Fainali ya ASFC | Yanga SC 3 (4) - 3 (1) Coastal Union | Uwanja wa Sheikh Amri Abeid | Yanga BINGWA

88' Sopu Goooooooooooaaal goal

Abdul Sopu anaipatia Coastal Union bao la pili, akijitwisha kichwa na kumuacha golikipa Diara akiangalia tu, Kijana hatari sana.

Yanga SC 2-2 Coastal Union
Hii sopu Sijui itakuwa brand gani

Nina mashaka na omo
 
Huyu Sopu aje tu Simba. Na tubadilihane Mgunda, tuwape Matola
 
Kumbe Yanga mna wazee
Wapi nimesema Yanga ina wachezaji wazee! Mimi nimesema Coastal ina wachezaji wengi vijana.

Kama unataka nikuelezee kuhusu Yanga, basi nitakuambia Yanga ina wachezaji wengi wazoefu na wenye vipaji vikubwa vya kuasakata kabumbu.

Timu yako ya simba ndiyo timu inayo ongoza kwa sasa, kwa kuwa na wachezaji wengi wazee. Hivyo usiisingizie kabisa timu ya wananchi.
 
Kwa hiyo Aziz Ki anashuhudia live toka uwanja wa Sheikh Amri Abeid Karume timu yake mpya wakitoana jasho na watoto wadogo hawa Coast?
 
Unanifokea au? Pambaneni na kombe lenu hilo
 
Mchezaji gani mzee ambaue yuko Simba kamzidi unri ronaldo?
 
Mpira unaendelea baada ya dakika 90 zinakamilika sasa ni wakati wa dakika za nyongeza.

Yanga SC 2-2 Coastal Union
 
Kuna Upuuzi Pale Nyuma, Mwamnyeto Hayuko Serious na Watu Wake Nyuma

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Tatizo la Mwamnyeto siku zote ni kuzubaa, kujisahau na pia kujiamini kupita kiasi.

Siyo beki ya kazi kazi kama ilivyokuwa kwa mabeki waandamizi wa Yanga, mfano Kelvin Yondani na Nadir Haroub Cannavaro.

Anyway, ngoja tuone itakuwaje. Ila mabeki wameonyesha udhaifu mkubwa kwenye goli la pili.
 
Shida ni kwamba hatuthamini vya kwetu huyo Sopu ni mzuri ila kwakua ni mtanzania basi akienda kwenye team kubwa hizi za kariakoo hawezi kupata muda wa kuvumiliwa kwakua sio mchezaji wa kigeni, dogo wa kitanzania hawezi kudekezwa na kuwekewa matumaini kama jinsi ambavyo wanapewa madogo(wa umri wake) wa nje.

Nikitakiwa kumshauri Sopu, nitamwambia aende Azam kama wametuma ofa.

Huyo VICTOR AKPAN ni player wa maana tu, kama anaweza kuonekana kwenye team kama Coastal basi kwenye team nzuri atafanya vizuri tu, kama SIMBA Sc tumemsajili basi tutakuwa tumelamba dume.
 
Sema sio mbaya si tayati mkononi mna jagi mlilo beba juzi.

Au na hili mna mpango wa kulizungusha mji mzima kama mwenge?
 
Kwa hiyo Aziz Ki anashuhudia live toka uwanja wa Sheikh Amri Abeid Karume timu yake mpya wakitoana jasho na watoto wadogo hawa Coast?
Huyu Yanga Sc kikawaida huwa hafui dafu kwa Coastal (tangu miaka huko nyuma) , ni vile tu binadamu tumeumbwa kusahau ndomaana uliwaona wakiwa na viburi.

Huyohuyo coastal ndo alitibua unbeaten run yao ya msimu uliopita.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…