Familia ya Mzee Wagagigikoko inaongozwa na Mama wa Kambo

Familia ya Mzee Wagagigikoko inaongozwa na Mama wa Kambo

The Legacy

JF-Expert Member
Joined
Jun 1, 2022
Posts
5,879
Reaction score
11,318
Enzi za Uhai wa Mzee Wagagigikoko aliongoza familia yake kwa mabavu hata mkewe hakua na Sauti yako maamuzi.
Familia ilinawili lakini watoto wa jirani waliolima shamba moja na mzee huyo walikonda kwa mateso na fitna sababu mzee huyu Katili hakupola chakula pekee toka kwa jirani zake Bali alipola uhai wa watoto na wazazi pia wa familia jirani.HAKIKA aliogopwa sana kwenye kijijini kile.

Kama Nakumbuka vizuri watoto wa wazee wafuatao ni vijana wenzangu waliopotea
Mtoto wa mzee Kitunza muda ,Mtoto wa mzee Nguo za jeshi

Kijana Wasiwasi pia aliuliwa kikatiki na watoto wa mzee Wagagigikoko.

Hakuishia Hapo alipotea mtumbuizaji Parokia alipokataa kutumbuiza kwenye sherehe ya mzee huyo. Lakini Akapatikana ametupwa kijiji cha usisemezane.ni baada ya Kijana wa mzee Wagagigikoko aitwae Mtumia Kombeo kusema kwamba atapatikana.
Mzee Wagagigikoko alikua na watoto watukutu kama Badiwochi na Ameshiba

Nakumbuka pia Mchuuzi maarufu Kaubeli alipotea na kupatikana.
Mzee Wagagigikoko alifariki Mwezi 12 mwaka 2003.
Hakika kijiji kilitulia wa usikitika walisikitika,wakulia walilia na wakufurahi walifurahi.
Ma majonzi na masikitiko Mke wa mzee Wagagigikoko akaanza kuitunza familia yake na kuendeleza mali za marehemu mumewe.

Mke wa mzee Wagagigikoko Mama Hidehea alijitahidi kutafuta upatanishi na majirani zake.alionekana kwenye sherehe za majirani misiba na kushiriki vikao vya kijiji miezi kadhaa.

Ghafla watoto wa jirani wakaanza kupotea,
Leo tumepata Msiba wa mzee Kofi na tunaelekea mazikoni.

ITAENDELEA…….
 
Azory Gwanda
Ben Saanane
Sabaya
Makonda
Mo Dewji
Mamake Wanu, mama Abdul
 
Back
Top Bottom