Fainali ipi ya 'UEFA Champions League' ilikuvutia kwa miaka 10 iliyopita?

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790

Tukiwa tunaelekea kwenye fainali ya Uefa Champions League ya msimu huu kati ya Manchetser City Vs Chelsea FC. Tujikumbushe katika miaka 10 iliyopita ni fainali gani ilikuvutia zaidi?

Mimi fainali niliyoikubali ni ile ya Real Madrid Vs Atletico Madrid, Sergio Ramos anasawazisha goli dakika za lala salama kabisa. Mpaka leo naamini Atletico alistahili kuwa bingwa kama sio Sergio Ramos kuwafanyia unyama.

Karibu utukumbushe na ya kwako.
 
Ile ya Manu vs Barcelona mpaka Sir Alex akaanza kutetemeka mikono.

Barcelona walikuwa katika ubora wa aina yake!

Sir Alex miaka kadhaa baadae alihojiwa kuhusu Fainali ile akasema alirudia kutazama zaidi ya mara mbili fainali ile akagundua Man Utd hamna sehemu walikosea ila walikutana na timu bora sana!
 
Fainali nyingi zilikuwa hovyo hasa miaka ya karibuni zimekuwa upande mmoja sana.

Ni fainali mbili tu miaka kumi iliyopita unaweza sema ilikuwa 50/50 timu zote zilipambana hadi sekunde ya mwisho

Dortmund v Bayern 2013
Paris v Bayern 2020


Fainali mbovu kuliko zote ni Liverpool v Spurs, ilikiuwa hovyo kupita hata ile ya Milan v Juve mwaka 2003 pale old traffold
 
Kwangu
2001 BAYERN BINGWA VS VALENCIA
2002 MADRID BINGWA VS BAYER LIVERKUSEN
2003 MILAN BINGWA VS JUVENTUS
2005 LIVERPOOL BINGWA VS AC MILAN
2006 BARCELONA BINGWA VS ARSENAL
2008 MAN U BINGWA VS CHELSEA
HIZI KWANGU ZILIKUWA FAINALI HASA.
Hapo pia utajua sisi watu tunajua mpira kwa kiasi gani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…