DOKEZO Familia ya Rais Kikwete yahusika ufisadi wa ESCROW

DOKEZO Familia ya Rais Kikwete yahusika ufisadi wa ESCROW

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
2lipodokezwa juu ya safari ya jk nchini marekani kwa mara nyingine miccm ilikuja hapa kwa mbembwe kukanusha!hv mnadhani kwa mliyoyashuhudia hili suala linashindikana?ikija julikana nikweli inasinzia 2li,mmekuwa kama misukule!get up and fight,mnakuwa wajinga wajinga 2!hasara kubwa kwa taifa,pambaf kabisa!kila ki2 mnafumba macho,mnataka mpaka mfanywe nin ndio muone nchi inatafunwa!i wish u come 2 ur senses smday!
Mnashangaza sana nyie mnaowaita CCM wale wote mnaotofautina kimtazamo. Hata mimi nilitofautina nanyi kuhusiana na safari ya JK marekani japo mimi siyo CCM.Tatizo siyo kutoa taarifa ya JK kusafiri, tatizo ni upotoshaji unaoambatana na taarifa zenu, kwani Rais kwenda Marekani ni siri?
 
Ufisadi wa dola 250m (zaidi ya 400bn) umetikisa nchi kwa kuikosesha takribani miradi ya sh 3trilion imefahamika. Kampuni ya PAP ilipewa dola 122m (200bn), na kusaini makubaliano kikao cha kunduchi beach hotel oct8.2013 kuwa kiasi kilichobaki (128m au zaidi ya 200bn), PAP watalipwa kila mwezi 8bn mpaka deni kwisha.

Kampuni hii ya PAP iliyopewa tuzo hiyo ya 400bn kwa kuwekeza 6mTsh tu ni ya nan? Kwa mujibu wa nyaraka za BRELA, 50% inililiwa na Singh Sethi(singasinga) na mwanae na asilimia 50% zinamilikiwa na kampuni ya Simba Trust ya Australia.

Simba trust ni nan.? Uchunguzi umeonesha kuwa Simba trust ya Australia inamilikiwa na watu wawili ambao ni salima Kikwete na Miraji Kikwete.

Uwepo wa majina haya mawili kama wamiliki wa PAP inatafsiriwa kuwa ndio sababu kuu ya JK kuvuta miguu huku nchi ikiumia.

Kwa mkataba huu wa IPTL wa 100MW wa miaka 20 (1995_2015), umeongezwa miaka mingine 20 (2013_2033)kwa kuzalisha 500MW.

Kwa mujibu wa mkataba huu, kampuni ya PAP italipwa 400m kila siku kama capacity charges . Maana yake singasinga mwenye 50% atapata 200m kila siku. Na watoto wawili wa JK watapata kila mmoja 100m kila siku hadi 2033.

Uwepo wa familia ya JK kwenye ufisadi huu inadaiwa ndio Kinga ya wahusika ; Muhongo, werema, maswi, mramba, likwilile na hata waziri mkuu kutetea

Ushahidi unakwenda kuonesha kuwa hata uamuzi wa Gavana kuruhusu fedha hiyo itoke kimakosa ni baada ya kupata MEMO kutoka Katibu wa rais Bw Mbena ikisema Rais kaelekeza.

Na ni sababu hiyo pia baada ya Dr Hosea kuwasilisha report kwa rais, JK alisoma na kumjibu achana nayo na ndio maana mpaka sasa report hiyo haijapelekwa kwa DPP ili.wahusika wafikishwe mahakamani


KAMA SEHEMU YA MWANGAZA.

Napenda kuwakumbusha Watanzania, Mataifa ya Ulaya na Marekani huwa hayakurupuki kutoa shutuma, ukiona wanatoa tamko ujue wana uhakika. Walieleza juu ya meli za Iran kutumia bendera ya Tanzania, Membe alikurupuka kukanusha kama kawaida yake, baadaye ikadhihirika ni kweli.
Mataifa ya Ulaya yalitishia kusimamisha misaada kutokana na ufisadi wa Richmond, kwanza serikali ilikanusha baadaye ilidhirika kuwa ni kweli kulikuwa na wizi.

Mataifa ya Ulaya yaliwahi kuelezea ufisadi katika manunuzi ya radar, serikali ikatoa maelezo marefu kuonesha hakuna ufisadi, baadaye ikadhihirika ni kweli.

