Faida ya kula Mboga na Matunda mbalimbali kwa Afya yako

Faida ya kula Mboga na Matunda mbalimbali kwa Afya yako

Mkuu samahani sana, huwa ni mpenzi mzuri wa mada zako lakini kwa hili naomba nikukosoe kidogo, matembele ni bonga ya wanawake, mwanaume kula matembele ni kutaka kujiletea changamoto tu, usiniulize kwanini?
 
Matembele ni mboga maarufu sana, pia ni mboga yenye virutubisho sana,
Lakini matembele yana faida nyingi katika miili yetu.

FAIDA ZA MBOGA YA MATEMBELE KWA UFUPI

1: Matembele yana madini ya chuma. Madini haya ndiyo muhimu katika utengenezaji wa damu, kwa hiyo mtu anapotumia matembele anakuwa anaongeza kiwango cha damu mwilini. Watu wenye upungufu wa damu na kina mama wajawazito wanashauriwa kula matembele kwa wingi.

2: Matembele yana vitamini A ambayo husaidia kuimarisha macho na hivyo kumsaidia mtu kuona vizuri hasa hasa nyakati za usiku.

3: Matembele yana vitamini C Ambayo humlinda mtu asipate kiseyenye (scurvy). Vitamini C huimarisha ngozi na fizi, unapotumia matembele fizi zako na ngozi huimarika na huzuia kuvuja damu kutoka kwenye fizi.

4: Matembele yana protini ambayo husaidia katika kuimarisha misuli na kusaidia katika ukuaji wa mwili. Wape watoto matembele ili wakue vizuri.

5: Matembele yanasaidia kuongeza damu kwa wingi mwilini ikiwa utayachemsha na kula na maji yake kila siku

6: Matembele yanasaidia kuongeza nuru na kuboresha Afys ya macho

7: Matembe yanasafisha damu na kutoa mafuta machafu

8: Kamba lishe zilizo kwenye matembele ni chanzo cha kupata choo kikubwa vizuri
Kwani zinaboresha mfumo wa usagaji ( digestion)

MATAYARISHO
ILI UPATE FAIDA HIZI NI BORA UKAWA UNACHEMSHA MATEMBELE YENYEWE TUU UKAWEKA NYANYA NA VITUNGU NA CHUMVI KWA MBALI
UKATUMIA BAKULI KUBWA MOJA KILA SIKU

ANGALIZO
KWA MTU MWENYE VIDONDA VYA TUMBO HAYAMFAI AU GESI NYINGI

Aaah weeeh [emoji23][emoji23][emoji23] ert ad nuru ya macho
Ushawah ona wapi mboga ya majani ikawa na protein [emoji28][emoji28][emoji28] broh
 

Faida 20 Mwilini za Kula Bamia​



BAMIA.jpg
JAPOKUWA bamia huchukuliwa na wengi kuwa ni chakula rahisi kinachotumiwa zaidi na kundi la watu wenye uchumi wa chini na kati, ukweli kwamba aina hiyo ya mboga ina maajabu ya aina yake mwilini.



Walaji wa bamia hunufaika kwa kupata utitiri wa viinilishe vilivyomo kwenye zao hilo, ambavyo humpatia mlaji faida za kiafya takribani 20.

Mojawapo ya faida za ulaji wa bamia ni kuwasaidia wanawake kuepukana na changamoto za kiafya zinazojitokeza kwa baadhi yao ambao huwa na siku zisizotabirika za mizunguko yao ya kila mwezi.



Wapo wanawake wanaosumbuliwa na hedhi za mara kwa mara, ulaji wa bamia utawasaidia kuondokana na tatizo hili.

Faida nyingine ya ulaji wa bamia ni kuondoa vimelea vya sumu kwenye ngozi ya mwanadamu.



Ulaji wa bamia husaidia pia kukabili ugonjwa wa pumu. Huongeza kinga ya mwili na mtu akiwa na kinga ya mwili, hawezi kushambuliwa na maradhi mara kwa mara.

Faida nyingine ya ulaji wa bamia ni kupata virutubisho aina ya nyuzinyuzi ambavyo husaidia katika kusaga chakula tumboni.



Aidha bamia ni protini ambazo husaidia kujenga mwili.

