Offshore Seamen
JF-Expert Member
- Mar 9, 2018
- 5,489
- 14,091
Kwa wale wanao agiza magari nchi za Japan,China,Singapore,UK,Canada na USA kipindi unapo agiza gari kama umenunua bidhaa nyingine mfano spare,electronics,nguo na machine ni vyema ukapakia ndani ya gari uliagiza ili kupunguza gharama za kusafirisha hizo bidhaa kwenye meli nyingine.
Unachotakiwa kufanya ni baada ya kununua gari kutoka kwa dealer kwenye nchi husika, inabidi utoe taarifa kuna mizigo utaipakia kwenye gari yako. Njia sahihi na salama inabidi mizigo itayopakiwa iandaliwe parking list hii itaonyesha ni vitu gani vimepakiliwa. Kama itawezekana anayepakia aandae loading report hii itaonyesha picha ya kila mzigo kabla na baada ya kupakiwa hii usaidia endapo kuna hupotevu wa mzigo.
Changamoto inayowakumba wengi baada ya gari kufika ni kufikiri mzigo ulipo ndani ya gari hautakiwi kulipiwa port charges na kodi.
Mzigo utaopakiwa ndani ya gari unaweza ukawa una Bill of Lading au hauna. Mzigo unaweza ukaunganishwa na Bill of Lading ya gari hivyo ukimpa kazi wakala wa Forodha haitomsumbua kwenye kufatilia malipo ya kodi na bandari. Mzigo pia unaweza ukawa na Bill of Lading yake na gari pia ina Bill of Lading yake hii haina shida.
Wengi hutumia njia ya Bill of Lading ya gari kuwa documented na mizigo anayopakiwa inakuwa haipo kwenye documents ya gari (unmafested cargo) na huwa hawaweki taarifa za vitu gani vilipakiwa.
Hii sio kosa kisheria ni njia halali na inatakiwa ulipe gharama za bandari na kodi stahiki wakati wa kutoa gari yako, gari italipiwa kodi yake na mizigo iliyo ndani.
Wenzetu wa Zambia,Rwanda,Malawi na DRC hutumia njia hii kuagiza gari na vifaa vya nyumbani,spare na mizigo ya biashara. Pia siku za karibuni hata watanzania wanao agiza maroli na basi za kichina hutumia njia hii kuagiza spares na vifaa kisha kupakia kwenye gari husika aliloagiza.
Unachotakiwa kufanya ni baada ya kununua gari kutoka kwa dealer kwenye nchi husika, inabidi utoe taarifa kuna mizigo utaipakia kwenye gari yako. Njia sahihi na salama inabidi mizigo itayopakiwa iandaliwe parking list hii itaonyesha ni vitu gani vimepakiliwa. Kama itawezekana anayepakia aandae loading report hii itaonyesha picha ya kila mzigo kabla na baada ya kupakiwa hii usaidia endapo kuna hupotevu wa mzigo.
Changamoto inayowakumba wengi baada ya gari kufika ni kufikiri mzigo ulipo ndani ya gari hautakiwi kulipiwa port charges na kodi.
Mzigo utaopakiwa ndani ya gari unaweza ukawa una Bill of Lading au hauna. Mzigo unaweza ukaunganishwa na Bill of Lading ya gari hivyo ukimpa kazi wakala wa Forodha haitomsumbua kwenye kufatilia malipo ya kodi na bandari. Mzigo pia unaweza ukawa na Bill of Lading yake na gari pia ina Bill of Lading yake hii haina shida.
Wengi hutumia njia ya Bill of Lading ya gari kuwa documented na mizigo anayopakiwa inakuwa haipo kwenye documents ya gari (unmafested cargo) na huwa hawaweki taarifa za vitu gani vilipakiwa.
Hii sio kosa kisheria ni njia halali na inatakiwa ulipe gharama za bandari na kodi stahiki wakati wa kutoa gari yako, gari italipiwa kodi yake na mizigo iliyo ndani.
Wenzetu wa Zambia,Rwanda,Malawi na DRC hutumia njia hii kuagiza gari na vifaa vya nyumbani,spare na mizigo ya biashara. Pia siku za karibuni hata watanzania wanao agiza maroli na basi za kichina hutumia njia hii kuagiza spares na vifaa kisha kupakia kwenye gari husika aliloagiza.