Sasa wametoa tamko kuwa hakuna msaada kutolewa kwa Tanzania mpaka waone taarifa ya CAG kuhusu ufisadi katika akaunti ya Escrow, serikali imekanusha hakuna ufisadi.

Vyombo vya habari vya Ulaya vimeeleza kuhusu kuhusika kwa serikali ya Tanzania, CCM na China katika biashara haramu ya pembe za ndovu, Membe kama kawaida yake amekurupuka kukanusha lakini mambo hayo yote yatakuja kudhihirika kuwa ni kweli kwa 100%.

Taarifa ya Escrow ipo tayari lakini yaliyomo ndani ni balaa maana ni zaidi hata ya wananchi walivyokuwa wakiitegemea.

Hii iliyopo chini ni kama tetesi lakini ni tetesi yenye uhalisia. Endeleeni kufuatilia kashfa hii kubwa inayogusa ofisi kubwa zote za nchi.
______________________________ ______________________________ ____________

Ikiwa ni siku chache tangu Baraza la Usalama la Taifa kukutana na kupitia ripoti ya uchunguzi ya PCCB kuhusu ufisadi wa zaidi ya shilingi bilioni 200 kwenye akaunti ya Tegeta escrow Benki Kuu, Taarifa za uchunguzi zinaeleza kuwa mkurugenzi wa PCCB Dr. Edward Hosea atamkabidhi Mh. Rais Jakaya Kikwete ripoti hiyo Jumatano ijayo kama ilivyoelekezwa na Baraza la Usalama wa Taifa.

Awali ripoti hiyo ilikuwa akabidhiwe Mh. Waziri Mkuu Mizengo Pinda, lakini taarifa za ndani zinabainisha kuwa uzito wa ripoti hiyo unastahili Mkuu wa nchi mwenyewe kwani kuna maeneo ambayo Waziri Mkuu atastahili kuwajibika.

Ofisi nyingine zilizohusika kwenye ufisadi huu kwa mamlaka yao ni Wizara ya Fedha, Benki Kuu, TANESCO, Wizara ya Nishati na Madini, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, TRA, na baadhi ya vigogo Ikulu.

RIpoti hiyo imekwenda mbali zaidi kuonesha baadhi ya majina ya watu maarufu waliojipatia fedha hizo kwa namna mbalimbali. Kwa mfano, akaunti ya kampuni ya VIP Engineering katika Benki ya Mkombozi iliyopokea hela za escrow imekutwa hela nyingi zimetoka kwenda kwa Wabunge,Mawaziri Majaji, na baadhi ya watu maarufu (hii ni kwa mujibu wa benki statement ya akaunti hiyo yenye kurasa 27 kuanzia tarehe 20 Januari mpaka tarehe 14 Agosti 2014).

Baadhi ya majina ndani ya benki statement hiyo yalitumiwa pesa kupitia akaunti hiyo ni pamoja na Waziri Anna Tibaijuka, Waziri wa zamani William Ngeleja, Mwanasheria Mkuu wa zamani Andrew Chenge, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi na mmoja wa Majaji wa mahakama kuu ya Tanzania Mujulizi. Katika orodha hiyo kuna Wabunge, wajumbe wa kamati ya Nishati na Madini, wote isipokuwa mmoja tu ambaye ni mtumishi mwandamizi wa zamani wa Serikali. Viongozi wawili wakuu wa vyama vya siasa vya upinzani nchini wameonekana katika orodha hiyo pia.
Juhudi kubwa zinafanywa hivi sasa kuzuia taarifa ya CAG na PCCB isikabidhiwe Bungeni kwani kama itakuwa wazi inaweza kusababisha kuibuka kwa mtikisiko mkubwa.

==============================================


Updates
Miraj Jakaya Kikwete amejibu shutuma hizi kwa kusema;
attachment.php
Mkuu hii nchi imeshauzwa bila sisi kujua napita tu.
 
