Familia ya Rais Magufuli mkiliachia hili jambo lipite bila ya kumburuza mahakamani Kabendera itakuwa ni usaliti wa karne!

Familia ya Rais Magufuli mkiliachia hili jambo lipite bila ya kumburuza mahakamani Kabendera itakuwa ni usaliti wa karne!

Kiongozi wa Kidini:

Mtume Muhammad alileta ujumbe wa Uislamu kutoka kwa Allah kupitia Qur'an. Alikuwa mjumbe wa mwisho katika mfululizo wa manabii, na alielezea imani ya kipekee kwa Mungu mmoja (Allah). Aliongoza watu katika ibada za kila siku, kama vile sala (Swala), na alifundisha mafundisho ya dini ya Kiislamu kwa njia ya mfano bora.

Aliweka mifumo ya kidini inayoongoza maisha ya kila mtu, kutoka kwa familia hadi jamii, na alisisitiza haki za wanawake, wanyonge, na maskini.


2. Kiongozi wa Kijamii:

Alianzisha mabadiliko makubwa katika jamii ya Kiarabu, akileta umoja katika jamii iliyokuwa imegawanyika na kuzaliana migogoro ya kikabila. Alianzisha Mkataba wa Madina (Sahifat al-Madina), ambao uliweka misingi ya usawa, haki, na uhuru wa dini kwa watu wa makabila mbalimbali na dini tofauti.

Alikuwa mzalendo wa haki na alitetea wanyonge, alikataa ubaguzi wa kijinsia, na alisisitiza umuhimu wa kuheshimu haki za kila mtu katika jamii.


3. Kiongozi wa Kisiasa:

Mtume Muhammad aliongoza kwa mfano na aliunda serikali thabiti katika mji wa Madina baada ya Hijra (hamia kutoka Makka). Alikuwa na uwezo wa kusimamia masuala ya kijamii, kisiasa, na kisheria kwa ufanisi mkubwa. Aliunda mfumo wa serikali wa kwanza wa Kiislamu, ambao ulilenga katika haki, usawa, na utawala wa sheria.

Aliwezesha amani katika jamii yake, na alifanikiwa kupambana na vikwazo vya nje kama vita vya Uhud na Badr, akiwa kiongozi wa jeshi na mratibu wa mikakati ya kijeshi.
Angalau sasa umejaribu kujibu japo historia inakupinga. Muhammad hakuwahi kuwa kiongozi wa kisiasa pale Madina na ilifika wakati mamlaka za mji zilianza kumsaka/kumtafuta kwa kosa la kuhamasisha vurugu na chuki na akakimbilia milimani huko. Huo uongozi alipewa na nani ikiwa alikimbia mji kwa kusakwa na mamlaka!?
 
Vigumu lakini sio impossible. Kuondoa dhana zozote kuhusu kupotea kwa Saanane, serikali ituambie yupo wapi. Lakini serikali haijawahi kufanya uchunguzi makini au kutoa tamko rasmi.
Ushahidi kuwa Rais Magufuli alimuua Ben uko wapi?
 
Angalau sasa umejaribu kujibu japo historia inakupinga. Muhammad hakuwahi kuwa kiongozi wa kisiasa pale Madina na ilifika wakati mamlaka za mji zilianza kumsaka/kumtafuta kwa kosa la kuhamasisha vurugu na chuki na akakimbilia milimani huko. Huo uongozi alipewa na nani ikiwa alikimbia mji kwa kusakwa na mamlaka!?
Kisa cha Mauaji ya "Qisas" (Adhabu ya Kisasi):

Katika kipindi cha utawala wa Mtume Muhammad, alikuwapo mshtakiwa aliyehusika na mauaji ya mtu mwingine. Kisa hiki kinahusiana na kifo cha Umair bin Ubaydah, ambaye aliuwa mtu kwa makusudi.

Hadithi ya "Kisa cha Mauaji ya Qisas":

Mara moja, mtu mmoja aliuwa mwingine kwa makusudi. Familia ya mtu aliyeuawa ilienda kwa Mtume Muhammad ili kutafuta haki. Walitaka kisasi (adhabu ya kifo kwa aliyemuua), jambo ambalo lilikuwa la kawaida kwa jamii za Kiarabu kabla ya Uislamu.

