Fanya hivi kunufaika na ongezeko la tozo katika miamala ya simu (M-Pesa, Tigo Pesa, Halo Pesa)

Fanya hivi kunufaika na ongezeko la tozo katika miamala ya simu (M-Pesa, Tigo Pesa, Halo Pesa)

MC RAS PAROKO

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2013
Posts
623
Reaction score
606
Ni matumaini yangu mu buheri wa afya, Bila kupoteza muda niende moja kwa moja kwenye hoja ya msingi. kwa kuwa kam tujuavyo kumekua na kilio kikubwa kutoka kila kona nchini kutokana na ongezeko la gharama za kutuma na kutoa pesa kupitia simu zetu (Mobile Money Transactions). Nikiwa ni muhanga mkubwa wa hili na kwa kugundua kulalamika au kulaumu serikali na watunga sera hakutanisaidia lolote nimeamua kuandika uzi huu ili ukusaidie na wewe angalau kupata mwangaza juu ya hili.

Kwa wakati kama huu tarajia watu wengi tuliozoea M-Pesa,Tigo,HaloPesa moja kwa moja tunahama na kurudi upande wa bank kwa sababu makato ni reasonable na kumtumia mtu pesa uliyonayo cash ni bure. Yaani leo niliwa na 100k nataka kuiituma Arusha nachukua tu account number ya muhusika namuwekea mzigo direct bila makato yoyote na nikiwa na kiwango hicho hicho na nikaamua kutoa kwa ATM makato si 1300 hadi 1000 kutegemeana na Bank unayotumia.

Nini kitatokea endapo watanzania wengi watarudi kutumia bank? La kwanza n kwamba bank zitapata wateja wapya wengi na wengine waliokua na dormant acc watazifufua, hii itapelekea bank kupitia mawakala wake walio maeneo mengi nchini watafanya miamala mingi na kuoneza mapato/faida kwa bank husika.

Ikiwa bank zitatengeneza faida kubwa zaidi ni faida kwa stakeholders ambao ni wanahisa na kwa bank kubwa Tz serikali inamiliki asilimia kadhaa ya hisa katika bank hizo mf CRDB, NMB.

Hapa umeshajua faida itaenda kuongezeka na wanahisa wanaenda kupata Dividents kubwa na Capital gain itaongezeka sababu ya wawekezaji kuvutiwa na ukubwa wa faida inayotengenezwa na Bank.

Je, nini ufanye uweze kuwa miongoni mwa wanufaikaji wa ongezeko la tozo hizi? Jibu ni rahisi tafuta Bank ambayo unaamini na umejiridhisha na mwenendo wake na hapo anza kuwekeza pole pole kwa kununua hisa zao online kwa kutumia App ya Hisa kiganjani. Ni rahisi na haihitaji uwe na pesa nyingi ili uweze kuanza kuwekeza katika sekta hii.

Sipati wala sikosi chochote kwa wewe kuwekeza katika hili ila ni kitu ninachokielewa na nimependa kushare nanyi siku ya leo. naamini uzi huu utamsaidia mmoja kati ya wasomaji wengi. Uwe na siku njema na Bwana akuongezee siku zako katika nchi aliyokupa.
 
Tuliamua kutumia mpesa, tigopesa etc kwa sababu ya mifoleni ya benki na conveniences za kutumia mitandao. Kurudi tena Benki kipindi Hiki cha korona ni risk na Haileti unafuu wowote. Suluhu ni kuenda mahakamani hizi tozo ziondolewe kwa sababu ziko kinyume na katiba
 
Watumiaji wa mitandao ya simu kwa kiasi ilibeba watu wengi kwa kuwa ni wa kipato cha chini na ni rahisi kumtumia 30000 bibi yangu kule kahama na akatoa bila hekaheka nyingi.

Bado mitandao ya simu ni muhimu hususa kwa watu tunaotima 5000 hadi 100000. Karibu kila mtu anamiliki line ya simu. Na kwa hili serikaki imepiga patamu. Yaani hapa watavuna si mchezo.

Kama kwa siku tu kima cha chini miamala mil1 inafanyika hiyo ni zaidi ya millioni miamoja wanakusanya.
 
Ninayo, naomba nielekeze matumizi yake
Kutoa Tsh 100,000 kutoka laini ya safaricom kwa kutumia wakala wa mpesa TANZANIA unakatwa TSH 1,200.

Kumtumia hela mtu alieko TANZANIA kwa kutumia laini ya safaricom unakatwa TSH 0

IMG_20210718_215745.jpeg
IMG_20210718_220337.jpeg
 
Tuliamua kutumia mpesa, tigopesa etc kwa sababu ya mifoleni ya benki na conveniences za kutumia mitandao. Kurudi tena Benki kipindi Hiki cha korona ni risk na Haileti unafuu wowote. Suluhu ni kuenda mahakamani hizi tozo ziondolewe kwa sababu ziko kinyume na katiba
Wapo mawakala wa bank kila kona ya mji
 
Ni matumaini yangu mu buheri wa afya, Bila kupoteza muda niende moja kwa moja kwenye hoja ya msingi. kwa kuwa kam tujuavyo kumekua na kilio kikubwa kutoka kila kona nchini kutokana na ongezeko la gharama za kutuma na kutoa pesa kupitia simu zetu (Mobile Money Transactions). nikiwa ni
Ni good idea but tz kuwekeza kwenye hisa ni majanfa, faida yake ndogo sana.. labda uwe na volume kubwa ya hisa ndo at least unaweza ona faida... But kama ni risk free investment basi wekeza angalau kwenye mutual fund kama utt..

Kwa kesi yahii miamala sijui serikali iliwaza nini lakini kama ni pesa kurudi kwenye mabenk nj kwamba hizi pesa zote zinazo zunguka kwenye miamala za simu huwa zina toka banks.. ni kwamba kila mtandao wa simu una main account trustee account) ambapo ndo pesa zote za hii mitandao hukaa(kwa lugha ya kibenk ni float account) so ukiweka pesa kwenye mpesa, account yako itasoma balance na the same balance itaongezeka kwenya trustee account ya mpesa iliyo bank fulan.. kwahiyo pesa zote za mzunguko wa mpesa. Airtel money sijui tigopesa zote zipo benk..

Shida ya hii tozo mpya itapunguza financial inclusion kwakua bank branches hazipo sehemu nying hivo matarajio ya serikali yanaweza yasitimie kama watu wata switch.
 
Tuliamua kutumia mpesa, tigopesa etc kwa sababu ya mifoleni ya benki na conveniences za kutumia mitandao. Kurudi tena Benki kipindi Hiki cha korona ni risk na Haileti unafuu wowote. Suluhu ni kuenda mahakamani hizi tozo ziondolewe kwa sababu ziko kinyume na katiba
Ni kweli kabisa maana watawala hawakuangalia hili la corona hasa upande wa Uchumi kutetereka Duniani kote.
 
Back
Top Bottom