Mkuu tetty nimependa maneno yako yenye kumfikishia ujumbe huyu gamba lizaboni. Mara zote maneno yake ni hayo hayo. Kuna siku alicoment " umekuja kutafuta mabwana humu nenda jukwaa husika". Ukiangalia na alivo coment kwanko ni same same. Hii inaonyesha ni mtu aliye ishiwa hoja na anatetea asicho kiamini. Tatizo la magamba ni hilo wana IDS zao fulani fulani humu ni lazima zitetee hata kama ikiandikwa kitu cha kitaifa zaidi, kwa maneno ya busara uliyo tumia nadhani huyu gamba atajifunza kuto tukana watu hovyo. Tz ni yetu wote and we are in for it NOW than ever before. Watch out Magambas.....
Mbona mnatumia nguvu nyingi sana kumshambulia LIZABONI? Haya ndiyo matatizo ya kutumwa kuja kitoa kashfa kwa viongozi. Hivi haya aliyoyaandika YERIKO NYERERE kumhusu Rais KIKWETE yana tofauti gani na kashfa alizokuwa akiziumia kumkashfu ZITTO KABWE ili afukuzwe uanchama kule CHADEMA? Bado hmtawashawishi watanzania kuwa mnao uwezo wa kushika dola, kama njia zenyewe mnazozitumia ni hizi. Na ripoti ya CAG na TAKUKURU ndiyo itamuumbua kabisa YERIKO na Genge lake
 
Mbona mnatumia nguvu nyingi sana kumshambulia LIZABONI? Haya ndiyo matatizo ya kutumwa kuja kitoa kashfa kwa viongozi. Hivi haya aliyoyaandika YERIKO NYERERE kumhusu Rais KIKWETE yana tofauti gani na kashfa alizokuwa akiziumia kumkashfu ZITTO KABWE ili afukuzwe uanchama kule CHADEMA? Bado hmtawashawishi watanzania kuwa mnao uwezo wa kushika dola, kama njia zenyewe mnazozitumia ni hizi. Na ripoti ya CAG na TAKUKURU ndiyo itamuumbua kabisa YERIKO na Genge lake
mkuu Tatamadiba ... lizaboni hajengi hoja yeye ni matusi hasa ya kuhusu wanaume. Sijui jinsia yake ni she au ni he, ila liza yaweza kuwa she.. ( na guess) ndo maana yuko hivyo. Madiba was a man of people na atabaki kuwa icon ya south africa na africa kwa ujumla. Kama jina lako umelitoa kwake basi na amini you dont believe in what u are standing for. Ndani ya moyo wako humaanishi unacho tetea bali unaipenda Tz na waTz wake. Karibu CDM tosa hao magamba wanaua nchi. Karibu sana kwenye ukombozi wa pili wa Tz hutu tatamadiba.
 
Yericko na bangi zake za kuvutia chooni anakuja kupotosha hoja ya ukweli huwa haiko hivyo mwambie zitto mjipange upya jk anafanya maendeleo kama haya
View attachment 200994
.......hoja jibiwe kwa hoja na wala sio mipasho, watanzania tumechoka watu wanapojificha kwenye kivuli cha amani na utulivu wakati wao wanaiba hadi kuvimbiwa; ukiwabana kwa hoja ndio utasikia maneno yanayofanana na ya kwako eti ooh anatumiwa na nchi za magharibi wakati huo huo viongozi wetu wanashinda kutembeza bakuli huko huko magharibi, amani ya nchi hii itakuja kumalizwa na hili kundi chache linalokula rasilimali za nchi kwa staili ya kuvimbiwa!!!!!! iba, sawa, si umetamani kuiba? lakini sio kwa kiwango hiki, afu tunaenda kuweka hela kwa wazungu, wakati huo huo tunabisha hatujaiba, nchi hii wananchi walio wengi ni wavivu na ama hawajishughulishi kabisa kufikiri, baadhi ya viongozi wao/wetu ndio kabisaaa wanataka wazungu wafikiri kwaletea maendeleo badala yao; ili mradi tumechagua ujinga na giza vituongoze na kuuona mwanga kama ukoma!!!!! na mzungu akikupenda na ama kukushabikia wewe kiongozi wa Afrika, ujue wewe ni poyoyo!!!!! NOTHING IS PERMANENT, BUT CHANGE.

sasa unajiuliza nini wakati mwanzo umetaja majina ya wamiliki wa hiyo kampuni? Acha kuchafua watu tena mbaya zaidi unamchafua mkuu wa kaya
.......ww ni nani hasa unayewasemea? acha kuwachosha watu kufikiri kwa ajili yako wakati pia nao wana yao ya kufikiri