Uamuzi wa Mtume:

Mtume Muhammad alikusanya pande zote mbili, yaani familia ya aliyekufa na familia ya muuaji, na akaendelea kuwasikiliza kwa uangalifu. Mtume alijua kwamba sheria za Kiislamu zilikuwa wazi kuhusu "qisas" (adhabu ya kisasi), ambayo ilikuwa inaruhusu familia ya mja aliyeuawa kulipiza kisasi kwa kumuua muuaji. Hata hivyo, alijua kwamba wema, msamaha, na huruma pia zilikuwa sehemu muhimu za mafundisho ya Uislamu.

Kuonyesha Upendo na Uadilifu:

Baada ya kusikiliza pande zote, Mtume Muhammad aliwaambia wafiwa na familia ya muuaji kwamba ingawa sheria ya qisas ilikuwa inaelekeza kwamba mfuate adhabu ya kifo, aliwasihi wawe na huruma na wasamehe. Aliwazungumzia kuhusu faida ya msamaha, kuwa ni bora zaidi mbele ya Allah. Alisema:
"Wasiwe na hasira dhidi ya yule aliyeuwa ndugu yao, kwani msamaha ni jambo bora zaidi mbele ya Allah."
Mtume Muhammad aliwashawishi wafiwa wanasamehe na hawakulazimika kuchukua kisasi. Hali hii ilileta utulivu kwa familia ya mwuaji na hakukuwa na upendeleo wowote kwa upande mmoja.

SOMA HAPA TENA
 
Tatizo la watu kama Kabendera huwezijua kama anaohuo ushahidi au Laa!

Familia inaweza kutamani kufanya ulichoshauri lakini ikiwa itabainika ni kweli. Nini kitatokea?

Hakuna ambaye yupo tayari kumvua Marehemu Baba au Mume nguo tena Akiwa kaburini
Kuna tuhuma zinatolewa kimtego sana ili watu wajae wazimawazima kudai ushahidi ndipo yafumuliwe madudu, ndiyo maana walengwa huchagua kupiga kimya
 
Keani kipindi cha jpm serikali haikuwepo? Ilikuwa imeenda likizo? Au hakujua ikulu anafanya nin. Who is supposed to investgate this scandal, mimi au serikali? Na nini maqma ya serikali. We hujielewi
Unahororoka tu. Hujaweka ushahidi.
 
Katika madai yote dhidi ya Rais Magufuli, hili dai la huyu mwandishi Eric Kabdendera, kuwa Rais Magufuli alimuua Ben Saanane kwa kumpiga risasi ya kichwa hapo Ikulu [nasadiki ni Ikulu ya Dar], ni dai kubwa na zito sana.

Ni kashfa kubwa sana. Kwa mtu tu wa kawaida, kutuhumiwa kuua mtu mwenzio si jambo dogo. Seuze Rais wa nchi?

Wengi wetu kwa sasa tutakuwa tumeshaiona hii excerpt ya hicho kitabu:
View attachment 3190381

Napata wakati mgumu sana kuamini kuwa Rais Magufuli anaweza kumuua kijana wa Kitanzania, ambaye ni mtu mdogo sana, in the grand scheme of things, kwa mikono yake mwenyewe tena kwenye nyumba ya wananchi, Ikulu.

Tumeshawazoea akina Lissu na wenzake kuropoka na kutoa tuhuma za ajabu ajabu bila kutoa wala kuonyesha ushahidi wowote ule zaidi ya kusema ‘nimeambiwa’ au ‘niliambiwa’.

Lissu keshawahi kusema mara kadhaa kuwa baada ya Magufuli kufariki, eti nyumbani kwake yalikutwa mabulungutu ya mahela, dola za Kimarekani, kwenye mamilioni.

Bila ushahidi wowote ule zaidi ya ‘kuambiwa’, tuhuma hizo zinabaki kuwa ni porojo tu za Lissu.

Na ndo maana pengine hata familia ya Rais Magufuli haijawahi kusema wala kufanya chochote dhidi ya madai hayo.

Ila hili la Magufuli kutuhumiwa kuwa ni cold-blooded murderer, si la kawaida na halipaswi kupuuziwa.

If not true, what Kabendera did is libelous and should sued.

Mimi si mtaalamu wa sheria za Tanzania. Lakini naamini sheria za libel zipo.

Licha ya kwamba Rais Magufuli alikuwa ni public figure, kuna vitu huwezi kuvisema dhidi yake bila ushahidi.

Tuhuma za mauaji kwa mtu yeyote yule, humtia doa kubwa sana kwenye jamii, mtu huyo.