Ulaji wa bamia husaidia pia kuimarisha afya ya nywele, kupambana na tatizo la uchovu wa mwili na pia msongo wa mawazo.

Kwa wale wenye tatizo la kupata choo kigumu, ulaji wa bamia husaidia kuondokana na tatizo hilo kwani husaidia kulainisha utumbo mkubwa (large intestines) kutokana na kazi yake ya kulainisha choo.



Bamia hutumika kwa kutibu vidonda vya tumbo, inasaidia kusawazisha asidi.

Fahamu kuwa bamia inaweza kukutoa katika hatari ya kupata ugonjwa wa kisukari kwa sababu ya uwezo wake wa kusaidia kuyeyusha au kumeng’enya sukari.

Pia, huweka sawa mfumo wa sukari mwilini.



Bamia ni aina ya chakula chenye utajiri wa makapimlo ambayo ni muhimu sana katika mwili hasa katika usagaji wa chakula.

Mojawapo ya faida ambayo ni muhimu ni kusaidia kumeng’enya sukari mwili au kuweka sawa mfumo wa sukari mwilini na pia tatizo la kukosa choo ni tatizo la kawaida kwa wagonjwa wa Kisukari.



Bamia ikiliwa mara kwa mara inasaidia kurekebisha mfumo wa umeng’enya chakula na sukari mwilini.

Angalizo kwa wagonjwa wa kisukari, msiache dawa zenu na kuanza kutumia bamia kama dawa.

Majimaji yanayotoka katika bamia yana uwezo wa kuondoa lehemu katika mishipa ya damu kwenye mwili.



Tumia bamia mara kwa mara kama tunda mboga linalosaidia kumeng’enya sukari mwilini na kuimarisha kinga ya mwili wako.

Tukiachana na kisukari, bamia huongeza na huboresha kinga ya mwili hasa kwa watu ambao kinga yao ya mwili imeshuka kama vile watu wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU).



Wataalamu lishe wanasema watu wengi wamekuwa wakila bamia kwa kuidharau ila huzuia magonjwa ya moyo kwa kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri.

Watu wenye matatizo ya vidonda vya tumbo, bamia huwasaidia kupunguza uwezekano wa kupata saratani ya tumbo na huongeza kiwango cha damu mwilini. Wengine wanatumia bamia kama dawa ya kuongeza kinga ya mwili kwa kutafuna zikiwa mbichi au kuzichemsha.



Faida nyingine ya ulaji wa bamia ni kuusaidia mwili kusafisha damu.

Ulaji wa bamia husaidia kutibu tatizo la upungufu wa damu. Bamia pia huondoa sumu mwilini na faida nyingine ni kuimarisha mifupa pamoja na mfumo wa uonaji kwa sababu ina chanzo kizuri cha vitamini A na Beta Carotene.



Bamia pia husaidia mwili kukabiliana na baadhi ya saratani. Utelezi wake huchuja uchafu unaoingia katika Kolestorali (cholesterol) na asidi ya nyongo inayoingia kutoka kwenye ini ambao usipodhibitiwa huenda ikasababisha matatizo ya kiafya.



Bamia ina Vitamin C ambayo inawafanya watoto wanaougua ugonjwa wa pumu kupumua vizuri wanapoitumia. Nusu kikombe cha bamia iliyopikwa, huwa na miligramu 13 ya vitamin C, ikiliwa husaidia sana.



Kwa wagonjwa wa kidondandugu (Cancer); wakitumia bamia husaidia kuweka utumbo kuwa na hali nzuri, hivyo kupunguza uwezakano wa kuugua ugonjwa huu wa kansa, hii hasa kwenye utumbo mkubwa.



Ulaji wa bamia pia husaidia mishipa midogo ya damu; kula kwa wingi kunasaidia kuimarisha mishipa hiyo midogo ya damu.

Watu wenye matatizo ya vidonda vya tumbo, bamia huwasaidia kupunguza uwezekano wa kupata saratani ya tumbo na huongeza kiwango cha damu mwilini
Wengine watakimbilia kula viba100 badala ya bamia.
 