Simba trust inamilikiwa na Miraji Kikwete na Salima Kikwete
......hii ndio amani na utulivu, ukihoji, umetumwa, lakini mimi huwa nasema na narudia kusema, hata kama viongozi wetu wanapata viburi vya kufanya haya kwa sababu inawezekana wameuweka sawa mfumo mzima wa ulinzi na usalama, yana mwisho haya, tumeona kwa Sadamu, wapi Uday na Qusay? kwa Gadaffi, wapi Saad, Mu utassin na Khamisi? wapi Mubarak!!!! masikini na sisi tunaomba Mungu, kuna siku atajibu viburi vya watawala wetu, AMINA!!!!1
 
Yeriko ni mzushi
Hakuna uchunguz wala nin
Nachoona hapo ni kuunganisha habari vipande vipande kutoka magazetini, vijiwe vya kahawa na vilinge vya bangi

Afu hii movie ya kulink watt wa mkulu na upigaji wa pesa naona imechuja sasa
Imetoka kwa riz now kwa hawa wengine

Ivi uzushi faida yake nini
 
400,000,000 x 12 x 19 years = 91,200,000,000. Hii ni capacity charge tu! Mtaua!
 
Issue ni mfumo wetu hasa katiba inampa mamlaka kubwa rais kiasi kwamba anaweza akafanya llte na hakuna mtu wa kumuhoji au kumzuia!Hapa hao wote ambao wana mamlaka ya kuchunguza na kupeleka suala mahakamani ni wateule wake hivyo hawawezi kwenda kinyume na yeye!Wasiwasi wangu sidhani kama serikali iliyopo itamaliza muda wake itakuwa kama mambo ya Richmond maana huu ufisadi mkubwa kweli umekuwa balaa na tatizo kubwa!!!!!
 
Yericko huwa hapepesi macho inapokuja ishu ya kuwalipua mafisadi

- Hivi Yericko si ndiye aliyesema Kamati Kuu ya CCM inakutana Dodoma kulivunja Bunge la Katiba na haikutokea, kweli kuna mtu anamuamini huyo kibaraka wa Mkono? please!!

Le Mutuz
 
Hayo ni mawazo yako yalipotoka mnona slaa alishindwa kupata hata kura elfu kumi akashindwa hata kusogea alipokuwa amesimama jk ni kiongozi hodari ndiyo maana kwa sasa tanzania haipo kwenye kundi la nchi 25 maskini duniani wakati2010 tulikuwa katika nchi kumi maskini soma hapa.
Hizi ni kwa mujibu wa takwimu za CCM.
Tunafahamu kabisa nchi yenye uchumi ulio imara ina sifa zifuatazo:-
Sarafu yenye nguvu...... hatuna sarafu yenye nguvu
matibabu ni shida hospitali hazina dawa
Madawati hatuna
elimu bora hatuna
umeme hatuna
gesi nchi itapata only 10% the rest inaenda Norway
CCM haitaki watu wanaofikiria, inataka mijitu tulale tuuuu ili watuibie...
Kataa CCM, Kataa katiba inayopendekezwa
 
Kwanini watanzania tusiongee ukweli kuhusu singasinga juu ya kukwepa kulipa kodi na kuwahonga maafisa waandamizi wa serekali akiwemo pinda, werema, na simba trust ambayo ni ya mama salma kikwete na miraji kikwete.
Na kwanini tunataka kukwepesha ukweli na kutaka kuwatoa watu wengine kafara?
Watanzania kwa sasa sio wajinga tumesoma na tunawezapambanua mambo.
Pia kumbe adi takukuru ni wala rushwa? Eti wanawaingiza watu wasiohusika kisa hawakuwapa rushwa.

Kuna watu ambao hawawezitoa rushwa kwa sababu ni watu wa kimaadili sana kwaiyo takukuru ni wala rushwa.

Takukuru imenuka kwa rushwa. Suala la escrow takukuru imeomba rushwa kwa baadhi ya wadau waliopewa msaada na vip engeneering kupitia mkombozi bank na bbaada yakutokuwapa rushwa takukuru ikaamua kuwaingiza wakat hawahusiki.

Watanzania hatutakubari viongozi waadilifu kutolewa kafara naaver ever patachimbika haki ya mungu.
 
