Fanya Haya Usafishe Nyota Yako kwa mwaka 2018

Fanya Haya Usafishe Nyota Yako kwa mwaka 2018

ubongokid

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2017
Posts
2,154
Reaction score
4,184
Mpendwa
Najua wote tunataka mafanikio na leo nataka niwashirikishe siri ndogo ya furaha kwa mwaka 2018

Mwaka unaenda kufika mwisho na kwa kuwa ninakujali napenda kukushirikisha ya kufanya ndani ya masaa machache yajayo

Kwanza nakushauri ufunge hesabu ya mwaka huu.Jiangalie ulipokuwa mwishoni mwa mwaka jana na ulipo sasa.
Jiulize je kipato chako kimekuwa au kimepungua,jiulize furaha yako imeongezeka au imepungua.Jiulize kuhusu mtindo wako wa maisha,marafiki je kuna lipi limeongezeka

Jiulize kwa mwaka uliosha ni jambo gani jipya ulilojifunza.Umejifunza nini katika fani yako,umejifunza nini katika maisha

Kama kuna makosa uliyofanya je umejifunza nini kutoka na makosa hayo.na kama kuna mambo mazuri pia uliyofanya yalikufundisha nin

Jiulize unajisikiaje kuwa hai leo.Ni nani watu waliocahngia katika kukufanya ujisikie jinsi ulivyo?

Je kuna uliyemkosea ambaye unatamani kumwomba msamaha?Mwambie mwombe radhi

Ukishamaliza kutafakari na kufanya hayo yote tafuta mtu mmoja ambaye ungependa ama kumwambia asante kwa jambo fulani au kumweleza hisia zako kama vile kumpenda n.k.Mtafute uwasiliane naye umweleza jinsi unavyojisikia kwa jambo alilokufanyia au kwa yeye kuwepo katika maisha yako.

Hatua inayofuata ni kuweka malengo ya maisha yako kwa mwaka ujao.Usiweke malengo ya kipuuzi.

Lengo lako la kwanza nikuwa na furaha,Amani na upendo katika Maisha Yako

Lengo lako la pili liwe ni wewe kuhakikisha unapata mahitaji yako ya msingi kwa kadiri ya uwezo wako

Lengo lako la tatu ni kugusa maisha ya watu kwa namna njema ili ufanyike kuwa baraka

Tumia masaa haya machache kufanya hayo na utakuwa umeuanza mwaka wako vyema
 
Back
Top Bottom