Majuzi hapa tumeona kituo cha televisheni cha Marekani, ABC, kilikubali kumlipa Rais Trump $15 milioni kwa sababu mmoja wa watangazaji wake alisema kimakosa kuwa Trump alipatikana na hatia ya ubakaji wakati si kweli.

Kubaka ni moja ya makosa yanayompa mtu doa la maisha.

Uuaji, kwangu mimi, ni kosa lililo juu ya ubakaji.

Sasa huyu jamaa Kabendera anakuja na tuhuma nzito namna hiyo tena kwa Rais mzima bila hata ushahidi wowote ule zaidi ya kusema kaambiwa na vyanzo vyake.

Hapana kwa kweli. Tuhuma kama hizo ni nzito sana kuachwa hivi hivi tu, la sivyo kama ni za ukweli.

Familia ya Rais Magufuli ikimwacha huyu jamaa bila kumburuza mahakani akatoe testimony yake huko under the penalty of perjury, itakuwa ni usaliti mkubwa sana kuwahi tokea nchini.

Yaani kabisa Rais Magufuli ampige risasi ya/za kichwa huyo Ben Saanane hapo Ikulu, halafu watu wa Magufuli waichukue maiti yake na kwenda kuitupa kwenye moto Rufiji?

Vigumu sana kuamini hilo.

Familia ya Rais Magufuli ni lazima ichore mstari mchangani na kuchukua hatua.

La sivyo, mtatufanya watu kama mimi tuamini kuwa yanayosemwa ni ya kweli.
Tatizo wakijaribu kwenda mahakamani tu kina Peter Madekela wataidaka hii kesi halafu watazidi kufukua file tujue na mengine hata ambayo hatujawahi tegemea kama mzee alifanya....Familia wanamjua mzee wao alikua ana roho ngumu kama jiwe ... wao wakae kimya hili litapita ...
 
Tatizo la watu kama Kabendera huwezijua kama anaohuo ushahidi au Laa!

Familia inaweza kutamani kufanya ulichoshauri lakini ikiwa itabainika ni kweli. Nini kitatokea?

Hakuna ambaye yupo tayari kumvua Marehemu Baba au Mume nguo tena Akiwa kaburini
Ndo maana nikasema wakiliacha hili suala bila kuchukua hatua, tuhuma zitaaminika!
 
Sawa, Mudi alikuwa kiongozi wa kitongoji gani..nitajie hata mtaa tu alioongoza.
Mahatma Gandhi (Kiongozi wa India)

Mahatma Gandhi alimheshimu Mtume Muhammad kwa uongozi wake bora na tabia yake. Alisema:
"Ninamheshimu Mtume Muhammad kama mtumishi wa kweli wa Mungu, ambaye aliongoza jamii kwa usawa na upendo. Alikuwa mtu wa umoja na alielewa vizuri mabadiliko ya jamii."

Gandhi aliona katika mafundisho ya Mtume, haki, msamaha, na dhamira ya kuleta amani. Alikubali kwamba Mtume Muhammad alikuwa na maono mapana ya kuleta umoja kati ya watu wa mataifa mbalimbali.
 
Kwamba yuko wapi na nani alimuua kwa kumpiga risasi kichwani ni mambo tofauti kabisa.
Tuanzie hapo hapo.....kutabu cha Eric then twende mbele....mahakamani ndio kuzuri zaidi nahisi....Eric atakuwa anajua alichoandika yeye sio kichaa na hata hasira zimepoa sasa naamini hakuandila kwa kazba....!! Open court hada za nje nchi zilizo huru...wakutane huko....tutajua ukweli!! Amechokoza mada ngumu...
 
Sawa, Mudi alikuwa kiongozi wa kitongoji gani..nitajie hata mtaa tu alioongoza.
Alphonse de Lamartine (Mwandishi wa Kifaransa)

Alphonse de Lamartine, mwandishi maarufu kutoka Ufaransa, alielezea kwa heshima kubwa tabia za Mtume Muhammad katika kitabu chake "History of Turkey" alichosema:
"Muhammad alikuwa ni mtu aliyeonyeshwa na dhamira ya kuleta mabadiliko kwa jamii na kuonyesha kwa vitendo kwamba alijali ustawi wa watu wake. Alikuwa na tabia nzuri na alikuwa na uongozi wa kipekee. Aliweza kuleta umoja katika hali ya migogoro."

