Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,147
- 2,008
USIMPIGIE MTU SIMU ZAIDI YA MARA 2 MFULULIZO
- labda kama ni jambo lenye haraka sana, subiri mpaka wakupigie.
UKIKOPA, LIPA!
-Rudisha kabla hata hujaoulizwa au kukumbushwa
UKITOLEWA DINNER AU LUNCH
-Usiagize vyakula vya gharama sana na mara nyingine ununue wewe
KUWA NA UTU
-Kwa wahudumu, wafanyakazi, madereva wa uber na watoa huduma wote
MFUNGULIE MLANGO ANAYEKUJA NYUMA YAKO
-Bila kujali umri, jinsia au hadhi
UKICHUKUA UBER/BOLT NA MWINGINE
-Akilipa wakati huo, wakati mwingine ulipe wewe!
HESHIMU MAWAZO YA WATU WENGINE
-Kwako ukiona 9, huenda kuna mwenzio anaona 6
USIINGILIE MWINGINE AKIONGEA
-Zamu yako itafika, subiri!
UKIMTANIA MTU
-Akionekana hajafurahishwa, acha mara moja na usirudie tena
SHUKURU
-Sema asante unaposaidiwa, kuwa na moyo wa shukrani
USIVUNJE AHADI
-Hilo ni deni, lazima lilipwe, kama huwezi usiahidi tafadhali
UKIAMBIWA JAMBO LA SIRI
-Kuwa na kifua na uadilifu hata kesho mkiamka maadui
UKIONESHWA PICHA KWENYE SIMU YA MTU
-Usikimbilie kuswipe kulia au kushoto, huwezijua utakalo kutananacho, tuliza macho na vidole vyako
JALI MUDA WA WATU
- Usipange muda wa jambo kama huwezi kutimiza, muda ni pesa
USIONGELEE SHIBE KWA WENYE NJAA
- Ukiwa Roma, fanya kama Warumi
Mna mambo yakuongezea Wakuu? Karibuni
- labda kama ni jambo lenye haraka sana, subiri mpaka wakupigie.
UKIKOPA, LIPA!
-Rudisha kabla hata hujaoulizwa au kukumbushwa
UKITOLEWA DINNER AU LUNCH
-Usiagize vyakula vya gharama sana na mara nyingine ununue wewe
KUWA NA UTU
-Kwa wahudumu, wafanyakazi, madereva wa uber na watoa huduma wote
MFUNGULIE MLANGO ANAYEKUJA NYUMA YAKO
-Bila kujali umri, jinsia au hadhi
UKICHUKUA UBER/BOLT NA MWINGINE
-Akilipa wakati huo, wakati mwingine ulipe wewe!
HESHIMU MAWAZO YA WATU WENGINE
-Kwako ukiona 9, huenda kuna mwenzio anaona 6
USIINGILIE MWINGINE AKIONGEA
-Zamu yako itafika, subiri!
UKIMTANIA MTU
-Akionekana hajafurahishwa, acha mara moja na usirudie tena
SHUKURU
-Sema asante unaposaidiwa, kuwa na moyo wa shukrani
USIVUNJE AHADI
-Hilo ni deni, lazima lilipwe, kama huwezi usiahidi tafadhali
UKIAMBIWA JAMBO LA SIRI
-Kuwa na kifua na uadilifu hata kesho mkiamka maadui
UKIONESHWA PICHA KWENYE SIMU YA MTU
-Usikimbilie kuswipe kulia au kushoto, huwezijua utakalo kutananacho, tuliza macho na vidole vyako
JALI MUDA WA WATU
- Usipange muda wa jambo kama huwezi kutimiza, muda ni pesa
USIONGELEE SHIBE KWA WENYE NJAA
- Ukiwa Roma, fanya kama Warumi
Mna mambo yakuongezea Wakuu? Karibuni