Ajabu kubwa ni kuwa baadhi ya wasanii wa muziki ndio wabebaji wakubwa wa huu unga kuingiza nchi na ni washirika wa wafanya biashara wa haya madawa, baada ya biashara kufanikiwa kuingia inatumiwa na hao hao wanamuziki na kuwaharibia kabisa maisha, ingekuwa poa wasanii wakaanzisha project yao ya kupiga madawa ya kulevya vita kwa kumaanisha na wakisikia kuna mmoja wao anahusika na hii biashara wampe onyo ikiwezekana wawape taarifa polisi ili muhusika achunguzwe, imekuwa rahisi wao kutumika kwa kuwa ndio wenye uwezo wa kufanya shoo za nje ya nchi mara nyingi na huko ndio hubebeshwa haya maunga.