada za watoto wake...maana wanasoma shule zenye ada ndefu...
yeye ni mwoga na hana muda wa kufanya biashara
Hii ni nzuri kweli kama una pesa nzuri unainjoy! Ukiwa na 1B basi unaweza ishi kama malaika tu hapa nchini. Chukulia gawio la 100M tu kila mwaka kwanini usiishi ki boss!
 
[emoji769]✓Kwa nchi zetu bado sana kwy kusimamia shughuli za kiuchumi, bado Mambo mengi yanaenda kisiasa zaidi
 
Hapo mimetoa mfano, lakini kama ukifuatilia kwenye zabuni za BOT ni kwamba faida itatategemea ile discount ya kununua treasury bills.

Ikiwa unapata discount kubwa basi ujue faida unayopata nayo itakuwa kubwa. Nakushauri u visit website ya BOT Kuna matokeo ya treasury bills auction zilizofanyika

Msaada wa kuelewa hii picha
TB.PNG
 
Je unaweza kuchukua mkopo bank ya biashara na ukawekeza kwenye treasury bill au bond ikakulipa na kuridisha mkopo bila wasi wasi wowote mkuu?
Boss commercial rate ni more than 15% na bills/bond at most you can make 10%..unachotaka kufanya doesnt make any sense
 
UTAJIRI MKUBWA ULIOPO KWENYE UWEKEZAJI WA DHAMANA ZA SERIKALI

Uwekezaji kwenye dhamana za serikali umegawanyika makundi mawili.

i) Dhamana za muda mfupi (treasury bills)
ii) Dhamana za muda mrefu (treasury bonds)

Kwa nchi yetu ya Tanzania biashara ya dhamana za serikali inasimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa niaba ya serikali ya Tanzania.

Dhamana za muda mfupi (treasury bills)
Hizi ni dhamana za muda mfupi ikimaanisha zinaiva ndani ya mwaka mmoja. Lengo kubwa hasa kwa serikali kuweka Treasury bills ni kupata fedha kwa ajili kukabiliana na mapungufu ya fedha katika bajeti na pale inapohitaji fedha kwa haraka.

Dhamana za muda mfupi zipo katika makundi manne kutegemea na mda zitakapoiva: ya siku 35, siku 91, siku 182 na siku 364.

Uwekezaji katika Treasury bill una faida zifuatazo kwa mwekezaji;
i)Hazina hatari yoyote kubwa (risk free) kwa mwekezaji na ni uwekezaji wa uhakika kwa sababu zinatolewa na serikali.

ii)Zaweza kuhamishika kutoka umiliki wa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Ikimaanisha pale mwekezaji anapotaka kuuza anaweza akafanya hivo.

iii)Zaweza kutumika kama dhamana za kuombea mikopo kwenye taasisi za fedha bila usumbufu wowote kwa sababu thamani ya treasury bill coupon haibadiliki kwa hiyo ni rahisi kwa taasisi za fedha kuzipa kipaumbele kutumika kwenye dhamana.

iv)Gawio ni kubwa pale unapowekeza kwenye treasury bills zaidi hata ya kuwekeza kwenye taasis yeyote ya fedha kupitia fixed deposits. (namaana ya kwamba riba katika treasury bills ni kubwa maradufu ya riba za benki)

Soko la treasury bills
Biashara na soko la treasury bills zinafanyika kwa njia mbili;

a) Soko la awali (primary market) hapa ni pale banki kuu ya Tanzania inapotoa kwa mara ya kwanza treasury bills kwa wawekezaji.

b) Soko la pili (secondary market) hii inahusisha kuuza na kununua treasury bills na hii inafanyika Dar es salaam stock exchange DSE. Hapa ndipo pale mtu anapotaka kuuza treasury bills anayoimiliki anaweza kwenda kuuza.

Kianzio cha kuwa mwekezaji wa moja kwa moja kwenye treasury bills kwa Tanzania ni sh. 5,000,000. Ina maana kwamba ukiwa na mtaji wa kuanzia milioni tano basi unaruhusiwa moja kwa moja kushiriki kwenye mnada wa treasury bills (treasury bills auction).