Mkuu samahani sana, huwa ni mpenzi mzuri wa mada zako lakini kwa hili naomba nikukosoe kidogo, matembele ni bonga ya wanawake, mwanaume kula matembele ni kutaka kujiletea changamoto tu, usiniulize kwanini?
Changamoto zipi hizo, au ndio maana sasa vifo vimeongezeka sana? Hali ngumu tunashindia tembele ,tunalalia tembele na kuamkia hilohilo tembele
 

SABABU ZA MBEGU ZA MABOGA KUIPIKU SUPU YA PWEZA​


maboga-1-1024x682.jpg

MBEGU za maboga zimekuwa kimbilio namba moja kwa baadhi ya watu, wakiwamo kina baba wanaozichangamkia kwa nia ya kujiongezea nguvu za kiume, sawa na ilivyo kwa samaki pweza na supu yake.

Madaktari na wataalamu wa lishe wanathibitisha kuwa mbegu za maboga zina kiwango kikubwa cha virutubishi vya vitamin na madini na hivyo kusaidia katika kuupa mwili nguvu na kuukinga dhidi ya maradhi mbalimbali yakiwamo ya baadhi ya aina za saratani, kisukari, moyo na ini.

Imeelezwa na wataalamu kuwa kama ilivyo kwa sifa ya mnofu wa pweza, mbegu za maboga pia zina sifa ya kuwa sawa na kifurushi cha madini yanayomfaidisha mlaji kwa wakati mmoja, baadhi yakiwa ni ya chuma, manganizi, maginizia, zinki na shaba. Walaji wa mnofu wa pweza hunufaika pia kwa wingi wa virutubishi kama protini, mafuta (fats) vitamin B12, selenium, madini ya chuma, shaba na vitamin B6.

Imebainika zaidi kuwa kufahamika zaidi kwa ukweli kuwa viini lishe vilivyomo ndani ya mbegu za maboga vina faida kubwa ikiwamo ya kuimarisha afya za uzazi ndiko kunakoongeza matumizi yake kiasi cha kutishia umaarufu wa supu ya pweza.

Mbegu hizo za maboga sasa huuzwa Sh. 3,000 kwa vipimo vidogo vya chini ya nusu kilo katika Soko la Mwananyamala, jirani na Kwa Kopa na pia katika baadhi ya maduka makubwa yakiwamo ya Tabata Segerea huuzwa hadi Sh. 15,000 kwenye mfuko wa ujazo usiofikia kilo moja.
MABOGA-4.jpg

Katika baadhi ya maeneo, wapo wafanyabiashara wanaopita kwa wanywaji kuwauzia mbegu hizo kwa bei ya wastani wa Sh. 2,500 kwa kikombe kidogo kama cha kahawa. Ni kwamba wateja wamekuwa wakiongezeka sana na wengi wanazifurahia kwa ladha yake nzuri na pia kuwasaidia kiafya, wanaume ndiyo wanazinunua sana huku wakisema kwamba zina faida kubwa kwao kama ilivyo supu ya pweza.

Maboga na mbegu zake vina faida nyingi mwilini na kwamba, kufahamika zaidi kwa taarifa zake katika siku za hivi karibuni kunaweza kuwa chanzo cha kuongezeka kwa watumiaji wake kila uchao.

Baadhi ya faida za mbegu na pia maboga yenyewe kwa walaji ni pamoja na kuwaepusha na uzito wa mwili kupita kiasi, kuwaongezea uoni wa macho kutokana na kuwa na viini viitwavyo ‘beta-carotene’ vinavyobadilishwa mwilini kuwa vitamin A; kuongeza mfumo wa kinga ya mwili dhidi ya magonjwa na pia kuwafanya walaji waonekane vijana zaidi.
MABOGA2.jpg

Faida nyingine ni kwa walaji kujipunguzia uwezekano wa kupata magonjwa ya kansa. Tafiti zinaonyesha kuwa watu wanaokula vyakula vyenye wingi wa virutubisho vya beta-carotene (vilivyomo kwenye maboga) huwa na uwezekano mdogo wa kupata baadhi ya aina za kansa, ikiwamo ya tezi dume na kansa ya mapafu.

