Freed Freed
JF-Expert Member
- Jun 27, 2017
- 6,547
- 7,167
Habari za pilika Wana JF Wenzangu.
Niende madani.
Kwa muda mrefu nimekuwa nikiwaza kwenye faili la Makabidhiano ya Urais Kuna nini ndani yake? Niliwaza hili wakati Rais Mkapa akikabidhi nchi kwa Rais Kikwete na Pia wakati Kikwete naye akimkabidhi Rais Magufuli. Hili jambo ni Muhimu kwani huu mwaka wa uchaguzi na sio ajabu akawepo Rais mpya.
Nimekuwa nikiwaza Ikulu inakabidhiwaje? Nchi inakabidhiwaje? Nimekosa mtu sahihi wa kunijuza na leo nikaja na mabunio au kubumba Kama sio assumptions zifuatazo.
1. Rais mpya hukabidhiwa Majengo yote ndani ya Ikulu kwa kutembezwa na kuoneshwa Kila jengo, chumba na matumizi yake ikiwa ni pamoja na faili la majengo hayo.
2. Rais mpya hukabidhiwa Rasilimali watu wote wa Ikulu na hivyo ni jukumu lake kubaki nao au laahh.
3. Rais mpya hukabidhiwa faili la maeneo yote ya nchi kuanzia idadi ya mikoa, wilaya, tarafa, kata, na idadi ya vijiji na mitaa yote nchini. Majina sio lazima, ni idadi tu.
4. Rais mpya hukabidhiwa idadi yote ya Mashirika ya umma na mamlaka mbalimbali za serikali na majina yake.
5. Rais mpya hukabidhiwa faili la majeshi yote ya ulinzi na usalama na idadi ya Askari Kila jeshi. Sio majina ya Askari, ni idadi tu kwa Kila jeshi.
6. Rais mpya hukabidhiwa faili la Rasilimali zote nchini Kama wanyama pori, madini, misitu, viwanda vya umma Kama vipo, maziwa, bahari, ukubwa wa aridhi ya Tanzania mfano km za mraba........, Gesi, Mafuta au petroli iliyopo aridhini na Rasilimali nyinginezo. Baadae huambiwa awe tayari kufa akizilinda. Aridhi yetu ndiyo imebeba vyote hivyo na ndiyo kitu cha kuanza kulindwa na Rais ktk Rasilimali.
7. Rais mpya hukabidhiwa faili la makadirio ya idadi ya Watanzania waliopo nchini, nje ya nchi na idadi ya wageni waliopo nchini.
8. Rais mpya hukabidhiwa majina ya wizara zote na muundo wa Kila wizara.
9. Rais mpya hukabidhiwa faili la mapato ya nchi na mwelekeo wa uchumi ktk kipindi husika. Hapa mchanganuo wa sekta inayochangia zaidi hadi ya mwisho bila kuandika longongo nyingi.
10. Rais mpya hukabidhiwa faili la msimamo wa nchi ktk masuala mbalimbali ya kitaifa. Taifa liegemee au kutogemea upande wowote.
11. Rais mpya hukabidhiwa kitabu cha katiba ya nchi aitetee na kuilinda.
12. Rais mpya hukabidhiwa kitabu cha ilani ya chama chake Kama Rais anayeondoka na ajaye wanatoka chama kimoja kutakiwa kuilinda na kuitekeleza. Hata Kama anacho atapewa upya.
13. Rais mpya hukabidhiwa faili la madeni ya nje na ndani. Madeni yote ambazo nchi inadaiwa.
14. Mwishowe huambiwa Mshahara wake na Rais anayemaliza muda wake.
Nawe njoo na mabunio yako. Nikipata bunio jingine nalileta.
Karibuni.
Mods chondechonde nipo chini ya miguu yenu. Hili jukwaa la Great Thinkers.
Niende madani.
Kwa muda mrefu nimekuwa nikiwaza kwenye faili la Makabidhiano ya Urais Kuna nini ndani yake? Niliwaza hili wakati Rais Mkapa akikabidhi nchi kwa Rais Kikwete na Pia wakati Kikwete naye akimkabidhi Rais Magufuli. Hili jambo ni Muhimu kwani huu mwaka wa uchaguzi na sio ajabu akawepo Rais mpya.
Nimekuwa nikiwaza Ikulu inakabidhiwaje? Nchi inakabidhiwaje? Nimekosa mtu sahihi wa kunijuza na leo nikaja na mabunio au kubumba Kama sio assumptions zifuatazo.
1. Rais mpya hukabidhiwa Majengo yote ndani ya Ikulu kwa kutembezwa na kuoneshwa Kila jengo, chumba na matumizi yake ikiwa ni pamoja na faili la majengo hayo.
2. Rais mpya hukabidhiwa Rasilimali watu wote wa Ikulu na hivyo ni jukumu lake kubaki nao au laahh.
3. Rais mpya hukabidhiwa faili la maeneo yote ya nchi kuanzia idadi ya mikoa, wilaya, tarafa, kata, na idadi ya vijiji na mitaa yote nchini. Majina sio lazima, ni idadi tu.
4. Rais mpya hukabidhiwa idadi yote ya Mashirika ya umma na mamlaka mbalimbali za serikali na majina yake.
5. Rais mpya hukabidhiwa faili la majeshi yote ya ulinzi na usalama na idadi ya Askari Kila jeshi. Sio majina ya Askari, ni idadi tu kwa Kila jeshi.
6. Rais mpya hukabidhiwa faili la Rasilimali zote nchini Kama wanyama pori, madini, misitu, viwanda vya umma Kama vipo, maziwa, bahari, ukubwa wa aridhi ya Tanzania mfano km za mraba........, Gesi, Mafuta au petroli iliyopo aridhini na Rasilimali nyinginezo. Baadae huambiwa awe tayari kufa akizilinda. Aridhi yetu ndiyo imebeba vyote hivyo na ndiyo kitu cha kuanza kulindwa na Rais ktk Rasilimali.
7. Rais mpya hukabidhiwa faili la makadirio ya idadi ya Watanzania waliopo nchini, nje ya nchi na idadi ya wageni waliopo nchini.
8. Rais mpya hukabidhiwa majina ya wizara zote na muundo wa Kila wizara.
9. Rais mpya hukabidhiwa faili la mapato ya nchi na mwelekeo wa uchumi ktk kipindi husika. Hapa mchanganuo wa sekta inayochangia zaidi hadi ya mwisho bila kuandika longongo nyingi.
10. Rais mpya hukabidhiwa faili la msimamo wa nchi ktk masuala mbalimbali ya kitaifa. Taifa liegemee au kutogemea upande wowote.
11. Rais mpya hukabidhiwa kitabu cha katiba ya nchi aitetee na kuilinda.
12. Rais mpya hukabidhiwa kitabu cha ilani ya chama chake Kama Rais anayeondoka na ajaye wanatoka chama kimoja kutakiwa kuilinda na kuitekeleza. Hata Kama anacho atapewa upya.
13. Rais mpya hukabidhiwa faili la madeni ya nje na ndani. Madeni yote ambazo nchi inadaiwa.
14. Mwishowe huambiwa Mshahara wake na Rais anayemaliza muda wake.
Nawe njoo na mabunio yako. Nikipata bunio jingine nalileta.
Karibuni.
Mods chondechonde nipo chini ya miguu yenu. Hili jukwaa la Great Thinkers.