Kwa wawekezaji wa mtaji chini ya milioni tano basi wao watashiriki kwenye mnada kupitia primary dealers ambao kwa urahisi ni mabrokers na commercial banks

Primary dealers ambao wamethibitishwa na BOT ni hawa wafuatao (ambao wale wenye mitaji chini ya milioni tano watapitia kwao) Akiba Commercial Bank Ltd, Citibank (T) Ltd, CRDB Bank Ltd, Diamond Trust Bank (T) Ltd, Eurafrican Bank (T) Ltd.Exim Bank (T) Ltd. Habib African Bank Ltd. International Commercial Bank (T) Ltd. Kenya Commercial Bank (T) Ltd.NBC Limited. NMB Ltd. Stanbic Bank (T) Limited Standard Chartered Bank Ltd.Orbit Securities Co. Ltd. Rasilimali Limited Solomoni Securities Ltd. Core securities Ltd. Tanzania securities Ltd. Vertex International Securities.

Unapata vipi pesa kupitia dhamana za muda mfupi?
Serikali kupitia BOT inapotoa treasury bills zinakuwa katika mfumo wa zabuni ikimaanisha kwamba wawekezaji watatakiwa kwa mfano kusema watanunua kila shilingi 100 ya serikali kwa kiasi gani? (hatua hiyo ya kwanza inaitwa bidding)

Ili kupata faida kwa wawekezaji wanatakiwa kutoa bei ambayo ipo katika discout, ikiwa na maana mwekezaji anaweza kununua shilingi 100 ya serikali kwa shilingi 93 hivo mda wa kuiva ukifika atapata faida ya shilingi 7.

Mfano serikali imetoa treasury bills ya siku 365. Kisha mwekezaji akaweka bid ya kununua kila shilingi 100 kwa shilingi 75. Kama mwekezaji atafanikiwa kwenye zabuni hiyo atapata treasury bill yenye (face value) ya Tzs 100,000,000 ingawaje kiasi alichotoa ni Tzs 75,000,000 kwa sababu ndicho kiasi alicho bid katika kabrasha la zabuni yake.

Baada ya treasury bills kuiva yaani kutimia siku 365, mwekezaji atalipwa na BOT kiasi cha TZS 100,000,000 ambayo italeta faida ya (TZS 100,000,000-TZS 75,000,000= TZS 25,000,000). Hivo faida itakuwa ni TZS 25,000,000.

Ukiweka katika asilimia ni kama ifuatavyo;
- Kanuni ya kukokotoa riba katika treasury bills:
Riba=(F-P)/P ×(365×100)/N

F= face value ya treasury bills ambayo ni 100
P= bidding price ambayo ni 75 kama mfano unavosema
N= idadi ya siku treasury bills itapoiva mfano wetu ni siku 365

Riba= (100-75)/75 ×(365×100)/365
=0.3333×100
Riba = 33.33%

Ikiwa na maana kwa pesa ambayo utatoa kununua treasusry bills utapata gawio la asilimia 33.33% ndani ya siku 365 yaani mwaka mmoja tu.

Piga mahesabu kama umewekeza milioni 100 ambazo huna matumizi nazo ina maana baada ya siku 365 utakuwa na faida ya kama milioni 30 ambazo hata kujazitolea jasho.

Nataka pia kuwamegea siri kwamba mabenki ya kibiashara na wafanyabiashara wakubwa ndio wamekuwa wakitajirikia hapa kwani wao wanawekeza kuanzia bilioni na kwenda juu. Kwa hiyo unaweza kufikiri ni pesa kiasi gani wanatengeneza.
Kuna watanzania wengi sana wana mamilioni ya pension benki hizi ndizo fursa za kuchangamkia ambazo huwezi kuzisikia zikitangazwa kwa maana ndipo pesa ilipo.

Kama hujaelewa waweza acha comment yako hapa then ntakujibu..


=========

SOMA PIA:

1) Tofauti ya uwekezaji wa hati fungani na masoko mengine ya mitaji kama Hisa - JamiiForums


2)
Umeongelea sana Treasury Bills,naomba maelezo kuhusu Treasury Bonds.
 
Umeongelea sana Treasury Bills,naomba maelezo kuhusu Treasury Bonds.
N a wewe si uingie youtube tuu ujifunze kama uko serious au google hizo info zipo in details , kwa kukusaidia zote ni sawa tofauti yake ipo kwenye muda wa maturity, treasury bills ni ya muda mfupi( year or less) na treasury bonds ni ya muda mrefu ( mpaka miaka 30)
 
N a wewe si uingie youtube tuu ujifunze kama uko serious au google hizo info zipo in details , kwa kukusaidia zote ni sawa tofauti yake ipo kwenye muda wa maturity, treasury bills ni ya muda mfupi( year or less) na treasury bonds ni ya muda mrefu ( mpaka miaka 30)
Nimechagua kujifunzia JF
 
Kipindi kile wanatuokota kwenye matangazo redioni et oooo unanunua hisa alafu na wewe unakuwa mmiliki wa voda unapiga tu miluzi ukiangalia wafanyakazi wako wanavyoingia kzn asubui.
 