Lamartine aliona kuwa Mtume Muhammad alileta mafundisho ya kipekee kwa jamii ya Kiarabu na ulimwengu wote kwa ujumla, akitambua umuhimu wa uongozi wake wa haki na uadilifu.
 
Tuanzie hapo hapo.....kutabu cha Eric then twende mbele....mahakamani ndio kuzuri zaidi nahisi....Eric atakuwa anajua alichoandika yeye sio kichaa na hata hasira zimepoa sasa naamini hakuandila kwa kazba....!! Open court hada za nje nchi zilizo huru...wakutane huko....tutajua ukweli!! Amechokoza mada ngumu...
Cold blooded murder is a serious allegation.

Kabendera must prove it.
 
Kisa cha Mauaji ya "Qisas" (Adhabu ya Kisasi):

Katika kipindi cha utawala wa Mtume Muhammad, alikuwapo mshtakiwa aliyehusika na mauaji ya mtu mwingine. Kisa hiki kinahusiana na kifo cha Umair bin Ubaydah, ambaye aliuwa mtu kwa makusudi.

Hadithi ya "Kisa cha Mauaji ya Qisas":

Mara moja, mtu mmoja aliuwa mwingine kwa makusudi. Familia ya mtu aliyeuawa ilienda kwa Mtume Muhammad ili kutafuta haki. Walitaka kisasi (adhabu ya kifo kwa aliyemuua), jambo ambalo lilikuwa la kawaida kwa jamii za Kiarabu kabla ya Uislamu.

Uamuzi wa Mtume:

Mtume Muhammad alikusanya pande zote mbili, yaani familia ya aliyekufa na familia ya muuaji, na akaendelea kuwasikiliza kwa uangalifu. Mtume alijua kwamba sheria za Kiislamu zilikuwa wazi kuhusu "qisas" (adhabu ya kisasi), ambayo ilikuwa inaruhusu familia ya mja aliyeuawa kulipiza kisasi kwa kumuua muuaji. Hata hivyo, alijua kwamba wema, msamaha, na huruma pia zilikuwa sehemu muhimu za mafundisho ya Uislamu.

Kuonyesha Upendo na Uadilifu:

Baada ya kusikiliza pande zote, Mtume Muhammad aliwaambia wafiwa na familia ya muuaji kwamba ingawa sheria ya qisas ilikuwa inaelekeza kwamba mfuate adhabu ya kifo, aliwasihi wawe na huruma na wasamehe. Aliwazungumzia kuhusu faida ya msamaha, kuwa ni bora zaidi mbele ya Allah. Alisema:
"Wasiwe na hasira dhidi ya yule aliyeuwa ndugu yao, kwani msamaha ni jambo bora zaidi mbele ya Allah."
Mtume Muhammad aliwashawishi wafiwa wanasamehe na hawakulazimika kuchukua kisasi. Hali hii ilileta utulivu kwa familia ya mwuaji na hakukuwa na upendeleo wowote kwa upande mmoja.

SOMA HAPA TENA
Niliposoma mwanzo tu "katika kipindi cha utawala wa mtume Muhammad" nikaishia hapo. Muhammad alitawala wapi? Nachojua alikuwa mwsnaharakati tu kama Che na wengine tunaowajua, utofauti wake yeye alikuwa mwanaharakati wa kidini. Hakuwahi kuwa kiongozi wa eneo lolote Duniani hata mtaa tu hakuwahi kuongoza ila alikuwa na wafuasi wake alioambatana nao kila alipokwenda.
 
Niliposoma mwanzo tu "katika kipindi cha utawala wa mtume Muhammad" nikaishia hapo. Muhammad alitawala wapi? Nachojua alikuwa mwsnaharakati tu kama Che na wengine tunaowajua, utofauti wake yeye alikuwa mwanaharakati wa kidini. Hakuwahi kuwa kiongozi wa eneo lolote Duniani hata mtaa tu hakuwahi kuongoza ila alikuwa na wafuasi wake alioambatana nao kila alipokwenda.
George Bernard Shaw (Mwandishi maarufu na Mchezaji wa Kiingereza)

George Bernard Shaw alielezea Mtume Muhammad kama kiongozi wa kipekee na mwenye uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko katika jamii. Alisema:
"Mtume Muhammad alikuwa ni kiongozi aliyelenga kuleta mabadiliko ya kimsingi kwa jamii ya Kiarabu, akiwaleta watu pamoja kwa misingi ya haki, usawa na uadilifu."
 
Back
Top Bottom