Maboga husaidia pia kukabili kisukari kwa kuimarisha kiwango cha sukari mwilini; kuongeza utulivu wa mwili pia kutokana na kuwapo kwa kiwango cha virutubisho viitwavyo ‘tryptophan’ vinavyowasaidia watu wenye matatizo ya kukosa usingizi (insomnia).

Faida za mbegu za maboga zina kiwango kikubwa cha madini kama ya Zinc ambayo yana faida nyingi mwilini. Mbali na faida hizo maboga huimarisha uwezo wa walaji katika kuonja na kunusa, ukuaji wa seli mbalimbali za mwili na pia kuwa na viinilishe vyenye kuongeza nguvu ya tendo la ndoa kwa wanaume.
MABOGA3.jpg

Mbegu za maboga zina vitamini E ingawa siyo kwa kiwango kikubwa lakini hiyo husaidia afya ya ngozi. Zina protini ambayo husaidia mwili kukabili maradhi kama kisukari, tezi dume na aina nyingine za saratani.

Faida nyingine ni kuongeza uzalishaji wa maziwa ya kiwango bora zaidi kwa kina mama wanaonyonyesha. Ni vizuri kwa walaji kutumia zaidi mbegu za maboga zilizo mbichi kwa sababu ndizo zenye madini zaidi kulinganisha na zile zilizokaushwa na pia wawe makini ili kuepuka kula mbegu zilizokaa kwa muda mrefu na kushambuliwa na fangasi. Wanaozikaanga wahakikishe kuwa haziwi kwenye kikaangio kwa zaidi ya dakika 15. Hii itasaidia kutozipotezea ubora wake.

Ukweli ni kwamba wengi na baadhi huzijumuisha katika vyakula maalumu vya lishe ya watoto. Wapo kina mama huzikausha na kuzisaga pamoja na chakula cha watoto. Hii ni lishe nzuri kwa sababu ina virutubisho vingi muhimu na vyote hupatikana kwa pamoja kwa walaji.

 
Matembele ni mboga maarufu sana, pia ni mboga yenye virutubisho sana,
Lakini matembele yana faida nyingi katika miili yetu.

FAIDA ZA MBOGA YA MATEMBELE KWA UFUPI

1: Matembele yana madini ya chuma. Madini haya ndiyo muhimu katika utengenezaji wa damu, kwa hiyo mtu anapotumia matembele anakuwa anaongeza kiwango cha damu mwilini. Watu wenye upungufu wa damu na kina mama wajawazito wanashauriwa kula matembele kwa wingi.

2: Matembele yana vitamini A ambayo husaidia kuimarisha macho na hivyo kumsaidia mtu kuona vizuri hasa hasa nyakati za usiku.

3: Matembele yana vitamini C Ambayo humlinda mtu asipate kiseyenye (scurvy). Vitamini C huimarisha ngozi na fizi, unapotumia matembele fizi zako na ngozi huimarika na huzuia kuvuja damu kutoka kwenye fizi.

4: Matembele yana protini ambayo husaidia katika kuimarisha misuli na kusaidia katika ukuaji wa mwili. Wape watoto matembele ili wakue vizuri.

5: Matembele yanasaidia kuongeza damu kwa wingi mwilini ikiwa utayachemsha na kula na maji yake kila siku

6: Matembele yanasaidia kuongeza nuru na kuboresha Afys ya macho

7: Matembe yanasafisha damu na kutoa mafuta machafu

8: Kamba lishe zilizo kwenye matembele ni chanzo cha kupata choo kikubwa vizuri
Kwani zinaboresha mfumo wa usagaji ( digestion)

MATAYARISHO
ILI UPATE FAIDA HIZI NI BORA UKAWA UNACHEMSHA MATEMBELE YENYEWE TUU UKAWEKA NYANYA NA VITUNGU NA CHUMVI KWA MBALI
UKATUMIA BAKULI KUBWA MOJA KILA SIKU

ANGALIZO
KWA MTU MWENYE VIDONDA VYA TUMBO HAYAMFAI AU GESI NYINGI


Umesahau #9; matembele yanaongeza nguvu dume.
 
Huwa napenda sana kuzisaga na kuweka kwenye uji wa watoto. Ila sasa safari hii zimepanda bei sana 10,000kg.
 
Back
Top Bottom