Bills na Bond zote hazina risk boss!..isipokuwa faida zinatofautiana kama nilivyoeleza.Ktu kingine serikali ina issue hz treasury ku control inflation pamoja na kupata pesa za kukamilisha budget endapo kuna uhitaji.Hv vtu vyote viwili kwa ww mwekezaji haita athiri faida yako.

Kila mkazi wa jumuiya ya africa mashariki anastahili kushiriki katika mnada wa dhamana za serikali za mda mfupi na mrefu in TSH..foreign currency hazitumiki serikali itapata hasara boss!

Mfano uliotoa ni sawa ila discount inakuwa bid price utakayoshinda sio in %.

Sent using Jamii Forums mobile app
Naomba kujua capital adequacy ya brokers na dealers wa DSE na sheria/kanuni gani zimeprovide the same.
 
Very good and educative post ....
Nina rafiki yangu anayeishi US ..., yeye aliwekeza haraka sana ktk uuzaji hisa wakati ule TBL , Twiga Cement , Kenya Airways na makampuni mengine yalipoji register na DSE ...

Kwa kipindi cha miezi 6 tuu tangu awekeze, alipata faida ya Tzs 30 mil alipoziuza hisa zake alizowekeza ktk solo la hisa .. Huyu mtu alinihamasisha sana kuwekeza DSE tangu wakati huo .., ilikuwa miaka ya 2005 kama sikosei ...

So Davion, keep teaching us broo about huu ubepari per see ...
Nataman ningempata mtu kma ulivyompata ww nataman kujua zaidi
 
UTAJIRI MKUBWA ULIOPO KWENYE UWEKEZAJI WA DHAMANA ZA SERIKALI

Uwekezaji kwenye dhamana za serikali umegawanyika makundi mawili.

i) Dhamana za muda mfupi (treasury bills)
ii) Dhamana za muda mrefu (treasury bonds)

Kwa nchi yetu ya Tanzania biashara ya dhamana za serikali inasimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa niaba ya serikali ya Tanzania.

Dhamana za muda mfupi (treasury bills)
Hizi ni dhamana za muda mfupi ikimaanisha zinaiva ndani ya mwaka mmoja. Lengo kubwa hasa kwa serikali kuweka Treasury bills ni kupata fedha kwa ajili kukabiliana na mapungufu ya fedha katika bajeti na pale inapohitaji fedha kwa haraka.

Dhamana za muda mfupi zipo katika makundi manne kutegemea na mda zitakapoiva: ya siku 35, siku 91, siku 182 na siku 364.

Uwekezaji katika Treasury bill una faida zifuatazo kwa mwekezaji;
i)Hazina hatari yoyote kubwa (risk free) kwa mwekezaji na ni uwekezaji wa uhakika kwa sababu zinatolewa na serikali.

ii)Zaweza kuhamishika kutoka umiliki wa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Ikimaanisha pale mwekezaji anapotaka kuuza anaweza akafanya hivo.

iii)Zaweza kutumika kama dhamana za kuombea mikopo kwenye taasisi za fedha bila usumbufu wowote kwa sababu thamani ya treasury bill coupon haibadiliki kwa hiyo ni rahisi kwa taasisi za fedha kuzipa kipaumbele kutumika kwenye dhamana.

iv)Gawio ni kubwa pale unapowekeza kwenye treasury bills zaidi hata ya kuwekeza kwenye taasis yeyote ya fedha kupitia fixed deposits. (namaana ya kwamba riba katika treasury bills ni kubwa maradufu ya riba za benki)

Soko la treasury bills
Biashara na soko la treasury bills zinafanyika kwa njia mbili;

a) Soko la awali (primary market) hapa ni pale banki kuu ya Tanzania inapotoa kwa mara ya kwanza treasury bills kwa wawekezaji.

b) Soko la pili (secondary market) hii inahusisha kuuza na kununua treasury bills na hii inafanyika Dar es salaam stock exchange DSE. Hapa ndipo pale mtu anapotaka kuuza treasury bills anayoimiliki anaweza kwenda kuuza.

Kianzio cha kuwa mwekezaji wa moja kwa moja kwenye treasury bills kwa Tanzania ni sh. 5,000,000. Ina maana kwamba ukiwa na mtaji wa kuanzia milioni tano basi unaruhusiwa moja kwa moja kushiriki kwenye mnada wa treasury bills (treasury bills auction).