Kwa mara nyingine nashuhudia mtambo wa kupika majungu ukiendelea kukaanga majungu ili Watanzania wale. Pole sana Ndugu. Prof Kikwete na familia yake hawawezi kuchafuliwa kijinga kama unavyoiga swaga za Yeriko
 
Huwezi kubaki salama ukiwa kwenye cheni ya kukomba hela za kifisadi. Wote lazima washughulikiwe, hakuna kupewa msaada kwenye hela za ufisadi ila kuna kugawana tu. Hayo madai ya kupewa msaada ni sehemu ya kutaka kujificha tu.
Ova
 
Mama Salma Kikwete na Miraji Kikwete bring back our money...

Nyie ni laana katika nchi..
 
Kwa mara nyingine nashuhudia mtambo wa kupika majungu ukiendelea kukaanga majungu ili Watanzania wale. Pole sana Ndugu. Prof Kikwete na familia yake hawawezi kuchafuliwa kijinga kama unavyoiga swaga za Yeriko

Watu wanataka kuona hatua zinachukuliwa.Wafadhili wamezuia Misaada lakini hatuoni umakini wowote wa Serikali kufuatilia suala hili.Wananchi wamepewa habari za ndani kuelezea sababu za ukimya wa Serikali ni uhusika wa vigogo hao.Kama ni uwongo tunataka kuona Kalasinga akikamatwa.
 
Kwanini watanzania tusiongee ukweli kuhusu singasinga juu ya kukwepa kulipa kodi na kuwahonga maafisa waandamizi wa serekali akiwemo pinda, werema, na simba trust ambayo ni ya mama salma kikwete na miraji kikwete.
Na kwanini tunataka kukwepesha ukweli na kutaka kuwatoa watu wengine kafara?
Watanzania kwa sasa sio wajinga tumesoma na tunawezapambanua mambo.
Pia kumbe adi takukuru ni wala rushwa? Eti wanawaingiza watu wasiohusika kisa hawakuwapa rushwa.

Kuna watu ambao hawawezitoa rushwa kwa sababu ni watu wa kimaadili sana kwaiyo takukuru ni wala rushwa.

Takukuru imenuka kwa rushwa. Suala la escrow takukuru imeomba rushwa kwa baadhi ya wadau waliopewa msaada na vip engeneering kupitia mkombozi bank na bbaada yakutokuwapa rushwa takukuru ikaamua kuwaingiza wakat hawahusiki.

Watanzania hatutakubari viongozi waadilifu kutolewa kafara naaver ever patachimbika haki ya mungu.

Hizo habari zako umezitoa wapi?

= hatutakubali
 
$$ My lovely country...!!!!!!

$$ The country with everything on earth...Tz..but WILL REMAIN ONE OF THE POOREST COUNTRY IN THE WORLD....

$$$ Reason is very simple...POOREST
GOVERNANCE ever seen & heard....$$
 
Kwa mara nyingine nashuhudia mtambo wa kupika majungu ukiendelea kukaanga majungu ili Watanzania wale. Pole sana Ndugu. Prof Kikwete na familia yake hawawezi kuchafuliwa kijinga kama unavyoiga swaga za Yeriko
Hivi huwa unpewa sh ngapi kwa unafiki ulionao?unatetea nini sasa,wakati kila kitu kiko wazi,umeshajiuliza kwanini bunge linasuasua kuiingiza ripoti ya cag ijadiliwe?acha unafiki,raslimali za nchi zinanufaisha wachache wakati hata mahospital I hakuna dawa,wao wakiugua matibabu nje ya nchi.
 
sasa hapa tunabishana juu ya nini?maana hizi pesa ilioneka kwamba zililipwa kwa wahusika na kumbe wamegawiwa watu ambao mnawaingiza sasa hivi kwamba na wao waligawiwa hii ni ajabu!baada ya kukana sasa mnadai hata wapinzani mliwagawia! kwa kazi gani?kama sio ufisadi?hawa wanaoitwa wapinzani kumbe ni wale wasemao ukweli! mna laana sana na Mungu hatawaacha,au mwadhani kwa kujilimbikizia mali ya dhuluma mtaabudiwa?maana mnazo fedha za kutosha na bado kila iitwapo leo ni skendo! ni hadi mtuuwe ndo muamini kwamba mmeyafanya maisha yetu kuwa hayawezekani?shauri yenu hatuna cha kupoteza! kama sio viongozi ni vipi ukweli wa jambo hili hauwekwi bayana?na mnaotetea Watanzania tusiujue ukweli mtapigwa kwa laana naam itakuwa aibu kubwa kwenu.
 
Back
Top Bottom