Kwa wawekezaji wa mtaji chini ya milioni tano basi wao watashiriki kwenye mnada kupitia primary dealers ambao kwa urahisi ni mabrokers na commercial banks

Primary dealers ambao wamethibitishwa na BOT ni hawa wafuatao (ambao wale wenye mitaji chini ya milioni tano watapitia kwao) Akiba Commercial Bank Ltd, Citibank (T) Ltd, CRDB Bank Ltd, Diamond Trust Bank (T) Ltd, Eurafrican Bank (T) Ltd.Exim Bank (T) Ltd. Habib African Bank Ltd. International Commercial Bank (T) Ltd. Kenya Commercial Bank (T) Ltd.NBC Limited. NMB Ltd. Stanbic Bank (T) Limited Standard Chartered Bank Ltd.Orbit Securities Co. Ltd. Rasilimali Limited Solomoni Securities Ltd. Core securities Ltd. Tanzania securities Ltd. Vertex International Securities.

Unapata vipi pesa kupitia dhamana za muda mfupi?
Serikali kupitia BOT inapotoa treasury bills zinakuwa katika mfumo wa zabuni ikimaanisha kwamba wawekezaji watatakiwa kwa mfano kusema watanunua kila shilingi 100 ya serikali kwa kiasi gani? (hatua hiyo ya kwanza inaitwa bidding)

Ili kupata faida kwa wawekezaji wanatakiwa kutoa bei ambayo ipo katika discout, ikiwa na maana mwekezaji anaweza kununua shilingi 100 ya serikali kwa shilingi 93 hivo mda wa kuiva ukifika atapata faida ya shilingi 7.

Mfano serikali imetoa treasury bills ya siku 365. Kisha mwekezaji akaweka bid ya kununua kila shilingi 100 kwa shilingi 75. Kama mwekezaji atafanikiwa kwenye zabuni hiyo atapata treasury bill yenye (face value) ya Tzs 100,000,000 ingawaje kiasi alichotoa ni Tzs 75,000,000 kwa sababu ndicho kiasi alicho bid katika kabrasha la zabuni yake.

Baada ya treasury bills kuiva yaani kutimia siku 365, mwekezaji atalipwa na BOT kiasi cha TZS 100,000,000 ambayo italeta faida ya (TZS 100,000,000-TZS 75,000,000= TZS 25,000,000). Hivo faida itakuwa ni TZS 25,000,000.

Ukiweka katika asilimia ni kama ifuatavyo;
- Kanuni ya kukokotoa riba katika treasury bills:
Riba=(F-P)/P ×(365×100)/N

F= face value ya treasury bills ambayo ni 100
P= bidding price ambayo ni 75 kama mfano unavosema
N= idadi ya siku treasury bills itapoiva mfano wetu ni siku 365

Riba= (100-75)/75 ×(365×100)/365
=0.3333×100
Riba = 33.33%

Ikiwa na maana kwa pesa ambayo utatoa kununua treasusry bills utapata gawio la asilimia 33.33% ndani ya siku 365 yaani mwaka mmoja tu.

Piga mahesabu kama umewekeza milioni 100 ambazo huna matumizi nazo ina maana baada ya siku 365 utakuwa na faida ya kama milioni 30 ambazo hata kujazitolea jasho.

Nataka pia kuwamegea siri kwamba mabenki ya kibiashara na wafanyabiashara wakubwa ndio wamekuwa wakitajirikia hapa kwani wao wanawekeza kuanzia bilioni na kwenda juu. Kwa hiyo unaweza kufikiri ni pesa kiasi gani wanatengeneza.
Kuna watanzania wengi sana wana mamilioni ya pension benki hizi ndizo fursa za kuchangamkia ambazo huwezi kuzisikia zikitangazwa kwa maana ndipo pesa ilipo.

Kama hujaelewa waweza acha comment yako hapa then ntakujibu..


=========

SOMA PIA:

1) Tofauti ya uwekezaji wa hati fungani na masoko mengine ya mitaji kama Hisa - JamiiForums


2)
Kufanya biashaea na serikali ni risk sana
 
Haki ya mungu Nikielekezwa hizo documents mbili nilizopost na kuzielewa wallah najiona sehemu baada ya Miaka kadhaa nitakuja humu na ushuhuda ....


Tangu Jana hiyo website ya BOT nadhani Mimi itakuwa nimekuwa kiumbe kilichoitembelea zaidi ..

Sent From My Nokia Ya Tochi
Mkuu tupe mrejesho plse!
 
Back
Top Bottom